50% ya Watanzania wananuka midomo!!

Nyani Ngabu said:
Usafi wa kinywa Watu wengi umetupitia kushoto. Ni wachache sana kati yetu tunaokwangua ndimi zetu mara mbili kwa siku. Ni wangapi tunajua hata kama kuna tongue scrapers zilizo mahsusi kwa kazi hiyo tu?

Tongue scrapers ni muhimu sana katika kupigana na bad breath. Wale anaerobic bacteria wanaosababisha mdomo kunuka hujizalia sana kwenye ndimi hasa kwa sehemu ya nyuma kule karibu na koromeo. Sehemu ingine ambao hao bacteria wanapenda kujihifahi ni kwenye paa la kinywa (palate). Huko nako mtu unapaswa kupitisha mswaki.

Flossing. Idadi kubwa kati yetu hawajui flossing ni nini. Flossing husaidia sana katika kuondoa mabaki ya chakula yaliyonasa katikati ya meno. Sasa fikiria mtu anakula mchemsho, viepe, kitimoto, na vinginevyo halafu hakuna cha kufloss wala nini. Badala yake anatumia kijiti. Yale mabaki ya chakula yakikaa sana katikati ya meno huwa yanatoa harufu.

Na vile vijiti huwa havifikii sehemu nyingi tu za meno na hata huko zinakofika huwa havifanyi kazi sawa na nyuzi za flossing. Mtu ambaye hajawahi kufloss humu ndani na ajaribu siku moja aone jinsi ambavyo flossing ilivyo effective.

Mouthwash. Ni wachache sana tunaotumia mouthwash. Hizi nazo husaidia sana katika kuua harufu mbaya. Mtu ukishamaliza kuukwangua ulimi wako, ukishamaliza kufloss, ukishamaliza kusugua meno yako pamoja na paa la kinywa na fizi unasukutua na mouthwash kabla ya kusukutua na maji. Mtu ukizingatia na kufanya huo mchakato utakuwa umelipunguza tatizo la harufu mbaya kwa kiasi kikubwa sana.

Mwisho watu wengi hawajui kuwa kikubwa kisababishacho harufu mbaya mdomoni ni anaerobic bacteria. Hawa ni bacteria ambao hushamiri pasipo na oxygen ya kutosha. Sasa mdomo mara nyingi huwa unafungwa na hivyo kupelekea hao bacteria kujizalia na kushamiri.

Kwa hiyo hapo la msingi, baada ya kuzingatia yote hayo yahusuyo usafishaji ni muhimu pia kuuweka mdomo kuwa oxygenated mara kwa mara. Na hili linawezekana kwa kunywa maji throughout the day. Sisemi unywe maji kama ng'ombe. Just space out your water intake without long intervals in between and you'll be straight for the most part.

Hayo yote ukiongezea na routine teeth cleaning performed by a qualified dentist should do it in getting rid of bad breath.
What's wrong with that?

Flossing is highly effective in keeping your teeth clean and healthy by getting rid of food debris that gets stuck between your teeth especially in those hard to reach areas of your mouth/teeth.


Nyani Ngabu said:
Jaribu kwenda kwenye maduka makubwa makubwa ya dawa baridi uwaulizie. Kwenye haya maduka yetu mengine ya akina Mangi sidhani kama unaweza kuzipata hizo dental floss.
Unasema ukweli lakini umezungumza lugha ambayo ni nje kabisa ya mtanzania wa kawaida,ama watanzania walio wengi.

Uko very out of touch,ushauri wako ni mzuri lakini you really have forgotten where you come from.

Kwa wengi wa watanzania,yote uliyoyasema ni kama anasa kwao...

Sikubaliani na analysis yako moja kwa moja....

Maelezo uliyoyatoa hata hivyo hayata resonate na wabongo wengi...
 
Mkuu shukran,
Sijafuatilia posts zote kwenye mjadala huu,na pengine nime imiss hiyo shule ya NN...
Na ndiyo maana nilisema i stand to be corretected.

