ACT-Tanzania: Challenges and Opportunities! (SEHEMU YA KWANZA)

ACT-Tanzania: Challenges and Opportunities! (SEHEMU YA KWANZA)

HUko kwa CAG mimi simo maana nakuwa Sielewi Chama cha Siasa kisichotumia KODI za WANANCHI inakuwaje kikaguliwe na CAG.
*Kibanga, Vyama vya siasa havitakiwi kuwa mali ya mtu, vinatakiwa kuwa mali ya umma.Hivyo ni lazima mambo yake yote yafanyike katika utaratibu unaoeleweka na wa wazi.

Ndugu Kibanga, wakati wote tumekuwa tukilalamika kwamba kuna fedha chafu zinaingizwa kwenye mzunguko kupitia vyama vya siasa na leo hii watu (ukiwemo wewe) unalalamika kwamba ACT-Tanzania (kwa mfano), inafadhiliwa na wafadhili (ambao hujawataja lakini unaonekana unaamini kwamba hawakutakiwa kukifadhili).Sasa CAG Anataka akague ili ajue chama kinapata wapi fedha zake, fedha hizo ni halali au si halali, na chama kinazitumia je fedha hizo; nyie nyie (ukiwemo wewe) mnaolalamika kuingia kwa fedha chafu ndani ya vyama; mnajenga hoja kwamba visikaguliwe maana havina ruzuku ya serikali wakati wenzenu wanasema vyamo vyote maadam ni vyama vya umma vikaguliwe.

Wakati wengine wanasema ni lazima vyama vyote (iwe vinapokea au havipokei ruzuku) ni lazima viwe na wahasibu wenye weledi unaokubalika yaani CPA, Wale wale wanaolalamika wanasema ya nini wakati vyama husika havipokei ruzuku.Halafu vikiachwa; watu wale wale wanalalamika kwamba vyama husika vinaendeshwa kihuni.Hivi watu wa dizaini hii tukiwategema ni nini hatima yetu kama taifa?


Turudi kwenye hoja yangu amabyo ni kuwa nimetoa tu angalizo, Kuwa HAKUJAWAHI kutokea CHAMA kipya KIKAFANYA VIZURI kushinda Hivyo Vilivyoanza NA MAGEUZI ,Miaaka 90.
*Hii nitakujibu kwenye post ya peke yake maana nataka nikukumbushe mijadala yetu mimi na wewe siku chache zilizopita.

Na ukwlei ni kuwa, baada ya Uchaguzi wa 2015 ndio itakuwa mwisho wa ACT maana kwa sasa wafadhili wao wanakihitaji kwa kuwa kimekuja nkupambana na Vyama Vingine vyote, ila baada ya 2015 kutakuwa hakuna tena mapambano na Mfadhili atajitoa.
*Hivi kibanga;Unaposema mfadhili wa ACT-Tanzania,ili hoja yako iwe na maana, unatakiwa ueleze kwamba mfadhili huyo ni nani, wewe umemjuaje, unavielelezo gani na unaweza je kututhibitishia kwamba vielelezo vyako ni vya ukweli kabla ya ya kuipa manani hoja yako na kuendelea kuijadili.Kinyume chake ni kwamba utakuwa umeamua kujadili vitu ambavyo ni objective kwa kutumia emotions! na mwendo huo utakupoteza kabisa na kuishia kuushangaza ulimwengu.

Kwa ujumla mpaka sasa hujaeleza kwamba unachoongelea wewe ni changamoto au fursa au vyote maana ndio hoja iliyoko mbele yetu.Ukitaka ueleweke; usichangie tu ilimradi bali soma kwanza mada uielewe na kisha uhakikishe kwamba michango yako katika hitimisho; inaenda kuonesha muonganikano na mada iliyoko mezani.
 
Hiki chama kimeanzishwa kuwapooza CCM waliotoa fedha kusambaratisha chadema.....ndio maana hata usajili kimepata kwa haraka pengine kuliko chama chochote cha upinzani.....MUNGU hakuwahi kusimama na wasaliti never
kwa hiyo ndugu hiyo ni challenge au ni oppurtunity kwa chama cha ACT-Tanzania?
 
