tcra

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (pia huitwa kwa Kiingereza: Tanzania Communications Regulatory Authority ambapo mara nyingi huitwa kwa kifupi: TCRA) ni taasisi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye majukumu ya kusimamia sekta za mawasiliano na utangazaji.

TCRA Ilianzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya mwaka 2003 kusimamia huduma za kielektroniki na posta na masafa ya mawasiliano nchini Tanzania. Mamlaka ilianza kazi tarehe 1 Novemba 2003 na inafanya shughuli za zilizokuwa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).

Mamlaka ya TCRA ni kusimamia sekta ya posta, mawasiliano ya kielektroniki na utangazaji katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na:
  • Kuzifanya shughuli za TCRA kuwa za kisasa kwa kutumia teknolojia sahihi;kuimarisha tafiti zenye ubora katika huduma zinazodhibitiwa, uwezo na umahiri wa watumishi.
  • Kukuza ufanisi; kuaminika na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya mawasiliano na matumizi yake.
  • Kukuza ufanisi na unafuu wa huduma za Mawasiliano na kuongeza upatikanaji wa huduma za Posta na TEHAMA katika maeneo yasiyohudumiwa ipasavyo na yale yasiyo na huduma kabisa.
  • Kulinda maslahi ya wadau na kukuza uelewa wa haki na wajibu wao.
  • Kufuatilia utendaji wa huduma zinazosimamiwa na kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na Kanuni kwa viwango vinavyostahili.
  • Kuratibu utekelezaji wa ahadi za kisekta kitaifa, kikanda na kimataifa.
  • Kufikia kiwango cha juu ya kuridhisha wateja kama ilivyoainishwa kwenye Mkataba wa Huduma kwa Mteja wa TCRA.
  • Kuendelea kuzingatia matakwa ya kisheria na kiusimamizi.

Sera zinazoathiri utendaji kazi wa TCRA ni pamoja na:
  • Sera ya Taifa ya Mawasiliano ya mwaka 1997
  • Sera ya TEHAMA ya mwaka 2003
  • Sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003
  1. Kapepo

    Mtandao wa simu mlichonifanyia kinaumiza sana moyo wangu

    Kwekweli leo nilikuwa na mihadi na demu wangu mpya sijawahi kula hata siku moja keshakula vyangu leo ijumaa tumepanga tukatiane namcheki muda huu naambiwa namba nayopiga imezuiliwa kupokea simu kwa sasa nijaribu tena baadaye hii hali inaniumiza mno kwakweli 😥😥😥😥
  2. TODAYS

    TCRA Msiache kuzima hizi makampuni za simu, voda ikiwemo

    Twende moja kwa moja kwa mada. Umemuomba mtu pesa ili ununue dawa kwa ajili ya mgonjwa uliyemuacha hospitali ukiwa njiani unasikia mlio wa meseji, unasogea pembeni kwa tashwishwi kuwa jamaa yako kakusapoti. Au unadhania ni taarifa kutoka hospitali ulipomuacha mgonjwa kuwepo kwa mabadiriko mara...
  3. idawa

    Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

    Binafsi nilijiandikisha tena mara mbili lakini nimefuatilia namba zangu NIDA kama naomba mkopo benki. Hakuna nilichoambulia. Uzembe wa NIDA usumbufu nabebeshwa mimi. Matokeo yake naambiwa nijiandikishe upya, yaani nianze taratibu za kwenda kwa Mtendaji, Uhamiaji halafu NIDA. --- Mambo ya...
  4. Babu Kijiwe

    TCRA fungeni haraka Laini yangu ili Branch na M-Power wasinisumbue

    Hawa wadai wangu wanapenda kunikumbusha kwa SMS hasa hawa Branch. Leo natangaza mwisho wao kwani line yangu inafungwa muda si mrefu sijui watamtumia nani SMS. Ikibidi TCRA yakwangu fungeni sasahivi, za wengine subirini sa 6 usiku. Ahsante NIDA kwa kutusaidia. Poleni M-Power poleni Branch...
  5. K

    TCRA na NIDA kubadilishana watumishi

    Hivi kwa nini hizi taasisi zisibadilishane watumishi yaani watumishi wa nida waende tcra na wale wa tcra waende nida ili wajaribu kuona jinsi ilivyo kazi kuwapatia watz wote vitambulisho kabla ya tarehe 20
  6. Craig

    Utapeli wa mtandao unaendelea kwa kasi, TCRA mpo wapi?

