2026 FIFA World Cup - Special Thread

2026 FIFA World Cup - Special Thread

Tatizo husomi post zangu.

Unafikiri hiyo mimi sijaiona?

Unafikiri kwanini nimesema waamuzi wote?

Hii ndio inayo tutofautisha mimi na wewe.

Argentina na Egypt kuna waamuzi wa mataifa mengine hapo wawili, umewaona?

Hii ndio inayofanya niseme katika rekodi za World Cup hakujawahi kutokea mechi moja ikawa na waamuzi wote kutoka nchi moja.
Sawa bwana Sacrs tumekuelewa... Ila angalia usipate sonona na pressure kwa kumchukia Messi
1000058869.jpg
 
Acha ubish maandazi Mzee Hilo tukio la Mo Salah beki aliucheza mpira kwanza akautoa miguuni mwa mo Salah na mo Salah akawa ameanza kutangulia kuanguka before mguu wake haujaugusa mguu wa beki wa Argentina, ingekuwa ni faulo endapo kama beki wa Argentina angekuwa ameugusa mguu wa mo Salah Bila ya beki huyo kuwa ameugusa mpira , Lakini beki akianza kuugusa mpira first akautoa nje ya contact foot ya mo Salah --- watu wenye Akili zao wamekaa wamepitia hizo review na hawaona kosa hapo
Ukweli ni kwamba simkubali Messi na Argentina.

Hii haijawahi kuwa siri nililiweka wazi from the scratch hadi tuliokuwa nao kwenye uzi wa World Cup ya 2022 wanajua hili.

Hoja ni kwamba, je ukweli wa hoja zangu unaupima kwa kuangalia uhalisia na ushahidi nilioweka au unaupima kwa kuangalia mapenzi yangu kwa Messi?

Labda nikupe mfano mmoja.

Baada ya Messi kukosa penalty kwenye mechi ya juzi, kuna mashabiki wa Argentina na Messi humu walisema "Messi hamna kitu"


Lakini kitu kama hiki hiki nikikisema mimi kinatafsiriwa tofauti kwasababu nafahamika kuwa simkubali.

Kitu ambacho nina uhakika nacho ni kwamba mimi naweza kujitetea kwa evidence, wewe utajitetea kwa hisia za ushabiki.

Na kama nilivyosema awali, naongea haya yote sio kwa lengo la kukufanya wewe na wengine mkubaliane na mimi.

Mimi naongea na kuambatanisha evidence kwa kuweka rekodi sawa just in case huu uzi unaweza kuja kutumiwa na wadau kama reference au watu wengine ambao wangetaka kusikia stori kutoka pande zote.

Nyinyi tayari mmeongea kuhusu positive za Argentina na Messi, na mimi nitaongea ule upande ambo nyinyi hamjaongea.

Audience itachagua iende na habari gani ndio maana najitahidi kuweka ushahidi.

Umesema Salah alijiangusha. Wacha nikubaliane na wewe kwenye hili, lakini kwanza unaelewa kihezo kilichotumika kukataa goli la pili la Egypt?

VAR baada ya kufanya review goli lilikataliwa kwasababu kwenye build up mchezaji wa Egypt Marwan Attia, alimkanyaga Lisandro Martinez. VAR ilionesha mgusano kati ya mguu wa Marwan Attia na Martinez

Lakini tukio la Mo Salah pia ni incident hii hii ambapo Julian Alvarez alimkanyaga Mo Salah ndani ya box dakika ya 92 na kuanguka na hata video ukiangalia inaonesha Mo Salah akikanyagwa.

Video hii hapa chini
View attachment 3625873
Mpaka hapo sidhani kama kuna utata kuwa Alvarez hakumkanyaga Mo Salah, wote tunaona. Hoja inabaki kuwa kwanini tukio hili halikupewa attention ya kuangaliwa kwenye VAR ilihali tunaona mtu akikanyagwa?

Umedai wachambuzi wengi wakubwa wamekubaliana kuwa Egypt haikuonewa. Umesema wengi ila hujataja kwa majina na kusema ni wangapi.

