CHADEMA haina mtu mwenye uwezo kushindana na Rais Samia katika sanduku la kura uchaguzi ujao

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,335
9,756
Ndugu zangu Watanzania,

Urais ni nafasi nyeti na kipekee sana, ni nafasi inayohitaji mtu mwenye akili kubwa ya kuweza kujuwa, kufahamu na kutambua namna ya kutumia akili kubwa zote nchini katika kuleta matokeo chanya katika maisha ya watu.

Ni nafasi inayohitaji mtu mwenye upeo mkubwa na maono ya mbali, ni nafasi inayohitaji mtu anayeweza kuona umbali wa miaka mia mbele na kuwa na mipango ya karne moja mbele, ni nafasi inayohitaji mtu mtulivu wa akili na mipango au maamuzi yake.

Ni nafasi inayohitaji mtu jasiri katika kufanya maamuzi kwa wakati bila hofu wala uoga, ni nafasi inayohitaji mtu mwenye hekima, busara na mwenye kuchunga ulimi wake.

Urais unahitaji mtu mwenye uwezo wa kuwaunganisha watu wa makundi yote, vyama vyote, rika zote na Dini zote, mtu mwenye uwezo wa kuvumilia na kuweza kukaa meza moja na mpinzani wake, mtu mwenye uwezo wa kusikiliza na kuthamini sauti zote, mtu mwenye uwezo wa kutoa haki kwa wengi na kuwasikiliza wachache.

Ndio maana mtu anaweza kuongoza vizuri wizara lakini akawa hana sifa hata kidogo ya kupewa Urais wa nchi kwa kuwa Urais unahitaji mtu mwenye akili, uwezo na macho ya kuzitazama wizara zote kwa usawa, inahitaji mtu ambaye makundi yote, Taasisi zote kuanzia viongozi wa Dini, wananchi, wanasiasa, vyombo vya ulinzi na usalama, n.k watajiona wana nafasi sawa na muhimu katika uongozi wako, watajiona hawatengwi na wana fursa sawa katika Taifa lao.

Urais unahitaji mtu anayejuwa kuwa akishapita anakuwa Rais wa wote kwa walio mchagua na ambao hawajamchagua, kwa wanao mpenda na wasio mpenda kwa maslahi yao, unahitaji mtu mwenye kifua kikubwa, mwenye kujua uongozi ni Jalala ambapo kila kitu utatupiwa wewe.

Unahitaji mtu shupavu, jasiri na madhubuti katika kukabiliana na mishale kutoka kila upande na kuweza kuhimili vishindo vyake na kubaki katika muelekeo wake na Dira yake pasipo kuyumba wala kuyumbishwa.

Urais hauhitaji mtu wa Hasira au visasi au chuki juu ya Wale waliokuwa wana mpinga kabla au waliomuumiza kabla, unahitaji mtu mwenye moyo wa kuachilia na kusamehe, unahitaji kujuwa nguvu yake ni kubwa kikatiba na kisheria inayohitaji busara katika kuitumia kwa watu. Inahitaji mtu mwenye hofu ya Mungu ili asitese watu hovyo, kuua watu hovyo, kuumiza watu hovyo na kububujisha watu machozi.

Sasa ukiangalia CHADEMA haina mtu mwenye sifa hizo, haina mtu mwenye uwezo wa kuwaunganisha Watanzania wa makundi yote na vyama vyote, haina mtu ambaye anaweza kutumainiwa na kutazamwa na watanzania kama mtu anayeweza akawahakikishia usalama na kuwatumikia pasipo visasi au chuki dhidi ya chama kingine au anayeweza kuwapa fursa sawa masikioni pake, CHADEMA haina mtu anayeweza akaviongoza vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kama Amiri jeshi mkuu.

Haina mtu anayeweza akatazamwa na watu wa Dini zote na makabila yote na makundi yote kama kiongozi wao na wakawa huru kuonana naye na kufanya naye mazungumzo, CHADEMA haina mtu anayeweza akawafanya watu wa makundi yote wakajiona kuwa wana nafasi sawa katika utawala wake.

CHADEMA haina mtu mwenye ulimi wa kujenga umoja wa Kitaifa na hili linathibitishwa kupitia majukwaa yao kwa namna wanavyotoa lugha za ubaguzi na uchochezi na chuki dhidi ya wale wote wanaokuwa kinyume nao au kutowaunga mkono kama walivyofanya kwa walimu, police N.k.

Ukija kwa Upande wa Rais samia unaona ni mtu na nusu,ni kiongozi aliye kamilika, ni kiongozi mwenye kipawa na Karama ya uongozi ,ni kiongozi mwenye upeo, maono na akili kubwa, ni kiongozi mwenye kifua, uvumilivu na utulivu wa hali ya juu sana, ni kiongozi mwenye ulimi wa kulinganisha Taifa na uliojenga umoja wa kitaifa.

