uchaguzi mkuu 2025

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Job Ndugai: Mimi ndiye Mke wenu Mkubwa

    Job Ndugai ameendelea kuonja joto ya jiwe kutoka jimboni kwake huko kwao Dodoma. Hali si hali, awashuku waliopangwa kumzomea mkutanoni akimwaga Sera.
  2. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Steve Nyerere: Polepole kumsema Rais vibaya siyo Miiko wa Maadili

    Msanii na mwanaharakati maarufu, Steve Nyerere, amemjibu aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, kufuatia matamshi yake ya kumkosoa Rais Samia Suluhu Hassan. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Steve Nyerere amesema kauli za Polepole hazioneshi...
  3. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Jokate: Vijana CCM baada ya Uchaguzi Makundi yavunjike, turudi Mezani kuijenga Jumuiya Yetu, na Chama

    Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Jokate Mwegelo, amesema vijana wanapaswa kuendeleza misingi ya ujamaa, amani, upendo na mshikamano hata baada ya kukamilika kwa uchaguzi wa wabunge wa viti maalumu ndani ya jumuiya hiyo. Ametoa wito kwa vijana wa CCM kutambua kuwa...
  4. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Salim Kikeke: Nitaongeza thamani ya Soko la Nguruwe Jimboni

    Mtia Nia wa Ubunge Jimbo la Moshi Vijijini ndugu Salim Kikeke amesema kuwa atasaidiana na wadau mbalimbali kutafuta soko na kuongeza thamani ya Nguruwe katika Jimbo hilo ikiwa pamoja na kuvutia wawekezaji na hatimaye mfugo huo upate soko la Kimataifa. Soma > Salim Kikeke mbunge mtarajiwa wa...
  5. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Arusha: Waliosema Rais Samia asichanganye Siasa na Mila, walipa faini ya Dume la Ng'ombe na kukwepa kuchapwa Fimbo 70

    Vijana wawili wa jamii ya kimasai Mkoani Arusha wamepigwa faini ya Dume moja badala ya kuchapwa fimbo 70 baada ya kumkashifu Rais Wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika eneo la kata ya Elerai Mkoani Arusha. Akizungumza katika Mkutano wa Mila ulioitishwa ili kulaani kitendo hicho Kiongozi wa...
  6. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Dkt. Albanie: Polepole anataka kuharibu Uchaguzi, apuuzwe

    Aliyekuwa mtia nia wa ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Mvomero mkoani Morogoro, Dkt. Albanie Marcossy, amejitokeza na kumtaka hadharani mwanachama wa chama hicho, Humphrey Polepole, kupuuzwa na wanachama wengine kwa madai kuwa kauli zake za hivi karibuni zimejaa "vihoja...
  7. DuaZaMama

    JamiiForums Tanzania GE2025 Watia Nia Wawili wa ubunge matatani Kwa kutoa Rushwa Kwa wajumbe

    Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Temeke, Holle Makungu, amesema kuwa katika kipindi cha Aprili hadi Juni mwaka huu, taasisi hiyo imewahoji na kuwaachia kwa dhamana watia nia wawili wa nafasi ya Ubunge katika Majimbo mawili tofauti kwa tuhuma za kushawishi na...
  8. The Watchman

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mgombea wa Nafasi ya Ubunge Viti Maalumu Kupitia UVCCM Vijana Jasmine Mumbi apiga magoti kuomba kura za wajumbe

    Mgombea wa Nafasi ya Ubunge Viti Maalumu Kupitia UVCCM Vijana ( Jasmine Mumbi ) akipiga Magoti Kuwaomba Kura za Ndio Wajumbe wa MKUTANO Mkuu Maalumu wa UVCCM Taifa .
  9. tonicimmobility

    JamiiForums Tanzania GE2025 Pwani: Wajumbe Kibaha wawakataa watia nia wa udiwani wakisema kuwa ni wazee

    Wajumbe kutoka wilaya ya Kibaha mkoani Pwani wamesusia mkutano wakiwa na lengo la kuwakataa watia nia wa udiwani na kudai ya kuwa ni wazee. Tukio hilo limefanyika leo agosti 1, 2025 likionyesha wajumbe wakiwa barabarani wakitoa maneno ya kuwakataa watia nia wa udiwani. Soma pia: CCM mlione...
  10. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mchengerwa: Tutamuomba Rais Rufiji iwe Mkoa

    Mtia Nia ya Ubunge wa Jimbo la Rufiji, Mohamed Omary Mchengerwa ambaye ndiye Mbunge anayemaliza muda wake, akinadi sera zake mbele ya wajumbe na kuomba kura kwa wajumbe wa Chama cha Mapinduzi Kata ya Mbwara iliyopo katika Jimbo hilo lililopo Mkoa wa Pwani, ameeleza kuwa kutokana na Maendeleo...
  11. R

