ACT-Tanzania: Challenges and Opportunities! (SEHEMU YA KWANZA)

ACT-Tanzania: Challenges and Opportunities! (SEHEMU YA KWANZA)

sasa ndugu yangu Bramo ,kwa kuwa mada iliyoko mbele yetu ni challenges na opportunities walizonazo Act-Tanzania, sasa sijaelewa vizuri kama hayo yote uliyozungumza hapo juu, ni challenges au ni opportunity.Ungefafanua kidogo ingependeza zaidi.
 
Last edited by a moderator:
betlehem

Kwa mtazamo wangu ACT-Tanzania hawakufanya utafiti wa nini wanatakiwa wafanye ili wapate mafanikio ya haraka wameendeleza makosa yale yale ya vyama vilivyotangulia.

Makosa ya ACT:

ACT imeingia kwa gia ya kupambana na vyama vyote badala ya kupambana na matatizo ya wananchi ref. Nyakarungu, kuanza kupambana navyo ni kukosa fulsa ya kuvuta wanachama wasio wana CCM.

Kwa mtazamo wa wengi ACT inaonekana imeji-associate sana na chama tawala kuliko vyama vya upinzani, inatia shaka chama cha upinzani kipigiwa upatu na viongozi waandamizi wa chama tawala akiwemo waziri mkuu bungeni.

Ukitaka kujua tabia ya mtu angalia marafiki zake, humu JF hata nje ya JF wakosoaji wa wapingaji wakubwa wa maendeleo ya upinzani ndio hao hao wamekuwa wapigadebe wakubwa wa ACT, memba kama abokaramo, badala ya kukiletea heshima chama anazidi kukichafua.

Ofisi na mazingira ya ofisi hayafai, nimejitahidi kufika eneo la ofisi za ACT zaidi ya mara tatu bila kuona uhai wowote wa kiofisi. Kwa vile mlikuwa mstari wa mbele kukosoa ofisi za Chadema nilifikiri ofisi yenu itakuwa angalau tofauti kabisa, hiyo ofisi ni sawa na kiosk cha gahawa tu.

Msitangaze mtaua vyama vingapi vya siasa au mmevuna viongozi wangapi wa Chadema tangazeni sera zetu kwa wananchi.
 
Last edited by a moderator:
Unanikumbusha makala za Dr Kitila zilizojibiwa kwa mfululiza na Dr Mwingine ikawa end of the story. Nikusaidie tena, hayo unayoyasema yangekuwa hivyo kama wananchama wenu mnawashusha kutoka Mbinguni. lakini kama mnategmea ccm na vyama vingine kupata wanachama wenu, mtakuwa na jipya gani? Samaki gani unamkunja angali mbichi? Bado hutatushawishi kisanii namna hii.
 
Vyama vyote vinavyofanya Vizuri kwa sasa ni Vilianzishwa Mwaka 1993/94 Baada ya kuanza kwa Vyama Vingine, Hakuna na haijawahi kutyokea chama kingine chochote kipya kilichoanzishwa baada ya hapo Kikafanya Vizuri.

Kila laheri kwa ACT hope watavunja hii record.
 
mkuu Feedback ,kwa uelewa wako,
1. Nyakarungu ni msemaji wa taasisi gani?
2.Lengo la chama cha siasa ni nini?
3.Unadhani falsafa na itikadi za Act-Tanzania zinafanana na za vyama vyote 20 vya kabla yake ispokuwa ccm?
4. Hivi inawezekana wa 22 kuwa wa kwanza bila kuwapita 21 wote wa kabla yake?
Hebu wakati fulani tutulize emotions!
 