Ni kiongozi ambaye makundi yote ndani ya Taifa letu yanajiona yana nafasi sawa na fursa sawa katika uongozi wake, ni kiongozi mwenye uwezo wa kusikiliza sauti zote masikioni mwake, pamoja na kuweza kukaa mezani na yeyote katika kutafuta suluhu, lakini pia ni kiongozi mwenye kifua kikubwa na chenye kuhimili vishindo pasipo kupoteza Dira au kupandwa na jazba.

Hii ndio maana kwa uwezo wake huo wa kiuongozi tangia Ameingia madarakani amerudisha utaratibu wa mikutano ya kisiasa ili watu wazungumze ya moyoni, japo sasa watu Hasa CHADEMA wanatumia uhuru huo kutukana matusi na kupandikiza mbegu za ubaguzi kwa misingi ya Udini , ukabila, ukanda na jinsia.

Amekaa na makundi na viongozi mbalimbali katika kujadili Masuala mbalimbali katika ustawi wa Taifa letu, amekaa na viongozi wa Dini,wa vyama na hata kwa mtu mmoja mmoja. Ni Rais anaye mtizama kila mtu kwa jicho la usawa na haki.

Hii ndio maana Rais Samia Anaendelea kuungwa mkono na mamilioni ya watanzania, hii ndio sababu ya upinzani kutokuwa na mtu wa kuweza kumshindanisha na Rais samia, hii ndio sababu kwa sasa upinzani umeishiwa hoja na kuishia kutoa Viroja na vihoja tu majukwaani kwa kuwa hoja za msingi zimefanyiwa kazi na serikali ya Rais Samia.

Ni busara kwa CHADEMA kuachana na wazo la kusimamisha mgombea Urais uchaguzi ujao ili kujiepusha kupoteza fedha zinazoweza kuwasaidia hata kujenga ofisi zao za chama au kufungua hata kituo cha TV kwa ajili ya kurusha matukio yao katika kuwafikia watu wengi sana kama ilivyo kwa chama makini cha CCM.

Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Samia ni mwepesi sana, kashindwa kuvaa viatu vya Magufuli. Samia ameuza bandari, na tarehe 1 mwezi 11 Waarabu wanaanza kazi.

Samia kauza Ngorongoro, yaani hakubaliki kabisa.

Mtaani anadharauliwa sana hata na wanaojiita chawa wa mama/ ChawaWaMama.

Bila matumizi makubwa ya jeshi, polisi, Tiss na wizi wa kura, anaangushwa mchana kweupe
Rasilimali zetu ni salama katika mikono salama ya Rais samia.Pia napenda kuendelea kusema ya kuwa hakuna mwenye uwezo wala ubavu wa kushindana na Rais samia katika sanduku la kura. Hayupo mtu huyo .kama yupo niambie ni nani ili nikupe uchambuzi wangu.
 
Tutaweka tume huru si ndio eeeeenh na TISS watakaa mbali eti eeeeenh. Vipi polisi nao, tutawaonya wawe mbali na wagombea?,

Wakurugenzi wa wilaya tutawaomba wawe fair?
Hata ije Tume ya Uchaguzi kutoka Marekani bado CCM na Rais Samia atashinda na kupitaa kwa kishindo,kutokana na kuwa na sera na ajenda bora zinazogusa maisha ya watanzania nazilizoleta matoke chanya katika maisha yao.
 
Kama unaamini hili andiko lako, hebu shauri huyo Rais wako uwekwe mjadala wa wazi na liwepo jopo lisiloegemea upande wowote, maswali yaulizwa na kila mmoja ajieleze hasa kwa miaka 10 ijayo ataisadiaje Tanzania kiuchumi, hasa kuhusu ukosefu wa dollar, kupanda kwa gharama za maisha, diesel na petrol bei yake kuwa juu, ukosefu wa umeme imara, hali duni ya maji vijijini na mjini na kuhusu suala la Ngorongoro
Pia kuhusu mikataba ya madini, bandari, gesi, makaa ya mawe, ardhi na misitu yetu, rushwa na kuteua viongozi wasio na uwezo
Kama hatakimbia na kusahau kire....mba jukwaani

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Kama unaamini hili andiko lako, hebu shauri huyo Rais wako uwekwe mjadala wa wazi na liwepo jopo lisiloegemea upande wowote, maswali yaulizwa na kila mmoja ajieleze hasa kwa miaka 10 ijayo ataisadiaje Tanzania kiuchumi, hasa kuhusu ukosefu wa dollar, kupanda kwa gharama za maisha, diesel na petrol bei yake kuwa juu, ukosefu wa umeme imara, hali duni ya maji vijijini na mjini na kuhusu suala la Ngorongoro
Pia kuhusu mikataba ya madini, bandari, gesi, makaa ya mawe, ardhi na misitu yetu, rushwa na kuteua viongozi wasio na uwezo
Kama hatakimbia na kusahau kire....mba jukwaani

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Hakuna suali linaloweza kumshinda wala kumbabaisha Rais Samia.kwa kuwa ni kiongozi mfuatiliaji na mwenye Taarifa zote kiganjani pake,lakini pia ni kiongozi aliyefanya makubwa katika Taifa letu ambapo hakuna wa kuweza kushindanishwa naye iwe katika mjadala au sanduku la kura.
 
