zitto kabwe

Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe (Zitto Kabwe)
Zitto Zuberi Ruyagwa Kabwe, maarufu kama Zitto Kabwe, ni mwanasiasa kutoka Tanzania kutoka chama cha ACT-Wazalendo. Zitto aliwahi kuwa mwanachama wa Chama Demokrasia na Mendeleo (CHADEMA) toka mwaka 1992 mpaka 2015 alipoachana na chama hicho.

Zitto ameshika nafasi ya Kiongozi wa Chama ACT-Wazalendo kwa miaka 9, mpaka March 2024 ambapo nafasi hiyo imechukuliwa na Dorothy Semu. Amewahi kuwa Mbunge wa Tanzania kwa vipindi viwili kuanzia 2005 mpaka 2015 akiwakilisha Jimbo la Kigoma Kaskazini.
  1. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Zitto Kabwe: Thamani ya uhai katika nchi yetu inapotea. Watu kama Watendaji wa Vijiji nao pia wanakamata, kutesa na kuua

    "Thamani ya uhai katika nchi yetu inapotea. Matendo ya utekaji wa watu kama vile kina Mdude, Kina Soka, Kina Sativa na watu wengine inawafanya watu kama watendaji wa Vijiji kuona kwamba wanaweza nao pia kukamata, kutesa mpaka kuua." Amesema Zitto. Zitto amebainisha kuwa Ibara ya 14 ya Katiba ya...
  2. Erythrocyte

    Godbless Lema ashangaa Porojo za Zitto Kabwe

    Soma hapa uone unafiki usioeleweka wa Zitto kabwe
  3. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Zitto Kabwe: Ukifanyia utani bunge, utakuwa umefanyi utani uhai wa taifa

    Kiongozi Mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema Ukifanyia utani bunge, utakuwa umefanyi utani uhai wa taifa na ili kuhakikisha bunge alifanyiwi utani watu wa Tabora pigine moyo konde tukapambane na kurejesha thamani bunge na kuibana serikali na kuzia wizi. Kupata matukio na...
  4. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Zitto Kabwe: Tusiwaache CCM peke yao kwenye uchaguzi. Twende tukapambane nao, twende tukalinde kura

    Tusiwaache CCM peke yao, twende tukapambana nao, twende tukalinde kura ndio maana tukasema oktoba linda kura inawezekana katika majimbo 222 tusipate zote lakini hatutakosa majimbo 40 au 50 na kuondoa bunge butu Alisema Zitto Kabwe katika Operesheni Ya Majimaji mkoani Tabora Kupata matukio na...
  5. Roving Journalist

    GE2025 Zitto Kabwe: Tusiruhusu Miaka mitano mingine ya Bunge kibogoyo

    Kiongozi Mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe akizungumza katika mkutano wa hadhara Mkoani Kigoma, leo Julai 2, 2025 amewataka Wananchi kutotoa nafasi nyingine ya miaka mitano kwa Bunge alilosema limeshindwa kuisimamia Serikali na kutetea maslahi ya Watu. Ameyasema hayo katika Uwanja...
  6. Roving Journalist

    GE2025 Zitto Kabwe: Watanzania Milioni 26 wanaishi katika dimbwi la umasikini kisha Viongozi wanasifia mabilioni ya Rais

    https://www.youtube.com/live/7OENoZqIQCM Updates Act Wazalendo tunataka kufanya mabadiliko ya nchi hii na mabadiliko ya nchi hii atuwezi kuyafanya kwa kuyabembeleza, wameshanogewa wameshakolea na wanaona wanaweza kufanya chochote, natunasema hatuikimbii hii vita na muhuni hasusiwi Simba Jike...
  7. BLACK MOVEMENT

    Zitto Kabwe simuoni akitoboa Kigoma na itakuwa ndio mwisho kabisa wa siasa zake. Kamanda Silo lazima alipe fadhili.

    Kamanda Silo lazima alipe fadhili kwa alioe .teua na hapo ndio pagumu kwa Zitto Kabwe. Simuoni akitoboa Kigoma na itakuwa ndio mwisho kabisa wa siasa zake, atakuwa na optional moja tu, ya kuwa kama Mrema. Hata wale wenzake wa ACT sioni Jimbo la wao kushinda labda kule Pemba.
  8. Just Pray

    Mnyukano mkali kati ya Zitto, Mwigulu na Profesa Tibaijuka kuhusu pendekezo la kutoza ushuru wa 10% kwenye mapato yaliyobaki (retained earnings)

    Wakuu Hapa nimewasogezea Mnyukano mkali niliokutana nao mtandao wa X kati ya Zitto Kabwe, Waziri wa fedha Mwigulu Nchemba na Profesa Anna Tibaijuka kuhusu pendekezo la kutoza ushuru wa 10% kwenye mapato yaliyobaki (retained earnings) Zitto Kabwe (12 Juni 2025): Alikosoa pendekezo la ushuru wa...
  9. W

