Akinyi Must Die (Ni lazima Akinyi Afe)

Akinyi Must Die (Ni lazima Akinyi Afe)

Umughaka siku nyingine uache ujinga mambo ya kuleta story alafu mwendelezo mpaka ubembelezwe komaa mpuuzi mmoja ww kama imekushinda acha kuandika mbona wenzio wakina singanojr Analyse hawana Maringo ya kibinti kama ww acha kutupa stress we dogo
Bro inaonekana una hormones nyingi za kike pia una roho mbaya na kauchawi kwa mbaaliiii maana si kwa gubu hili. Hili ni gubu la mawifi mzee maana kila uzi na stoty humu wewe ni kuleta gubu.
 
Akinyi Must Die (Ni lazima Akinyi Afe) - 05



Sauti ya kike "Kama nilivyo ahidi kwenye kikao cha kwanza,nitahakikisha kila kitu kinakwenda sawa"

Aliendelea "Malipo yenu nitamwambia muhasibu awaingizie kwenye akaunti muda siyo mrefu"

Sauti ya kike "Ok nadhani tutawasiliana"

Sauti "Sawa Madam"

Sauti ya kike "Halafu Amigo ukitoka nje naomba uniitie Mudy"

Amigo "Sawa "

Yalikuwa ni mazungumzo kati ya mwanamke mmoja wa makamo aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiselikari la JERUSALEM IS OUR HOME(JoH)lililokuwa likijihusisha na Utoaji wa misaada kwa watu wasiojiweza.

Alipenda sana watu na watumishi wenzie wamuite Madam Suzy lakini jina lake halisi alifahamika kama Suzanne Mtigandi Galabi.Watumishi wenzie walimuogopa kutokana na misimamo yake na alikuwa si muongeaji sana bali alikuwa ni mtekelezaji tu.

Ni katika makao makuu ya ofisi za kampuni yake yaliyopo Jijini Mwanza katika wilaya ya Ilemela ndipo mara zote alikuwa akifanya vikao na wahusani pamoja na watu wake wa karibu.Safari hii alikuwa na kikao na jamaa watatu ambao aliwapa kazi ya kuifanya na alikuwa akipokea mrejesho wa kazi yenyewe.

Mudy "Yes Madam"

Suzanne "hebu rudishia huo mlango vizuri!"

Aliendelea "Sasa naomba unisikilize kwa makini jembe langu"

Suzanne "Roby amenipa taarifa kuna jamaa wana mzigo wa dhahabu hapo Geita na taarifa zilizopo wamepata escoti ya G4s kuuleta hapa Mwanza kwa ajili ya kuuzwa,nimezungumza na askari wetu ambao tunashirikiana nao nahitaji mkafanye ambush haraka,bado naendelea kuwasiliana na Roby na nitaomba uondoke wewe na Kerry"

Mudy "Sawa Madam,ni leo hii au"

Suzanne "Yeah Jamaa wanaleta leo,siunajua Roby ndiye infomer wetu kule,sasa kabla hawajafika Mwanza kamalizeni shughuli"

Mudy "Sawa Madam nimekupata"

Suzanne "Mchukue Kerry muondoke,chukueni hiyo Prado nyeusi na muwe makini"

Mbele ya macho ya watu lile shirika la JoH lilikuwa likijifanya kutoa misaada kwa watu wenye matatizo mbalimbali lakini ukweli ni kwamba,nyuma ya pazia kuna mambo ya hovyo yalikuwa yakiendelea ikiwemo kuutoa wa uhai wa binadamu ili kujipatia fedha haramu.Suzzane Galabi aliyekuwa akionekana muungwana mbele za watu hakuwa hivyo kama watu walivyodhani,alikuwa ni mwanamke mwenye uchu na tamaa ya mali za wenzie kupita maelezo.

Kwenye ile Prado kulikuwa na watu wawili ambao kimuonekano usingedhani ni mafia waliokubuhu;ile gari ilikuwa ikiendeshwa na mwanamke mzuri na mrembo aliyejulikana kama Kerry na pembeni yake alikaa Mudy ambaye alikuwa akiaminiwa sana na Suzanne.