    Wezi wa kupitia mitandao wanaendelea kuibia watu kwa kutumia kila namna mitandao ya simu haitoi ushirikiano wa kutosha kwa wateja wao. TCRA nini maana ya kusajili laini kwa vidole na kitambulisho? Hawa wahalifu kwanini wasipewe adhabu iwe fundisho kwa wengine?
  7. Mstahiki Mea

    Fanya hivi kuepuka kukosa mawasiliano utakapofungiwa na TCRA kama hujasajili kwa alama za vidole

    Muda wa kutumia simu kadi ambazo hazijasajiliwa unafika ukingoni January 20 huku kukiwa na siku mbili tu mbele. Watanzania lukuki bado hawajakamilisha zoezi hili muhimu huku sababu kubwa ikitajwa ni NIDA kuwa na mwendo wa kinyonga, pamoja na hayo TCRA wametoa msisitizo kuwa hawataongeza muda...
  8. K

    TCRA na NIDA mtembelee Kigoma, Kagera na Ngara

    Natoa ushauri wa bure kabisa kwa Wakurugenzi Wakuu wa NIDA na TCRA kutembelea mikoa tajwa hapo juu kabla ya tarehe 20 mwezi huu ambapo line za simu zote zisizo na usajili wa kitambulisho cha NIDA zitasitishiwa huduma. Kama tukiendelea kuwafanyia Waha, Wahangaza na Wanyambo mambo tunayowafanyia...
  9. kagombe

    TCRA wakishazima line za simu waje mitaani sasa

    TCRA wakishazima line za simu waje mitaani sasa kuna kaujanja kanafanywa na hawa vijana wanasajili line mtaani. Tena ni hatari wanayofanya hawa vijana wasio waaminifu sijui ni tamaa ya pesa au njaa yao. Hapa tuwe makini tunaokwenda kusajili hapa kuna mchezo wanafanya usipokuwa makini unaweza...
  10. K

    Zikiwa zimesalia siku 4 TCRA wanena

    Zikiwa zimebaki siku nne laini za simu zisizosajiliwa kwa alama za vidole kufungiwa, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewaagiza Watanzania waliokamilisha usajili wa laini zao kuhakiki upya kwa kupiga namba *106#. “Kama mnavyofahamu, mwisho wa kutumika kwa laini za simu ambazo...
  11. Mau

    Hivi TCRA wanaitambua hii biashara ya Vodacom?

    Kuna kabiashara ka mkopo kameanzishwa na kampuni ya Vodacom, wanacharge riba pamoja na processing fee. Swali nililojiuliza ni mbona sipati message za mgawanyo wa hayo mapato kwa serikali kama vile wanavyotutumia ukinunua voucher? You have received an overdraft of TZS.10,107.00 You will be...
  12. beth

    Naibu Waziri Nditiye aagiza TCRA kukagua mabasi yote yanayosafirisha vifurushi bila kuwa na leseni

    Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, ameitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kuhakikisha wanasimamia na kukagua mabasi yote yanayosafirisha vipeto, bahasha na vifurushi bila ya kuwa na leseni kutoka Mamlaka hiyo na kuwataka wanaofanya hivyo kuacha...
  13. Analogia Malenga