    PreGE2025 Zitto atoa shule kwa lugha nyepesi kuhusu operesheni yao kwa ambao hamkuelewa

    Zitto anazidi kutoa shule huko X kwa wananchi wanaohoji ni kwa vipi watafanikiwa na operereshin yao ya #lindaKura "Kwa lugha nyepesi: tutalinda kura kwenye kituo cha kupigia kura kwa kupiga kura, kusimamia ikihesabiwa na matokeo kubandikwa. hakuna kura bandia itaingia kituoni hakuna wakala wa...
  10. W

    PreGE2025 Zitto: Wizi wa kura ni uhuni

    Zitto kabwe kupitia ukurasa wake wa X alipokuwa akimjibu Sativa ameandika kuwa "Kanuni imehalalisha wizi wa kura? Wizi wa kura ni uhuni. Mtu anayefanya uhuni na hatendi kwa mujibu wa sheria hushughuliki naye kinyonge na kwa mujibu wa sheria. Oktoba #LindaKura Tunayo njia. #MuhuniHasusiwi"
  11. Kyenju

    Wakuu! Vipi ili tangazo la Salimu Kikeke na Zitto Kabwe

    Hii ni sehemu sahihi ya kuwekeza, au ni upigaji mpya. ================= Ufuatiliaji uliofanywa na JamiiCheck kwa kutumia utafutaji wa maneno muhimu (Key word search) umejiridhisha kuwa video hiyo imepotoshwa kutoka kwenye video halisi ambayo ni sehemu ya matangazo mbashara ya kipindi cha...
  12. Heparin

    PreGE2025 John Mrema ajisahau kubadili Akaunti ya X, atumia ya CHAUMMA kumtolea povu Zitto Kabwe. Asema ACT ipo kata 2 tu Tanzania Bara

    John Mrema amejisahau kubadili Akaunti ya X, ametumia ya CHAUMMA kumtolea povu Zitto Kabwe. Amesema Zitto Kabwe ameshindwa kukuza chama cha ACT, kwa Tanzania bara kipo kata 2 tu za Tunduru na mojawapo ipo Kigoma. Haya yanajiri baada ya Zitto Kabwe kuwakaribisha wanachama wa vyama vingine...
  13. Yoda

    Mahubiri ya Gwajima yamuibua Zitto Kabwe akichukizwa na mauaji ya watoto na raia wasio na hatia huko Gaza!

  14. W

    PreGE2025 CCM Arusha yapinga madai ya kuifadhili CHAUMMA, Yasema kama ni kuiua CHADEMA ingewekeza nguvu kwa Zitto Kabwe

    Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Katibu Mwenezi wake wa Mkoa wa Arusha, Saipulani Ramsey, kimepinga vikali madai yanayoenezwa mitandaoni kuwa kinakiwezesha Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), hususan kiuchumi. Baadhi ya watumiaji wa mitandao wamehoji chanzo cha fedha za CHAUMMA na kasi ya...
  15. Erythrocyte

    Zitto Kabwe afunguliwa kesi na Harbinder Singh kisa sakata la IPTL

    Kiongozi Mkuu mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa zamani Zitto Kabwe amefunguliwa Kesi na Harbinder Singh Seth akidaiwa kumkashifu mfanyabiashara huyo na kumvunjia heshima mbele ya jamii Akizungumza na wanahabari leo Zitto Kabwe amesema kuwa kesi hiyo imetokana na yeye kuzungumzia...
  16. Yoda

    Kwanini Zitto Kabwe anataka watu wapoteze muda kujadili viporo vya IPTL/ESCROW wakati huu?

    Ni kwamba Zitto Kabwe hajui wazi hakuna mtu mwenye akili timamu mwenye muda wa kufuatilia tena na IPTL/ESCROW nyakati hizi, hakuna mtu mwenye akili timamu atakayefuatilia suala ambalo inajulikana hakuna pesa zilizokwapuliwa zinazoweza kurujeshwa tena au mtu yeyote aliyekwapua atakayewajibishwa...
  17. Roving Journalist

    Zitto Kabwe anatoa tamko, asema Seth amemfungulia kesi, atakiwa kulipa bilioni kadhaa

    https://www.youtube.com/watch?v=lWxel_pUiVk Kiongozi Mkuu mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa zamani Zitto Kabwe amefunguliwa Kesi na Harbinder Singh Seth akidaiwa kumkashifu mtu huyo na kumvunjia heshima mbele ya jamii. Akizungumza na wanahabari leo Zitto Kabwe amesema kuwa kesi...
Back
Top Bottom