Last edited by a moderator:
mkuu Feedback ,kwa uelewa wako,
1. Nyakarungu ni msemaji wa taasisi gani?
2.Lengo la chama cha siasa ni nini?
3.Unadhani falsafa na itikadi za Act-Tanzania zinafanana na za vyama vyote 20 vya kabla yake ispokuwa ccm?
4. Hivi inawezekana wa 22 kuwa wa kwanza bila kuwapita 21 wote wa kabla yake?
Hebu wakati fulani tutulize emotions!
Hiyo falsafa ya kuwapita wote kwanza ndiyo itakayowafanya mchoke kabla ya kufikia malengo yenu, it will take a century.
 
sasa ndugu yangu Bramo ,kwa kuwa mada iliyoko mbele yetu ni challenges na opportunities walizonazo Act-Tanzania, sasa sijaelewa vizuri kama hayo yote uliyozungumza hapo juu, ni challenges au ni opportunity.Ungefafanua kidogo ingependeza zaidi.

Betlehem ya uyahudi alikozaliwa mtoto,
Nadhani umemsoma feedback hapo juu. ACT umedai haina kashfa na makosa km vyama vingine. Kwani chama ndio kinakuwa na kahsfa au watu wanaokiongoza chama? Kwa mantiki hiyo ACT imezaliwa na dhambi ya asili. Yaani kimeridhi dhambi ya wazazi wake, mwigamba, Kitila, (sijui Zitto yumo au hayumo..). ACT tayari imeridhi dhambi ya usaliti kutoka kwa viongozi wake. Maana yake walioanzisha ACT hawakuianzisha kwa nia njema bali kwa hasira ya kufukuzwa kutoka chama kingine! Timing yenu imekuwa very bad.

kwa hiyo badala ya viongozi hawa wa ACT waingie moja kwa moja kwenyekuelezea sera zao inabidi kwanza wafanye kazi kuwa ya kujustify ujo wao kwenye siasa. Na justification hii inafanywa kwa kuisema vibaya chadema na kudai eti mmekeuja kupambana na vyama vyote. kwa sera hiyo tayari potential members yeyote anaanza kuhisi kuelemewa uzito wa kazi mliyonayo mbele yenu...kupambana na vyama vyote...! Kwa hivyo hakuna mtu mwenye akili timamu atajiunga nanyi kwa sera ya namna hii! haina mvuto kwa mwananchi yeyyote wa kawaida. Yaani maleengo yenu sio realistic na yemekaa kitoto kitoto na Kihasira hasira! Pia arrogance ya viongozi wenu waliofukuzwa chadema mmeihamishia kwenye chama. Yaani kujiona nyie ndio wenyewe na hakuna mwingine anayeweza zaidi yenu! Na hii ndio maana hasa ya kudai vyama vingine vyote vimeshindwa kuindoa CCM kwa hiyo nyie pekee ndio mtaweza kwa kuanza kupambana kwanza na vyama vya upinzani na baadaye CCM! Kweli mnaamini watanzania watawaamini kwa kauli km hizi?

Mnataka kutuambai kwamba kwamba faulo ambazo CM wamekuwa wakicheza ili kushinda chaguzi mbali mbali hamzijui? Mnawezaje kushinda uchaguzi ndani ya katiba ambayo bado inakipendelea chama tawala?

Kosa lingine kubwa ni kitendo cha nyie chama cha upinzani kushabikiwa sana na chama tawala na serikali yake! Mmemwahi ona wapi kitu ya namna hiyo duniani? Inasikitisha mmefeli kabla ya kuanza! Kwa sera zenu hizi ambazo sio realistic na retrossive dhani progressive sidhani km kuna msomi mwenye akili timamu atajiunga nanyi!
 
Unanikumbusha makala za Dr Kitila zilizojibiwa kwa mfululiza na Dr Mwingine ikawa end of the story. Nikusaidie tena, hayo unayoyasema yangekuwa hivyo kama wananchama wenu mnawashusha kutoka Mbinguni. lakini kama mnategmea ccm na vyama vingine kupata wanachama wenu, mtakuwa na jipya gani? Samaki gani unamkunja angali mbichi? Bado hutatushawishi kisanii namna hii.

upo kaka yangu! kwa hiyo hiyo unayosema nadhani ni challenge, sasa wewe unadhani changamoto hiyo inaweza kushughulikiwa je! au na wewe huna solution lakini solution inayotolewa nayo huitaki vilevile! kaazi kweli! ok! sawa tu lakini, kila mtu na kichwa chake!

