oktoba

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. DuaZaMama

    Mke asimulia alivyompoteza mume wake vurugu za Oktoba 29,2025

    Simanzi imetawala wananchi walioathiriwa na vurugu zilizotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 waliposimulia walichoshuhudia katika matukio hayo, wakieleza walichoshuhudia baadhi ya waathirika wa matukio hayo wakiwemo waliopigwa risasi wao au waliofiwa na wapendwa wao na...
  2. Roving Journalist

    Wazee wanatoa maazimio yao juu ya kilichotokea tarehe 29 Oktoba

    https://www.youtube.com/live/EJPutwDEwWI MAAZIMIO YA MAZUNGUMZO YAWAZEE KUHUSU UJENZI WA AMANI, UMOJA NA HAKI NCHINI TAREHE: 22 JANUARI 2026 MAHALI: DARES ES SALAAM, UKUMBI WA MWALIMU NYERERE FOUNDATION Imewasilishwa na: Mzee Joseph W. Butiku, M/Kiti Bodi ya Wadhamini,Mwalimu Nyerere...
  3. M

    Mzee Butiku: Watanzania tujitathmini kwa utulivu baada ya vurugu za Oktoba 2025

    Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), imewataka Watanzania kuendelea kushikamana na misingi ya Taifa, hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inatafakari matukio ya vurugu za Oktoba 29, 2025 kupitia Tume iliyoundwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Hayo yameelezwa jijini Dar es Salaam leo, Alhamisi...
  4. W

    SI KWELI ICC itatoa hukumu mwezi huu January 2026, kuhusu mauaji yaliyotokea Oktoba, 2025

    Wakuu nimekutana na Taarifa huko mtandaoni inayoeleza kuwa; "=AZYgKkVELthfF2or8cz9hZgtDA2u2RiBdMfdI8maVSNICA04cSYXXbdXRplfrWQvl_7jXQwbtQeqJ-AHtoRziO5eE5VYJ6t4oaVOH482QFJ6S9hWcWKyFVkANFBRfLwvaufqlpK135He2ochFj0XJkUCngvoo0g2yoYg_jBY6fBEDX62nxo0jsmwKYNFNTfLS8Y1EhB4LKO4uYtMX6BoU9IN&tn=*NK-R']#Kesi...
  5. DuaZaMama

    PostGE2025 George: Nilipigwa risasi Oktoba 29, 2025 nikapoteza mguu

    "Nilikataa kukatwa mguu, lakini madaktari waliniambia nimechelewa kupata matibabu." Huo ni ushuhuda wa kusikitisha wa George Chipeta (24), fundi wa umeme wa magari mkazi wa Banana, mkoani Dar es Salaam aliyetoa maelezo mbele ya Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Oktoba 29, 2025. George, ambaye...
  6. Prof_Adventure_guide

    Oktoba 29: Hatma ya Watanzania na Mustakabali wa Tanganyika Yetu

    Tarehe 29 Oktoba imebeba uzito mkubwa katika historia ya Watanzania. Ni siku inayochochea hisia, matumaini, hofu na maswali mengi kuhusu mwelekeo wa taifa letu. Kwa uhalisia, hatma ya Watanzania haitegemei tukio lenyewe pekee, bali namna tunavyolielewa, tunavyolishughulikia, na maamuzi...
  7. Bawabu wa pili

    Waziri Kombo: Vurugu za Oktoba 2025 zimebadili taswira ya Tanzania duniani

    Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo amesema mwaka 2025, Tanzania ilikabiliwa na vurugu wakati wa uchaguzi ambazo hazijawahi kutokea tangu nchi ilipopata uhuru mwaka 1961. Soma pia: Waziri Kombo: Tumestahimili mtihani mzito wa Oktoba 29, Dunia...
  8. Bawabu wa pili

    PostGE2025 DW yathibitisha aina ya Risasi zilizotumika kwenye mauaji ya Oktoba 29, 2025 zilikuwa ni za Polisi na Jeshi la Tanzania

    https://www.youtube.com/watch?v=-ZZrAoiAmqc Uchunguzi wa DW umebaini ushahidi wa kuaminika unaoonyesha kuwa vikosi vya usalama vilitumia nguvu za kikatili dhidi ya raia wakati wa vurugu zilizofuata uchaguzi wa Oktoba 29 nchini Tanzania. Maandamano yalizuka katika miji mikubwa ikiwemo Mwanza...
  9. Waufukweni

    Mama wa mtoto aliyepigwa risasi Oktoba 29, atuma ‘salamu’ kwa Rais

    Mama wa mtoto aliyepigwa risasi Oktoba 29, 2025 atuma ‘salamu’ kwa Rais
  10. R

    PostGE2025 Mwabukusi: Kuna watu wameuawa Oktoba 29 wamepigwa risasi ndugu wakaambiwa waseme wamekufa kwa homa ili wapewe maiti

    Akizungumza na Jambo TV leo Januari 09.2025, Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Wakili Boniface Mwabukusi amesema wananchi wamekuwa wakipeleka malalamiko kuwa kuna ndugu zao waliuawa Oktoba 29 kwenye vurugu wakaambiwa kusema wamekufa kwa homa ili wapewe maiti na hata vyeti vya vifo...
  11. W