Ile gari ilipofika maeneo ya Usagara ilisimama kisha wakapanda jamaa wawili ambao mmoja wao alikuwa amebeba begi la kuning'iniza mkononi.Baada ya jamaa kupanda ile gari iliondoka kuitafuta Kigongo ferry ili wavuke.Baada ya kuhakikisha wamevuka salama upande wa pili,ile gari iliondoka kwa spidi uli kuwahi katika utekelezaji wao huo wa mpango haramu,walipofika Sengerema katika kijiji cha Igaka kwa mbele,waliamua kuweka kambi hapo.

Walifanya mawasiliano na Roby ambaye alikuwa Geita kama infomer wa Madam Suzanne na kujihakikishia ya kwamba zile gari zimeshatoka na zikaribia maeneo waliyokuwepo wao.

Baada ya kupewa taarifa hiyo,mmoja wa wale jamaa wawili alifungua lile begi lililokuwa na nguo upande wa juu na chini lakini katikati kulikuwa na silaya 2 aina ya SMG,walitoa zile silaha na kuwa tayari kwa ajili ya shambulizi.

Ilikuwa ni mida ya saa 9 alasiri milio ya risasi ilianza kurindima katika njia ile ambayo hakusogea mtu bali zilisikika sauti za vishindo vikubwa,baada ya kufanikiwa kwenye shambulizi lao hilo walichukua mzigo wa dhahabu na kutokomea.Suzzanne na vijana wake walikuwa hawapati usumbufu kabisa kwasababu wakuu wengi wa Idara katika jeshi la polisi alikuwa anakula nao sahani moja,akipatacho basi walikuwa wakigawana ili kila mtu afe na chake,ilikuwa ni toa nikulinde ukipata nimepata.

---------------



Mara zote Bhoke alipokuwa akifunga shule iwe likizo ndogo au kubwa alikuwa akikaa kwa mwanamke ambaye alizaliwa na Mwalimu Veronica tumbo moja,Mwalimu Veronica yeye alikuwa mkubwa kwa mwanamke huyu ambaye alikuwa akijishughulisha na biashara ya Samaki pamoja na Dagaa kuwatoa Musoma na kuwapeleka Arusha,bhoke alikuwa akimuita mwanamke huyu Mama Mdogo.

Baada ya kuhitimu masomo yake ya kidato cha sita hali haikuwa nzuri,alipata matokeo ambayo yasingemwezesha yeye kupata mkopo wa chuo bali alipaswa gharama zote za chuo ziwe juu yake,kutokana na ugumu wa maisha wa nyumbani kwao,Bhoke aliamua asiende chuo bali aingie mtaani kujichanganya na vijana wenzie kuisaka riziki,binti Bhoke alijikuta safari hii ameangukia kwenye uchimbaji wa madini aina ya Tanzanite yanayopatikana Tanzania pekee eneo la Mirerani.
Kutokana na ile kariba ya Kikurya iliyomjenga tangu mdogo,Bhoke hakupata tabu sana kuungana na wana apolo wengine katika maduara na kuanza kuchoronga miamba ili kujipatia riziki.Ingawa alikuwa ni binti mrembo sana ambaye tangu udogo wake hadi kukua kwake hakuwahi kumjua mwanaume,aliamua kuishi kikauzu na kampani yake muda mwingi ilikuwa watoto wa kiume.

Kila mwanaume alipokuwa akimtazama Bhoke aliishia tu kumtamani na hakukuwa na uwezekano wa kumpata kwasababu katika kuwa yake hakutaka kabisa masuala ya kujihusisha na wanaume,wanaume ambao walikuwa watu wake wa karibu mwanzo walipata taabu kutokana na uzuri wake lakini walipomzoea akawa mshikaji wao wa kufa na kuzikana.

Siku kubwa kabisa ya kusherehekea siku ya mfanyakazi duniani ijulikano kama mei mosi ilikuwa ikifanyika Arusha,taasisi pamoja na mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali yalikutanika kwa pamoja na kusherehekea siku hii muhimu katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini hapo.

