3 Bedroom House, toa changamoto!

3 Bedroom House, toa changamoto!

Store ( kitchen store ) mbona ipo nje mkuu?
Kwamba mtu kuchukua Unga store mpaka....
Utoke kwenye Verandah? Au nimeelewa vibaya?
Kwamba sio kitchen store.....

Pia atakayechora isometric ya water supply.....
Na waste water atapata tabu kidogo.
 
Viwanja vingi vya mjini Ni 20/15.
Kuna sehemu aliweka kipimo Cha chumba kimoja kua ni 3.5mita, almost futi 12.

Ukingalia
mapana yake anajumla vyumba Kama vinne, ambapo jumla Ni futi 48. Almost mita16 mapana.

Ukiacha mita 1 ya ujirani mwema kila upande, jumla ni mita 18. Na hapo bado hajaacha mita 2 kila upande za kujengea fensi

NB: hapa Imezingatiwa hajapakana na barabara yoyote Ile pembeni anapotakiwa kuacha mita 3 barabara ya TARURA au mita 5 za barabara za tanroad.

NB: kwa nyumba Hii ili kujenga fensi pembeni Lazima awe na mapana ya kuanzia mita 22 nakuendelea.

Ukienda kwa marefu,
Makadirio ni marefu ya vyumba vitatu vya futi 12 kila kimoja, ambapo jumla Ni futi 36.ambayo ni sawa na mita 12.

Ukiacha mita 1 ya ujirani mwema kila upande, jumla mita 14. Na hapo bado hajaacha mita 2 kila upande ili kujenga fensi. Ambapo Itakua jumla mita 18.

NB:
1. hapa Imezingatiwa hajapakana na barabara yoyote Ile pembeni anapotakiwa kuacha mita 3 barabara ya TARURA au mita 5 za barabara za tanroad.

2. kwa nyumba Hii ili kujenga fensi mbele na nyuma, Lazima awe na marefu ya kuanzia mita 18 nakuendelea.


Hitimisho,
Kwa kujibana bana Sana,
Unaona kabisa anahitaji kiwanja Cha mapana 22 na marefu 18,
Na hapo imezingatiwa Yuko landlocked, hajapakana na barabara yoyote Ile.

Ili nyumba hii ikae vizur,
Tena iwe na barabara ya kuingilia gari mpaka nyumbani na Apate parking na sehemu angalau ya kufua,kuanika nguo, watoto kucheza.

Ni Lazima marefu yaongezeke kufikia angalau mita 30 na mapana yawe mita 25.

Na hiki kwa mjini,
Kukipata sio kiwanja kidogo Wala Cha pesa ndogo mkuu.
Good analysis. Nimependa mchanganuo huu, na imenipa mawazo mazuri
 
Rafiki yangu ERoni hebu weka vipimo vyote kila chumba na upana na urefu wa nyumba nikufanyie marekebisho machache niliyoyaona kuanzia store na walk away kaka
Hizi ndio mambo zako nini mkuu Glenn.?

Sio mimi ninqyeichora, kuna jamaa alisema ataitengeneza kwa vipimo..sijui amefikia wapi mzee
 
Sawa,hivi msingi wa mawe na wa tofali upo mzuri?
Msingi wa mawe ukipata mtaalam wa kuyapanga na kuyaweka vizuri naamini ni imara zaidi. Muhimu anayejenga huo msingi awe vizuri. Huko kwenu mwanza si mawe kama yote.
 
Msingi wa mawe ukipata mtaalam wa kuyapanga na kuyaweka vizuri naamini ni imara zaidi. Muhimu anayejenga huo msingi awe vizuri. Huko kwenu mwanza si mawe kama yote.
Eee mi nimejenga msingi wa mawe
Yapo mengi sana
 
Back
Top Bottom