    TCRA yafichua utapeli mpya wa fedha mitandaoni

    Angalizo hilo limetolewa baada ya kuibuka kwa kundi la watu waliobuni mbinu mpya kwa kutumia fursa hiyo kufanya utapeli jijini Mwanza kwa kuwashawishi kuwa usajili wa laini za simu kwa alama za vidole kwa kutumia kitambulisho cha taifa unaendana na uhakiki wa akaunti ya benki ya mhusika...
  14. Nancyjoa13

    TCRA, NIDA waanika siri kukwama usajili laini

    BENJAMIN MASESE - MWANZA MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) zimeeleza sababu zilizochangia wengi kushindwa kusajili laini za simu zao kwa wakati. Zimesema hadi kufikia Desemba 31, mwaka jana, laini za simu zilizokuwa zimesajiliwa kwa njia ya...
  15. Miss Zomboko

    TCRA yazipiga faini kampuni za simu kwa kushindwa kutekeleza masharti ya huduma bora

    Dar es Salaam. Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imezipiga faini kampuni saba za simu baada ya kushindwa kutekeleza masharti ya leseni na kukidhi viwango vya ubora wa huduma kwa mujibu wa Kanuni za Ubora wa Huduma za mwaka 2018. Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi na Utekelezaji wa Sheria wa...
  16. Kilele9

    TRA, NIDA na TCRA zishirikiane

    Viongozi na wataalamu wa TRA, TCRA na NIDA shirikianeni msiwe kama mpo nchi tofauti. Inavyoonekana hamuishauri serikali ipasavyo kwa kutokushirikiana kwenu. Serikali inapata kiasi kikubwa cha fedha kama kodi kupitia miamala inayofanyika kupitia mitandao ya simu. Kufungwa kwa laini za simu hata...
  17. MakinikiA

    TCRA mtakapofunga Simcard za watu mjiandae kulipa madeni ya kwenye simu

    Ebwana eee kwa yule anayeweza kukopa kwenye simu muda ndio huu kopa kopa kopa kwa bidii mlipaji yupo kwa maana fedha zipo pale TCRA za kulipa hayo madeni ,hakuna kampuni itakayokubali hasara kirahisi, Mpawa tu wana kama bilions of money hazijarejeshwa, ebwana wekeni mikakati kupata vitambulisho...
  18. Richard

    TCRA kufunga simu zisizosajiliwa ni mpango wa serikali kuwabana wale wanaotumia simu kusambaza habari za uzushi au fake news

    Habari za uzushi za kutekwa kwa mdhibiti mkuu wa fedha za serikali wa zamani Profesa Assad zimezusha taharuki kubwa. Na mpaka ilipoibuka video mitandaoni ambapo Profesa Assad anaonekana yupo salama na mwenye afya njema, watu wengi waliingiwa na hofu kubwa. Ifikapo tarehe 31 Desemba mwaka huu...
  19. Suley2019

    TCRA: Laini zote ambazo hazijasajiliwa kwa namba za NIDA zitafungwa kufikia Desemba 31, 2019

    Mamlaka hiyo imesema kwamba hakuna laini ya simu itakayofungwa kabla ya tarehe hiyo. Aidha, imesema wananchi wanatakiwa kwenda kusajili laini zao kwa kutumia vitambulisho vya uraia, na kuthibitisha usajili huo kabla ya muda uliowekwa kwa kuwa hakutakuwa na mabadiliko ya kuzifunga. Akizungumza...
  20. S

    Hivi TCRA wanaweza kutupa sababu za msingi kwa nini bei ya internet Tanzania ni zaidi ya mara kumi ya bei ya internet Rwanda?

    Bei za internet ya wastani kwa Tanzania na baadhi ya nchi zinazotuzunguka ni kama ifuatavyo: Source: Worldwide mobile data pricing: The cost of 1GB of mobile data in 230 countries Reference: Worldwide Mobile Data Pricing League | Cost of 1GB in 230 countries - Cable.co.uk Hivi TCRA wanaweza...
Back
Top Bottom