Simon " Wanangu mnajua Tripple A kesho TmK Wanaume Family ndani ya nyumba"

Wenzie "Hiyo haina kufeli babuu huko lazima twende"

Bhoke "Kleruu ameenda wapi?"

Simon "Jamaa atakuwa ameenda kwenye masanga kama kawaida yake"

Bhoke "Asije akaenda kuhonga malaya zake hela yangu mbwa yule"

Simon "Unamdai?"

Bhoke "Hela yangu ya mzigo wa jana hajanipa"

Simon "Andika maumivu"

Bhoke "Asiponipa najua wapi nitakapomkamatia,atanipa tu labda amenisahau!"


Walipomaliza kufanya shughuli zao siku hiyo walikubaliana kesho wangeondoka kuelekea Arusha kwa ajili ya kuwaona TmK wanaume family kila mtu alikuwa na shauku ya kwenda kumuona Sir Nature na kundi lake ambalo kwa wakati huo ndiyo ilikuwa habari ya mjini.



Itaendelea..............
 
Hilo jina Akinyi sio geni kwangu.
Akinyi na Mamaake walipanga kumuua mzee mmoja tajiri wa kizungu.
Mzee alikua kashajichokea kiasi anakunywa bia zake anajikojolea mpk afike ndani kwake apande ghorofa msala.
Sasa Akinyi kwanza kaondoka, mama nae sijui yuko wapi mjumba mkubwa kweli.
Niko na mzee garden tunachoma nyama ananisimulia maisha yake ujanani mpk hapo alipo.
Mara akaja kijana wake wa mke mkubwa.
Hakupita mlango wa mbele, karuka senyenge kazama ndani.
Namuuliza mzee huyu nani?
Akasema ni kijana wangu mkubwa huyu.
Tukasalimiana wakabishana sana na babaake.
Kumbe kijana anataka apewe mali za babaake walizochuma na mamaake.
Otherwise zitapotea kwa Akinyi na mamaake.
Hii story mzee kanisimulia mwenyewe.
Baada ya kuchoka.
Mzee kaomba nimshikilie aende akalale.
Aisee tumebebana mzee mwenyewe yuko tough na kashazitwanga.
Kumbe wale washenzi wanajua anapoangukaga mlangoni.
Likategwa li jambia kali haswa🤦‍♂️
Aisee mungu yupo jamani ningekua na kesi ya mauaji mpk sasa.
Tunaingia hapo mlangoni namkokota yule mzee tukapiga mweleka hapo km kawaida yake.
Lile bisu lilitegwa kiufundi sana mlangoni yaani akifungua mlango litachomoka nayeye aliangukie kwenye moyo kazi iishe.
Sasa hapo misheni ikashindikana
Nilimrescue yule mzee jambia huko,
Nikampeleka chumbani akalale zake.
Aisee ndio baadae Akinyi huyu hapa kaja na polisi kabisa🥲
Na mamaake katokea from no where.
Akinyi -babaangu kauliwa.
Polisi -nani unamuhisi?
Huyu hapa👆
Walikua wote mda mwingi huko garden.
Nikadakwa hapo ndani inteligensia zifuate.
Wananiuliza namimi nawauliza mzee gani kafa.?
Si huyu mwenye hili ghorofa.
Nikawaambia kafa sa ngapi??
Mi nimempeleka mpk ndani kwake juu kalala.
Khe Twende tukamuone, tukapanda juu mzee mzima kazimika tu.
Ikabidi pale kuulizwa ilikuwaje?
Kusimulia scenario yote ya jioni ile na mambo yaliyotokea,
Akinyi kageuza kibao kwamba niliwaita huyu km kaniibia hela,🤔
Nikasachiwa sina senti na nawadai.
Ikabidi polisi waniombe sorry kwa usumbufu.
Nikaondoka.
Akinyi na mamaake ndani.
Lakini baadae wakatoka yule mzee alikua mzima.
Kumbe pale wanagombea urithi tu.
Mzee alikua tajiri sana huko Kenya.
Akinyi na mamaake ni wakenya
Yule kijana aliruka senyenge ni mzungu piwa.
Nilisoma baadae kwenye magazeti walimmaliza huyo mzee wakadakwa.
Kwa hasira huyo Akinyi akajichanganya siku moja party nje huko sio kwao nikamtengeneza vizuri tu kulipia uongo wake ule.
Hii imenitokea mwenyewe zamani huko
Sorry UMUGHAKA nimepandisha story kwenye uzi wako
 