Kuna yanayosemwa humu ndani ambayo pia inabidi usiyameze mazima mazima.

Mnapozungumzia unukaji wa mdomo, mnazunguzmia nyakati gani za siku?

Certainly huwezi kuona kuwa kuna mtu anaweza asinuke mdomo asubuhi na badaye mchana akawa ananuka mdomo?

Hapana mkuu,

Tumeongea mambo mengi ambayo tunayajua nje ndani na pia mbinu ambazo tunazitumia kupambana na hili tatizo... Binafsi limenisumbua kwa muda hadi nilipoamua kuchukua hatua za makusudi...Ukienda page 1-4 utaona tuliyoyasema.

Suala la breakfast linaweza kuwa na ukweli kwa sababu kuacha mdomo muda mrefu bila kuufungua na kuingiza hewa ya Oxygen kunasababisha harufu mbaya kwa sababu kunatoa mazingira mazuri kwa bacteria wanaoishi mdomo kuzaliana haraka na kutoa gesi zenye kiwango kikubwa cha sulfa ambazo ndio chanzo cha harufu mbaya ya mdomoni!!
 
Ukila breakfast,inazuia ile harufu mbaya kutoka tumboni kuweza kutoka through mdomo...

So inawezekana pia ukapiga mswaki vyema tu na hizo dawa za meno lakini bado mdomo ukanuka!

Njaa ndo sababu kubwa,then Hygiene...

Again i stand to be corrected!

Mkuu njaa sio sababu kubwa, ni usafi wakawaida mkuu. Bacteria ndio wanaleta harufu mbaya kinywani kutokana na kutosafisha mdomo vizuri.mabaki ya chakula yanaoza mdomoni, did u know flossing is more important than brushing ur teeth? Sasa tujiulize wangapi wetu wana floss?
 
Hapana mkuu,

Tumeongea mambo mengi ambayo tunayajua nje ndani na pia mbinu ambazo tunazitumia kupambana na hili tatizo... Binafsi limenisumbua kwa muda hadi nilipoamua kuchukua hatua za makusudi...Ukienda page 1-4 utaona tuliyoyasema.

Suala la breakfast linaweza kuwa na ukweli kwa sababu kuacha mdomo muda mrefu bila kuufungua na kuingiza hewa ya Oxygen kunasababisha harufu mbaya kwa sababu kunatoa mazingira mazuri kwa bacteria wanaoishi mdomo kuzaliana haraka na kutoa gesi zenye kiwango kikubwa cha sulfa ambazo ndio chanzo cha harufu mbaya ya mdomoni!!

Naunga mkono mkuu maneno yako.
 
Mkuu njaa sio sababu kubwa, ni usafi wakawaida mkuu. Bacteria ndio wanaleta harufu mbaya kinywani kutokana na kutosafisha mdomo vizuri.mabaki ya chakula yanaoza mdomoni, did u know flossing is more important than brushing ur teeth? Sasa tujiulize wangapi wetu wana floss?

Ukiachana na kufloss ambao ni msamiati mgumu kwa watu wa kawaida...kuna mambo madogo madogo ambayo hayahitaji utaalamu mkubwa wala si gharama sana ila yanasaidia sana kupunguza tatizo la harufu mbaya mdomoni...Kupiga mswaki, kunywa maji mara kwa mara, kuhakikisha mdomo haufungwi kwa muda mrefu na kupunguza vyakuka vinavyowasaidia bacteria kuzaliana sana! Haya ni rahisi sana kufanyika...Na wenzio yametusaidia sana!

Ila kubwa zaidi ni kuwa na mwenza ambaye anakuwa wazi kukusaidia. Mathalani, kuna wakati (kama mtu una homa au stress) mtu unakuwa na harufu kali sana na bila kuambiwa unadunda sana mtaani.
 