E bana kama una copy (soft) za hivi vitu vya ACT-Tanzania naomba unitumie nami nipate fursa ya kujifunza kuhusu hiki chama kama ulivyofanikiwa wewe kufanya hivyo...
mkuu mfano, mimi nimesoma uzi;
[h=1]ACT-Tanzania (Alliance for Change and Transparency): Taarifa kwa Umma.[/h]Nimeona kuna document imekuwa attached hapo yenye misingi ya chama cha ACT-Tanzania. Kama wewe hujaupitia na ukaisoma hiyo misingi, hebu na wewe anza na hiyo misingi kwanza halafu ukishaimaliza urudi kwenye mada yetu ambayo ni Fursa na changamoto zinazokikabili chama kipya cha ACT-Tanzania.

Kinaconishangaza ni kwamba kila anayesoma misingi hiyo harudi na wanaorudi wanaenda nje ya mada kwa kuzungumza vitu ambavyo ukiwauliza wamevipata wapi wanakuambia hawana majibu ya kueleweka.

Yaani ndugu yangu tuna tatizo kubwa sana katika jamii zetu hizi ambalo tunatakiwa tuwe na collective actions kulishughulikia vinginevyo tutaendelea kuzunguka pale pale kila siku tukilalamikia mambo yale yale yakifanywa kwa style ile ile.
 
Katika siasa za Tanzania ni aidha utakuwa Ccm au upinzani, ukiwa upinzani watu wanakutegemea kutokubaliana na Ccm na kutopingana na wapinzani wenzako.
Mkuu na hapo ndipo tunapokosea sana na kwa makosa hayo hayo ndipo tunapotoa mwanya hata kwa baadhi ya wanasiasa kuingia madarakani kwa kutumia hila na mwishowe wanakuwa mizigo nasi tunabaki tukilalama kumbe nasi ni sehemu ya tatizo.

Wewe ukisema na ku- tune akili yako kwamba kazi ya upinzani ni kuipinga CCM tu kuna mambo yafuatayo,
1, CCM nao wata- tune akili zao kwamba kazi yao ni kukupinga tu na kutakuwa hakuna sababu ya kuwalaumu kwa kuwa wanafizikiwa wanasema kwa kila msukumo/nguvu kuelekea muelekeo fulani, kuna nguvu sawa sawa inayosukuma kuleta ukinzani(sijui kama nimetafsiri sawa sawa).Mchuano wa aina hii hauwezi kuwa na masilahi kwa nchi hata siku moja na ndio maana watu wazalendo na wanaojitambua, hawafurahii michuano ya namna hii hata siku moja.

2.Matendo ya vyama vya upinzani yatakuwa hayatabiriki; bali yatakuwa yanaamuliwa na matendo na muelekeo wa CCM kitu ambacho ni hatari sana kwa ustawi wa vyama vyenyewe na taifa kwa ujumla.Kwa mfano;Inapotokea mjadala juu ya idadi ya serikali, itabidi upinzani usubiri kwanza uangalie muelekeo wa CCM ili wao waupinge.Kwa maana hiyo ni kwamba; kama CCM watasema wanataka serikali mbili (kwa mfano) upinzani itabidi waseme wanataka tatu (si kwa kuwa tatu ni nzuri, bali kwa kuwa wanaamini kwamba wana wajibu wa kupinga.Hii maana yake ni kwamba; kama CCM wakiamua kutetea serikali tatu kwa mfano, itabidi upinzani watetee mbili (si kwa kuwa mbili ni nzuri bali kwa kuwa wanaamini wao kazi yao kupinga).Hii ni tafsiri duni kabisa ya upinzani ambayo kimsingi inastahili kupigwa vita kwa nguvu zote.kuonesha ni kwa jinsi gani fikra hizo potofu zilivyoota mizizi; ndio maana hata katika bunge la katiba, ulikuwa unaona watu wengi wanaotetea serikali mbili, badala waeleze ubora wa serikali mbili, wanaeleza udhaifu wa serikali tatu na kinyume chake.

Hizo zi athari chache tu ambazo nimezitaja kwa sasa zinazotokana na mtizamo huo potofu.

Tukirudi kwenye hoja yako ya kwamba si sahihi kwa chama pinzani kukipinga chama pinzani kingine; hapa mimi nitakuuliza maswali tu unipe conclusio mwenyewe.

1. Kuna kipindi chadema waliwaita CUF kuwa ni CCM 'B' JE CUF walipaswa kukubaliana na CHADEMA katika hili kwakuwa wote ni wapinzani?

