GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Mishahara lazima iendane na uwezo wa Ukuaji wa uchumi, Ofisi za serikali zimejaa uvivu, story, nyodo muda wa kazi, Lunch masaa mawili, Pesa kubwa mnazotaka wakati hamtoi huduma bora kwa wakulima na wafanyabiashara zitatoka wapi?
Nyongeza ya mshahara aliyoitoa Samia mwaka huu inabidi mshukuru sana, Tunaoenda kuumia na kulipia hiyo gharama ni sisi wafanyabiashara na wakulima, Zigo la kodi kulipia hiyo nyongeza ni kubwa sana, Ni zaidi ya mabilioni yameongezeka kwenye bili ya mshahara kwa serikali, Zigo linahamishiwa kwenye kodi ya sisi wakulima na wafanyabiashara ili tulipie gharama hiyo ya nyongeza ya mishahara
Kada ya utumishi wa serikali inaongoza kwa kuwapotezea muda wakulima na wafanyabiashara wafikapo kufuata huduma, Wafanyakazi wa serikali hamjali muda mnaotupotezea muda, Tutazalisha saa ngapi ili kodi ipatikane na Nyie mnufaike?
Wafanyakazi wa Serikali mlipoambiwa Fedha za ndani zinajenga nchi,mlifikiri zinatoka wapi? Ni sisi wafanyabiashara na wakulima tulibanwa koo kwa kabali kisawa sawa kwa kulipishwa kodi kuwezesha miradi ya barabara, Flyovers na vituo vya afya
Mtu anasema nyongeza ni ndogo, Unataka nyongeza kubwa kwa kazi gani ya maana unayofanya Jumatatu mpaka Ijumaa ofisini, Ofisi nyingi za serikali siku ya ijumaa ni kama haipo, Watu wanaunganisha ile muda wa kuswali ijumaa moja kwa moja nyumbani
Unataka pesa kubwa kwa masaa mangapi unayozalisha?
Unataka pesa kubwa kwa huduma gani bora unayatoa kwa wakulima na wafanyabiashara?
Ukiondoa kada ya Afya na ulinzi wa nchi na Raia, Wafanyakazi wa taasisi za serikali wamejaa nyodo, dharau na uvivu hasa akina Dada pale unapofika kuuliza huduma
Wengi ya wafanyakazi wa serikali wana uelewa mdogo sana bado hawajaelimishwa kuwa mishahara yao ni kodi za sisi wafanyabiashara na wakulima ukijumlisha na kodi toka wafanyakazi wa sekta binafsi
Ukifika ofisi za NSSF au Psssf kwa wazee wanaofuatilia mafao yao, Majibu ya wale akina Dada vijana na wale watoto wa kiume kwa wazee yamejaa dharau sana, Wanasahau kuwa bila kodi za wananchi wasingekuwa pale
Kwa miaka mitano iliyopita wafanyabiashara tumepigwa kodi za kutosha kuhudumia Flyover na mabarabara, Tumeumia kujenga shule na hospitali za kata
Je wafanyakazi mlipoambiwa Fedha za ndani mlijua zinatoka wapi? na ni nani analipa hizo kodi?
Ni muda muafaka wa wafanyakazi wa serikali kuelimishwa kuwa pesa za mishahara sio mikopo bali ni kodi za wakulima na wafanyabiashara
Hakuna Taifa linalolipa mishahara kwa pesa za mikopo, Bili ya mishahara kwa mwezi ni kodi zinazokusanywa toka kwa wakulima na wafanyabiashara
Mambo yafuatayo yasipokoma au kubadilika maofisini ni ngumu sana sisi wakulima na wafanyabiashara kuweza kugharamia nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa serikali
1. Uvivu na dharau, Kuchart na simu huku unatusikiliza kwa sikio moja, Baada ya Kuchart utasikia ulikuwa unasema nini vile au Wewe Bibi, Mzee tuliishia wapi, Hapo muda wa zaidi ya saa moja la kuzalisha limepotea na Biashara yako Umefunga kwa muda huo
2. Lunch masaa zaidi ya moja, Bado mtu amerudi lunch anapiga umbea huku akiendeleza kula mezani masalia ya chakula yaliyobaki na kuyafungasha toka canteen au kwenye mgahawa, Hapo muda wa kuzalisha ulishapoteza
3. Habari za njoo kesho au njoo baada ya week mbili, Huwezi endesha biashara yako hapo unasubiri kibali cha manispaa au Halmashauri kwa siku mbili, Hakuna uzalishaji
4. Bosi amesafiri hakuna wa kuweka saini, Hapa unakuta ni saini ya mtu mmoja tu wa Mazingira ili kuruhusu biashara iendelee lakini utasubiri mwezi na kusimamisha uzalishaji wa biashara yako
5. Kaa pale Subiri wameenda kula, Tuna semina uje kesho, Hiyo ni semina isiyo na kikomo ambayo hawamuachi hata mtu mmoja wa kusaidia wafanyabiashara na wakulima
6. Faili lako halionekani, Tunatafuta tutakupigia simu, Hiyo ujue ndio kimoja, Ni Jibu wanalotoa ili uondoke ofisini waendelee na soga na umbea wa mitaani bila kujua tayari wamepoteza kodi ya serikali
Kwa staili kama hizi, Tutazalisha muda gani? Mapato yataongezeka kutoka wapi? Muda wa kuzalisha watu wanakupiga kalenda na danadana, Siku ya Mei mosi unasikia tunataka nyongeza Kubwa, Nyongeza toka kwa kodi ya nani?
