2026 FIFA World Cup - Special Thread

2026 FIFA World Cup - Special Thread

Kuhusu Ubingwa wake ambao timu zenu zinatoana macho kugombea
IMG_0710.jpeg
 
Ecuador na Mexico zinacheza saa tatu usiku saa za ukanda wa mashariki.

Ni chini ya masaa mawili kuanzia sasa ndo mechi inaanza.
Nimejichanganya... Ni saa 10 alfajiri kwa saa za EA, gmt+3, sijui niliwaza nini..
Sema US majimbo kadhaa mnatofautiana muda...
Bado lisaa na dkk kadhaa match ianze..

Drc watacheza leo jioni.. Kwa US itakuwa alasiri ama mchana...
 
France kidogo anaweza akateteleka kwa Colombia,Argentina ila hawa wengine atajipigia sana. Ureno wana middle bora ulaya za kutosha,ndio hivyo kocha hawana ila nao wangesumbua sana kwenye michuano hii.
Mkuu hata Mimi kiukweli naona France wako vizuri na wanaweza kuchukua World Cup hii, ila ukweli ni kwamba hawajapata changamoto kucheza na timu ngumu... Sasa hawa Sweden hata ukiwakabidhi Colombia si wanakula nyingi.. Hata wakikutana na Morocco wanapasuka vizuri tu...

France sana sana wako vizuri pale Mbele yaani Mbappe, Dembele, Olise na hao Madogo akina Doue na Barcola... Ila beki yao akija kukutana na moto wa wanaume tutakuja kuongea lugha moja, Siku wamekutana na Messi ameamka na mashetani yake hao akina Kounde, Upamecano eti Digne watabondeka vibaya.

Kuhusu Portugal wanaangushwa na Ronaldo anazurura tu uwanjani na pia hamna kocha pale..
 
Ecuador tayari amesha elekea kwenye mlango wa kutokea,zimebaki kama hatua tano tu ili ajikute yupo nje.
Kipindi cha pili equador kachangamka sana ila bahati tu haipo upande wao kipindi cha kwanza ni makosa sana wamefanya hasa upande wa beki wa kushoto huyu jau sana ila yote game Walianza nayo kwa kuichukulia poa
 
Back
Top Bottom