Afisa TRA - mtoto wa miaka 2 kumiliki ghorofa

Afisa TRA - mtoto wa miaka 2 kumiliki ghorofa

matunge88

Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
58
Reaction score
26
Kutoka kwenye kipindi cha clouds fm live - PB na Gerald Hando. MWENYEKITI WA WAFANYA BIASHARA AWACHANA MAAFISA WA TRA. Anasema anaushahidi mtoto wa afisa wa TRA miaka 2 anamiliki ghorofa. Je Kama ni kweli hao maafisa wanapata hela zao kihalali, na amesema anaushahidi mfanyabiashara mmoja hulipa mil 60 kama kodi lakini hupewa risiti ya mil5.
Je Tanzania tutafika. Takukuru tusaidieni.

TANZANIA YA MWAGA MBOGA MIMI NAMWAGA UGALI

Source: CLOUDS FM POWER BREAKFAST NA GERALD HANDO
 
Mbona yako wazi makusanyo kila siku hayaonekani maofisini, ukilipa airport mil20 kwenye risit zinaandikwa mil2.

Na hii ndio inalazimisha serikal ione njia bora ni kuongeza kodi, lkn tofauti hata kodi ya bandar ya dar tuu pekee yake kama itakusanywa kihalali inatosha kuongoza nchi.
 
Huu mgomo utafichua mengi ; wajue tu hakuna anayetoa rushwa mwenye siri sababu hakuna apendaye kutoa pesa "bure" at sababu tu wewe uko nyuma ya dawati!!!!!
 
Kuna makubwa yanakuja nyie subirini!mfumo wa ulipaji kodi tanzania unasikitisha!
 
Kazi ipo. Hii tanzania na jamaa amewachana kweli. Nimemsikia. Amesema mambo mengi sana. Ikiwemo ya maafisa hao wa TRA kumiliki ukwasi kutoka kwenye kodi za hao business man. Yawezekana hata PAYE wanazikamua
 
Hivi tuna taasisis za kufuatilia haya mambo au nao wamezibwa mdomo. Kweli Tz inahitaji PAUL KAGAME
 
Haya sasa wameanza kutajana, Afisa wa TRA "anasaidia" MFANYABIASHARA kukwepa kodi kwa ujira fulani, kwa hiyo tatizo ni kwa wafanyabiashara wenyewe wanaokwepa hizo kodi na kutoa rushwa, kwa nini usilipe kodi by the book ili huyo afisaa asiguse senti yako?!!!..Lakini hata hivyo serikali imesikia kilio chenu wajasiriamali, NUNUENI MASHINE muepukane na usumbufu huo wote, kila siku unakagua mwenyewe unajua serikali inakudai kiasi gani, hakuna rushwa hakuna longolongo hakuna kukadiriana!
 
na bado ndo maana ukitaka kuoa unaulizwa unafanya kazi TRA au? ukisema hapana atakuuliza sasa wapi mbona hueleweki asee.....dah na wawaumbue tuu tumechoka.
 
Hivi tuna taasisis za kufuatilia haya mambo au nao wamezibwa mdomo. Kweli Tz inahitaji PAUL KAGAME

hatumwitaji Kagame hata kidogo kwani yeye ni Yesu??tunahitaji self committed toka kwa mtu mmoja mmoja tuache siasa tufanye kazi
 
akatoe taarifa TRA. issue ni wao kulipa kodi na kutumia mashine. Ukikamatwa na gongo huwezi sema wapo wengi. kwa wakati huo wewe ndio umekamatwa!
 
Mtoto wa miaka 2 atafanya vipi kazi tra? Hen rekebisha Uzi wako
Maana yake maofisa wa TRA wanajenga na kununua majumba kwa majina ya watoto/ndugu zao ili siku ya siku wasikamatwe
 
Back
Top Bottom