Nyongeza ya mshahara aliyoitoa Samia mwaka huu inabidi mshukuru sana, Tunaoenda kuumia na kulipia hiyo gharama ni sisi wafanyabiashara na wakulima, Zigo la kodi kulipia hiyo nyongeza ni kubwa sana, Ni zaidi ya mabilioni yameongezeka kwenye bili ya mshahara kwa serikali, Zigo linahamishiwa kwenye kodi ya sisi wakulima na wafanyabiashara ili tulipie gharama hiyo ya nyongeza ya mishahara
Kada ya utumishi wa serikali inaongoza kwa kuwapotezea muda wakulima na wafanyabiashara wafikapo kufuata huduma, Wafanyakazi wa serikali hamjali muda mnaotupotezea muda, Tutazalisha saa ngapi ili kodi ipatikane na Nyie mnufaike?
Wafanyakazi wa Serikali mlipoambiwa Fedha za ndani zinajenga nchi,mlifikiri zinatoka wapi? Ni sisi wafanyabiashara na wakulima tulibanwa koo kwa kabali kisawa sawa kwa kulipishwa kodi kuwezesha miradi ya barabara, Flyovers na vituo vya afya
Mtu anasema nyongeza ni ndogo, Unataka nyongeza kubwa kwa kazi gani ya maana unayofanya Jumatatu mpaka Ijumaa ofisini, Ofisi nyingi za serikali siku ya ijumaa ni kama haipo, Watu wanaunganisha ile muda wa kuswali ijumaa moja kwa moja nyumbani
Unataka pesa kubwa kwa masaa mangapi unayozalisha?
Unataka pesa kubwa kwa huduma gani bora unayatoa kwa wakulima na wafanyabiashara?
Ukiondoa kada ya Afya na ulinzi wa nchi na Raia, Wafanyakazi wa taasisi za serikali wamejaa nyodo, dharau na uvivu hasa akina Dada pale unapofika kuuliza huduma
Wengi ya wafanyakazi wa serikali wana uelewa mdogo sana bado hawajaelimishwa kuwa mishahara yao ni kodi za sisi wafanyabiashara na wakulima ukijumlisha na kodi toka wafanyakazi wa sekta binafsi
Ukifika ofisi za NSSF au Psssf kwa wazee wanaofuatilia mafao yao, Majibu ya wale akina Dada vijana na wale watoto wa kiume kwa wazee yamejaa dharau sana, Wanasahau kuwa bila kodi za wananchi wasingekuwa pale
Kwa miaka mitano iliyopita wafanyabiashara tumepigwa kodi za kutosha kuhudumia Flyover na mabarabara, Tumeumia kujenga shule na hospitali za kata
Je wafanyakazi mlipoambiwa Fedha za ndani mlijua zinatoka wapi? na ni nani analipa hizo kodi?
Ni muda muafaka wa wafanyakazi wa serikali kuelimishwa kuwa pesa za mishahara sio mikopo bali ni kodi za wakulima na wafanyabiashara
Hakuna Taifa linalolipa mishahara kwa pesa za mikopo, Bili ya mishahara kwa mwezi ni kodi zinazokusanywa toka kwa wakulima na wafanyabiashara
Mambo yafuatayo yasipokoma au kubadilika maofisini ni ngumu sana sisi wakulima na wafanyabiashara kuweza kugharamia nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa serikali
1. Uvivu na dharau, Kuchart na simu huku unatusikiliza kwa sikio moja, Baada ya Kuchart utasikia ulikuwa unasema nini vile au Wewe Bibi, Mzee tuliishia wapi, Hapo muda wa zaidi ya saa moja la kuzalisha limepotea na Biashara yako Umefunga kwa muda huo
2. Lunch masaa zaidi ya moja, Bado mtu amerudi lunch anapiga umbea huku akiendeleza kula mezani masalia ya chakula yaliyobaki na kuyafungasha toka canteen au kwenye mgahawa, Hapo muda wa kuzalisha ulishapoteza
3. Habari za njoo kesho au njoo baada ya week mbili, Huwezi endesha biashara yako hapo unasubiri kibali cha manispaa au Halmashauri kwa siku mbili, Hakuna uzalishaji
4. Bosi amesafiri hakuna wa kuweka saini, Hapa unakuta ni saini ya mtu mmoja tu wa Mazingira ili kuruhusu biashara iendelee lakini utasubiri mwezi na kusimamisha uzalishaji wa biashara yako
5. Kaa pale Subiri wameenda kula, Tuna semina uje kesho, Hiyo ni semina isiyo na kikomo ambayo hawamuachi hata mtu mmoja wa kusaidia wafanyabiashara na wakulima
6. Faili lako halionekani, Tunatafuta tutakupigia simu, Hiyo ujue ndio kimoja, Ni Jibu wanalotoa ili uondoke ofisini waendelee na soga na umbea wa mitaani bila kujua tayari wamepoteza kodi ya serikali
Kwa staili kama hizi, Tutazalisha muda gani? Mapato yataongezeka kutoka wapi? Muda wa kuzalisha watu wanakupiga kalenda na danadana, Siku ya Mei mosi unasikia tunataka nyongeza Kubwa, Nyongeza toka kwa kodi ya nani?