    Mwabukusi awashangaa wanaosema kwa lugha nyepesi tusameheane baada ya mauaji ya Oktoba kama vile mtu amekanyaga tu kitumbua

    Rais Wa Chama cha mawakili Tanganyika ameeleza kuwa mauaji yaliyotokea Oktoba ni makubwa hayakuwahi kutokea Toka Tanganyika ijulikane na si Muarabu, Mjerumani wala Muingereza aliyefanya mauwaji makubwa hivi. Awashangaa watu wanaozungumza kwa lugha nyepesi tu kuwa tusameheane kama vile mtu...
  12. K

    ITV: Waliopigwa risasi na kuuwawa mnamo tarehe 29 Oktoba 2025 hawakuwa waandamaji - Tume ya Jaji Chande

    Nipo hapa napata Moja baridi na Moja baridi nchi jirani huku nikofuatilia ITV HABARI kupitia YOUTUBE, huyu mtangazaji wa ITV anayeitwa Asiraji Mvungi, ameripoti Kwamba Tume ya Jaji Chande imekutana na wahanga na waathirika wa vurugu baada ya uchaguzi, na waathirika hao wamemwambia Jaji Chande...
  13. M

    PostGE2025 Abdallah Makame: Oktoba 29 watu waliokuwa na silaha waliua wenzao na kuvamia vituo vya polisi

    Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Dkt. Abdallah Makame(CCM) amesema kuwa waliofanya mauaji, kuvamia vituo vya polisi, maduka na kuchoma mali ni watu waliokuwa na silaha ambao mpaka sasa hawajajulikana ni kinanani hasa na walizipata wapi. Ameongeza kuwa hata Sheikh Sharrif Majini aliuawa kwa...
  14. Lord Denning

    TEC huyu mama anawabeep. Tunaomba muandike barua kwenda ICC kuieleza mna ushahidi wa Mauaji yaliyofanyika Oktoba 29 na mpo tayari kuutoa

    Huu ni wito kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania TEC. Nyie ni chombo nyeti sana na mna aminika dunia nzima. Huyu kibibi anawabeep sana. Anawashambulia, anawateka, na kuwafanyia mashambulizi ya kutaka kuwaua. Sasa akishirikiana na wapumbavu wake wa tiss na bakwata anaandaa vikundi vya...
  15. upupu255

    PostGE2025 Askofu Musomba: Tumepoteza mwelekeo kwa yaliyotokea Oktoba 29

    Askofu wa Jimbo Katoliki la Bagamoyo, Mhashamu Stephano Lameck Musomba, amesema Taifa limepitia mwaka wenye majonzi makubwa uliodhihirisha kupotea kwa mwelekeo wa maadili na mshikamano wa kijamii, akisisitiza umuhimu wa Watanzania kurejea kwa Mungu, haki na kuheshimiana ili kulinda amani ya...
  16. S

    Tatizo ni kwamba, baada ya mauaji ya Oktoba 2025, hata muongee maneno mazuri kiasi gani, ICC ya The Hague inawasubiri!

    Nadhani kuna watu wanafikiri wakiongea maneno matamu matamu basi watu wa ICC kule The Hague watasahau amri za kuua walizotoa na mauaji ya kutisha ya Oktoba 2025. Hakuna kitu kama hicho. Anzeni kujipanga kwenda kwenye kesi, na hata kutangaziwa International Arrest Warrants. Ushahidi upo wa wazi...
  17. M

    baruti zinazopigwa usiku huu wa mwaka mpya zingepigwa marufuku, zinaleta kumbukumbu mbaya za milio ya risasi ya 29 Oktoba 2025

    Sikutegemea kama usiku huu wa kuamkua 2026 mwaka mpya utanivuruga kisaikolojia Nilizoea kufurahia baruti za mwaka mpya lakini kwa mara ya kwanza nimehuzunika kila ninaposikia milio ya baruti, akili inarudi kwenye milio ya 29 Oktoba mwaka jana
  18. Black Opal

    Ipo siku watakubali na kujuta waliyofanya Oktoba 29 kama Mkapa alivyojutia ya Januari 2001? Waliohusika watawajibishwa?

    January 27, 2001 yalifanyika maandamano yaliyoitishwa na chama kikuu cha upinzani CUF kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 2000 uliyompa ushindi mgombea wa CCM Dkt. Amani Abeid Karume dhidi ya mgombea wa CUF, Maalim Seif Hamad. Kutokana na maandamno hayo kulitokea vifo kadhaa...
  19. DuaZaMama

    PostGE2025 Tume ya kuchunguza matukio ya Oktoba 29 yakutana Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF), Jenerali Jacob Mkunda

    TUME ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu, leo Desemba 30, 2025, imekutana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF), Jenerali Jacob Mkunda. - Kikao hicho ni muendelezo wa majadiliano kati ya tume, waathirika wa matukio ya ghasia wakati na baada ya...
  20. I

    Mauwaji ya Oktoba 29: wagombea wachunguzwe historia ya ubinadamu wao.

    Wajumbe. Ubinadamu kazi. Na kila mwanadamu anapita njia nyingi sana katika makuzi yake. Ipo dhana moja muhimu sana. Dhana ya utimamu wa kihisia. Hisia za mwanadamu huwa na athari chanya au hasi katika akili yake. Mathalan, mwanadamu ambae enzi za utoto wake alikulia katika familia zenye...
Back
Top Bottom