Ajali mbaya yaua Ubungo njia panda

Ajali mbaya yaua Ubungo njia panda

dereva mzuri anatakiwa kujua kua kuna watumiaji wengine wa barabara na wanaweza fanya makosa yatayo sababisha ajari. hivyo ni wajibu wa kila dereva kujilinda yeye na watumiaji wengine wa barabara hata kama wao ndio wenye makosa. dereva makini huwezi gonga tu wengine eti kwakua wao ndio wanamakosa. ukifanya hivyo basi ujue haufai kuendesha chombo cha moto.
 
Nimeishuhudia kwa mbali kidogo. Barabara zetu hazitoi mwanya wa kukusanya umbea na picha. Ukicheza unasababidha ajali nyingine. Swali nililojiuliza kwa haraka. Je mwendo kasi hayana break?! Na Je bajaji hakujua matumizi sahihi ya barabara hizo au tatizo pesa mbele mauti nyuma?
Ujue hawa bajaji na boda washazoea kuchomekea daladala na magari madodo, sasa wanafkiri haya makubwa ni kama hayo waliyoyazoea, haya makubwa wakati mwingine dereva hakuoni kwa urahisi,
Kama ushawahi kuendesha gari hapa mjini ukakutana na kadhia ya madereva bajaji na boda wala hushangai kuskia wamepata ajali.
 
Madereva bajaj wengi wana kiherehere sana.. utafikiri wanaendesha boda boda.. wanachomekea sana, na hawaoni ni hatari... unaweza kuona taa nyekundu.. ila bajaj au bodaboda akaibia akapita chaaaaaaap... kama mshale vile... hawajui ni hatari sana... naamini hapa dereva bajaj atakuwa kachomekea labda..!!
 
RIP marehem Dereva
Ila kifo chao ni Mawaidha tosha kwa Drivers wa Bajaji na wenye kuuibia njia kama wewe.
 
Kilichoniuma mnooo ni kwamba ndio bajaji yaweza ikawa ana makosa ila kibinadam kumburuta mtu vile lami na kumchuna ukicheck umetoka njia panda na brake unazo kwann usipunguze tu mwendo. Daah, sio poa kabsa.
Bajaji na pikipiki wanazingua sana,kwanza unaujua urefu wa hizo meter alizotaja mleta mada,hizo meter kwa basi kama hilo ni ndogo sana ulitaka afunge breki awamwage abiria wake?
 
Tatizo hawa boda muda wote wao wana HARAKA wanataka kuwahi wanakoenda. Mwingine anakuovateki vibaya afu unamkuta mita chache hapo mbele kapaki hana hata chembe ya wasiwasi. Kiukweli kwa saivi kama kuna watu wanaoendesha kwa wasiwasi barabarani ni waendesha magari kwa sababu ya vurugu ya boda, yaani hujui atatokea upande gani kushoto au kulia wanachomoka tu. Saivi naangalia taarifa hapa inasema boda watano hufa kila siku nchini.

Tafadhali wanaboda mjionee huruma.

R.I.P
 
Kuna ajali mbaya imetokea Ubungo njia panda, basi la mwendo kasi na bajaji kugongana na kisha bajaji kuburutwa na basi hlo umbali wa kama meter 60.

Bajaji imeharibika haifai na dereva kaburutwa kachunika vibaya mno na kukata roho hapo hapo huku damu zikitapakaa barabarani.

Kumetokea hali ya taharuki kubwa baada ya wananchi wenye hasira kali kutaka kuleta fujo wakidai dereva huyo wa mwendo kasi alikua amekusudia.

Angalizo: Tuwe makini sana katika junction hizi za barabara tuwapo kwenye vyombo vya moto.


Chanzo: Nimepita eneo la tukio

Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa. Roho ya marehemu ipumzike palipo pema. Amen
Ukigongwa kwenye barabara ya mwendo kasi kama sio kwenye zebra zake wewe ndo una kosa, anyway, mola ailaze mahali pema roho ya marehemu.
 
Tujifunze kuheshimu alama za barabarani,hatuwezi kumhukumu marehemu lkn nasisitiza makosa achukiwe sheria ,kama ni huyo aliyetangulia mbele za haki hiyo tumwachie Mungu.
 
Bus lilikuwa speed gani? Asije akakwepa bajaj akapindua bus.
 
Kilichoniuma mnooo ni kwamba ndio bajaji yaweza ikawa ana makosa ila kibinadam kumburuta mtu vile lami na kumchuna ukicheck umetoka njia panda na brake unazo kwann usipunguze tu mwendo. Daah, sio poa kabsa.
Hawa wenye bajaji na pikipiki ni careless sana. Mdogo wangu akiwa ndani ya basi la mwendo kasi alivunjika kidole kwa kuwa dereva wa basi alifunga brake ya ghafla ili kuepuka kumgonga mwenyewe bodaboda alieingia barabara ya lile basi bila umakini. As a result mdogo wangu kutokana na kule kuyumbishwa ndani ya basi kidole chake cha mkono wa kulia kikapata fracture ambayo ilibidi afanyiwe upasuaji. Hawa wanajifanya vichaa, wakifa sana akili zitawarudi wale ambao watasalimika
 
Seem ingine hatari ni njiapanda sheklango. Taa za kuruhusu gar kutoka manzes kwenda sinza zinawaka muda mfupi sana wkt seemu yenyewe ina watumiaj weng hasa hao boda/bajaj.
 
Nimeishuhudia kwa mbali kidogo. Barabara zetu hazitoi mwanya wa kukusanya umbea na picha. Ukicheza unasababidha ajali nyingine. Swali nililojiuliza kwa haraka. Je mwendo kasi hayana break?! Na Je bajaji hakujua matumizi sahihi ya barabara hizo au tatizo pesa mbele mauti nyuma?
Pesa kwanza mauti bahati mbaya
 
Back
Top Bottom