ACT Wazalendo wapendekeza Bima ya Afya ifungamanishwe na PSSSF na NSSF

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
1681127889720.jpeg

Hatua hiyo inafuatia Ukaguzi uliofanywa na CAG kubaini hasara ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), imeongezeka kutoka Tsh. Bilioni 104 mwaka 2020/21 hadi kufikia Tsh. Bilioni 205 mwaka 2021/22.

ACT imependekeza Mifuko hiyo ya Hifadhi ya Jamii iwe na Fao la Matibabu ambapo 20% ya Michango ya wanachama itawasilishwa #NHIF kila mwezi na makusanyo yake yatakuwa Tsh. Bilioni 530 kwa mwaka.

Uchunguzi wa CAG kwa mwaka 2021/22 umebaini Kadi za Bima ya Afya 21,042 zilitumika kupata huduma za Afya za Tsh. Bilioni 1.78 bila kuchangia chochote. Pia, Wategemezi 104,729 wasio na sifa walisababisha ongezeko la madai ya Tsh. Bilioni 15.17.

=========

Katika ripoti yake ya ukaguzi CAG amebaini hoja zifuatazo kuhusu Mfuko wa NHIF;

i.Wafanyakazi wa NHIF kujikopesha bila utaratibu na kushindwa kurejesha fedha za wanachama Matumizi mabovu ya fedha michango bilioni 41.42 kama mikopo isiyorejeshwa kwa watumishi wa NHIF ambapo alibaini kuwa wafanyakazi wa NHIF wamelimbikiza deni la shiingi bilioni 41.42 ambazo wamekuwa wakikopeshana.

Mfuko wa NHIF unatumia fedha za uendeshaji kufadhili mikopo ya wafanyakazi kinyume na Sera ya Mikopo kwa wafanyakazi ya NHIF uliopaswa kuwa na mfuko wa kuzungusha fedha.

ii. Malipo hewa

Vituo binafsi vya huduma za afya vinaongoza kwa kulipwa na NHIF madai yasiyo ya kweli ambapo CAG amebaini kuwa jumla ya shilingi bilioni 14.5 zililipwa kwa madai ya uongo na kugushi. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 10.38 (72%) zililipwa kwa vituo binafsi, vituo vya mashirika ya dini ilikuwa ni biliioni 2.49 (17%) na vituo vya Serikali ilikuwa bilioni 1.57(11%).

iii. Wanufaika wasiochangia

Uwepo wa wanuafaika wa huduma ambao hawachangii chochote ambapo CAG ameabaiini uwepo wa kadi hai 21,042 za NHIF ambazo zilitumika kupokea huduma mbalimbali za afya zenye thamani yashilingi bilioni 1.78 ingawa wachangiaji wao hawakutoa mchango wowote.

iv.Wategemezi waliokosa sifa

Wategemezi wa Zaidi ya Umri wa miaka 18 watumia shilingi bilioni 15.2 ambapo CAG amebaini uwepo wa wategemezi 104,729 wenye umri Zaidi ya miaka 18 ambao walinuafaika na huduma mbalimbali za afya ambazo madai yake yalifikia shilingi 15.17 bilioni.

Mfuko wa NHIF unakufa kwa sababu ya hoja zilizoainishwa hapo juu na vile vile Mfumo wetu wa Bima ya Afya sio endelevu na lazima ungekufa tu. Jitihda zote za Serikali kuokoa NHIF zimejikita kwenye ama kuongeza wachangiaji au kupunguza mafao na huduma kwa wanachama. Zimekuwa ni juhudi za kuokoa Mfuko badala ya kuokoa Mfumo wa huduma za Afya Nchini.

ACT Wazalendo inapendekeza kufanya mabadiliko makubwa ya mfumo mzima wa Bima ya Afya nchini kwa kufungamanisha Bima ya Afya na Hifadhi ya Jamii. Tunapendekeza; Moja, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (NSSF na PSSSF) iwe na Fao la Matibabu ambapo kila mwanachama wa Mifuko hiyo awe moja kwa moja mwanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (ulioboresha).

