ACT-Tanzania: Challenges and Opportunities! (SEHEMU YA KWANZA)

ACT-Tanzania: Challenges and Opportunities! (SEHEMU YA KWANZA)

Hiki chama kimeanzishwa kuwapooza CCM waliotoa fedha kusambaratisha chadema.....ndio maana hata usajili kimepata kwa haraka pengine kuliko chama chochote cha upinzani.....MUNGU hakuwahi kusimama na wasaliti never
 
falsafa, itikadi na sera zake.



E bana kama una copy (soft) za hivi vitu vya ACT-Tanzania naomba unitumie nami nipate fursa ya kujifunza kuhusu hiki chama kama ulivyofanikiwa wewe kufanya hivyo...
 
Mwigamba ni rafiki yangu lakini haya ni maoni yangu.

Katika siasa za Tanzania ni aidha utakuwa Ccm au upinzani, ukiwa upinzani watu wanakutegemea kutokubaliana na Ccm na kutopingana na wapinzani wenzako. Katika hali halisi ukikubaliana na Ccm na kupingana na wapizani wenzako utaitwa majina kama kibaraka, pandikizi au msaliti. Ukiwa mpinzani kama ACT na ukakubaliana na wapinzani wenzako na mbaya zaidi ukawa umetokea au kufukuzwa toka vyama hivyo watu watashindwa kujua kwa nini wakuunge mkono wewe na siyo wale waliokufukuza. Upinzani wao wanao na wameishi nao then kwa nini wewe?

Hii ndiyo sababu ya kuanguka kwa vyama au kushindwa kushamiri kwa vyama vinavyoanzishwa kwa hasira baada ya kutokubaliana au kufukuzwa kwenye vyama vya awali. Mifano ni mingi ya watu waliojaribu kuanzisha vyama walishindwa vibaya, mfano mzuri ni TLP na ADC. TLP walitokea NCCR na ADC walikimbia toka CUF, leo hii jiulize vyama hivi vilivyoanzishwa na vile walikotoka nani wako imara zaidi? TLP simjui kiongozi mwingine zaidi ya Mrema na ADC bendera zinazidi wingi wanachama.

Kuna propaganda zinapigwa eti kuna wabunge 17 watahamia ACT kutoka Ccm na Chadema! Huu ni upuuzi ambao hata mwendawazimu hawezi kuukubali. Mbunge kutoka Ccm au Chadema akajiunga ACT ni sawa kutoka baharini ukaingia kwenye dimbwi, hakuna mwanasiasa mjinga namna hiyo. Labda wanaoeneza propaganda hiyo wanataka tuwaamini wale wanaosema chama hiki kimeanzishwa kama ilivyokuwa CCJ (vyama vinavyoanzishwa mwaka mmoja kabla ya uchaguzi) Vinginevyo ACT na rafiki yangu kipenzi Mwigamba nina hakika wataanuguka kabala ya kusimama.
 
mpk, ACT wasitegemei kupata mbunge hata mmoja 2015 kama awaamini maneno yangu wayaweke haya maneno ya gogo la shamba alafu waniulize baada ya uchaguzi,chama ambaco hakina mwenyekiti
 
Hakuna hata viongozi ngazi ya Mkoa wanafikiria kushinda Ikulu.....
 
Hakuna hata viongozi ngazi ya Mkoa wanafikiria kushinda Ikulu.....

Si wapate hata wa kitaifa maana nasikia mwenyekiti yupo kwa mkopo toka ADC, hii ni kwa mjibu wa Yerico!
 
Mungu wao ndio Mungu wenu!

Kwani Kenye ODM ilikuwepo tangu lini wakuu? Ukongwe wa Chama si umadhubuti wa kuhimili au kuaminiwa na wananchi. Mwishowe wote mtaonekana wahuni wa vijiweni na limbukeni wa kisiasa.
 
Kuna kitu kinaitwa "Falsafa ya kuwapita wote kwanza!" kama ipo ni falsafa ya chama gani? yaani concept simple kabisa tu hujaelewa! au umeelewa na unafanya makusudi tu ili kusababisha utata usio wa lazima? Wakati fulani ni bora kujibu maswali unapoamua kujitosa katika mjadala badala ya kukimbilia conclusion zisizoeleweka. Nakuuliza tena:Hivi kama mtu kajiunga na mbio, wakati anajiunga na mbio, wenzake 20 walishaondoka kabla yake na yeye anataka akimbie hadi ahakikishe anakuwa mshindi wa kwanza (yaani anakuwa mbele kuliko wote), kwa akili ya kawaida tu, tunategemea kwamba anatakiwa afanyeje? na atakapokimbia akafika mbele (mwanzo) tutasema kafanya je? kwa nini tunajichanganya wenyewe na hali tunajua na tuna uhakika kabisa kwamba tunajichanganya? hivi unajua unavyoitumia akili yako na unavyojizoeza kuwa ndivyo unavyokuwa hivyo hivyo!
betlehem,

Concerpt yenu ya kuwa wa kwanza itawachukua muda mrefu sana kufikia malengo yenu kwa vile imejengwa katika misingi ya matokeo kwanza badala ya kazi kwanza. Ni hatari wa chama cha siasa kujengwa hivyo kwa vile kisipofikia malengo yake kuna hatari ya kulazimisha kuyapata kwa njia zisizo halali.