"Bado hutatushawishi kisanii namna hii" Sasa ndugu yangu;
1. Kwanza sitawashawishi wewe na nani?
2.Sitawashawishi kwenye nini? maana mada iliyoko mbele yetu ni :Changamoto na fursa ambazo chama kipya cha ACT-Tanzania kinazo.Sasa unaposema sitawashawishi!(wewe na hao unaowasemea) maana yake ni kwamba hamkubali kwamba ACT-Tanzania inakabiliwa na changamoto na vile vile ina fursa!? au ambacho hamtashawishika nacho ni nini hasa!?

Hivi ndugu Mikael P Aweda ndio umefikia hatua hii? au pengine mimi tu ndio sijakuelewa!
 
Last edited by a moderator:
Nadhani umemsoma feedback hapo juu. ACT umedai haina kashfa na makosa km vyama vingine. Kwani chama ndio kinakuwa na kahsfa au watu wanaokiongoza chama?
Ahaa! ok! sawa.Kwa hiyo wewe unachotaka kutuambia ni kwamba hata CCM haina shida bali kuna watu wenye shida ndani ya CCM! sawa kabisa.Kwa kiwango kikubwa mimi nakubaliana nawe katika hii na ndio maana wakati mwingi nimekuwa nikisema kwamba tanzania tuna tatizo kubwa la watu kuliko tulivyo na tatizo la vyama vya siasa, na matatizo tunayoyaona kwenye vyama, si matatizo ya vyama bali ya watu ndani ya vyama hivyo kwa kuwa chama sio kitu "concrete" bali ni 'wazo'(kitu cha kufikirika tu kilichowekewa kanuni na sheria fulani).Sawa kabisa yaani wewe unaonekana unaelewa sana mambo.

Sasa basi; kama tunakubaliana kwamba tatizo ni watu na watu hao wenye matatizo wako kwenye jamii yetu cha kufanya ni nini basi maana hao watu wenye matatizo wataendelea kuwa na matatizo mpaka pale tu kutakapokuwa na mfumo wa kuwageuza kuwa watu wazuri au kuwathibiti vinginevyo hawawezi kubadilika wenyewe.Sasa basi tuna machaguo mawili, tuamue kutokuwajibika tuwaache watu hao wafanye walitakalo huku tukilalamika tu! au tuamue kuwajibika kwa kutafuta mfumo ama wa kuwarekebisha au kuwadhibiti na kudhibiti mfumo kuufanya uzalishe watu wazuri sasa.

Katika level hiyo; ndio sasa mimi nasema kwamba ACT-Tanzania kama taasisi ambayo bila shaka itakuwa na mifumo; kwa uchanga wake ina fursa ya kutengeneza mechanisms ambayo inaweza kuwabadili watu wenye matatizo kuwa watu wazuri au kuwathibiti kuliko ilivyo kwa vyama vingine ambavyo watu hao washajikita na kuweka mizizi.Kama wewe unakataa hoja yangu, basi ukubaliane na wale wanaodhani kwamba matatizo ya CCM na matatizo ya nchi hii yanaweza kutatuliwa ndani ya ccm yenyewe (kwa kuwa chenye matatizo si CCM bali watu).na kama utakuwa unakataa vyote halafu huna pendekezo mbadala! utakuwa ndio wale wale! Au vinginevyo useme kwa hoja yako hiyo ulikusudia kusema kwamba ACT-Tanzania haina fursa yeyote bali changamoto tu! hapo utaeleweka.

Hata hivyo dunia hii ni yetu na chaguo ni letu!ni hiari ya mtu kufanya lile linalomjia kichwani mwake hata kama halina mantiki maadam tu havunji sheria.

