herman joshua
JF-Expert Member
- Dec 30, 2018
- 2,303
- 3,987
We jamaa mambo ya utakatishaji pesa sisi hayatuhusu, furaha yetu ipo ndani ya dk 90,Dalili ya mvua ni mawingu.
Tushaona upendeleo waliofanyiwa Argentina kwa maamuzi yaliyoinyonga Egypt.
Tumeona jinsi Rais wa FIFA akiweka wazi hisia zake kwa Argentina.
Tumeona namna Rais wa FIFA alikasirika baada ya Egypt kufunga bao la pili (japo baadaye kwenye game ya Colombia alionekana akishika bendera ya Egypt ili kuua soo ku clear tukio lake la kukasirika baada ya Egypt kufunga bao)
Tumeona jinsi Rais wa AFA ambaye saizi anakabiliwa na kashfa ya utakatishaji fedha wa zaidi ya dola milioni 57 akiwa yupo kwenye uchunguzi chini ya FBI.
Na mbaya zaidi tumeona jinsi Raisi huyo wa AFA bwana Claudio Chiqui Tapia akikumbatiana na Raisi wa FIFA Gianni Infantino kwa furaha ya kushangilia bao la tatu la Argentina.
Haya matukio yote yanakufikisha kwenye hitimisho moja, there's something fishy going on in this tournament
Umekaa kisiasa sana thats why unatafuta hata mambo ya nje ya uwanja ili mradi tu upate furaha kwa kuikosoa Argentina, we endelea kuteseka huku sisi tukisheherekea.