Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,198
- 7,539
Wadau, baada ya kupotea kidogo, leo ningependa nilete kwenu mjadala kidogo kuhusu chama kilichosajiliwa hivi karibuni ACT-Tanzania.
Inafahamika wazi kwamba chama cha ACT-Tanzania ni chama cha 23 kusajiliwa kama sio cha 22.Kama vilivyo vyama vingine(ikiwa kweli vinaamini hivyo), ACT-Tanzania nayo inaamini na inapigania kuwa chama cha kwanza kwa kukubalika zaidi na hivyo kuiongoza nchi na kutekeleza falsafa, itikadi na sera zake.Sasa swali la kujiuliza tu ni ikiwa ni jambo lipi hasa litakalokifanya chama cha ACT-Tanzania kufikia lengo hilo kama vyama zaidi ya 20 vilivyotangulia kwa miaka nenda rudi vimeshindwa kufikia lengo? na je ni nini cha ziada ambacho ACT-Tanzania inacho tofauti na watangulizi wao ? maswali haya pamoja na mengine; yanabakia kuwa mambo ya mjadala.
Kwa leo mimi ningependa tu kugusia kidogo changamoto na fursa zinazoikabili ACT-Tanzania angalau (02) tu kwa uchache wake.
1. Uchanga wa Chama:
i) Kwa sasa ACT-Tanzania ndicho chama kichanga kuliko vyote; hivyo kama ni mtoto, tunaweza kusema ni 'kichanga'.Sasa changamoto ni kwamba ni kwa vipi ACT-Tanzania inaweza kukimbia kutoka chini mwisho hadi kufika juu mwanzo na kasi hiyo kitaitoa wapi!.
ii) Pili Vyama vyote vya upinzani vilivyotangulia kuanzia kuanzishwa kwa sera ya vyama vingi hadi leo, havijaweza kufikia lengo la kuunda serikali.Sasa changamoto ni kwamba ni kwa vipi ACT-Tanzania itaweza kufikia lengo ikiwa wa kabla yao kwa miaka nenda rudi wamekwama, na ni kwa vipi hasa ACT-Tanzania itaweza kukabiliana na changamoto zilizowashinda watangulizi wake.
iii) Angalau ukiangalia misingi ya ACT-Tanzania;Unagundua kwamba inaitofautisha kabisa ACT-Tanzania dhidi ya vyama vyote vilivyotangulia kabla yake.Sasa kazi kubwa ni ikiwa chama kitaweza kutembea katika misingi hiyo.
ii) Angalau ACT-Tanzania inaonekana kuwa na watu wengi wenye utaalam na upeo mzuri juu ya masuala ya siasa pamoja na dhamira ya dhati.Kwa hiyo kama watajituma na kushawishi watu wengine wenye Uzalendo wa kweli,vipaji na uoni kuwaunga mkono, hiyo itaweza kukisaidia sana chama hiki kichanga kuliko vyote kupiga hatua.
2:Imani.
Katika hali ya kawaida, ili chama kiweze kusonga mbele kwenda juu na pengine hadi kufikia kushika nafasi ya kwanza (yaani kushika dola) ni lazima kiaminiwe na imani haiji yeyewe tu bali hujengwa na imani thabiti ni ile inayojengwa kwa matendo na si maneno matupu.
ii) Watanzania ni wale wale, kwa hiyo wafuasi watakaoiunga mkono ACT-Tanzania na pengine kugombea na kupata uongozi wa chama ni watanzania hawa hawa ambao ni 'Heterogenious' . Sasa upo uwezekano wa watu ambao hawakuwa waadilifu kwenye vyama vingine, kuingia ACT, Kwa dhumuni lile lile la kufanya uharibifu nchini na hivyo kuifanya ACT-Tanzania nayo isiaminike na wasioiami wawe na uhalali wa kufanya hivyo.
i) Uchanga wa chama wenyewe ni fursa; Waswahili husema samaki mkunje angali mbichi. Kama chama cha ACT-Tanzania kitatengeneza kanuni na mifumo thabiti na kuisimamia kuanzia mwanzo kwa nguvu moja na kuhakikisha kwamba wasimamizi wa misingi na kanuni hizo nao ni waadilifu na wasafi, basi hiyo inaweza ikakisaidia chama hiki kichanga kuliko vyote nchini.
ii) Chama cha ACT-Tanzania bado hakijawa na makando kando; kwa hiyo kikianza kuonesha kwa matendo tokea mwanzo kwamba kinatenda kinayoyasema; basi walioumwa na nyoka kidogo kidogo wataanza kuona tofauti ya nyoka na majani 'Objectively'. Kwa kuwa mazoea hujenga tabia, kwa kuanza na kujizoeza kutembea katika yale ambayo chama kinayasema; itajenga tabia ya chama, na tabia ya namna hiyo inakuwa ni tabia 'Possitive' ambayo kimsingi ndiyo inayotakiwa.
Kwa leo niishie hapa na nitaendelea kueleza changamoto na fursa nyingine kwa kadiri Mungu atakavyotujaalia.Tumuombe Mungu atupe afya njema na atuongezee ujuzi elimu na maarifa ili tuweze kuelimishana, kujadiliana na kuijenga nchi yetu kwa maslahi ya watu wetu kwa kizazi cha sasa na kizazi kijacho.
