uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. K

    GE2020 TAKUKURU toeni ripoti ya ukweli kuhusiana na uchaguzi jimbo la Rorya

    Tarehe 21 Julai, 2020 kulikuwa na mchujo wa watia nia kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Rorya. Mambo hayakwenda kama ilivyotarajiwa na kulikuwa na harufu kubwa ya rushwa. Wengi waliopata alama za juu aidha kuna mbinu iliyotumika na kuwawezesha kupata kura nyingi. Tunaiomba Takukuru...
  2. T

    GE2020 Akili nje ya Usalama: Undeni special unity kufuatilia maudhui ya mikutano ya uchaguzi 2020

    Nawaza nje ya Box naipenda Tanzania na ipenda amani yetu na penda taifa langu na viongoz wake. Kipenda kimepulizwa na tume ya uchaguzi na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi amesha sema sasa ruhusa watu kujinadi. Ila nawaza ikiwa idara zetu zimejiandaaje kwa uchaguz wa mwaka huu ambao utakuwa tofauti...
  3. GE2020 Rais Magufuli avitaka Vyombo vya Ulinzi kutotumia nguvu pasipostahili wakati wa Kampeni na Uchaguzi

    Rais Dk John Magufuli amevitaka vyombo vya ulinzi kutotumia nguvu mahali ambapo hapastahili kutumia nguvu wakati wa kampeni na uchaguzi wa mwaka huu, huku akiamini kuwa kampeni zote zitafanyika kistaarabu kwa amani. Rais Magufuli ametoa kauli hiyo hii leo wakati akizindua Jengo la Tume ya...
  4. GE2020 Malalamiko: Ukiukwaji wa taratibu za Uchaguzi jimbo la Handeni Vijijini

    KATIBU MKUU CHAMA CHA MAPINDUZI, S. L. P. 50 DODOMA 22/07/2020 Ndugu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Dkt Bashiru Ally YAH: UKIUKWAJI WA TARATIBU ZA UCHAGUZI JIMBO LA HANDENI VIJIJINI Husika na kichwa cha Habari, Kwa heshima kubwa kwanza tunakupongeza kwa kusimamia taratibu, kanuni na...
  5. S

    GE2020 Wajumbe wa Kamati ya Uchaguzi CCM jimbo la Butiama mtalaaniwa

    Wajumbe wa Kamati ya Uchaguzi wa CCM jimbo la Butiama, mmefanya kitendo kibaya sana. Katika kura za maoni mmeshindwa kumuenzi Baba wa Taifa Mwl. Nyerere kwa kumchagua mtoto mmoja wa Baba wa taifa kweli mmeshindwa? Familia ya Baba wa Taifa imetoa wagombea wawili katika hao mmeona hakuna...
  6. CHADEMA msichekelee wabunge wenu waliohamia CCM kupigwa chini kura za maoni. Waliobaki zamu yao ya kupigwa chini inakuja Uchaguzi Mkuu Oktoba

    Kuna msemo usema mwenzio akinyolewa wewe tia maji CHADEMA msichelee wabunge wenu waliohamia CCM kupigwa chini kura za maoni ndani ya CCM Hao wenu Waliobaki huko wasijione kuwa salama watashinda na kuzomea wenzao wahamiaji walioshindwa kura za maoni !!! Hao waliobaki CHADEMA watakoshindana na...
  7. M

    Kwa CCM ni ipi dhana ya kuwa uchaguzi kwa watia nia?

    Habari wakuu! Kila siku Kuna habari mpya nchi Tanzania kutokana na Taifa linaenda kuingia katika uchaguzi wa viongozi. Mnamo 20/07/2020 uchaguzi kwa WATIA NIA ya kugombea upande wa chama Tawala ulianza na mpaka hivi Sasa unaendelea, lakin Jana mida ya saa 1 nimepata kuona kapost Fulani...
  8. Q

    GE2020 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC): Uchaguzi Mkuu utafanyika Oktoba 28, 2020

    Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetangaza tarehe rasmi ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani ambayo ni Oktoba 28, 2020. Aidha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetoa ratiba ya wateuzi wa Wagombea kiti cha Rais, Makamu wa Rais, Ubunge na Udiwani utakuwa ni Agosti 25, na...
  9. Leo imedhihirika kuwa bila CCM imara Tanzania itayumba. Tanzania kwa takribani wiki nzima imesimamishwa na Uchaguzi wa CCM

    Kwa kweli yaliyofanyika kuanzia Uchaguzi wa kuwapata wagombea Urais kule Zanzibar kuanzia ile tarehe 8 mpaka leo nchi yetu imesimama kwa maana ya uwazi wa mchakato wa uchaguzi ulivyokuwa Haijawahi kutokea popote Duniani kwa chama chochote tangu kuumbwa kwa Dunia kuwa na mvuto kama wa CCM mwaka...
  10. NEC igeni CCM jinsi ya kuhesabu kura. CCM mmeonyesha mfano

    Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM, ameagiza kwamba kura za maoni za Ubunge, uwakilishi na udiwani zinazoanza leo zihesabiwe hadharani kama ilivyokuwa wakati kuhesabu kura za Wagombea Urais wa Zanzibar.
  11. Kipi kifanyike baada ya uchaguzi wabunge wasiowajibika kwa wananchi

    Wana jamii, kwa sasa tunashuhudia majimboni wagombea mbalimbali wakipambana kuwa wawakirishi wa wananchi. Ukizingatia wananchi wote hatuwezi kwenda bungeni kujadili maendeleo yetu. Hivyo ni lazima watu wachache wachaguliwe ili kuwawakilisha wananchi baada ya kufanya mikutano na wananchi hivyo...
  12. GE2020 Singida Magharibi na Halmashauri ya Wilaya Ikungi msiachie lulu hii

    Na Fundi madirisha, Nawasalimu sana ndugu zangu wananchi wa jimbo la Singida Magharibi. Mwafanga naa! Amuchii! Kwa ufupi ndugu zangu wa jimbo la Singida Magharibi hasa wapiga kura za maoni nataka niwadokezee kidogo, mna mtu mmoja mpambanaji na ni mtu wa kazi sana anaitwa HAMISI LISSU MAHANJU...
  13. GE2020 Kwanini kura za Uchaguzi Mkuu hazihesabiwi hadharani kama za CCM kuchagua wagombea?

    Napendekeza na kura za uchaguzi mkuu kuanzia Udiwani, ubunge na urais zihesabiwe kwa uwazi mbele ya wapiga kura kama wanavyofanya CCM katika kura za urais na ubunge? Naomba mwaka huu iwe hivyo
  14. J

    Wazee Kilimanjaro wamuandalia Rais Magufuli zawadi maalumu, mangi Mareale amuahidi ushindi wa kishindo Uchaguzi Mkuu

    Viongozi wa kimila mkoani Kilimanjaro wamemuandalia zawadi maalumu Rais Magufuli pindi atakapozuru mkoani humo hivi karibuni Mangi Marealle amesema mwaka 2015 hawakumpa Rais Magufuli kura za kutosha lakini mwaka huu wanamuahidi ushindi wa kishindo kutoka pande zote za mkoa wao. Chanzo: ITV...
  15. J

    Uchaguzi huru na haki maana yake nini?

    Je, mpinzani akishinda ndiyo huru na haki? Au kuna vigezo vingine?
  16. Serikali ihamishie maslahi ya wabunge kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya

    Kazi ya Bunge ni kutunga sheria na kuishauri Serikali. Lakini kama mkuu wa wilaya akiongezewa kazi za kusimamia kabisa kila shughuli za maendeleo ya wilaya huku akihakikisha mgawanyo wa keki ya taifa wilayani kwake atakuwa anafanya kazi kubwa kuliko Mbunge. Napendekeza Ili kuwapiga chenga za...
  17. Uchaguzi 2020-Huduma ya Strategic Campaign Management and Analytics

    Habari za Wakati huu: Kama ilivyo ada sisi watazam fursa huwa tunaangalia ni namna gani tunaweza kutoa huduma tofauti kwa watu tofauti. Masoko Consultants Tunakuletea huduma adhimu na ya kipekee kabisa wewe Mgombea wa nafasi ya Ubunge na Udiwani.Ni huduma ya Strategic Campaign Managament and...
  18. Mchango wa WanaJF Kuelekea Uchaguzi wa Kidemokrasia 2020

    Ndugu wana JF, Ninawasilisha ombi kwenu kujitolea kuchangia nchi yetu iweze kufanikisha uchaguzi wa kidemokrasia (2020) kwa lengo la kuimarisha utawala bora katika taifa letu. Pengine tuanze kutoa ushauri wa kitaalam kwa vyama vya siasa na wagombea kila mara wawe wanakuja hapa kuchota maarifa...
  19. T

    Chama cha wamiliki wa silaha/bunduki nchini Marekani wametangaza kumuunga mkono Trump Uchaguzi Mkuu

    Chama cha wamiliki wa bunduki wa Marekani, National Riffle Association kimetangaza kumuunga mkono Rais Donald J. Trump au maarufu kama Tarrif Man kwenye uchaguzi mkuu ujao wa November 3, 2020 NRA wanasema mtu pekee ambae anaweza kuwahakikishia uhuru wao wa kumiliki siraha ni Trump kwani Biden...
  20. Uchaguzi Mkuu 2020: Brigedia Jenerali, John Mbungo, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU awaonya Wafanyabiashara na Wanasiasa

    TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru) nchini Tanzania, imetahadharisha wafanyabishara kutojihusisha na vitendo vya rushwa, kupitia dhana ya ufadhili wa gharama za uchaguzi ndani ya vyama vya siasa. Hayo amesema Brigedia Jenerali, John Mbungo, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…