So namimi nikikuonesha evidence ya kuonesha wachambuzi na ma legend wa mpira wakikubali kuwa Egypt amedhulumiwa, utasemaje? Utawaita hater?

Hawa wote walisema Egypt imenyongwa na mwamuzi.

Rob Green, Gary Neville, Garry Kasparov, Rob Green, Alan Shearer, Ian Wright, Jamie Carragher na Jose Mourinho.

Na hawa hapa chini ndio waliosema yalikuwa ni maamuzi fair
Pierluigi Collina: (Huyu ni mkuu wa waamuzi wa FIFA), Dr. Joe Machnik na Nikhil Naz

Zlatan na Henry hawakuzungumzia kabisa kuhusu controversial ya matukio na maamuzi yaliyoamuliwa.
wewe umeweka clip sijui Ina second 4 what are you trying to hide !?

Kwanini haujaweka move ya Mo Salah ilipo kuwa imeanzia wakati anajaribu kuingia ktk box !? Huo mpira beki alitangulia kuucheza first before hiyo miguu ya Salah na huyo beki haujaugusana

Tukienda kwenye faulo ya misri iliyo changia goli lao kukataliwa yule mchezaji wa misri sio tu kwamba mguu wake uligusana na beki wa Argentina but ukweli ni kwamba alimkanyaga na pia nyuma ya mgongo alikuwa anamvuta jersey yake kwanini mnaficha ukweli 😁😁😁

Hizo review sote tumezipitia , Tena baada ya watu wengi kuzipitia wamejikuta wanawaona Egypt wapumbavu cause wanalalamikia kitu ambacho hakipo wana wacheka Kwa kushindwa kwao kukaza msuli kuzuia magoli yasirudi , Egypt walipatia chance wameichezea wao wenyewe hakuna upendeleo wowote uliofanywa Kwa Argentina

And BTW tufanye Argentina na Messi wana pendelewa
Nimejiuliza swali huyo GOAT wako Aliwahi kuisaidia nini Portugal walau kufika nusu final tu ya kombe la Dunia ktk nyakati zote ambazo Amewahi kushiriki !?

Je Amewahi kufunga goli la kuwapeleka nusu final halafu likakataliwa !? Kama hajawahi hata kufanya hivyo mara 6 zote alizowahi kucheza WC hizo guts za kumchukia Lionel Messi anapofanya mazuri mnaitoa wapi !? 😁😁😂

Scars
 
Acha ubish maandazi Mzee Hilo tukio la Mo Salah beki aliucheza mpira kwanza akautoa miguuni mwa mo Salah na mo Salah akawa ameanza kutangulia kuanguka before mguu wake haujaugusa mguu wa beki wa Argentina, ingekuwa ni faulo endapo kama beki wa Argentina angekuwa ameugusa mguu wa mo Salah Bila ya beki huyo kuwa ameugusa mpira , Lakini beki akianza kuugusa mpira first akautoa nje ya contact foot ya mo Salah --- watu wenye Akili zao wamekaa wamepitia hizo review na hawaona kosa hapo
Kwanza kuna kitu ambacho unakiepuka kabisa kukiongea hapa na sijui kwanini.

Unataka kuniambia ukiangalia hiyo video huoni mguu wa Alvarez ukikanyaga mguu wa Mo Salah? Kwasababu nakuona unazunguka tu kuongelea habari za kuucheza mpira kwanza na kuacha hili tukio muhimu.

Pili unatakiwa kujua kuucheza mpira kwanza hakumpi kinga kwa mchezaji aliyecheza faulo.
 
