A Million Dollar Question...

A Million Dollar Question...

Hili shitaka la sumu limeingizwaje au DAWA YA USINGIZI imekuwa sumu? Tena Lwakatare amesisitiza kabisa kwamba hiyo dawa ni zile zinazotumiwa na "malaya" na huwa fahamu zinarudi baada ya masaa 3. Asiteswe wala kuuliwa lest there will be public sympathy

Vijana wa chadema wanafikiri hili ni swala la kishabiki kama hadithi za masalia. Hii iko mikononi mwa vyombo vya dola na jamaa wakifanya mchezo jamaa anaenda na chama kwa sababu chama kimeshajitoa muhanga kumtetea kabla hata hakijajua anashitakiwa kwa makosa gani!!!
 
Wewe nae ni limbukeni tu, mbona suala la sumu limetajwa kwenye video clip hiyo hiyo? Yaani maana yake una post kitu ambacho hata haujakithibitisha au haujakisoma na kukisikiliza kwa kina. Tafuta ile video clip urudie kuisikiliza kwa makini. Ushabiki mwingine mbaya sana, najua mmefurahi sana ccm kwa sababu mnahisi kuwa hii single itahit sana, lakini ngoma ikivuma sana mwishowe hupasuka....jitahidini sana, maana hii ndiyo karata yenu ya mwisho, lakini nawahakikishia, mwisho mtashindwa kwa sababu hakuna muanzisha vita vya uonezi ambaye huwa anashinda vita hiyo, tutawashinda tu, no matter how long will it take!!!

Unayajua makosa manne aliyoshitakiwa Lwakatare leo Kisutu?
Kama hujui uliza uambiwe...
 
Kama lengo ni kuhabarisha matukio ya kigaidi ili Jeshi la polisi na Serikali lichukue hatua nadhani yote haya ni muhimu kuwepo hapa. Hii ni Serikali ya CCM ambayo inatuhumiwa. Nasubiri Jeshi la Polisi lije kuchukua ushahidi huu.

Serikali ya CCM ndio iliyofikishwa leo Kisutu kwa shitaka la kutoa sumu ya kudhuru binadamu?
 
this is not a one million dollar question...

ulichofanya ni kuunga-unga tu ya wenzako
 
Jiulize kwanin Kova alikimbilia kusema kukamatwa kwa Lwakatare hakuhusiani na chama?

Kova alisema haihusiani na chama lakini dr. Slaa akasisitiza kuwa inahusiana na chama. Kwahiyo lolote atakalokutwa nalo Lwakatare ni la chadema sio lake peke yake. Chadema ilikuwa na fursa ya kumkana Lwakatare lakini ikamkumbatia kwa hiyo suicide bomb aliyovaa hawezi kuiepuka...
 
this is not a one million dollar question...

ulichofanya ni kuunga-unga tu ya wenzako

A Million Dollar Question ni iwapo kijana Ben Saanane aliyewahi kutajwa kutumiwa na chadema kutegeshea watu sumu atatajwa tena kwenye kesi hii. This is very original, hakuna kuunga unga hapo...
 
Vijana wa chadema wanafikiri hili ni swala la kishabiki kama hadithi za masalia. Hii iko mikononi mwa vyombo vya dola na jamaa wakifanya mchezo jamaa anaenda na chama kwa sababu chama kimeshajitoa muhanga kumtetea kabla hata hakijajua anashitakiwa kwa makosa gani!!!

Mimi ni CHADEMA damdam ndo maana nimeuliza haya mambo ya sumu yametoka wapi. Nimetazama definition ya poison. Sidhani kama dawa ya usingizi inafit description ya poison. Labda kama wanania ya kuyaibua na yasiyohusiana na ile footage
 
Ludovick na Lwakatare wote ni washtakiwa. Wanashtakiwa kuwa wameconive.
Kuna mmoja anayekufahamu kwa ID yako amesema unawasiwasi kwamba utatajwa kuhusika kuandaa njama na Makama January,Wassira Zoka,Inghondu,Mwiguru,Nape na Ridhiwani sijui kwa nini anasema Kundi lenu la kimafia limemea mizizi lakini an hisi litakuja kumwngusha Kikwete vibaya atamaliza vibaya sana kama unataka nikupe mengi ni PM
 
Mimi ni CHADEMA damdam ndo maana nimeuliza haya mambo ya sumu yametoka wapi. Nimetazama definition ya poison. Sidhani kama dawa ya usingizi inafit description ya poison. Labda kama wanania ya kuyaibua na yasiyohusiana na ile footage

Mkuu hapo nadhani kuna kitu umechanganya.
ile ya video ni kosa jingine na hii ya kutoa sumu ni kose jingine.