2.Unakumbuka kadhia ya CUF kuitwa maliberali; unadhani CUF walitakiwa kukubaliana na hilo kwa kuwa waliokuwa wamewaita hivyo walikuwa wapinzani wenzao? n,k

3. Tuchukulie mfano wa ripoti ya CAG, Kuna vyama ambavyo havina account bank! tunatakiwa kuviunga mkono katika hilo kwa kuwa ni vyama vya upinzani (wenzetu)

Kama tutakuwa tunaleana kwa nadharia ya "hawa ni wenzetu" kwa nini tuwashangae wenzetu nao wakileana kwa nadharia hiyo hiyo ya kwamba "hawa ni wenzetu"? Au unadhani kinachoweza kutusaidia na kuisaida nchi hiii, ni ile nadharia ya mkuki kwa ngurue? inasikitisha na kufedhehesha sana kwa kweli! .Ni bora tukaamua kubadilika!

cc mayange , RockSpider
 
Last edited by a moderator:
Hakuna hata viongozi ngazi ya Mkoa wanafikiria kushinda Ikulu.....
Mkuu,
Iko hivi:Kitu chochote huanza na Wazo.Wazo hupelekea nia,kisha kinachofuata ni kutengeneza nadharia, kisha kuweka mikakati,kisha kutengeneza mifumo, na kisha ndio utekelezaji wa mikakati kulingana na wazo la msingi.Sasa wewe unapoona mtu anataka kuanzisha kampuni ambayo itakuwa na matawi Afrika nzima; halafu anakupa wazo lake, wewe uanamwambia unataka kuwa na kampuni yenye matawi Afrika nzima wakati hapa tanzania tu haijawa na matawi nchi nzima; sijui kwamba utakuwa unafikiri sawa sawa.
 
Mungu wao ndio Mungu wenu!

Kwani Kenye ODM ilikuwepo tangu lini wakuu? Ukongwe wa Chama si umadhubuti wa kuhimili au kuaminiwa na wananchi. Mwishowe wote mtaonekana wahuni wa vijiweni na limbukeni wa kisiasa.
Mkuu uko sahihi kabisa! ujue tatizo letu tulio wengi tuna uwezo lakini hatujui kwamba tunao, na kuna ambao hawana uwezo, wanaweza kupata uwezo ila hawajiamini.Wwanashindwa kuelewa kwamba aliempa nyerere akili ndiye huyo huyo aliye kupa wewe akili na kwa kadiri mtu anavyotumia akili yake ndivyo inavyokuwa na wa kadiri anavyoacha kuitumia ndivyo inavyolala.

Hawajui kwamba dunia hii ina fursa nyingi ambazo zinaweza kutumiwa na yeyote, na kinachotokea ni ubunifu tu na kujaribu kuyakabili matatizo ya mwanadamu kwa kutumia akili na mazingira yako na ndio maana leo hii unaweza ukadhani kama vitu vyote vishavumbuliwa lakini kila siku wenzako wanavumbua vitu vipya halafu wakishavumbua ndio unashangaa! hee! kumbe!.Wanashindwa kuelewa kwamba kwa mfano mifumo ya kiutawala duniani kwa sasa imeundwa na watu na waliounda mifumo hiyo hawana vichwa viwili.

Sasa kama mjadala wetu unavyojieleza "ACT-Tanzania; challenges and opportunities, mtu anakuja hapa anasisitiza tu haiwezekani! haiwezekani! ukimuuliza kwa nini haiwezekani hana majibu ya kueleweka! ukimuuliza sasa hiyo ni changamoto au ni fursa, anapotea! Yaani ndugu yangu;tuna kazi kubwa sana aisee.

 
mkuu mfano, mimi nimesoma uzi;
[h=1]ACT-Tanzania (Alliance for Change and Transparency): Taarifa kwa Umma.[/h]Nimeona kuna document imekuwa attached hapo yenye misingi ya chama cha ACT-Tanzania. Kama wewe hujaupitia na ukaisoma hiyo misingi, hebu na wewe anza na hiyo misingi kwanza halafu ukishaimaliza urudi kwenye mada yetu ambayo ni Fursa na changamoto zinazokikabili chama kipya cha ACT-Tanzania.

Kinaconishangaza ni kwamba kila anayesoma misingi hiyo harudi na wanaorudi wanaenda nje ya mada kwa kuzungumza vitu ambavyo ukiwauliza wamevipata wapi wanakuambia hawana majibu ya kueleweka.

Yaani ndugu yangu tuna tatizo kubwa sana katika jamii zetu hizi ambalo tunatakiwa tuwe na collective actions kulishughulikia vinginevyo tutaendelea kuzunguka pale pale kila siku tukilalamikia mambo yale yale yakifanywa kwa style ile ile.