Acha ubish maandazi Mzee Hilo tukio la Mo Salah beki aliucheza mpira kwanza akautoa miguuni mwa mo Salah na mo Salah akawa ameanza kutangulia kuanguka before mguu wake haujaugusa mguu wa beki wa Argentina, ingekuwa ni faulo endapo kama beki wa Argentina angekuwa ameugusa mguu wa mo Salah Bila ya beki huyo kuwa ameugusa mpira , Lakini beki akianza kuugusa mpira first akautoa nje ya contact foot ya mo Salah --- watu wenye Akili zao wamekaa wamepitia hizo review na hawaona kosa hapo
Mimi sina ushabiki, sio mfuasi wa ronaldo wala mesi. Na timu yangu ya senegali ilishatoka. Ila kiuhalisia kinacholaumiwa ni VAR, inshu sio kuwa na uhalali au kutokuwa na uhalali wa tukio husika inshu ni kwanini refa hakujisumbua hata kwenda kwenye VAR ??. na tukio kama hilohilo na mechi hiyohiyo ila refa kakimbilia VAR kwa spidi ya mwanga tena bila kuzongwazongwa na wachezaji wa argentina

Misri siwapendi kabisa, ila tukiweka ushabiki wowote pembeni , Iyo game Argentina alibebwa.
 
Mimi sina ushabiki, sio mfuasi wa ronaldo wala mesi. Na timu yangu ya senegali ilishatoka. Ila kiuhalisia kinacholaumiwa ni VAR, inshu sio kuwa na uhalali au kutokuwa na uhalali wa tukio husika inshu ni kwanini refa hakujisumbua hata kwenda kwenye VAR ??. na tukio kama hilohilo na mechi hiyohiyo ila refa kakimbilia VAR kwa spidi ya mwanga tena bila kuzongwazongwa na wachezaji wa argentina

Misri siwapendi kabisa, ila tukiweka ushabiki wowote pembeni , Iyo game Argentina alibebwa.
Unatakiwa ufahamu kwamba refa yeye siye anaye control VAR refa Huwa haendi kwenye VAR Mpaka marefa wanao monitor VAR wamwambie that's why unaona anavaa kifaa Cha mawasiliano kwaajili ya kucontact na marefa wanao control VAR ,

Mods wa VAR kazi Yao nikupitia matukio yanayo endelea uwanjani so wanapo Ona kuwa Kuna tukio lenye mashaka wana muambia refa aende kujiridhisha lakini Hawa muamulii maamuzi refa akisha kwenda kupitia kwenye machine yeye ndiye wakutoa jibu kuwa ni sahihi au la !!!! So unamlaumu refa ili iweje !?

Argentina haijabebwa ni vile kile kilichotokea it wasn't goes beyond of your expectations 😁😁

Hicho ndio kinacho wauma
 
Unatakiwa ufahamu kwamba refa yeye siye anaye control VAR refa Huwa haendi kwenye VAR Mpaka marefa wanao monitor VAR wamwambie that's why unaona anavaa kifaa Cha mawasiliano kwaajili ya kucontact na marefa wanao control VAR ,

Mods wa VAR kazi Yao nikupitia matukio yanayo endelea uwanjani so wanapo Ona kuwa Kuna tukio lenye mashaka wana muambia refa aende kujiridhisha lakini Hawa muamulii maamuzi refa akisha kwenda kupitia kwenye machine yeye ndiye wakutoa jibu kuwa ni sahihi au la !!!! So unamlaumu refa ili iweje !?

Argentina haijabebwa ni vile kile kilichotokea it wasn't goes beyond of your expectations 😁😁

Hicho ndio kinacho wauma
Ni ushabiki tuu ndio unaponza tusikiri uhalisia, ila matukio ya kitata na kubebwa timu moja ni mengi tu kwenye hiyo mechi.

Hilo la mawasiliano kati ya VAR room na muamuzi nalifahamu vizuri. Wewe watu wameenda mpaka kufunga goli ndio madhambi yanaonekana. Emu Kuwa serious mkuu, tumia hata logic tu.

Kifupi matukio ya kitata ni mengi kwenye hiyo game na mbona yanaonekana dhahiri vizuri tuu. Basi tuu ushabiki upofu
 
Ni ushabiki tuu ndio unaponza tusikiri uhalisia, ila matukio ya kitata na kubebwa timu moja ni mengi tu kwenye hiyo mechi.