Hii sumu haina uhusiano wowte na ile video. Hii ina ushahidi wake mwingine, na hili walilifanya Kinondoni (wanashutumiwa)

Subiri magazeti ya kesho utapata taarifa kamili ya makosa manne aliyoshitakiwa Lwakatare.
 
A Million Dollar Question ni iwapo kijana Ben Saanane aliyewahi kutajwa kutumiwa na chadema kutegeshea watu sumu atatajwa tena kwenye kesi hii. This is very original, hakuna kuunga unga hapo...

Kuna jirani yangu hapa pembeni anasema unasound Kama Prezzo yule aliyetajwa na kijana Ben kwamba eti ni Zitto ,anatuambia hapa vijana anasema angalia mtiririko wa maneno yako eti unajidefend kwa sababu mitaani tayari habari ya Lwakatare kutaka kumpa sumu Msacky wengi wanasema ni game la Zitto ambalo nasikia wanasheria wa Lwakatare watahakikisha mahakamani anaitwa
 
Kama lengo ni kuhabarisha matukio ya kigaidi ili Jeshi la polisi na Serikali lichukue hatua nadhani yote haya ni muhimu kuwepo hapa. Hii ni Serikali ya CCM ambayo inatuhumiwa. Nasubiri Jeshi la Polisi lije kuchukua ushahidi huu.

NAIBU Waziri wa Ujenzi anayeugua ugonjwa uliozusha utata mkubwa serikalini, Dk. Harrison Mwakyembe, ameandika waraka mahususi unaoeleza kile anachokiamini kuwa ni chanzo cha ugonjwa wake, Tanzania Daima Jumatano limebaini.

Waraka huo ambao gazeti hili limeuona mbali ya kueleza kile ambacho Mwakyembe mwenyewe anaamini kuwa ni chanzo cha ugonjwa wake, unaeleza pia jinsi alivyoanza kuugua, watu anaowashuku kuwa nyuma ya mpango huo, siku na tarehe aliyodhani kuwa ndiyo aliyowekewa sumu hiyo.

Kama hiyo haitoshi, Mwakyembe katika waraka wake huo pasipo kueleza chanzo halisi cha undani wa taarifa zake, anaeleza mbinu iliyotumika kumdhuru na mahala mpango huo wa kumdhuru ulipopangwa.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kwamba Dk. Mwakyembe ambaye kwa sasa yuko nchini India ameusambaza waraka huo kwa ndugu, jamaa na marafiki zake wa karibu.
Katika waraka huo, Dk. Mwakyembe anaeleza kwamba anaamini alipewa sumu hiyo akiwa ofisini kwake huku akitaja majina ya watu anaowatuhumu kuwa nyuma ya mpango huo ambao gazeti hili kwa sasa linahifadhi majina yao.

Kwa mujibu wa Dk. Mwakyembe, mara tu baada ya kuwekewa sumu hiyo alianza kuwashwa mwili kabla ya hali kuendelea kuzorota na kuwa mbaya.

Akionekana kujibu hoja za Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, mwanasiasa huyo katika waraka wake anaeleza kwamba hakuwekewa sumu hiyo kwenye chakula, bali kwenye sabuni na kitaulo cha kujifutia, ambacho huwekwa kwenye chumba maalumu ofisini kwake kwa ajili ya kusafisha mikono na huduma nyingine awapo ofisini.

Vyanzo vyetu vya habari kutoka kwa ndugu na marafiki wa karibu wa Dk. Mwakyembe vilisema kuwa, naibu waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela, amefikia hatua ya kuandika waraka huo kwa lengo la kutaka kuijulisha familia yake na taifa kile anachoamini anakabiliana nacho endapo atapoteza maisha kabla ya ukweli kamili kubainishwa.
Hata hivyo, kutokana na ukweli kwamba suala hilo la afya ya Dk. Mwakyembe liko katika hatua za uchunguzi, Tanzania Daima Jumatano haliwezi kuandika kwa undani kuhusu waraka huo kwa sasa.

