Afrika ilishaachwa na Mungu tangu kitambo

Afrika ilishaachwa na Mungu tangu kitambo

Kwa kuwa hako kakitabu hakatabadili uhalisia wa mambo, jiandikieni tu, lakini msisahau kujiandaa.
 
Mswaada wakuanzisha

Nimebaini waafrika
tunaamini kisichochetu,
tumemetelekeza
kuendeleza imani yetu na
Mungu wetu na badala
yake tunamwabudu
Mungu wamasimulizi ya
Ukalidayo nakuamini dini
za kuletwa kwa majahazi,
Hivyo kwaheshima ya Dini
yakale ya Kiafrika na
Mungu wetu
, nimeaamua
kuanzisha Mchakato wa
uandikaji wa Biblia ya
Dini ya Kiafrika na
Uundwaji na usimikwaji
wa MUNGU wa Afrika.
Bibilia hii itaundwa kwa
vitabu vikuu VITANO,
ambavyo itakuwa ni
mkusanyo wa vitabu
vifuatavyo, Afrika ya
Mashariki, Afrika
Magharibi, Afrika
Kaskazini, Afrika ya Kati,
Afrika Kusini.
Mitume tutakaowafuata
maono yao ni pamoja na
Chifu Mkwawa, Kitabu
A.Msh Tagk, Chifu
Monziyno, Kitabu A.Magh
Nigr. Nk.
Pia wataalamu na
waamuzi mbali
watakuwemo kama vile
Ng'wanamalundi,
Umuvuginza, nk.
Ninakaribisha maoni ya
Uandikaji wa biblia hii.

Kitaitwa kitabu cha uafrika,

Tayari mchakato unaendelea, nakaribisha maoni ya wadau

Angalia humo kwenye red. Sijui kama unajua haswa unachokiandika!
Tunaandika tunachokifikiria, nadhani umekosea kuanzia kwenye KUFIKIRIA ndio mana makosa yanajitokeza kwenye uandishi pia. Hebu FIKIRIA UPYA.
Unachokikataa ndicho hicho hicho unachokikubali.

Unakataa dini zilizoletwa kwa majahazi lakini unafuata MFUMO na MTINDO wa dini hizo hizo katika kuandika hicho uanachotaka kuandika.

Mtindo(style) unaotaka kutumia umetumika katika biblia ya dini ya kikristo ambayo kwa mtazamo wako IMELETWA na wageni. Huoni unataka kutunywesha mvinyo wa zamani katika chupa mpya?

Hapo kwenye blue: hebu tueleze dini ya kiafrika ikoje? Na huyo "Mungu wetu" kwa mtazamo wa kiafrika yukoje? Je kwa mujibu wa hiyo dini ya kiafrika ambayo kwa tafsiri mbinuko(mafhuum mukhalafa) ya maandiashi yako ni kuwa ilikuwepo huko nyuma, je dini hiyo ilikuwa na vitabu huko zamani? Au suala la vitabu unataka kuitia hiyo dini yako ya kiafrika "uchekibobu"(usasa) ili iendane na dini "zilizoletwa" kwa majahazi?
Cc: ukhty FaizaFoxy, kahtaan, Mkoroshokigoli
 
Yericko Njaa inakupeleka pabaya kijana.
Umefilisika mawazo ya miundo mbinu mpk unafikiria kuwaiga kina babu wa loliondo.

Wenzako waliwahi, we unakuja kushtuka 2015! ?
Mi nakushauri uanze na Kioski cha sigara kwanza halafu tafuta na Fundi viatu kaa nae hapo. Hutokosa hela ya kula.
Mtaji ekfu 50 inatosha. Na km huna njoo nikusaidie usije athirika kwenye ubongo kabla ya saa.
 
I concur. Nyerere sometimes una kosha sometimes unazingua.

Hii idea ni njema sana sema uandishi huo utahitaji mchakato mrefu sana.
Hili jambo kuna wale wengi waoga watumwa wajinga wasiotaka kufikiri vizuri sababu wanaogopa moto na vitisho vingine watakuona punguani.

Waafrika tutaburuzwa sana na hii miungu feki. Ila ipo siku itakuja, vilembwe wa vilembwekeze wetu watakapokuja kushtukia danganya toto hii, ndio africa will emerge again.
 
Hivi huyu #Yeriko nyerere ameshalipa zile fedha alizotapeli kwa yule kijana aliyeshinda uandishi bora wa kiswahili kwenye mtandao wa twiter?
 
