Salaam, Shalom!
CDM na CCM hoyee!
Twende haraka kwenye mada.
HOJA ya swali hapo juu ni kutaka kujadili madhara na faida za kuingiza siasa michezoni.
Tumeona hivi sasa imeibuka TABIA ngeni ambayo tangu uhuru hatujawahi kuiona ikiendelea kuzoeleka.
Michezo tangu uhuru imekuwa ni chanzo Cha UMOJA na kuunganishwa makundi yote na KUIMARISHA UMOJA na mshikamano wetu kitaifa.
Tumekuwa tukiona viongozi wa Upinzani wakiweka mbali mavazi Yao ya kisiasa na kuvaa jerzey na kufurahia burudani ya mpira bila kujali itikadi zao za kisiasa.
Ilikuwa ni kawaida kumkuta Mbowe akiwa amekaa pamoja na Rizwani KIKWETE wakishangilia timu Yao ya Yanga bila kuvaa sare zao za vyama.
Huu Utaratibu mgeni wa kuingia na mabango na picha za viongozi wa chama viwanja vya michezo unalenga nini?
Yaani mechi ya simba na yanga, unakutana na watu wamevaa sare za chama na PICHA kubwa na MABANGO ya kiongozi wa chama zenye jumbe zisohusiana na michezo, jumbe ni za kisiasa na hawakemewi wanapoingia.
Lengo la kuingiza siasa michezoni Lina faida na HASARA zipi?
Ikiwa Mdude, Dr. Slaa na Mwabukusi nao wakianza kuingia viwanja vya michezo na mabango ya kisiasa Viwanjani wataruhusiwa?
Na Hali hii ikizoekeka, katika chaguzi zijazo tukapiga kura Kwa kufuata timu zetu za Simba na Yanga, nani ataibuka mshindi?
Na Hali ikiwa hivyo, UMOJA wetu wa kitaifa utaendelea kuwa kama ulivyo?
Nani aje atukemee, Ili tujirekebishe?
Karibuni 🙏
CDM na CCM hoyee!
Twende haraka kwenye mada.
HOJA ya swali hapo juu ni kutaka kujadili madhara na faida za kuingiza siasa michezoni.
Tumeona hivi sasa imeibuka TABIA ngeni ambayo tangu uhuru hatujawahi kuiona ikiendelea kuzoeleka.
Michezo tangu uhuru imekuwa ni chanzo Cha UMOJA na kuunganishwa makundi yote na KUIMARISHA UMOJA na mshikamano wetu kitaifa.
Tumekuwa tukiona viongozi wa Upinzani wakiweka mbali mavazi Yao ya kisiasa na kuvaa jerzey na kufurahia burudani ya mpira bila kujali itikadi zao za kisiasa.
Ilikuwa ni kawaida kumkuta Mbowe akiwa amekaa pamoja na Rizwani KIKWETE wakishangilia timu Yao ya Yanga bila kuvaa sare zao za vyama.
Huu Utaratibu mgeni wa kuingia na mabango na picha za viongozi wa chama viwanja vya michezo unalenga nini?
Yaani mechi ya simba na yanga, unakutana na watu wamevaa sare za chama na PICHA kubwa na MABANGO ya kiongozi wa chama zenye jumbe zisohusiana na michezo, jumbe ni za kisiasa na hawakemewi wanapoingia.
Lengo la kuingiza siasa michezoni Lina faida na HASARA zipi?
Ikiwa Mdude, Dr. Slaa na Mwabukusi nao wakianza kuingia viwanja vya michezo na mabango ya kisiasa Viwanjani wataruhusiwa?
Na Hali hii ikizoekeka, katika chaguzi zijazo tukapiga kura Kwa kufuata timu zetu za Simba na Yanga, nani ataibuka mshindi?
Na Hali ikiwa hivyo, UMOJA wetu wa kitaifa utaendelea kuwa kama ulivyo?
Nani aje atukemee, Ili tujirekebishe?
Karibuni 🙏