Ukiacha hilo, Dk. Mwakyembe katika waraka huo ameelezea historia ya maisha yake kisiasa na mikasa iliyompata kiasi cha kujijengea maadui.
Ameeleza jinsi alivyonusurika kuuawa mara kadhaa na kwamba taarifa zote za mikasa yake aliziripoti polisi, lakini hakuna hatua zilizochukuliwa na Jeshi hilo la Polisi.
Baadhi ya mikasa aliyoitaja kwenye waraka huo ni pamoja na tukio la kunusurika kuuawa kwenye ajali ya gari iliyotokea Mei 21, mwaka 2009. Ajali hiyo ilitokea eneo la Ihemi, kilomita 40 kutoka Iringa mjini akiwa safarini kutokea Mbeya kwenda Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa waraka huo, gari alilokuwa akisafiria aina ya Toyota Land Cruiser T 362 ACH, liliacha njia saa moja asubuhi baada ya kukanyaga shimo na tairi ya upande wa kulia kuchomoka na dereva wake, Joseph Msuya (30), kupoteza mwelekeo kabla ya gari hilo kutoka nje ya barabara upande wa kushoto na kuparamia mti kisha kupinduka.
Ajali hiyo ilitokea wakati dereva wa Dk. Mwakyembe akijaribu kulipita lori kabla ya kukanyaga shimo hilo.
Anasema katika ajali hiyo aliokolewa na wasamaria wema pamoja na trafiki wawili waliokuwa kwenye basi dogo waliokuwa wakisafiri kutoka Iringa kwenda Njombe.
Anasema katika waraka huo kuwa, baada ya ajali hiyo alilazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Iringa kutokana na kuumia taya kisha alihamishiwa Dar es Salaam kwa matibabu zaidi.
Kwa mujibu wa waraka huo, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema, aliunda tume iliyoongozwa na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani wakati huo, Kamanda James Kombe, kuchunguza chanzo cha ajali hiyo.
Matokeo yalionesha kwamba ilisababishwa na uzembe wa dereva wake, Msuya wakati Dk. Mwakyembe akiamini kwamba ajali hiyo ilipangwa.
Februari 9, mwaka 2011, Dk. Mwakyembe aliandika barua kwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Said Mwema, akimpa taarifa juu ya kuwapo kwa njama za kutaka kumuua yeye pamoja na viongozi wengine.
Wengine aliowataja katika barua hiyo ni pamoja na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela.
Katika orodha hiyo ya Mwakyembe kwa IGP, hadi sasa kiongozi mwingine ambaye anaumwa ni Profesa Mark Mwandosya.
Wizara tatu zakorogana
Katika hatua nyingine, mwendelezo wa mjadala kuhusu ugonjwa unaomsumbua Dk. Mwakyembe unaonekena kuzikoroga wizara tatu za serikali ya Rais Jakaya Kikwete.
Mkorogano huo unajitokeza katika Wizara ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Afya na ile ya Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Duru za siasa zinahoji umakini wa serikali kutokana na kushindwa kwake kuwa na kauli ya pamoja iliyofanyiwa utafiti wa kutosha.
Kwa nyakati tofauti, Wizara ya Mambo ya Ndani, kupitia kwa Waziri wake, Shamsi Vuai Nahodha na baadaye kwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, imetoa taarifa iliyoibua mjadala.
Wakati Manumba akikaririwa akisema uchunguzi uliofanywa na Jeshi la Polisi ikiwa ni pamoja na kupata ripoti ya kitabibu kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, umebaini kwamba Dk. Mwakyembe hajalishwa sumu.
Siku mbili baada ya kauli hiyo ya Manumba, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Haji Mponda, alimshangaa Manumba alikopata ripoti hiyo.
Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC), Waziri wake mwenye dhamana, Samuel Sitta, anasisitiza Dk. Mwakyembe amelishwa sumu.
Wachambuzi wa mambo wanasema kuwa mgogoro na ukinzani uliojitokeza katika wizara hizo tatu, umeziondolea imani kwa wananchi.
Ingawa taarifa za ndani kutoka Jeshi la Polisi zinaonyesha kuwa kulikuwa na mawasiliano kati ya Wizara ya Mambo ya Ndani na Wizara ya Afya kama ambavyo Manumba alisema.
Lakini pia taarifa hizo zinaeleza kuwa Manumba alikurupuka.
Ingawa kilichosababisha hasa ugonjwa wa Mwakyembe bado hakijabainika kutokana na kauli yake mwenyewe kuwa madaktari wanaomtibu katika Hospitali ya Apollo nchini India, bado wanahangaika kujua kitu kilichoko kwenye uboho (bone marrow) kinachochochea hali ya maradhi yake.


