Basi mkuu umeeleweka.Mimi nimekuelewa na vile vile ni matumaini yangu kwamba wadau wote watakuwa wamekuelewa kwamba kimsingi ACT-Tanzania kwa sasa imepata kashfa ya "Mapinduzi" eeeh! "Kujaribu kupindua maoni ya wananchi" kama unavyosema na chanzo cha taarifa hiyo ni wewe mwenyewe.Vile vile unatuambia kwama jaribio hilo la mapinduzi, ni jaribio baya zaidi na hivyo ndio kashfa kubwa zaidi kuliko kashfa nyingine zilizowahi kutokea nchini na hivyo chama Hicho ndicho kibaya kuliko vyote na hivyo hakina fursa yeyote ya kufanya vizuri.Kaka umeuliza mwananchi ni nani na bahati nzuri Katiba imetoa maana ya neno "mwananchi" kwamba ni yule ambaye (kwa umoja wao) madaraka na mamlaka ya uendeshaji wa nchi hutoka kwao na hukabidhi mamlaka haya kwa wachache (watawala) ili waendeshe nchi kwa niaba yao (wananchi).
Ni ajabu kwamba hawa ACT-Tz wanashirikiana na baadhi ya watawala kutaka kupindua maoni ya wananchi juu ya uendeshaji wa nchi yao. Chama cha aina hii huwezi kusema eti "hakina kashfa". Kama nilivyosema, usaliti (kushiriki kupindua maoni ya wananchi) ni kashfa mbaya zaidi pengine kuzidi hata ufisadi na uchafu mwingine.
naomba ushaidi juu ya chama kutangaza uchaguzi kabla ya katiba.akili ya kufugwa inamatatizo.uchaguzi utafanyika baada ya rasimu ya katiba kupitishwa.acheni propaganda za kitoto.
Tuanze na wewe kwanza; je! wewe unajua maana yake? kama unajua, ushawahi kuwaelimisha wangapi ili nao wajue, na kama hujawahi kuelimisha yeyote, elimu hiyo unakaa nayo ya nini na kwa faida ya nani na mpaka lini? na kama hujui maana yake; je ushawahi kuwauliza wanaojua wakujuze? kama hujawahi kuuliza, je umeemua kubaki hivyo hivyo bila kujua? kama uliuliza; je! uliowauliza wote hawajakuambia! kama wamekuambia unacholalamika nini?ni watanzania wangapi wa naelewa maana ya jina la chama hiki?
By Haki sawa
Hiki chama ni cha hovyo sana, yaani uchaguzi wa vitongoji mpaka taifa unatangazwa kabla ya katiba kupitishwa, hivi huo muundo wa uongozi mmeutoa wapi wakati hamna katiba?
mwenezi ambaye ni verified hapa......
Kwa faida ya muuliza swali na umma kwa ujumla: tunapenda kulitolea ufafanuzi tena na tena jambo hili.Tunapenda kufafanua tena kwa wale ambao hawakuona ufafanuzi wetu wa awali kwamba ACT-Tanzania ina katiba (rasimu) ambayo ndiyo chama kimeitumia kupata usajili.Rasimu hii inaelekeza mambo yote ya msingi ikiwemo misingi, itikadi na falsafa ya chama.Vile vile inaelekeza muundo mzima wa chama.Hata hivyo chama kilishatoa ufafanuzi kwamba Kamati kuu ya muda iliunda jopo la kudurusu (revise) rasimu hiyo kwa kuwa wawanachama na wadau wengine waliona kuna makosa katika baadhi ya sehemu kwenye rasimu hiyo ikiwemo makosa ya kiuchapaji na kisarufi.Hivyo basi kama chama kilivyotoa ratiba hapo juu; imeelezwa ni nini kinaendelea na bila shaka rasimu yenye mabadiliko itakapokabidhiwa katika kikao kilichokuwa kimeunda jopo la marejeo ya katiba hiyo na kikao kukubali kwamba marekebisho yaliyofanywa ni sahihi; jamii nzima inaweza kupatiwa tena rasimu hiyo pengine hata kabla ya mkutano mkuu ili wadau wengine nao waweze kutoa ushauri na maoni yao.
Vile vile wote tufahamu kwama ACT-Tanzania ni bado ni mtoto wa siku kumi (10), sasa mtoto anakuwa taratibu.Chama kinashauri kwamba ni bora wadau kutoa ushauri na kukosoa kila inapostahili ili chama kiweze kuwa bora badala ya kulalamika tu.
1. Ndugu yangu; umesoma mada vizuri na kuielewa kabla ya kuchangia? Hebu kama huna uhakika juu ya hili soma tena na tena.Kwa uandishi huu na elimu yako uliyonayo inashangaza kuwa unataka kufisadi time kwa kujadili chama cha mamluki na wanafiki,please niambie hoja gani Zitto aliyowahi kuianzisha na akaisimamia hadi mwisho??! Mabilioni ya Uswisi- filamu imeishia wapi??!
!
Kwani ndugu Haki sawa , kwa mujibu wa ratiba hiyo iliyotolewa; mkutano mkuu maalum wa katiba unakaa lini na uchaguzi wa chama ni lini?ni kipi kinachoanza kabla ya kipi? je! ni sahihi hicho kinachoanza kuanza kabla ya mwenzake? kama ndio ni kwa sababu gani na kama sio ni kwa sababu gani?
Wewe haki sawa inaonekana una uelewa mzuri kweli na unaweza kutoa elimu nzuri sana kwa maslahi ya watu wengi.Hebu fafanua kidogo.
mkuu sikuelewi unajadili nini hasa! ngoja mimi nikuache sasa pengine wadau wenzangu watakuwa wanakuelewa unajadili nini.kwenye ye uzi nimekutumia tayari wamebadilisha ile original version na huu ndio ujanja ujanja wa ACT unapoonekana ....uzuri nilishaucopy Uzi original .....aibu yenu enyi wajanja wajanja .....
1. Ndugu yangu; umesoma mada vizuri na kuielewa kabla ya kuchangia? Hebu kama huna uhakika juu ya hili soma tena na tena.
2.Kwenye mjadala huu, kuna mahali katajwa zitto? kama sio, wewe zitto unamuingiza je hapa?
3. Zitto ni mwanachama wa chama gani na wewe umejua je?na unaweza kuleta ushahidi wa uanachama wake?
4.Ujuavyo wewe; chama cha siasa ni nini?
5. Unafiki ni nini na ni kwa vipi ACT-Tanzania ni chama cha wanafiki (vielelezo vya uthibitisho vitakuwa na nguvu zaidi) na ni kivivi hii inahusiana na mada ilioko mbele yetu?
6. Mamluki ni watu wa namna gani na ni vipi ACT-Tanzania ni chama cha mamluki na wewe umejua je!na hili linahusiana vipi na mada iliyopo mbele yetu?
7. Ufisadi ni nini na ACT-Tanzania wamefisidi nini na ushahidi wako ni nini?
Mkuu nimekuuliza maswali mengi sana na bado nilikuwa natamani kukuhoji zaidi ila ngoja tu niishie hapo kwanza.Unaweza kujibu yote, baadhi, moja au ukaayaacha yote kama utaona hayakufai.Ndio demokrasia hiyo ndugu yangu!
7
Kwani kwa sasa ujuavyo wewe ; kwa sasa viongozi wa ACT-Tanzania ni akina nani? Ujuavyo wewe, mtu akkifukuzwa au kutoka chadema kimsingi ni msaliti wa nchi?Kwani usaliti ni nini? Katika mchango wako ulioutoa hapa; unachotaka kutuambia ni kwamba kwa mujibu wa uzi; ACT-Tanzania wana challenges lakini hawana opportunities!? au unataka kusema nini maana nimepitia mchango wako najaribu kuuoanisha na mada ni kama mimi sijaona muunganiko na mada yenyewe! au hujaelewa mada?Unaposema kama watu wake watakuwa waadilifu, hivi hujui kuwa viongozi wa ACT ni walewale wasaliti wa taifa wanaotumiwa na ccm kukwamisha harakati za wananchi kujikomboa kutoka mikononi mwa mafisadi ccm, namaanisha walisati waliasi Chadema ambao ni Zitto kabwe, Dr asiyejielewa Kitila Mkumbo, Samsoni Mwigamba, na vidudu mtu vingine ambavyo vilifukuzwa kitambo kwa usaliti, fedha wanazotumia ni kodi zetu wanazoiba mafisadi ambazo zingetumika kwenye maendeleo, siku zote wanaopita katika maovu hawafanikiwi kamwe, kwani wafanyayo ni laana mbele za Mungu.
1. Kwani kaka uzandiki ni nini na maswali yangu yanakuwa ya kizandiki kivipi? Je! ni maswali yote saba ni ya kizandiki? kama sio nijubu basi angalau hata mawili ambayo si ya kizandiki ila kama yote saba ya kizandiki; basi no comment!Mkuu sitohangaika na maswali ya kizandiki ila ipo wazi huwezi kitenganisha ACT na Zitto,Kitila na Mwigamba!! Mwanzo wote walikana n'a kuapa ni CHADEMA ila leo Mwigamba na Kitila rasmi ni ACT n'a wamesema watamualika Zitto agombee uenyekiti na Zitto hajawahi kukana kuhusishwa n'a ACT zaidi anasema subiri kesi iishe!!
!
Ambapo hiyo ni challenge au oppurtunity?Chama kinachomsubiri MTU mpaka amalize ubunge wake?
Unaposema kama watu wake watakuwa waadilifu, hivi hujui kuwa viongozi wa ACT ni walewale wasaliti wa taifa wanaotumiwa na ccm kukwamisha harakati za wananchi kujikomboa kutoka mikononi mwa mafisadi ccm, namaanisha walisati waliasi Chadema ambao ni Zitto kabwe, Dr asiyejielewa Kitila Mkumbo, Samsoni Mwigamba, na vidudu mtu vingine ambavyo vilifukuzwa kitambo kwa usaliti, fedha wanazotumia ni kodi zetu wanazoiba mafisadi ambazo zingetumika kwenye maendeleo, siku zote wanaopita katika maovu hawafanikiwi kamwe, kwani wafanyayo ni laana mbele za Mungu.
ni kweli mkuu; ukiona mtu anakosea na ukamsahihisha unakuwa umeufahamu wajibu wako na kuutekeleza.yaani kuna comment nyingine kuicha kama ilivyo itakua jf haijakusaidia we mchangiaji ......,...,.hebu nikuulize kitu 1 ivi chadema ni taifa?