Hapana mkuu,

Tumeongea mambo mengi ambayo tunayajua nje ndani na pia mbinu ambazo tunazitumia kupambana na hili tatizo... Binafsi limenisumbua kwa muda hadi nilipoamua kuchukua hatua za makusudi...Ukienda page 1-4 utaona tuliyoyasema.

Suala la breakfast linaweza kuwa na ukweli kwa sababu kuacha mdomo muda mrefu bila kuufungua na kuingiza hewa ya Oxygen kunasababisha harufu mbaya kwa sababu kunatoa mazingira mazuri kwa bacteria wanaoishi mdomo kuzaliana haraka na kutoa gesi zenye kiwango kikubwa cha sulfa ambazo ndio chanzo cha harufu mbaya ya mdomoni!!

Mkuu Dark City, nimekupata,

Ninachosema hapa,kuna sababu nyingi tu za mdomo kuweza kunuka,na mimi pia nimeangalia na jamii hiyo inayosemekana kuwa asilimia zaidi ya 50,wananuka midomo,sometimes tunajisahau huku mitandaoni,tunakuwa hatujadili issue base on reality nchini mwetu...

Ni ukweli usiopingika kuwa pumzi mbaya inaweza pia kusababishwa ie kama mtu amefunga (fasting). Ama hata kuwa na tumbo tupu kwa muda mrefu.

Katika ukosefu wa chakula, kuna kasoro ya kutolewa kwa juisi kwamba huanza kuvunja na pia ina athari juu ya bitana ya tumbo(lining of the stomach) ambapo hali hiyo inaweza kusababisha harufu chafu ambayo harufu kama chakula kilichooza!

Kufunga pia matokeo katika kupunguza katika mtiririko mate katika kinywa na kusababisha ukavu wa oral cavity, ambayo inaweza kusababisha harufu mbaya ya mdomo.

Sababu kubwa hapa ni due to the bacterial buildup inayotokea as the saliva is not present to swill out the bacteria from the surfaces of the teeth and the tongue...Hilo pamoja na kurise kwa digestive juices, huchangia odor emanating from the breath.

Wakati mtu anaendelea bila kula kwa muda mrefu, ukosefu wa chakula husababisha mwili huanza kubreak down fat reserves. Hii break down ya fat, in turn ketoni inakuwa released,hence bad breath.

Kwa kifupi,sikatai kuwa sababu zilizotolewa na NN kuwa ni sahihi, nianchozungumzia mimi,ni kwamba njaa pia inaweza kusababisha kunuka mdomo.

Sasa niambie ni asilimia ngapi ya wananchi wa Tanzania wana njaa?50% ama more?
 
Unasema ukweli lakini umezungumza lugha ambayo ni nje kabisa ya mtanzania wa kawaida,ama watanzania walio wengi.

Hapo nakubaliana na wewe.

Uko very out of touch,ushauri wako ni mzuri lakini you really have forgotten where you come from.

Quite the contrary Mangi. I am not out of touch as you think I am. I have never forgotten where I come from. As a matter of fact, if you need to know, I go back home twice a year. And I don't only end in Dar. I go all the way to Ikungu. Ask those in the know and they will tell you.

Kwa wengi wa watanzania,yote uliyoyasema ni kama anasa kwao...

Sasa hata kama kwa wengine ni anasa ndo tusiseme? Kuna wengine yako kabisa ndani ya uwezo wao lakini bado basic oral hygiene imewapiga chenga. Sasa tusiwape shule kama tuna ujuzi wa ku-share? Come on man...Nadhani wengi wanaokuja humu JF wako sophisticated enough kuelewa nilichoandika. Na wao wata share ufahamu walioupata hapa na wengine huko. Each one reach one and teach one.

Sikubaliani na analysis yako moja kwa moja....

No problem. Just enumerate the reasons as to why you disagree with me and we'll go head to head and toe to toe. I ain't never scared.

Maelezo uliyoyatoa hata hivyo hayata resonate na wabongo wengi...