Samia ni mwepesi sana, kashindwa kuvaa viatu vya Magufuli. Samia ameuza bandari, na tarehe 1 mwezi 11 Waarabu wanaanza kazi.

Samia kauza Ngorongoro, yaani hakubaliki kabisa.

Mtaani anadharauliwa sana hata na wanaojiita chawa wa mama/ ChawaWaMama.

Bila matumizi makubwa ya jeshi, polisi, Tiss na wizi wa kura, anaangushwa mchana kweupe
Sisi chawa ndiyo dawa yenu. Tumewashinda kabisa kihoja. Poleni
 
Sisi chawa ndiyo dawa yenu. Tumewashinda kabisa kihoja. Poleni
Kw aiyo wewe unalipwa bei ngapi ili usababishe wananchi wa Hali ya chini kuishi Maisha ya tabu naomba utwambie na kuliweka bayana hili mikopo kibao kusainisha mikataba isiyo na tija kutuweka lehani wananchi vitu kupanda bei tunomba mnaotwambia katiba mpya msamarise basi tufahamu kinachojiri ktk hiyo katiba mnaoelekeza sisi tuiombe
 
Kw aiyo wewe unalipwa bei ngapi ili usababishe wananchi wa Hali ya chini kuishi Maisha ya tabu naomba utwambie na kuliweka bayana hili mikopo kibao kusainisha mikataba isiyo na tija kutuweka lehani wananchi vitu kupanda bei tunomba mnaotwambia katiba mpya msamarise basi tufahamu kinachojiri ktk hiyo katiba mnaoelekeza sisi tuiombe
Uzushi na uongo. Hakuna mikopo wala kuuzwa sijui nini. Ni propaganda tu nyie wahuni tulishawazoea
 
Uzushi na uongo. Hakuna mikopo wala kuuzwa sijui nini. Ni propaganda tu nyie wahuni tulishawazoea
Mwananchi nisie na chama naitaji kuwa Mahala pazuri tarifa zinazotrend ndio izo sasa ww unawezaje kusema sio kwer ni swala la muda tu tunaomba msamarise iyo katiba nasi tujue tuna pingana kwa hoja zipi nasio kupiga makelele kutuuumiza masikio
 
Nchi haina Rais na hata 2025 sioni wa kugombea bora aliepo aendelee tu maana heri uozo tunao ujua kuliko uozo mpya.
Nchi ina Rais Imara, shupavu ,jasiri na madhubuti madarakani ndio maana unaona uchumi wetu ukiendelea kufanya vizuri sana,maisha ya watanzania yakiendelea kuwa bora na yenye kuleta matumaini,huduma za kijamii zikiendelea kupelekwa karibu zaidi ya wananchi. Miradi ya maendeleo ikiendelea kujengwa kila mahali inayochochea maendeleo na fursa za ajira kwa maelfu ya vijana.
 
Nchi ina Rais Imara, shupavu ,jasiri na madhubuti madarakani ndio maana unaona uchumi wetu ukiendelea kufanya vizuri sana,maisha ya watanzania yakiendelea kuwa bora na yenye kuleta matumaini,huduma za kijamii zikiendelea kupelekwa karibu zaidi ya wananchi. Miradi ya maendeleo ikiendelea kujengwa kila mahali inayochochea maendeleo na fursa za ajira kwa maelfu ya vijana.
Bado sijaona knachokiongelea apa maendeleo gani hayo mpka rufiji inanyufa zakutosha😂
 
Ndugu zangu Watanzania,

Urais ni nafasi nyeti na kipekee sana,ni nafasi inayohitaji mtu mwenye akili kubwa ya kuweza kujuwa,kufahamu na kutambua namna ya kutumia akili kubwa zote nchini katika kuleta matokeo chanya katika maisha ya watu,Ni nafasi

0742-676627.
Tumekisikia.. Sasa hebu iwepo tume huru isiyokua nominated na Rais!! Then ile article ya matokea ya urais marufuku kupelekwa Mahakaman na tume ya uchaguzi kutoshtakiwa viondolewe kwanza!! Iwe fair grounds, ndipo uongee haya...
 
Back
Top Bottom