Moshi25
JF-Expert Member
- May 6, 2022
- 1,803
- 2,890
Huwa naona watu ni wengi sana asubuhi saa 12 hadi saa 3 wakiwa tayari kuvuka kutoka Kigamboni kuja Ferry na Mv Magogoni ikijaza magari tu na watu wengi kubaki wakiwa wamefungiwa kama kuku kusubiri kivuko kiende na kurudi ndo kiwachukue, wagonjwa wanachelewa hospitali na wafanyakazi wanachelewa kazini na wanafunzi wanachelewa shuleni
Nashauri asubuhi MV Magogoni ibebe abiria tu na MV Kigamboni ibebe magari tu
Namuomba Bakhresa atuletee kivuko kipya saizi ya Mv Magogoni kiwe cha kubeba abiria tu bila magari. Hizi Sea Taxi hazitoshi Kigamboni kuna watu wengi sana kwasasa vivuko havitoshi
Enzi kama hizi eti bado tunaishi kizamani watu wazima na madevu yao kukimbilia kivuko na kuanguka kwa utelezi ni aibu sana kwa nchi yetu!
Nashauri asubuhi MV Magogoni ibebe abiria tu na MV Kigamboni ibebe magari tu
Namuomba Bakhresa atuletee kivuko kipya saizi ya Mv Magogoni kiwe cha kubeba abiria tu bila magari. Hizi Sea Taxi hazitoshi Kigamboni kuna watu wengi sana kwasasa vivuko havitoshi
Enzi kama hizi eti bado tunaishi kizamani watu wazima na madevu yao kukimbilia kivuko na kuanguka kwa utelezi ni aibu sana kwa nchi yetu!