Dini za mababu zetu zilienda wapi? Nani aliziua? Kwasababu gani? Mbona walikuwa wanaabudu miaka nenda miaka rudi? Na walichoomba walifanikiwa?

Siamini kama dini zilizoletwa na wazungu ni sahihi kwa bara letu. Inabidi turudi kwenye dini za mababu zetu.
 
Umsahau na MWANAMALUNDI mtenda miujiza mkuu wa usukumani, huyu umpe unabii.
 
I concur. Nyerere sometimes una kosha sometimes unazingua.

Hii idea ni njema sana sema uandishi huo utahitaji mchakato mrefu sana.
Hili jambo kuna wale wengi waoga watumwa wajinga wasiotaka kufikiri vizuri sababu wanaogopa moto na vitisho vingine watakuona punguani.

Waafrika tutaburuzwa sana na hii miungu feki. Ila ipo siku itakuja, vilembwe wa vilembwekeze wetu watakapokuja kushtukia danganya toto hii, ndio africa will emerge again.

Wewe ndio umeandika point kati ya wachangiaji wote mkuu! Hebu tujiulize karne ya 15 kurudi nyuma waafrika tulikuwa tynaabudu nini? Bila shaka tulikuwa na MUNGU wetu. Ona sasa tumemdharau tukadandia miungu ya kuletwa ya waarabu na wazungu na ndio hii inatuangamiza.😡
 
Hii miungu ya wazungu na waarabu itatutesa sana. Jiulizeni kabla ya kuletwa hii miungu waafrika tulukuwa tunaabudu nini?
 
Kabla ya kuanza kuafikiria namshauri aanze na kujielimisha kwanza kutoka kwa wanaozifuata hizo imani.
Ajue maana ya imani, Mungu, kwanini imani, baada ya hapo atajua kwa nini yeye aandike na kwa vipi aandike.

Je Yeriko nadhani unajua vitabu hivi huandikwa ndani ya imani na sio kwa ajili ya watu baki kusoma.

Msukumo wa kuwa na kitabu unatokana imani kubwa ya mwandishi kuhusu anachoandika na uwezo anaousikia unampa nguvu ya tofauti sana. Sio elimu ya mambo mbalimbali.
Ndio sababu kwa hao wa majahazi hivi vitabu vinaitwa vitakatifu au vitukufu.

Kuna maandishi yameandikwa mengi tu kuhusu imani tofauti za kiafrika ni mambo mazito naomba utafute usome.
 
Wewe ndio umeandika point kati ya wachangiaji wote mkuu! Hebu tujiulize karne ya 15 kurudi nyuma waafrika tulikuwa tynaabudu nini? Bila shaka tulikuwa na MUNGU wetu. Ona sasa tumemdharau tukadandia miungu ya kuletwa ya waarabu na wazungu na ndio hii inatuangamiza.😡

I concur. Nyerere sometimes una kosha sometimes unazingua.

Hii idea ni njema sana sema uandishi huo utahitaji mchakato mrefu sana.
Hili jambo kuna wale wengi waoga watumwa wajinga wasiotaka kufikiri vizuri sababu wanaogopa moto na vitisho vingine watakuona punguani.

Waafrika tutaburuzwa sana na hii miungu feki. Ila ipo siku itakuja, vilembwe wa vilembwekeze wetu watakapokuja kushtukia danganya toto hii, ndio africa will emerge again.

Hebu someni post #10 halafu tusaidieni majibu juu ya hoja mnayoiunga mkono
 
Wanaompenda Yesu bila kumwona live wako wengi ingawa wanamwona kwenye runinga wakati mwingine akiwa na sura tofauti kumbe ni yule mzungu aliyeigiza matendo ya Yesu. Wanashangilia kama mazuzu lakini huyu jamaa anataka waafrica tuwe na Mungu wetu watu wanamwona chizi!!!! Mbona ninyi hatuwaoni machizi kwa kumwamini yule mzungu mkiamini ndiye Yesu kumbe siye?
 
Ni heri mimi na Wakristo wenzangu tuonekane machizi au Mazuzu kwa Kumshangilia Yesu Kristu Mungu Wetu na Mwokozi wetu kuliko Kuonekana mjanja kwa ku-support Imani Zisizokuwa na Kichwa wala miguu wala Kiwiliwili.

Yesu yule mzungu tunayemwona kwenye mabango mbalimbali ndiye huyo Mungu wenu?
 
Daah,,ukianza kuandika usinisahau na mim
Maana Babu yangu alikuaga Mtemi,alinirithisha vitu vyake vyote!👣
 
Back
Top Bottom