 
Hiyo falsafa ya kuwapita wote kwanza ndiyo itakayowafanya mchoke kabla ya kufikia malengo yenu, it will take a century.
Kuna kitu kinaitwa "Falsafa ya kuwapita wote kwanza!" kama ipo ni falsafa ya chama gani? yaani concept simple kabisa tu hujaelewa! au umeelewa na unafanya makusudi tu ili kusababisha utata usio wa lazima? Wakati fulani ni bora kujibu maswali unapoamua kujitosa katika mjadala badala ya kukimbilia conclusion zisizoeleweka. Nakuuliza tena:Hivi kama mtu kajiunga na mbio, wakati anajiunga na mbio, wenzake 20 walishaondoka kabla yake na yeye anataka akimbie hadi ahakikishe anakuwa mshindi wa kwanza (yaani anakuwa mbele kuliko wote), kwa akili ya kawaida tu, tunategemea kwamba anatakiwa afanyeje? na atakapokimbia akafika mbele (mwanzo) tutasema kafanya je? kwa nini tunajichanganya wenyewe na hali tunajua na tuna uhakika kabisa kwamba tunajichanganya? hivi unajua unavyoitumia akili yako na unavyojizoeza kuwa ndivyo unavyokuwa hivyo hivyo!
 
sasa ndugu yangu Bramo ,kwa kuwa mada iliyoko mbele yetu ni challenges na opportunities walizonazo Act-Tanzania, sasa sijaelewa vizuri kama hayo yote uliyozungumza hapo juu, ni challenges au ni opportunity.Ungefafanua kidogo ingependeza zaidi.

ACT opportunity pekee mliyo nayo ni kula pesa za CCM za malipo ya usaliti kabla hawaja stop hiyo misaada maana kazi ya usaliti imewashinda.
Thats the only opportunity you have...
Challenge kubwa mliyonayo ni jinsi ya kuendelea kuwa kwenye chama kama chambo ambapo wahusika wakuu wamekaa mbali na hawata wajoin Mpaka utimilifu wa dahali
 
Last edited by a moderator:
Vyama vyote vinavyofanya Vizuri kwa sasa ni Vilianzishwa Mwaka 1993/94 Baada ya kuanza kwa Vyama Vingine, Hakuna na haijawahi kutyokea chama kingine chochote kipya kilichoanzishwa baada ya hapo Kikafanya Vizuri.
.
Na ndio maana wale walioamua kujilazimisha kufikiri nje ya duara; wanasema lazima lipo tatizo na dawa ya tatizo ni kulitatua! sio kulalamika tu.Mfano; katika ripoti ya CAG, Anasema kuna vyama vinne ambavyo havina kabisa account za benk.Sasa ndio tuviunge mkono kwa tabia hiyo, etio tu kwa kuwa ni vyama vya upinzani? CAG anasema ripoti zilizowasilishwa kwake, hakuna iliyoandikwa kwa kufuata kanuni za kitaalam za kihasibu, sasa ndio tuunge mkono tu kwa kuwa eti chama husika hakiko madarakani? haya yote yanastahili kupingwa pamoja na kupinga kutokaguliwa kwa hesabu za CCM.Hilo ndilo linalotakiwa.

Sasa ushangae; hapa mjadala ni changamoto na fursa zinazokikabili chama kipya cha ACT-Tanzania lakini wachangiaji wengi wanachofanya ni kulalamikana kulaumu tu badala ya kuchangia mada iliyoko mbele yao! kwa staili hii ndio maana huwa hatutoboi!
 
ACT opportunity pekee mliyo nayo ni kula pesa za "CCM za malipo ya usaliti" kabla hawaja stop hiyo misaada maana kazi ya usaliti imewashinda.
Mkuu umeeleweka vizuri tu! asante kwa mchango wako ambao kimsingi utawaelimisha wengi.
 
