Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,879
Takriban watu 17 wamejeruhiwa na shambulizi la angani la Urusi kwenye hospitali ya Mariupol, kulingana na utawala wa kijeshi wa Ukraine katika eneo la mashariki la Donetsk.
Wafanyikazi na wanawake walio katika harakati za kijifungua walikuwa miongoni mwa waliojeruhiwa, maafisa walisema.
Pavlo Kyrylenko, mkuu wa utawala wa kijeshi wa Ukraine katika eneo la Donetsk, alisema idadi ya watoto waliojeruhiwa "ni sifuri, namshukuru Mungu, na ninatumai itasalia kuwa hivyo".
BBC Swahili