Inafahamika wazi kwamba chama cha ACT-Tanzania ni chama cha 23 kusajiliwa kama sio cha 22.Kama vilivyo vyama vingine(ikiwa kweli vinaamini hivyo), ACT-Tanzania nayo inaamini na inapigania kuwa chama cha kwanza kwa kukubalika zaidi na hivyo kuiongoza nchi na kutekeleza falsafa, itikadi na sera zake.Sasa swali la kujiuliza tu ni ikiwa ni jambo lipi hasa litakalokifanya chama cha ACT-Tanzania kufikia lengo hilo kama vyama zaidi ya 20 vilivyotangulia kwa miaka nenda rudi vimeshindwa kufikia lengo? na je ni nini cha ziada ambacho ACT-Tanzania inacho tofauti na watangulizi wao ? maswali haya pamoja na mengine; yanabakia kuwa mambo ya mjadala.
Kwa leo mimi ningependa tu kugusia kidogo changamoto na fursa zinazoikabili ACT-Tanzania angalau (02) tu kwa uchache wake.
1. Uchanga wa Chama:
- Changamoto,
i) Kwa sasa ACT-Tanzania ndicho chama kichanga kuliko vyote; hivyo kama ni mtoto, tunaweza kusema ni 'kichanga'.Sasa changamoto ni kwamba ni kwa vipi ACT-Tanzania inaweza kukimbia kutoka chini mwisho hadi kufika juu mwanzo na kasi hiyo kitaitoa wapi!.
ii) Pili Vyama vyote vya upinzani vilivyotangulia kuanzia kuanzishwa kwa sera ya vyama vingi hadi leo, havijaweza kufikia lengo la kuunda serikali.Sasa changamoto ni kwamba ni kwa vipi ACT-Tanzania itaweza kufikia lengo ikiwa wa kabla yao kwa miaka nenda rudi wamekwama, na ni kwa vipi hasa ACT-Tanzania itaweza kukabiliana na changamoto zilizowashinda watangulizi wake.
- Fursa,
iii) Angalau ukiangalia misingi ya ACT-Tanzania;Unagundua kwamba inaitofautisha kabisa ACT-Tanzania dhidi ya vyama vyote vilivyotangulia kabla yake.Sasa kazi kubwa ni ikiwa chama kitaweza kutembea katika misingi hiyo.
ii) Angalau ACT-Tanzania inaonekana kuwa na watu wengi wenye utaalam na upeo mzuri juu ya masuala ya siasa pamoja na dhamira ya dhati.Kwa hiyo kama watajituma na kushawishi watu wengine wenye Uzalendo wa kweli,vipaji na uoni kuwaunga mkono, hiyo itaweza kukisaidia sana chama hiki kichanga kuliko vyote kupiga hatua.
2:Imani.
Katika hali ya kawaida, ili chama kiweze kusonga mbele kwenda juu na pengine hadi kufikia kushika nafasi ya kwanza (yaani kushika dola) ni lazima kiaminiwe na imani haiji yeyewe tu bali hujengwa na imani thabiti ni ile inayojengwa kwa matendo na si maneno matupu.
- Changamoto
ii) Watanzania ni wale wale, kwa hiyo wafuasi watakaoiunga mkono ACT-Tanzania na pengine kugombea na kupata uongozi wa chama ni watanzania hawa hawa ambao ni 'Heterogenious' . Sasa upo uwezekano wa watu ambao hawakuwa waadilifu kwenye vyama vingine, kuingia ACT, Kwa dhumuni lile lile la kufanya uharibifu nchini na hivyo kuifanya ACT-Tanzania nayo isiaminike na wasioiami wawe na uhalali wa kufanya hivyo.
- Fursa;
i) Uchanga wa chama wenyewe ni fursa; Waswahili husema samaki mkunje angali mbichi. Kama chama cha ACT-Tanzania kitatengeneza kanuni na mifumo thabiti na kuisimamia kuanzia mwanzo kwa nguvu moja na kuhakikisha kwamba wasimamizi wa misingi na kanuni hizo nao ni waadilifu na wasafi, basi hiyo inaweza ikakisaidia chama hiki kichanga kuliko vyote nchini.
ii) Chama cha ACT-Tanzania bado hakijawa na makando kando; kwa hiyo kikianza kuonesha kwa matendo tokea mwanzo kwamba kinatenda kinayoyasema; basi walioumwa na nyoka kidogo kidogo wataanza kuona tofauti ya nyoka na majani 'Objectively'. Kwa kuwa mazoea hujenga tabia, kwa kuanza na kujizoeza kutembea katika yale ambayo chama kinayasema; itajenga tabia ya chama, na tabia ya namna hiyo inakuwa ni tabia 'Possitive' ambayo kimsingi ndiyo inayotakiwa.
Kwa leo niishie hapa na nitaendelea kueleza changamoto na fursa nyingine kwa kadiri Mungu atakavyotujaalia.Tumuombe Mungu atupe afya njema na atuongezee ujuzi elimu na maarifa ili tuweze kuelimishana, kujadiliana na kuijenga nchi yetu kwa maslahi ya watu wetu kwa kizazi cha sasa na kizazi kijacho.