[TD="bgcolor: #ffffff"]
Dk. Mwakyembe sasa aandika waraka wa siri

Ausambaza kwa ndugu, jamaa na marafiki zake wa karibu
Na Mwandishi wetu


[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #ffffff"] [/TD]


 
Kuna jirani yangu hapa pembeni anasema unasound Kama Prezzo yule aliyetajwa na kijana Ben kwamba eti ni Zitto ,anatuambia hapa vijana anasema angalia mtiririko wa maneno yako eti unajidefend kwa sababu mitaani tayari habari ya Lwakatare kutaka kumpa sumu Msacky wengi wanasema ni game la Zitto ambalo nasikia wanasheria wa Lwakatare watahakikisha mahakamani anaitwa

Achana na porojo za mitaani, tujadili kilichojiri mahakamani leo ili kupata jibu la Million Dollar Question...
 
Mkuu hapo nadhani kuna kitu umechanganya.
ile ya video ni kosa jingine na hii ya kutoa sumu ni kose jingine.

Hii sumu haina uhusiano wowte na ile video. Hii ina ushahidi wake mwingine, na hili walilifanya Kinondoni (wanashutumiwa)

Subiri magazeti ya kesho utapata taarifa kamili ya makosa manne aliyoshitakiwa Lwakatare.
Wapelelezi wa JF wamegundua eti kuwa wewe unaujua mchoro mzima ,chama kinajua unavyojishughulisha ,wananchi wanajua na dunia itajua karibuni tuu ,kwa sababu mchana ulikuja jamvini ukieleza kusikia uchache wa wafuasi wa chadema mahakamani lakini ITV ikakuumbua
 
Achana na porojo za mitaani, tujadili kilichojiri mahakamani leo ili kupata jibu la Million Dollar Question...

unaishi mbinguni tuko mitaanibaada ya taarifa ya habari ya ITV saa mbili kijiwe kimechangamka watu wote wanasema lazima Zitto awe anajua nadhani ni hilo la urafiki na msacky na Zitto kudai anatishwa kuuliwa na wenzake nadhani wanasema ni wakati mzuri wanasheria wa Lwakatare wamuite mahakamani kama shaidi athibitishe sumu anazotishiwa
 

[TD="bgcolor: #ffffff"]
Dk. Mwakyembe sasa aandika waraka wa siri

Ausambaza kwa ndugu, jamaa na marafiki zake wa karibu
Na Mwandishi wetu
[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #ffffff"][/TD]


Tafadhali jitahidi kuzungumzia topic ya thread. Hizi nyingine itakuwa vizuri iwapo utazifungulia thread zake. Ninaamini unatambua kuwa unachokifanya ni kinyume na sheria za JF na unafahamu kuwa JF huwa ina uaratibu wake wa adhabu.

Tunaheshimu mchango wa kila mmoja, lakini tusipindishe mijadala kwa makusudi. KUfanya hivyo ni kutokulitendea haki neno "great thinkers" na kuwaongezea mzigo wa kazi MODs...
 
unaishi mbinguni tuko mitaanibaada ya taarifa ya habari ya ITV saa mbili kijiwe kimechangamka watu wote wanasema lazima Zitto awe anajua nadhani ni hilo la urafiki na msacky na Zitto kudai anatishwa kuuliwa na wenzake nadhani wanasema ni wakati mzuri wanasheria wa Lwakatare wamuite mahakamani kama shaidi athibitishe sumu anazotishiwa

Ya Zitto hayanihusu. Atayajibu mwenyewe akitoka JKT. Kule hakuna regular access to JF.
 
Unasema hii ishu ni nyepesi wakati ishu hii imehatarisha maisha ya binadamu mpaka kiongozi akaahidi kuangamizi mpaka panya wote katika nyumba ya mhusika.

Matumizi ya sumu ya kudhuru binaadamu kwenye siasa ni jambo jepesi only to an oligophrenic.

Najua wewe ni mchumia tumbo.
Ni kama ki changu kinachojipendekeza walau mkono uende Kinywan.
Kawaambie Mabwana zako kuwa huku kugumu mnoo.
Watu chuki yetu Juu ya CCM ime triple.
Yaan mabwana zako walicho expect kimekuwa Kinyume.
 
Najua wewe ni mchumia tumbo.
Ni kama ki changu kinachojipendekeza walau mkono uende Kinywan.
Kawaambie Mabwana zako kuwa huku kugumu mnoo.
Watu chuki yetu Juu ya CCM ime triple.
Yaan mabwana zako walicho expect kimekuwa Kinyume.

Wewe ndio walewale...
 
Back
Top Bottom