Hata yaki resonate na wawili...the fact that they resonated with somebody is gratifying to me.
 
Kwa kuongezea;

Piga mswaki mchana baada ya kula chakula. Japo hili ni gumu kwa baadhi yetu lakini kwa wale wanaofanya kazi maofisini naamini linatekelezeka.

Pia utumiaji wa green tea unasaidia kupunguza harufu mbaya ya kinywa. Kula punje chache za bizari nyembamba (bizari nzima, uzile, cumin) baada ya chakula pia kunaweza kusaidia

Ulaji wa matunda na mboga mboga ni muhimu kwa afya ya kinywa chako kwa jumla

Note: ipo miswaki ambayo imekuwa packed vizuri kiasi na kufanana na lipstick au mascara ambayo wanawake wanaweza kutembea nayo kwenye handbags Kama wanavyotembea na vipodozi vyengine
 
TravelToothbrush_xl.jpg
These can be carried in the pocket, purse, or clutch.
 
Natumaini watu wakipita hapa watapata darasa la kutosha ila tatizo letu wabongo kusoma kitu ambacho kina maelezo marefu hata kama kina msaada ni ishu
 
Nina wasiwasi na dawa za meno tunazozitumia nyingi aziui vijidudu vinavysababisha kualibika kwa meno na baadae meno yaliyoaribika kutoa harufu mbaya,recommendetion from doctors ni colgate

Nilishapata habari za kuaminika kuwa kuna upinzani mkubwa kati wa madaktari wa meno, na watengenezaji wa dawa, viwango vinavyotakiwa na madaktari ili afya zetu ziwe nzuri, ni gharama hivyo watafuta namna na kupata sympathy wa watu wa viwango. kwa hiyo dawa nyingi za kibiashara hazikidhi matakwa ya madaktari, sio Tanzania tu ila sehemu nyingi,
 
Natumaini watu wakipita hapa watapata darasa la kutosha ila tatizo letu wabongo kusoma kitu ambacho kina maelezo marefu hata kama kina msaada ni ishu

It is very interestiing kwa faida yetu wenyewe lakini wabongo, hembu muoe mwita alivyojibu hapo juu....huyu jamaa anawakilisha some ideas ya wabongo, yeye kusoma insha hataki hata kama ina faida. Lol
 
Nilishapata habari za kuaminika kuwa kuna upinzani mkubwa kati wa madaktari wa meno, na watengenezaji wa dawa, viwango vinavyotakiwa na madaktari ili afya zetu ziwe nzuri, ni gharama hivyo watafuta namna na kupata sympathy wa watu wa viwango. kwa hiyo dawa nyingi za kibiashara hazikidhi matakwa ya madaktari, sio Tanzania tu ila sehemu nyingi,

Nakubaliana na wewe na ndio maana madktari wengi wanasisitiza matumizi ya colgate...lakini hata hizi Alove za kichina nina mashaka nazo sana.
 
Nyani Ngabu said:
No problem. Just enumerate the reasons as to why you disagree with me and we'll go head to head and toe to toe. I ain't never scared.
Nyani Ngabu,

Nisome vyema,sijakataa uliyosema.

Pia sijawahi kumaanisha kuku scare on anything mkuu.

Nilichosema mimi ni kuwa inategemea na hiyo sampling yao kwenye hiyo survey/utafiti wao.

Mimi nimechukulia factors nyingine ambazo zinaweza kuendana na hoja ya njaa kwa sababu unajuwa wananchi asilimia ngapi ni mlo mmoja kwa siku? Again, survey si msahafu.

Kabla hujazungumzia mambo ya kununua hiyo dawa ya meno,kuna ambao bado wanatumia miswaki ya vijiti...Kuna ambao kwa kupenda na wengine kwa kutokupenda.

However ushauri wako uanonekana uko relevant humu,kwani wana JF wa Tanzania si wale walalahoi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom