Abiria tunaovuka Kivuko cha Kigamboni leo ni kero tupu, kivuko kimoja tu ndio kinafanya kazi

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Leo Novemba 28, 2023 sisi Wakazi hasa wa Kigamboni tumepata changamoto ya Kivuko.

Yaani leo kivuko kinachofanya kazi ni MV Kazi tu, kingine wanasema ni kibovu, watu wanachelewa makazini, Azam ameleta kivuko kidogo kimoja nacho ni kama kinazidiwa kutokana na idadi ya watu wanaohitaji kuvuka.

Najiuliza kwa nini wasimruhusu Azam aweke vyote viwili kisha MV Kazi ipakie magari tu?

Hali hii ikiendelea hivi, ikifika jioni tutakaokuwa tunavuka kutoka Kivukoni kwenda Kigamboni hapo ndipo shughuli itakuwa kubwa.

Changamoto kama hizi zimekuwepo kwa muda mrefu tangu kuanza kwa mwaka huu, ile pantoni nyingine ikienda kwenye matengenezo kunakuwa na usumbufu mkubwa, foleni za magari zinakuwa ndefu, kwa ufupi ni kero juu ya kero.
 
Leo Novemba 28, 2023 sisi Wakazi hasa wa Kigamboni tumepata changamoto ya Kivuko.

Yaani leo kivuko kinachofanya kazi ni MV Kazi tu, kingine wanasema ni kibovu, watu wanachelewa makazini, Azam ameleta kivuko kidogo kimoja nacho ni kama kinazidiwa kutokana na idadi ya watu wanaohitaji kuvuka.

Najiuliza kwa nini wasimruhusu Azam aweke vyote viwili kisha MV Kazi ipakie magari tu?

Hali hii ikiendelea hivi, ikifika jioni tutakaokuwa tunavuka kutoka Kivukoni kwenda Kigamboni hapo ndipo shughuli itakuwa kubwa.

Changamoto kama hizi zimekuwepo kwa muda mrefu tangu kuanza kwa mwaka huu, ile pantoni nyingine ikienda kwenye matengenezo kunakuwa na usumbufu mkubwa, foleni za magari zinakuwa ndefu, kwa ufupi ni kero juu ya kero.
Nawashauri wakazi wenzangu wa Kigamboni tutumie njia ya darajani ili kuepuka usumbufu huu
 
Kama unajua unataka kwenda na muda mara zote pita njia ya darajani sio huko lazima ukwame kidogo
 
CCM hakuna wanachoweza, kuanzia UMEME, MWENDOKASI hadi KIVUKO... yaani miaka yote wameshindwa kuja na SULUHU ya kudumu pale? ... mnashindwa nini kuipa SEKTA BINAFSI?... mna maslahi na ile hali pale?
 
Back
Top Bottom