Kimantiki huwezi kufananisa matokeo ya siasa na ya riadha, siasa inapimwa kwa uzito wa hoja zinazolenga kuisaidia jamii nzima lakini riadha inalenga kujinifaisha binafsi. Lakini hata kwenye riadha kufanikiwa sio lazima uwe wa kwanza hata kuwa wa pili ni mafanikio pia. NCCR ina takriban miaka 20 kwenye siasa hutuwezi kusema kwa vile haijawa ya kwanza basi haina mafanikio.

Mnachotakiwa kama chama, ni ku-address matatizo yanayowagusa wananchi badala ya kukimbilia kulilia kuwa wa kwanza.
 
Mkuu Feedback Katiba mpya ya nchi hii haijaanza kudaiwa mwaka 2010 kama unavyotaka watu waamini. Tumeanza kudai Katiba kuanzia miaka ya 1990. Madai ni kama nilivyoyaeleza hapo juu. Tulifanikiwa kupata moja ambalo ni kukubaliwa mfumo wa vyama vingi. Pamoja na kukubalika kwa mfumo wa vyama vingi lakini Katiba hiyo ilikuwa ni ya Chama kimoja, kimantiki. Kuna baadhi ya Ibara zilibaki kama vile za Chama kimoja, sheria mbalimbali pia hazikurekebishwa.

Sasa imekuja fursa hii hatutaki kuitumia. Nimesema kama CCM wanalilia Serikali mbili tuwaachie ili tupate Tume Huru ya Uchaguzi, Mgombea Huru, nk. Twende kwenye uchaguzi ambao utakuwa huru na haki.

Sasa kama tunakimbia na kuiachia CCM basi tunaziacha fursa nyiiingi kwa kupambania ya mfumo.

mkuu; kuna mtu alileta uzi humu akijenga hoja yake kwamba laiti ccm wangeamua tyoka mwanzo kukomaa kwamba wanataka serikali tatu, basi kuna kundi kubwa miongoni mwa wanaotaka serikali tatu kwa sasa lingeibuka na kutaka serikali mbili kwa nguvu zote kwa hoja ya kwamba linatoa upinzani na ikibidi lingegomea mchakato likiona linakaribia kushindwa.Hapo mimi ndipo ninapoona kwamba watanzania wengi tumeshindwa kabisa kuielewa vizuri concept ya ya kuwa na vyama vya upinzani na ni kwa vipi vyama vya upinzani vinaweza kuchangia katika mabadiliko chanya katika nchi yetu.

Hata hivyo kwa kuwa mjadala huu hauhusiani kabisa na katiba, ningependa kutoingia ndani sana katika hili ili kuepuka kupoteza muelekeo wa mada ya msingi ambayo ni changamoto na fursa ambazo chama kipye cha ACT-Tanzania kinazo.
 
Hamuwezi kuwa na akili timamu kwa kuandaa sera za kushindana na cdm au cuf au nccr, wakati sie hatuli at mlo mmoja.
Ndugu yangu!,

1. Wewe tayari umeshaziona sera za ACT-Tanzania na ukaona zinashindana na za CHADEMA na NCCR? Kama hujaziona, hiki unachozungumza unakizungumza kutokea wapi hasa, na unapata wapi nguvu ya kukizungumza hivyo unavyokizungumza?

2.Kwa uelewa wako; ACT-Tanzania ilitakiwa kuwa na sera zinazofanana na zile za NCCR na vyama vingine vya upinzani? kama ndio kwa nini?

3.Kwa uelewa wako, vyama vya upinzani vilivyoko Tanzania kwa sasa , vinafanana kisera? na kama vinafafana(na ufanano huo ndio unaotakiwa) kwa nini sasa visiwe chama kimoja? na kama havifanani, sasa kwa nini unadhani ACT-Tanzania inatakiwa kufanana?na unadhani kama ACT-Tanzania itakuwa na falsafa, itikadi na sera zinazofanana na vyama ulivyovitaja; itakuwa na sababu ya kuwepo?

Hebu naomba unijibu hayo kwanza.
 
Back
Top Bottom