Hilo la mawasiliano kati ya VAR room na muamuzi nalifahamu vizuri. Wewe watu wameenda mpaka kufunga goli ndio madhambi yanaonekana. Emu Kuwa serious mkuu, tumia hata logic tu.

Kifupi matukio ya kitata ni mengi kwenye hiyo game na mbona yanaonekana dhahiri vizuri tuu. Basi tuu ushabiki upofu
Unaotumia logic fallacy unakosa mantiki kabisa ingekuwa hivyo basi na faulo ambazo Huwa zinaidhinishwa na VAR mngekuwa mnazipinga basii 😆😆😆
How many time inatokea faulo refa anaacha mpira unaendelea kuchezwa then VAR mods wana muita refa na kumwambia kwamba Kuna faulo ilichezwa mbona Huwa hamlalamiki

You guys are seriously!??

BTW ZICO mchezaji wa misri alipofunga goli la 2 Alivua jezi lakini refa hakumpa card ya njano wakati inafahamika kuwa kuvua jezi wakati mchezo unaendelea ukiwa uwanjani ni kinyume Cha Sheria , so mbona hatujawasikia mkilalamika na kumshutumu refa kuwa aliwapendelea misri Kwa kutompa ZICO card ya njano wakati Alivua jersey!?

Why mnafanya double standard zaajabu !?? Aisee chuki itawaua 😁
 
Unaotumia logic fallacy unakosa mantiki kabisa ingekuwa hivyo basi na faulo ambazo Huwa zinaidhinishwa na VAR mngekuwa mnazipinga basii 😆😆😆
How many time inatokea faulo refa anaacha mpira unaendelea kuchezwa then VAR mods wana muita refa na kumwambia kwamba Kuna faulo ilichezwa mbona Huwa hamlalamiki

You guys are seriously!??

BTW ZICO mchezaji wa misri alipofunga goli la 2 Alivua jezi lakini refa hakumpa card ya njano wakati inafahamika kuwa kuvua jezi wakati mchezo unaendelea ukiwa uwanjani ni kinyume Cha Sheria , so mbona hatujawasikia mkilalamika na kumshutumu refa kuwa aliwapendelea misri Kwa kutompa ZICO card ya njano wakati Alivua jersey!?

Why mnafanya double standard zaajabu !?? Aisee chuki itawaua 😁
Unaacha faulo mpaka goli linafungwa ndio faulo inatafutwa kupitia VAR, ulishaona wapi ??, tena WC mtoano kwa game yenye tention namna ile. Hata ingekuwa chandimu angepigwa mawe huyo refa.

Hilo la kuvua jezi ZICO mbona logically ndio linathibitisha bila shaka kuwa refarii alikuwa na mipango yake mfukoni, simply refa alijua anaenda kufuta goli la misri, angalia tu hata matukio VAR chap chap kwa spidi ya mwanga utakumbuka lini kutoa kadi kwa tukio la ZICCO ilihali kichwani unajua kabisa naenda kufuta goli lililofungwa ???.

Mkuu tukiweka ushabiki pembeni kwenye ile game argentina kuwateta ni kama mlima. Walibenwa na refa Iko wzizi mbona
 
wewe umeweka clip sijui Ina second 4 what are you trying to hide !?

Kwanini haujaweka move ya Mo Salah ilipo kuwa imeanzia wakati anajaribu kuingia ktk box !? Huo mpira beki alitangulia kuucheza first before hiyo miguu ya Salah na huyo beki haujaugusana
Kwanza madai yako hayakanushi kwamba Alvarez hakumkanyaga, hayakanushi kwamba clip haioneshi tukio kuu lililobeba mjajala linalo lalamikiwa la MO Salah kukanyagwa.

Malalamiko yako yamejikita kwenye sekunde 4, kiufupi sijajua ulikuwa unataka kuona nini ambacho kinathibitisha kuwa mguu wa Alvarez haukumkanyaga MO Salah.

Sasa hapa namimi naomba nikuulize ni clip ya dakika ngapi ambayo inatosha wewe kukufanya uone tukio hili la Alvarez akimkanyaga Mo Salah?