Asante mkuu nimeisoma, ni nzuri, kama kweli inatoka kwa mtu anayewakilisha chama.
Ninalo jambo moja dogo kuwashauri watu mnaoiunga mkono ACT especially hapa JF, kuanzia Nyakarungu; Njano 5 na hata wewe. Punguzeni defensive languages mnapoongelea au mnaporespond kwenye challenging ideas. Naamini viongozi wa ACT kama watasoma hapa watalifanyia kazi hilo pungufu...
Nikipata mda nitaweka kabisa uzi wa kuwashauri hilo Inshaalah...
 
Last edited by a moderator:
kwa hiyo ndugu hiyo ni challenge au ni oppurtunity kwa chama cha ACT-Tanzania?
ndugu hiyo ni Obstacle....hakuna challenge wala opportunity (refer O&OD) kwa hicho chama hicho chama ni kama pain killer maumivu yakipungua na chenyewe kinapotea
 
kwanza unge declare interest yako ili tujue una maslahi na chama au la maana naona unatoa defense sana
 
kwanza unge declare interest yako ili tujue una maslahi na chama au la maana naona unatoa defense sana
Dah! kwa hiyo wewe katika mada hii imeona hakuna cha kujadili bali umeona mjadala utakaofaa ni kunijadili mimi!? Hebu jiulize, ukianza kunijadili mimi, wewe utapata faida gani, au chama chako kitapata faida gani, au jamii yako itapata faida gani au nchi yako itapata faida gani? kama hakuna yeyote atakaye pata faida yeyote; ni bora ukaacha biashara hiyo na ukarudi kwenye mada ya msingi ikiwa unapenda kufanya kazi zenye manufaa.
 
Asante mkuu nimeisoma, ni nzuri, kama kweli inatoka kwa mtu anayewakilisha chama.
Ninalo jambo moja dogo kuwashauri watu mnaoiunga mkono ACT especially hapa JF, kuanzia Nyakarungu; Njano 5 na hata wewe. Punguzeni defensive languages mnapoongelea au mnaporespond kwenye challenging ideas. Naamini viongozi wa ACT kama watasoma hapa watalifanyia kazi hilo pungufu...
Nikipata mda nitaweka kabisa uzi wa kuwashauri hilo Inshaalah...

Mkuu uzi wako utakuwa muhimu sana hasa kama utajitahidi kuwa objective.Hata hivyo kuhusu hiyo hoja ya difensive, sijakuelewa vizur.

Tuna vitu vitatu katika muktadha unaouzungumzia; tuna Defensive (kama unavyosema), kuna Neutral halafu Kuna offensive. Sasa ingesaidia zaidi kama ungefafanua kwamba kwa nini watu wasiwe defensive, na ungependekeza wawe neutral au offensive na kwa nini.Kusema ukweli ungekuwa umesaidia sana.

Kadhalika ingependeza kama ungefafanua ikiwa watu wanapaswa kujiepusha kuwa defensive kwa ACT-Tanzania pekee! au kwa vyama vyote na kwa nini.Hapo mjadala ukwekwenda vizuri zaidi kwa vile nionavyo mimi.

Asante.
 
Challenge kubwa nizionazo mimi, ni

1. Tayari hamtendi yale mnayoyasema. Mmetwambia kuwa moja ya misingi yenu ni uwazi.
ACT- Tanzania inaamini katika uwazi kwenye mambo yote ya kijamii na kitaifa. Hivyo basi viongozi na wanachama wa ACT-Tanzania wana wajibu wa kupigania uwazi katika mambo yote wanayofanya kwa ajili ya umma. Uwazi huu ni msingi wa kupambana na vitendo vya ukosefu wamaadili na ufisadi na hivyo tunaamini njia sahihi ni kuhakikisha kuwa

wanachama na wananchi waliotupa dhamana ya uongozi wanajua yanayofanywa na chama na serikali yao.
Mna challenge ya kuwa wawazi kama mlivyojitangaza, na hivyo tunapenda muanze uwazi huo kwa kutuwekea wazi gharama ambazo chama chenu kimetumia katika hatua hizi za awali za kupata usajili hadi sasa. Pamoja na kufafanua gharama hizo, mtueleze wazi hizo fedha zimetoka wapi na ni kiasi gani toka kila chanzo.

Hayo yakishindikana chama kitapata sifa ya ULAGHAI!