Hilo jina Akinyi sio geni kwangu.
Akinyi na Mamaake walipanga kumuua mzee mmoja tajiri wa kizungu.
Mzee alikua kashajichokea kiasi anakunywa bia zake anajikojolea mpk afike ndani kwake apande ghorofa msala.
Sasa Akinyi kwanza kaondoka, mama nae sijui yuko wapi mjumba mkubwa kweli.
Niko na mzee garden tunachoma nyama ananisimulia maisha yake ujanani mpk hapo alipo.
Mara akaja kijana wake wa mke mkubwa.
Hakupita mlango wa mbele, karuka senyenge kazama ndani.
Namuuliza mzee huyu nani?
Akasema ni kijana wangu mkubwa huyu.
Tukasalimiana wakabishana sana na babaake.
Kumbe kijana anataka apewe mali za babaake walizochuma na mamaake.
Otherwise zitapotea kwa Akinyi na mamaake.
Hii story mzee kanisimulia mwenyewe.
Baada ya kuchoka.
Mzee kaomba nimshikilie aende akalale.
Aisee tumebebana mzee mwenyewe yuko tough na kashazitwanga.
Kumbe wale washenzi wanajua anapoangukaga mlangoni.
Likategwa li jambia kali haswa
Aisee mungu yupo jamani ningekua na kesi ya mauaji mpk sasa.
Tunaingia hapo mlangoni namkokota yule mzee tukapiga mweleka hapo km kawaida yake.
Lile bisu lilitegwa kiufundi sana mlangoni yaani akifungua mlango litachomoka nayeye aliangukie kwenye moyo kazi iishe.
Sasa hapo misheni ikashindikana
Nilimrescue yule mzee jambia huko,
Nikampeleka chumbani akalale zake.
Aisee ndio baadae Akinyi huyu hapa kaja na polisi kabisa🥲
Na mamaake katokea from no where.
Akinyi -babaangu kauliwa.
Polisi -nani unamuhisi?
Huyu hapa
Walikua wote mda mwingi huko garden.
Nikadakwa hapo ndani inteligensia zifuate.
Wananiuliza namimi nawauliza mzee gani kafa.?
Si huyu mwenye hili ghorofa.
Nikawaambia kafa sa ngapi??
Mi nimempeleka mpk ndani kwake juu kalala.
Khe Twende tukamuone, tukapanda juu mzee mzima kazimika tu.
Ikabidi pale kuulizwa ilikuwaje?
Kusimulia scenario yote ya jioni ile na mambo yaliyotokea,
Akinyi kageuza kibao kwamba niliwaita huyu km kaniibia hela,
Nikasachiwa sina senti na nawadai.
Ikabidi polisi waniombe sorry kwa usumbufu.
Nikaondoka.
Akinyi na mamaake ndani.
Lakini baadae wakatoka yule mzee alikua mzima.
Kumbe pale wanagombea urithi tu.
Mzee alikua tajiri sana huko Kenya.
Akinyi na mamaake ni wakenya
Yule kijana aliruka senyenge ni mzungu piwa.
Nilisoma baadae kwenye magazeti walimmaliza huyo mzee wakadakwa.
Kwa hasira huyo Akinyi akajichanganya siku moja party nje huko sio kwao nikamtengeneza vizuri tu kulipia uongo wake ule.
Hii imenitokea mwenyewe zamani huko
Sorry UMUGHAKA nimepandisha story kwenye uzi wako
So Akinyi wako ndo uyo uyo wa UMUGHAKA au majina tu yameingiliana.
 
Back
Top Bottom