20% ya Michango ya Wanachama wa Mifuko hii itawasilishwa NHIF kila mwezi kwa ajili ya kugharamia Fao la Matibabu. Kwa Pendekezo hili NHIF itapata wanachama wapya milioni 1.9 waliopo kwenye mifuko kutoka sekta rasmi na makusanyo ya takribani shilingi bilioni 530 kwa mwaka.

Pili, Serikali itoe kivutio kwa watu waliopo sekta isiyorasmi kama vile wafanyabiashara wadogo, wavuvi, wakulima, wafugaji, mamalishe nk kujiunga na Skimu ya Hifadhi ya Jamii kwa kuwachangia theluthi ya mchango wa kila Mwezi yaani shilingi 10,000 (Matching Scheme). Moja ya chanzo cha fedha cha kivutio hiki ni 10% ya mapato ya ndani ya Halmashauri kama ilivyopendekezwa hapo juu. Kwa Pendekezo hili takribani watu milioni 7.4 watakuwa wanachama wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na hivyo hivyo wanachama wa NHIF na makusanyo ya USD 266M
kwa kugharamia Matibabu.

Tatu, Serikali iwalipie asilimia 100 wafaidika wa TASAF kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii na hivyo kuwa wanachama wa NHIF. Pendekezo hili takribani watu milioni 6.3 watapata Fao la Matibabu na makusanyo ya USD 205M kwa Mfuko.

Nne, ili kutekeleza mapendekezo yote hapo juu Serikali itenge kwenye bajeti ya kila mwaka asilimia 2.5 ya Pato la Taifa kwa ajili ya kugharamia matibabu na hivyo kuwezesha Watu wazima Milioni 11 kuwa na Bima ya Afya pamoja na wategemezi wao. Kwa mfumo huu Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya hautakufa na ndoto ya Bima ya Afya kwa wote itafikiwa.

Tano, kutokana na Hali ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ilivyo kufuatia hoja za ukaguzi zilizobainishwa na CAG, tunapendekeza kuwa Bodi na Menejimenti yote ibadilishwe, Muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote uandikwe upya kuzingatia mapendekezo yetu hapo juu na sheria mpya ya NHIF itungwe ili kuimarisha mifumo ya huduma za Afya nchini.

ACT WAZALENDO
 

Attachments

  • Muhtasari Uchambuzi Ripoti CAG 2021_2022.pdf
    403.7 KB · Views: 2
Unajua Zitto amekaa kwenye Siasa za hii serikali kwa Muda Mrefu lakini kwenye haya mapendekezo kaingia kichwa kichwa sana Njaa sasa inamsumbua huyu jamaa.

Sasa NHIF na PSSF haya ni mashurika mawili tofauti, huwezi kuunganisha nhif ambayo inatibu watu au inatoa huduma kulingana na mahitaji, uunganishe na pssf ambao kazi yao ni kuhifadhi pesa za wafanyajazi ambao wanasubiria mtu astaafu ndio watoe pesa akiwa na miaka 65+

Ni suala ka kutumia akili tu katika kutoa hoja otherwise atufafanulie ana maana gani katika kusema mashirika yaunganishwe.
 
Unajua Zitto amekaa kwenye Siasa za hii serikali kwa Muda Mrefu lakini kwenye haya mapendekezo kaingia kichwa kichwa sana Njaa sasa inamsumbua huyu jamaa.

Sasa NHIF na PSSF haya ni mashurika mawili tofauti, huwezi kuunganisha nhif ambayo inatibu watu au inatoa huduma kulingana na mahitaji, uunganishe na pssf ambao kazi yao ni kuhifadhi pesa za wafanyajazi ambao wanasubiria mtu astaafu ndio watoe pesa akiwa na miaka 65+

Ni suala ka kutumia akili tu katika kutoa hoja otherwise atufafanulie ana maana gani katika kusema mashirika yaunganishwe.
 