Azam fc tangu kuanza kwake haijatimiza muongo hata mmija (miaka 10).
Yanga imetimiza miongo saba miaka(78)simba miaka karibia na hiyo.
Pima maendeleo ya azam dhidi ya timu za simba na yanga.
Mbeya city na uchanga wake ipo tatu bora.
 
Nashangaa kuona hata wewe unashiriki kupotosha ukweli kuhusu katiba lakini nyote mnaopindisha kuna siku ukweli utawaumbua.

Unakumbuka nani aliyesimamia vuguvugu la kuwepo kwa mchakato wa katiba? unakumbuka matamshi ya viongozi waandamizi wa CCM akiwemo mwanasheria mkuu wa serikali Werema? Nani wanaopinga maoni ya wananchi waliyoyatoa kwenye tume ya Warioba, umesikia maneno ya katibu mkuu wa CCM kuwa katiba haina manufaa yeyote so kwa akili yako huru unaona nani anataka tukose katiba mpya.

Mkuu Feedback Katiba mpya ya nchi hii haijaanza kudaiwa mwaka 2010 kama unavyotaka watu waamini. Tumeanza kudai Katiba kuanzia miaka ya 1990. Madai ni kama nilivyoyaeleza hapo juu. Tulifanikiwa kupata moja ambalo ni kukubaliwa mfumo wa vyama vingi. Pamoja na kukubalika kwa mfumo wa vyama vingi lakini Katiba hiyo ilikuwa ni ya Chama kimoja, kimantiki. Kuna baadhi ya Ibara zilibaki kama vile za Chama kimoja, sheria mbalimbali pia hazikurekebishwa.

Sasa imekuja fursa hii hatutaki kuitumia. Nimesema kama CCM wanalilia Serikali mbili tuwaachie ili tupate Tume Huru ya Uchaguzi, Mgombea Huru, nk. Twende kwenye uchaguzi ambao utakuwa huru na haki.

Sasa kama tunakimbia na kuiachia CCM basi tunaziacha fursa nyiiingi kwa kupambania ya mfumo.

 
Last edited by a moderator:
Kuna kitu kinaitwa "Falsafa ya kuwapita wote kwanza!" kama ipo ni falsafa ya chama gani? yaani concept simple kabisa tu hujaelewa! au umeelewa na unafanya makusudi tu ili kusababisha utata usio wa lazima? Wakati fulani ni bora kujibu maswali unapoamua kujitosa katika mjadala badala ya kukimbilia conclusion zisizoeleweka. Nakuuliza tena:Hivi kama mtu kajiunga na mbio, wakati anajiunga na mbio, wenzake 20 walishaondoka kabla yake na yeye anataka akimbie hadi ahakikishe anakuwa mshindi wa kwanza (yaani anakuwa mbele kuliko wote), kwa akili ya kawaida tu, tunategemea kwamba anatakiwa afanyeje? na atakapokimbia akafika mbele (mwanzo) tutasema kafanya je? kwa nini tunajichanganya wenyewe na hali tunajua na tuna uhakika kabisa kwamba tunajichanganya? hivi unajua unavyoitumia akili yako na unavyojizoeza kuwa ndivyo unavyokuwa hivyo hivyo!

Tatizo sio kukuta watu wangap na ww kujiunga ,zen kuwapita.

Tattizo ni kwamba pambana na umasikini wetu sie ndo tutakwambia uwe wa mwisho au wa kwanza kutokana na ukweli kwamba utakuwa ukitutetea sie.

Hamuwezi kuwa na akili timamu kwa kuandaa sera za kushindana na cdm au cuf au nccr, wakati sie hatuli at mlo mmoja.

Ridhaa ya kuwa wa kwanza haipo kwenu kama chama bali ipokwetu wananchi.
 
