ACT - Wazalendo Wamnyooshea kidole Zitto!

ACT - Wazalendo Wamnyooshea kidole Zitto!

Act ni kachama kadoogo saana ambako kamejulikana sana baada ya zzk kuhamia kule....hili la kuweka picha ya zitto sambamba na wagombea ni ili kuwapa kiki wagombea wasio na majina na chama chenyew...that way watu wakiona picha ya zitto wanaona na picha ya mgombea wa chama ambacho zitto anakisimamia
 
tatizo la watz ambao ni wanasiasa vijana niwepesi kujaa viburi pale wapojulikana ,zito ni miongoni mwao amesahau kabisa katokawapi , mzee Lowasa kipindi akiwa kijana alikuwa akitii wazee walomlea ndo maana kakomaa vizuri kisiasa pamoja na changamoto alozipitia bado watz waliowengi wanaimani nae .Sasa kwa kile anachokifanya zito ndani ya act cjui kama miaka ishirini ijao wtz watakuwa na imani na mwanasiasa huyu .

Angekuwa ni mtiifu kweli asinngeingia kwenye black book la Nyerere....???
 
Wewe ni mbuzi wakizungu kweli chama kina wana chama 1,200,000 wanao lipa ada(hai) sasa kitakosaje kula 100,000?

Kawadanganye wajinga wenzako huko,act ipate wapi wanachama hao?wanachama act hawazidi 100000
 
Kura walizo pata kwenye uchaguzi wa wenyevimiti ni zaidi ya hizo. Nenda kwenye website yao utaipata idadi ya wana chama wao sio kila kitu ni ubishi wewe wapi?
 
Wajumbe wa kamati kuu ya ACT wazalendo wamnyooshea kidole zitto kwa kile wanacholalamika kuwa anatumia nafasi yake ya uongozi wa chama vibaya.

Moja ya mjumbe huyo (jina tunalihifadhi) amesema zitto ni mbinafsi, hashirikishi chama katika utendaji, akija na ajenda zake hataki zijadiliwe anazipitisha kama zilivyo.

Anasema ndani ya chama wengi tulipenda tusisimamishe mgombea urais kutokana na bajet yetu kuwa ndogo, tukapendekeza tuwekeze nguvu kwenye wabunge na madiwani sehem ambazo tunanguvu, lkn zitto aling'aka sana na kukataa katukatu kwa kisingizio cha kupata ruzuku katika chama kama tutamsimamisha mgombea urais.

Mpaka sasa hali ya kifedha ndani ya chama inaogopesha, fedha alizozihaidi zitto zitatoka hatuzioni, na mpaka sasa hatujajua hatma ya kampen za mgombea urais, alisema mjumbe huyo.
Katika kila hoja ya Uongozi ni muhimu sana wasomaji kuipima na kuzungumzia UHALISIA uliopo maana mwelekeo wa chama unatokana na agenda zake. Sasa huyu mwanachama ambaye alitaka chama kiweke nguvu kubwa kwa wabunge karibu 300 wangeweza vipi kufanya kazi hiyo ikiwa chama hakina fedha?

Je, sii akili kubwa kuwekeza kwa mtu mmoja ambaye anaweza kuwapa wabunge pasipo kugombea kuliko kuwekeza kwa wabunge 300 ikiwa hamna uwezo huo? Kama ACT ingelikuwa na fedha za kutosha na wakashindwa kuwekeza kwa wabunge wake hapo ningeelewa lakini fedha hawana Wataweza vipi kumudu wabunge 300?

Je, mnafikiri matumaini ya CCM na UKAWA sio Magufuli na Lowassa kwanza? kwa nini waweke nguvu kubwa kwa viongozi hao maana siasa zetu ni za popularity sio mwenye wabunge wengi ndiye ataingia Magogoni Ila kuna uwezekano wa mgombea Urais kupata nafasi za wabunge kutokana na ushindi wake..

Hata hivyo vyama vingine vimeweka wagombea Urais wao wakitegemea kupata nafasi za Ubunge kupitia njia hiyo kwa sababu kumpitisha mbunge mmoja katika vyama 20 ni vigumu kuliko kumpitisha mgombea Urais kati ya wagombea 5. Kama mwananchi mpiga kura hamtaki Magufuli wala Edo atamchagua nani?
 
Wangetumia fursa vizuri kwa kuweka mabango ya mgombea urais mikoa mbalimbali badala ya kuweka mabango yenye picha ya Mwami Zitto wakati hagombei urais. Ni very simple logic lakini ingewasaidia sana, Zitto anagombea Kigoma, mabango yenye picha yake yanafanya nini Dar na Morogoro ambako hakuna bango la Anna mgombea uraisi. Ukata wa kujitakia

Hapo umenena vema kuna mabango ya zitto yamebandikwd hapa mwanza utafikiri yeye ndio mgombea wakati ya mama hakuna. Anamabango mengi kuliko wagombea ubunge wake hapa mwanza.
 
Hapo umenena vema kuna mabango ya zitto yamebandikwd hapa mwanza utafikiri yeye ndio mgombea wakati ya mama hakuna. Anamabango mengi kuliko wagombea ubunge wake hapa mwanza.
Samahani hivi kweli wewe utamchagua mgombea kwa sababu ana mabango mengi mitaani? Hizi siasa zenu kwanza mnafanya makosa kabisa iwe CCM, UKAWA na hata ACT kwa sababu hakuna sababu ya mgombea Urais kuwekwa bango lake kila mtaa, yeye atajieleza zaidi ktk mikutano, vyombo vya habari iwe magazeti, radio ama TV akiuza sera za chama chake.

Mijimboni yanatakiwa mabango ya wagombea Udiwani na wabunge tu ambao kazi yao kubwa itakuwa kuwatembelea wananchi majumbani mwao na kuzungumza nao iwe kwa kupitia wanachama walojitolea ama yeye mwenyewe binafsi kutambua mahitaji na hali halisi ya wananchi katika jimbo lake..
 
Hahaha act wasaliti nao wamesalitiwa na ccm , ccm wamegoma kuwasapoti hahaha kweli muosha naye uoshwa.
 
pamoja na yote zzt kisiasa anaimulikia taa act, yule mama Anna mie ntampigia kura ,sababu siamini ktk ccm a and b
 
pamoja na yote zzt kisiasa anaimulikia taa act, yule mama Anna mie ntampigia kura ,sababu siamini ktk ccm a and b

Kura yako ni siri hapa unamwambia nani? Hujui kuwa act ni ccm b?
 
Back
Top Bottom