Viwanja vingi vya mjini Ni 20/15.
Kuna sehemu aliweka kipimo Cha chumba kimoja kua ni 3.5mita, almost futi 12.
Ukingalia
mapana yake anajumla vyumba Kama vinne, ambapo jumla Ni futi 48. Almost mita16 mapana.
Ukiacha mita 1 ya ujirani mwema kila upande, jumla ni mita 18. Na hapo bado hajaacha mita 2 kila upande za kujengea fensi
NB: hapa Imezingatiwa hajapakana na barabara yoyote Ile pembeni anapotakiwa kuacha mita 3 barabara ya TARURA au mita 5 za barabara za tanroad.
NB: kwa nyumba Hii ili kujenga fensi pembeni Lazima awe na mapana ya kuanzia mita 22 nakuendelea.
Ukienda kwa marefu,
Makadirio ni marefu ya vyumba vitatu vya futi 12 kila kimoja, ambapo jumla Ni futi 36.ambayo ni sawa na mita 12.
Ukiacha mita 1 ya ujirani mwema kila upande, jumla mita 14. Na hapo bado hajaacha mita 2 kila upande ili kujenga fensi. Ambapo Itakua jumla mita 18.
NB:
1. hapa Imezingatiwa hajapakana na barabara yoyote Ile pembeni anapotakiwa kuacha mita 3 barabara ya TARURA au mita 5 za barabara za tanroad.
2. kwa nyumba Hii ili kujenga fensi mbele na nyuma, Lazima awe na marefu ya kuanzia mita 18 nakuendelea.
Hitimisho,

Kwa kujibana bana Sana,
Unaona kabisa anahitaji kiwanja Cha mapana 22 na marefu 18,
Na hapo imezingatiwa Yuko landlocked, hajapakana na barabara yoyote Ile.
Ili nyumba hii ikae vizur,
Tena iwe na barabara ya kuingilia gari mpaka nyumbani na Apate parking na sehemu angalau ya kufua,kuanika nguo, watoto kucheza.
Ni Lazima marefu yaongezeke kufikia angalau mita 30 na mapana yawe mita 25.
Na hiki kwa mjini,
Kukipata sio kiwanja kidogo Wala Cha pesa ndogo mkuu.