Ajali mbaya yaua Ubungo njia panda

Ajali mbaya yaua Ubungo njia panda

Senior Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2011
Posts
3,405
Reaction score
3,702
Kuna ajali mbaya imetokea Ubungo njia panda, basi la mwendo kasi na bajaji kugongana na kisha bajaji kuburutwa na basi hlo umbali wa kama meter 60.

Bajaji imeharibika haifai na dereva kaburutwa kachunika vibaya mno na kukata roho hapo hapo huku damu zikitapakaa barabarani.

Kumetokea hali ya taharuki kubwa baada ya wananchi wenye hasira kali kutaka kuleta fujo wakidai dereva huyo wa mwendo kasi alikua amekusudia.

Angalizo: Tuwe makini sana katika junction hizi za barabara tuwapo kwenye vyombo vya moto.

Chanzo: Nimepita eneo la tukio

Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa. Roho ya marehemu ipumzike palipo pema. Amen
 
RIP dereva wa bajaj......

Mleta mada hiyo junction ni ya palr baada ya kituo cha rombo?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ingependeza kama ungeweka na picha kabisa ili watu waone....pia tujaribu kuwa makini na haya magari ya mwendokasi maana wao wanacheza na alama za barabarani na ni mara chache sana kukuta wamemgonga mtu kwa bahati mbaya.......R.I.P
 
AISEE,,kama nikweli, Huyo dereva hana ubinadamu hata kidogo,,hata km mwenye Bajaj alikuwa na makosa,,,sasa amepata faida gani kamuua Mtanzania mwenzie sababu yakujiona tu yupo juu kwakuendesha ilo jeneza,,,Mungu amlaze mahala pema marehemu,
 
Ingependeza kama ungeweka na picha kabisa ili watu waone....pia tujaribu kuwa makini na haya magari ya mwendokasi maana wao wanacheza na alama za barabarani na ni mara chache sana kukuta wamemgonga mtu kwa bahati mbaya.......R.I.P
wewe picha ya nini? unasema kabisa ingependeza sana ingekuwepo picha
 
Kuna ajali mbaya imetokea Ubungo njia panda, basi la mwendo kasi na bajaji kugongana na kisha bajaji kuburutwa na basi hlo umbali wa kama meter 60.

Bajaji imeharibika haifai na dereva kaburutwa kachunika vibaya mno na kukata roho hapo hapo huku damu zikitapakaa barabarani.

Kumetokea hali ya taharuki kubwa baada ya wananchi wenye hasira kali kutaka kuleta fujo wakidai dereva huyo wa mwendo kasi alikua amekusudia.

Angalizo: Tuwe makini sana katika junction hizi za barabara tuwapo kwenye vyombo vya moto.


Chanzo: Nimepita eneo la tukio

Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa. Roho ya marehemu ipumzike palipo pema. Amen
oh unakuta familia yake inasubiri baba arudi nyumbani alete kitoweo bila kufahamu mwenyewe kashatoweka hapa duniani rest in peace nieumia sana.....
 
Ingependeza kama ungeweka na picha kabisa ili watu waone....pia tujaribu kuwa makini na haya magari ya mwendokasi maana wao wanacheza na alama za barabarani na ni mara chache sana kukuta wamemgonga mtu kwa bahati mbaya.......R.I.P
Katika ufwatiliaji wangu...madereva wa mwendokasi wanafwatisha sana alama za barabarani....hata sehemu ya kivuko.....kama kuna watu lazma asimame awapishe wavuke.....tatizo la bajaj na pikipiki uwa wanakurupuka kila mahali........
 
oh unakuta familia yake inasubiri baba arudi nyumbani alete kitowep nila kufahamu mwenyewe kashatoweka hapa duniani rest in peace nieumia sana
Ndiyo hvyo.....haijulikani siku wala saa......
 
  • Thanks
Reactions: BAK
oh unakuta familia yake inasubiri baba arudi nyumbani alete kitowep nila kufahamu mwenyewe kashatoweka hapa duniani rest in peace nieumia sana
Kilichoniuma mnooo ni kwamba ndio bajaji yaweza ikawa ana makosa ila kibinadam kumburuta mtu vile lami na kumchuna ukicheck umetoka njia panda na brake unazo kwann usipunguze tu mwendo. Daah, sio poa kabsa.
 
Nimeishuhudia kwa mbali kidogo. Barabara zetu hazitoi mwanya wa kukusanya umbea na picha. Ukicheza unasababidha ajali nyingine. Swali nililojiuliza kwa haraka. Je mwendo kasi hayana break?! Na Je bajaji hakujua matumizi sahihi ya barabara hizo au tatizo pesa mbele mauti nyuma?
 
Katika ufwatiliaji wangu...madereva wa mwendokasi wanafwatisha sana alama za barabarani....hata sehemu ya kivuko.....kama kuna watu lazma asimame awapishe wavuke.....tatizo la bajaj na pikipiki uwa wanakurupuka kila mahali........
Kweli unachosema...hawa jamaa wapo makini sana na wanjali alama za barabarani kuliko kawaida..hapo kwenye hyo ajali lazima kuna namna..
 
Katika ufwatiliaji wangu...madereva wa mwendokasi wanafwatisha sana alama za barabarani....hata sehemu ya kivuko.....kama kuna watu lazma asimame awapishe wavuke.....tatizo la bajaj na pikipiki uwa wanakurupuka kila mahali........

kaka kwa ufuatiliaji wako ikiwaka taa ya kijani kama dereva unatakiwa ufanyenye?
 
Back
Top Bottom