ACT imekufa kabla haijashiriki uchaguzi, vyama Tanzania ni Chadema, CUF, NCCR na CCM sababu ina dola, ikipoteza dola inapotea

Na kinachochipukia ni APPT - Maendeleo, ambacho ngome yake ipo same, UDP na TLP vinaelekea shimoni.
 
Mkuu Feedback Katiba mpya ya nchi hii haijaanza kudaiwa mwaka 2010 kama unavyotaka watu waamini. Tumeanza kudai Katiba kuanzia miaka ya 1990. Madai ni kama nilivyoyaeleza hapo juu. Tulifanikiwa kupata moja ambalo ni kukubaliwa mfumo wa vyama vingi. Pamoja na kukubalika kwa mfumo wa vyama vingi lakini Katiba hiyo ilikuwa ni ya Chama kimoja, kimantiki. Kuna baadhi ya Ibara zilibaki kama vile za Chama kimoja, sheria mbalimbali pia hazikurekebishwa.

Sasa imekuja fursa hii hatutaki kuitumia. Nimesema kama CCM wanalilia Serikali mbili tuwaachie ili tupate Tume Huru ya Uchaguzi, Mgombea Huru, nk. Twende kwenye uchaguzi ambao utakuwa huru na haki.

Sasa kama tunakimbia na kuiachia CCM basi tunaziacha fursa nyiiingi kwa kupambania ya mfumo.


Naunga Mkono Hoja ila nashaka kama watakubali hivyo vitu Vipatikane.
 
Na ndio maana wale walioamua kujilazimisha kufikiri nje ya duara; wanasema lazima lipo tatizo na dawa ya tatizo ni kulitatua! sio kulalamika tu.Mfano; katika ripoti ya CAG, Anasema kuna vyama vinne ambavyo havina kabisa account za benk.Sasa ndio tuviunge mkono kwa tabia hiyo, etio tu kwa kuwa ni vyama vya upinzani? CAG anasema ripoti zilizowasilishwa kwake, hakuna iliyoandikwa kwa kufuata kanuni za kitaalam za kihasibu, sasa ndio tuunge mkono tu kwa kuwa eti chama husika hakiko madarakani? haya yote yanastahili kupingwa pamoja na kupinga kutokaguliwa kwa hesabu za CCM.Hilo ndilo linalotakiwa.

Sasa ushangae; hapa mjadala ni changamoto na fursa zinazokikabili chama kipya cha ACT-Tanzania lakini wachangiaji wengi wanachofanya ni kulalamikana kulaumu tu badala ya kuchangia mada iliyoko mbele yao! kwa staili hii ndio maana huwa hatutoboi!


HUko kwa CAG mimi simo maana nakuwa Sielewi Chama cha Siasa kisichotumia KODI za WANANCHI inakuwaje kikaguliwe na CAG.

Turudi kwenye hoja yangu amabyo ni kuwa nimetoa tu angalizo, Kuwa HAKUJAWAHI kutokea CHAMA kipya KIKAFANYA VIZURI kushinda Hivyo Vilivyoanza NA MAGEUZI ,Miaaka 90.

Na ukwlei ni kuwa, baada ya Uchaguzi wa 2015 ndio itakuwa mwisho wa ACT maana kwa sasa wafadhili wao wanakihitaji kwa kuwa kimekuja nkupambana na Vyama Vingine vyote, ila baada ya 2015 kutakuwa hakuna tena mapambano na Mfadhili atajitoa.
 
Watanzania tuna shida kubwa sana, tunaishi maisha ya kishabiki kuliko uhalisia, Mtoa maada ametoa neno lililotakiwa kujadiliwa kwa weledi na uono mpana lakini kinachoonekana mjadala umetawaliwa na nani ni nani kama bunge la katiba - rasimu imeachwa imebakia mbili tatu. wapaendwa rudini kwenye mada vinginevyo msiwashangae wabunge wa bunge la katiba kwani mnafanana nao tofauti ni location tu. tujitafakari kama Taifa
 
Back
Top Bottom