Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,997
Wazo la leo:
Tanzania haiitaji Rais kijana... kwani tunapeleka Ikulu mbeba vyuma au mtunisha misuli au atakuwa na kazi ya kupiga push ups ofisini? Na hatuwezi kumkataa mtu kwa sababu ni mzee kwani anaenda kubebeshwa viroba vya mchele au kukimbia marathon?
Tena hata hatuhitaji Rais msomi wa kivile! Mwaka 2015 Watanzania wanahitaji Rais ambaye atavunjilia mbali sera zilizoshindwa za CCM, kuifumua mifumo mibovu ya kiutawala iliyodumu kwa miaka karibu hamsini sasa na kutupa uongozi wa kutufanya tujiamini kuwa tunaweza na akatuongoza katika kujenga taifa la kisasa lenye kujali utu wa watu na siyo vitu vya watu.
Tunahitaji rais na pamoja naye viongozi wenye UWEZO wa kufikiri kwa usahihi, kuamua kwa usahihi na kutenda kwa usahihi wakitambua dhamana ya uongozi ambao taifa linawapa. RAIS ajaye wa Tanzania ni lazima awe na UWEZO; UMRI wake usihusishwe kabisa na uwezo huo.
Kiongozi ajaye basi ni lazima we ni MTU WA WATU; ambaye amejitofuatisha katika mambo makubwa yafuatayo: Wazo hili litaendelea...
Tanzania haiitaji Rais kijana... kwani tunapeleka Ikulu mbeba vyuma au mtunisha misuli au atakuwa na kazi ya kupiga push ups ofisini? Na hatuwezi kumkataa mtu kwa sababu ni mzee kwani anaenda kubebeshwa viroba vya mchele au kukimbia marathon?
Tena hata hatuhitaji Rais msomi wa kivile! Mwaka 2015 Watanzania wanahitaji Rais ambaye atavunjilia mbali sera zilizoshindwa za CCM, kuifumua mifumo mibovu ya kiutawala iliyodumu kwa miaka karibu hamsini sasa na kutupa uongozi wa kutufanya tujiamini kuwa tunaweza na akatuongoza katika kujenga taifa la kisasa lenye kujali utu wa watu na siyo vitu vya watu.
Tunahitaji rais na pamoja naye viongozi wenye UWEZO wa kufikiri kwa usahihi, kuamua kwa usahihi na kutenda kwa usahihi wakitambua dhamana ya uongozi ambao taifa linawapa. RAIS ajaye wa Tanzania ni lazima awe na UWEZO; UMRI wake usihusishwe kabisa na uwezo huo.
Kiongozi ajaye basi ni lazima we ni MTU WA WATU; ambaye amejitofuatisha katika mambo makubwa yafuatayo: Wazo hili litaendelea...