    JamiiForums Tanzania GE2025 Hatma ya Watanzania wanaoishi diaspora kushiriki uchaguzi mkuu 2025 bado haieleweki

    Uchaguzi Mkuu wa Tanzania wa 2025 unakaribia kwa kasi, lakini bado Watanzania wanaoishi nje ya nchi wanaendelea kutengwa na mchakato wa kidemokrasia. Pamoja na miaka ya mijadala na ahadi kutoka kwa viongozi wa kisiasa kuhusu mageuzi ya uchaguzi, hakuna hatua madhubuti zilizochukuliwa kuwezesha...
  12. The Watchman

    JamiiForums Tanzania GE2025 Jesca Magufuli: Nitakuwa sauti ya vijana na kuwatetea

    Mgombea Ubunge wa Viti Maalum kupitia kundi la Vijana, Jesca Magufuli (29), ameomba kura mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, akiwani nafasi mojawapo kati ya sita zinazogombewa upande wa Tanzania Bara. Jesca ni msomi mwenye Shahada ya...
  13. The Watchman

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mgombea ubunge viti maalum mwenye umri mdogo zaidi akiomba kura aahidi kuwasemea vijana kuhusu ajira

    Mgombea Ubunge wa Viti Maalum kupitia kundi la Vijana, Lightness Greyson Kihombo (23), ameomba kura mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, akiwania mojawapo ya nafasi sita kwa upande wa Tanzania Bara. Lightness, ambaye ni mgombea mwenye...
  14. The Watchman

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mkurugenzi wa Uchaguzi INEC: Changamoto ya mawakala tumejirekebisha

    Tume ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imesema imezifanyia kazi changamoto mbalimbali mawakala katika chaguzi zilizopita na kuwa hazitatokea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Jumatano, Oktoba 29, 2025. Hakikisho hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Kailima Ramadhani leo Ijumaa...
  15. R

    JamiiForums Tanzania GE2025 Jesca Magufuli Mgombea Ubunge Viti Maalum Kundi la Vijana Geita akiomba kura kwa wajumbe

    Mgombea wa Nafasi ya Viti Vya UBUNGE Viti Maalumu CCM Kupitia Vijana tokea Mkoani Geita, Jesca John Magufuli akijitambulisha Mbele ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa UVCCM Leo Dodoma
  16. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 RC Chalamila: Atakayetujaribu, tutafanya kweli. Hakuna atakayetikisa Amani ya Taifa hili

    Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akizungumza kwenye ufunguzi wa Kituo cha Biashara na Usafirishaji Afrika Mashariki (EACLC) Ubungo, leo tarehe 1 Agosti, 2025 amesema; "Mhe. Rais, wewe unagombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, sisi vijana wako tunakuombea kila la heri na...
  17. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Wakili wa Lissu, Nshala: Askari Magereza anakujaje Mahakamani amefunika uso Kininja?, Yeye siye ambaye anamshitaki Tundu Lissu

    Wakili wa Tundu Lissu, Rugemeleza Nshala amesema kitendo cha Mahakama kuruhusu Askari Magereza kuingia Mahakamani wamejifunika Kininja ni kinyume cha Katiba. "Inakuaje mahakama ambayo ni muhimili huru inakubali kuingiliwa na askari magereza" Soma > Askari Magereza wamsukuma Lissu kidogo...
  18. R

    JamiiForums Tanzania GE2025 Wajumbe Mkutano Mkuu UVCCM kupiga kura kuchagua wabunge viti Maalum, Dodoma

    Wajumbe Mbalimbali wa Mkutano Mkuu Wa UVCCM hapa Mtumba Dodoma, Kwenye Mkutano Mkuu Maalumu , ambapo Leo Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wanapiga kura kuchagua Wabunge wa Viti Maalumu watakaowakilisha Vijana wa Chama Hicho
  19. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mwenyekiti wa INEC: Hakuna Sheria inayoruhusu Diaspora kupiga Kura Oktoba 29,2025

    Mwenyekiti wa Tume ya Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufaa Jackobs Mwambegele, wakati akizungumza na Wahariri wa vyombo vya Habari Jijini Dar es Salaam amesema hakuna sheria inayoruhusu Diaspora Kupiga Kura katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29 mwaka huu.
  20. Waufukweni

    JamiiForums Tanzania GE2025 Mwenyekiti wa INEC: Hakuna Sheria inayoruhusu Kura za mapema kupigwa

    Tume ya Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imesema hakuna sheria inayoruhusu kura za mapema kupigwa kwa upande wa Tanzania bara katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29 mwaka huu. Kura hiyo ni ile ambayo itapigwa Zanzibar na baadhi ya watu, ambazo siku ya uchaguzi watakuwa na majukumu ya...
Back
Top Bottom