Hatua stahiki zishachukuliwa sioni umuhimu wa kubadilisha menejimenti, Tungefocus na kuonyesha mazuri ya huu mfuko kwa namna unavyotusaidia sisi Wenye vipato duni ingependeza zaidi. Wanachama pia tuache kuuhujumu huu mfuko binafsi nimeshuhudia baadhi ya wanachama wasio waaminifu kugawa kadi zao na kutumiwa pia na watu wengine wasio wanachama, hii inawaletea hasara kubwa NHIF
 
Watanzania tujifunze kusoma ripoti nzima na kuelewa maana yake, hii mikopo iliyoelezewa hapa ni mikopo kama ilivyo mikopo mingine na hapo hakuna fedha ambayo imeropotiwa kupotea, tujifunze kuelewa na sio kuishambulia NHIF na kusahau mazuri yote yanayofanywa na Mfuko.

Kuna maelfu ya Watanzania wako Hospitalini muda huu na wanachotegemea ni NHIF, wapo ambao gharama zao kwa wiki ni zaidi ya Milioni moja na hizo gharama ni kwa maisha yao unadhani bila NHIF inawezekana? Tuache kuzua taharuki kwenye huu Mfuko unayo mazuri mengi unafanya.

Hii ripoti tuisomage kwa ujumla wake. Mbona inaonesha kabisa kwamba Mfuko unachukua hatua kwa vituo vinavyowasilisha madai ya udanganyifu na tayari takriban Bil. 7 zimesharejeshwa kwa Mfuko kati ya takriban Bil. 14 za udanganyifu zilizolipwa. Aidha vituo 32 vimeshasitishiwa mkataba na kuripotiwa kwa mamlaka husika

Halafu ukisoma vizuri unaona kabisa CAG anasema kutokana na taarifa za uchunguzi zinazofanywa na NHIF ndio udanganyifu huu umebainika. Ina maana NHIF wenyewe wanapambana kubaini udanganyifu na kuchukua hatua ripoti za NHIF stahiki

Hizi Bilioni 14 ambazo CAG amezionesha hapa ni jitihada kubwa ya Mfuko ambayo imefanywa kubaini vituo ambavyo viliwasilisha madai yenye udanganyifu na mpaka sasa kati ya hizi 14 Bilioni tayari bilioni 7 zimesharejeshwa na Vituo hivyo na iliyobaki inaendelea kurejeshwa.

Tuielewe vizuri hii ripoti ya CAG na tuwapongeze NHIF kwa jitihada zao za kubaini haya ambayo hata CAG amekuta tayari hatua zimechukuliwa.

Kwanza kuna wanachama mnahujumu Mfuko halafu mnakimbilia hapa kushinikiza Uongozi uondolewe ili muendelee kuuibia, wapo watoa huduma ambao mnashirikiana na wachama kuhujumu Mfuko mbona hamsemi?

Mchango wa NHIF anaolipa mwanachama ni mdogo sana haulingani na huduma mnazopata hilo nalo kwani hamlioni

Halafu wewe Zitto acha uhuni wako wa upotoshaji huu Mfuko unasaidia Mamilioni ya Watanzania ambao hawana fedha za kujitibia kama wangeambiwa wajilipie hivyo chambua kisomi.

Mapungufu ya NHIF yaangaliwe kwa umakini kwani mengine yamesababishwa na kutoongezeka kwa michango, wizi wa vituo, wanachama kuuza kadi zao na kuwatibia watu wasiostahili, kwa mawazo yangu NHIF inastahili pongezi na sio haya
 
Kwa mfumo huu ambao zaidi ya Bima ymza Afya 21,042 zilitumika kupata huduma za Afya za Tsh. Bilioni 1.78 bila kuchangia chochote.

Na Wategemezi 104,729 wasio na sifa walisababisha ongezeko la madai ya Tsh. Bilioni 15.17 kwa nini mfuko usipate hasara?

Wakati mwingine inatakuwa tubaki kwenye uhalisia na tusiendeshwe kwa mihemko katika kuhoji, Wananchi wenyewe inaonekana tunauhujumu mfuko.
 
Back
Top Bottom