Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,930
- 141,891
Sijaelewa ni kwanini kuna watu wanauhusisha uteuzi wa Dkt. Bashiru kuwa katibu mkuu kiongozi na Rais Magufuli kuongeza muda kuiongoza Tanzania kwa zaidi ya mihula miwili.
Dkt. Bashiru amewahi kunukuliwa akisema kuwa anapendelea iwe hivyo? Yaani Rais Magufuli aongezewe muda wa kutawala?
Au ni kiwewe tu cha wasiompenda Magufuli? Maana kiwewe huwa kinavuruga akili ya mtu.
Kiwewe kinaweza kumfanya mtu aione 1 ni 3 na 3 ni 2!
Kiwewe kinaweza kumfanya mtu alione giza ni mwanga na mwanga ni giza, salamu ni tusi na tusi ni salamu.
Halafu ni kama vile kuna watu wanaombea Magufuli kweli aongezewe au aongeze muda ili wapate sababu za kumsema na kujipatia vijipointi vya kisiasa.
Na asipojiongezea, watu hao watakuwa disappointed sana maana atakuwa ‘kawaangusha’.
Mimi bado naamini endapo ataendelea kuwa mzima, basi ataongoza kwa idadi ya mihula inayoruhusiwa na katiba tuliyonayo sasa.
Otherwise, uhusiano wa Dkt. Bashiru kuwa katibu mkuu kiongozi na uongezwaji wa muda Rais Magufuli kuendelea kuwa Rais ni nini?
Dkt. Bashiru amewahi kunukuliwa akisema kuwa anapendelea iwe hivyo? Yaani Rais Magufuli aongezewe muda wa kutawala?
Au ni kiwewe tu cha wasiompenda Magufuli? Maana kiwewe huwa kinavuruga akili ya mtu.
Kiwewe kinaweza kumfanya mtu aione 1 ni 3 na 3 ni 2!
Kiwewe kinaweza kumfanya mtu alione giza ni mwanga na mwanga ni giza, salamu ni tusi na tusi ni salamu.
Halafu ni kama vile kuna watu wanaombea Magufuli kweli aongezewe au aongeze muda ili wapate sababu za kumsema na kujipatia vijipointi vya kisiasa.
Na asipojiongezea, watu hao watakuwa disappointed sana maana atakuwa ‘kawaangusha’.
Mimi bado naamini endapo ataendelea kuwa mzima, basi ataongoza kwa idadi ya mihula inayoruhusiwa na katiba tuliyonayo sasa.
Otherwise, uhusiano wa Dkt. Bashiru kuwa katibu mkuu kiongozi na uongezwaji wa muda Rais Magufuli kuendelea kuwa Rais ni nini?