2. Mmeanzisha chama na mara moja mmeonekana kuchukua mali za baadhi ya vyama. Huo ndio uzalendo? Huo ndio uwajibikaji? Nikisema huo ni uhuni utakuwa na hoja gani za kukataa.

Kutokana na hilo, pamoja na kuonyesha kabisa kupambana, basi wale mnaopambana nao watajilinda (self defence). Hamtakuwa na muda wa kukua kwa amani.

3. Hapa JF, tunaona wana CCM kama akina Simiyu Yetu na Msalani ndio wanatetea ACT. Sisi wengine tuliokinai mambo ya CCM mnatuweka njia panda.
 
2. mmeonekana kuchukua mali za baadhi ya vyama. Huo ndio uzalendo? Huo ndio uwajibikaji? Nikisema huo ni uhuni utakuwa na hoja gani za kukataa.
Mhh! Hii challenge ni kiboko! Dah! kwa hiyo ni uporaji tu! aisee!
 
huwa sijadili vyama vya mifukoni vilivyopo kwa lengo la kuchuma pesa toka ccm! Hiki chama kumbukeni kimeanzishwa na wasaliti na masalia kwa lengo la kushibisha matumbo yao,kwao tumbo ni zaidi ya utu na ubinadamu wao!
 
ACT tz ndio tumain letu jipya c magaidi wauwaji wa cmd na kesho nntatoa Uzi kuelezea mauvu unyanyasaji na ugaidi wa cmd nadhani c siri kwa watanzania wanao Fanya utafiti c waha makada waopewa 30000 kwa mwezi kwa ajili ya kuitetea cmd humu jf.
 
ACT tz ndio tumain letu jipya c magaidi wauwaji wa cmd na kesho nntatoa Uzi kuelezea mauvu unyanyasaji na ugaidi wa cmd nadhani c siri kwa watanzania wanao Fanya utafiti c waha makada waopewa 30000 kwa mwezi kwa ajili ya kuitetea cmd humu jf.

Ni vigumu sana kujua tofauti ya ACT na CCM kwa sababu hoja zao zinafanana. Ugaidi????
 
huwa sijadili vyama vya mifukoni vilivyopo kwa lengo la kuchuma pesa toka ccm! Hiki chama kumbukeni kimeanzishwa na wasaliti na masalia kwa lengo la kushibisha matumbo yao,kwao tumbo ni zaidi ya utu na ubinadamu wao!

Mtu yeyote mwenye akili timamu hawezi kushabikia hili tawi la ccm!
 
Challenge kubwa nizionazo mimi, ni

1. Tayari hamtendi yale mnayoyasema. Mmetwambia kuwa moja ya misingi yenu ni uwazi.

Mna challenge ya kuwa wawazi kama mlivyojitangaza, na hivyo tunapenda muanze uwazi huo kwa kutuwekea wazi gharama ambazo chama chenu kimetumia katika hatua hizi za awali za kupata usajili hadi sasa. Pamoja na kufafanua gharama hizo, mtueleze wazi hizo fedha zimetoka wapi na ni kiasi gani toka kila chanzo.

Hayo yakishindikana chama kitapata sifa ya ULAGHAI!

2. Mmeanzisha chama na mara moja mmeonekana kuchukua mali za baadhi ya vyama. Huo ndio uzalendo? Huo ndio uwajibikaji? Nikisema huo ni uhuni utakuwa na hoja gani za kukataa.

Kutokana na hilo, pamoja na kuonyesha kabisa kupambana, basi wale mnaopambana nao watajilinda (self defence). Hamtakuwa na muda wa kukua kwa amani.

3. Hapa JF, tunaona wana CCM kama akina Simiyu Yetu na Msalani ndio wanatetea ACT. Sisi wengine tuliokinai mambo ya CCM mnatuweka njia panda.

Usipate shida mkuu,hili ni tawi la ccm ndio maana watetezi wake ndio hawa buk 7 imean Msalani,ifweero,simiyu,lizaboni,big show na wachuia tumbo wengineo.Hiki chama kitabaki jf na facebook tu!
 
Usipate shida mkuu,hili ni tawi la ccm ndio maana watetezi wake ndio hawa buk 7 imean Msalani,ifweero,simiyu,lizabon i,big show na wachuia tumbo wengineo.Hiki chama kitabaki jf na facebook tu!
Sasa na Ludovick aliyenunuliwa na Mwigulu kajitokeza wazi

 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom