Ccm haitambi, bali madaraka ya urais yanayotumika vibaya kuteka watu, kuua wapinzani, kunajisi uchaguzi na uhayawani mwingine kama huo ndio yamayotamba. Kinachofanyika katika kuibeba ccm na kuifanya ionekane imara ni kiburi cha madaraka ya urais ya mwenyekiti wake. Kuna wakati Iddi Amin, Moi, Mugabe nk waliamini vyama vyao ni imara, sio kwakuwa kweli vilikuwa imara, bali yalikuwa ni madaraka ya viongozi hao kutumia vyombo vya dola kutoa upendeleo kwa vyama vyao, ndio waliitafsiri wao na wapambe wao kuwa vyama vyao ni imara.
Kama kweli kuongea kwa kujinyeyekeza kwa ccm kunavipa nafasi vyama vya siasa, basi vyama vinavyojipendekeza kwa ccm kama TLP, UDP, NCCR, CUF nk vingekuwa na nafasi huko kwa wananchi. Mtu mjinga ya kama ww ndio anaweza kuamini ccm hii ni imara. Chama imara hakishindi uchaguzi kwa kutumia udhaifu wa katiba na shuruti, nakushauri urudi shule ukajifunze uimara wa chama ni nini.