Mfano naweza kuweka hivi



Au hivi


Na hivi


Lakini ukiwa shabiki lia lia wa huyu
1783617860786.png


Huwezi kuona hata ukifanywa hivi
1783618044466.png
 
Unaacha faulo mpaka goli linafungwa ndio faulo inatafutwa kupitia VAR, ulishaona wapi ??, tena WC mtoano kwa game yenye tention namna ile. Hata ingekuwa chandimu angepigwa mawe huyo refa.

Hilo la kuvua jezi ZICO mbona logically ndio linathibitisha bila shaka kuwa refarii alikuwa na mipango yake mfukoni, simply refa alijua anaenda kufuta goli la misri, angalia tu hata matukio VAR chap chap kwa spidi ya mwanga utakumbuka lini kutoa kadi kwa tukio la ZICCO ilihali kichwani unajua kabisa naenda kufuta goli lililofungwa ???.

Mkuu tukiweka ushabiki pembeni kwenye ile game argentina kuwateta ni kama mlima. Walibenwa na refa Iko wzizi mbona
Una matatizo 😄

Kwahiyo faulo zote zilizowahi kuamuliwa na VAR kuwa zipigwe bada ya move ya faulo kupita ni faulo batili ???

Mind you zicco Alivua Jersey baada ya kufunga goli la pili lililokubaliwa , hii statement Yako ya kusema kwamba Hakupewa card baada ya kuvua jersey kwakuwa refa Alikuwa na mipango ya kulikataa goli inaonyesha wazi kwamba upo kwaajili ya kubishana na sio ku-spin fact , Yes ingekuwa upo kwaajili ya ku-spin fact ingekuwa umesha tambua muda mrefu kwamba goli alilofunga Zicco na kuvua jersey sio lile goli ambalo lilikataliwa, Bali ni goli la pili lilokubaliwa. Humble be
 
Una matatizo 😄

Kwahiyo faulo zote zilizowahi kuamuliwa na VAR kuwa zipigwe bada ya move ya faulo kupita ni faulo batili ???
Kuhusu uhalali au ubatili sifahamu

Ila leta faulo ilioamuriwa baada ya goli kufungwa, ndio sembuse WC ?
 
So kama haufahamu uhalali na ubatili, kwanini tunabishana !?
Hiyo nilijibu statement yako ya kwamba “inaama faulo zote zilizoamriwa na VAR baada ya mpira kuendelea ni batil ?”.

Ndio nimejibu hapo kuwa kuhusu ubatili au uhalali wa izo faulo unazozisemea sifahamu, sababu sijaziona izo faulo. ILA HII FAULO YA EGYPT NA ARGENTINA NIMEIONA LIVE NA DUNIA NZIMA IMEIONA.
 
Tukienda kwenye faulo ya misri iliyo changia goli lao kukataliwa yule mchezaji wa misri sio tu kwamba mguu wake uligusana na beki wa Argentina but ukweli ni kwamba alimkanyaga na pia nyuma ya mgongo alikuwa anamvuta jersey yake kwanini mnaficha ukweli 😁😁😁
Unajua nini? Miimi sipingi kwamba mchezaji wa Egypt hakumkanyaga mchezaji wa Argentina, kama unadhani mimi nhuu ndio msimamo wangu basi utakuwa husomi vizuri nacho kiandika.

Kitu ambacho kwangu ni rahisi kukifanya ni kuweka hoja kwa ushahidi. Wakati nyie wenzangu kitu rahisi kwenu ni kuongea maneno matupu ambayo hayapo supported na references yeyote.

Hii ndio inatofautisha kati ya mjadala na mabishano

Hata Messi mwenyewe kwenye ile daylight robbery yake ingekuwa ndio kesi ina amuliwa mahakamani na nyinyi ndio mmesimama kama mawakili wake, kwa hiki mnachokiandika mngekuwa tayari mmeisha mfunga ndugu yenu maana hoja zenu zinam expose zaidi.
 
Back
Top Bottom