Pesa zinazokusanywa ni kwajili ya kuendeleza Dar, Dodoma na Zanzibar ? mikoa mingi imekuwa vyanzo vya mapato bila kupewa umuhimu kwenye maendeleo

Pesa zinazokusanywa ni kwajili ya kuendeleza Dar, Dodoma na Zanzibar ? mikoa mingi imekuwa vyanzo vya mapato bila kupewa umuhimu kwenye maendeleo

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
2,574
Reaction score
7,751
Kuna mikoa huchangia mamia ya mabilioni ya kodi kila mwaka kupitia biashara, kilimo, madini na shughuli nyingine za kiuchumi.

Lakini ukifika hata makao makuu na majiji ya mikoa hiyo, maendeleo hayaendani kabisa na mchango wao,

Inasikitisha kuona kuwa sehemu kubwa ya mapato hayo yanaelekezwa zaidi kwenye maendeleo ya Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar,

hali hii inafanya mikoa mingine kuonekana kama mbwa wa mawindo, thamani yake ipo kwenye kuwinda tu, baada ya mawindo anarushiwa mifupa.

Wananchi hawahitaji huruma, wanahitaji usawa. Kama wanachangia kwa nguvu zote kwenye uchumi wa nchi, basi ni haki yao kuona maendeleo yakirejea kwao pia. Taifa lenye usawa haliwezi kujengwa kwa kuacha baadhi ya maeneo kuwa vyanzo vya mapato pekee bila kunufaika na matunda ya jasho lao.
 
Tangu siku za Uhuru "think tank" ya chama tawala ilikabidhiwa kwa wazee wa Pwani.
 
Kahama , ukifika unaweza toa chozi, yani Barbara na Kodi inayokisanywa mbingu na ardhi
viongozi wa kitaifa hawawezi kuzielewa changamoto za kila eneo kwa ziara za siku moja tu. Waziri ambaye ni mbunge wa jimbo la mkoa wa mbali anafika kwa ndege akiwa na escort kufanya ukaguzi wa barabara, anakaa masaa machache halafu anaondoka kesho yake. Hawezi kujua mateso ya barabara, maji, afya na huduma nyingine kuliko wenyeji wanaoishi hapo kila siku.
 
Vipi serikali za majimbo. Huenda ikatatua changamoto
Wanaogopa mfumo wa serikali za majimbo utapunguza nguvu zilizojikusanya kwa viongozi hasa wa kitaifa. Kwenye mfumo wa majimbo, kila jimbo lina serikali yake ndogo yenye mamlaka ya kufanya maamuzi mengi bila kusubiri serikali kuu.
 
Kuna mikoa huchangia mamia ya mabilioni ya kodi kila mwaka kupitia biashara, kilimo, madini na shughuli nyingine za kiuchumi.

Lakini ukifika hata makao makuu na majiji ya mikoa hiyo, maendeleo hayaendani kabisa na mchango wao,

Inasikitisha kuona kuwa sehemu kubwa ya mapato hayo yanaelekezwa zaidi kwenye maendeleo ya Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar,

hali hii inafanya mikoa mingine kuonekana kama mbwa wa mawindo, thamani yake ipo kwenye kuwinda tu, baada ya mawindo anarushiwa mifupa.

Wananchi hawahitaji huruma, wanahitaji usawa. Kama wanachangia kwa nguvu zote kwenye uchumi wa nchi, basi ni haki yao kuona maendeleo yakirejea kwao pia. Taifa lenye usawa haliwezi kujengwa kwa kuacha baadhi ya maeneo kuwa vyanzo vya mapato pekee bila kunufaika na matunda ya jasho lao.
Kwa trend iliyopo mpaka kufika 2030 nchi itakuwa haina barabara ya lami
 
Kuna mikoa huchangia mamia ya mabilioni ya kodi kila mwaka kupitia biashara, kilimo, madini na shughuli nyingine za kiuchumi.

Lakini ukifika hata makao makuu na majiji ya mikoa hiyo, maendeleo hayaendani kabisa na mchango wao,

Inasikitisha kuona kuwa sehemu kubwa ya mapato hayo yanaelekezwa zaidi kwenye maendeleo ya Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar,

hali hii inafanya mikoa mingine kuonekana kama mbwa wa mawindo, thamani yake ipo kwenye kuwinda tu, baada ya mawindo anarushiwa mifupa.

Wananchi hawahitaji huruma, wanahitaji usawa. Kama wanachangia kwa nguvu zote kwenye uchumi wa nchi, basi ni haki yao kuona maendeleo yakirejea kwao pia. Taifa lenye usawa haliwezi kujengwa kwa kuacha baadhi ya maeneo kuwa vyanzo vya mapato pekee bila kunufaika na matunda ya jasho lao.
Suluhisho ni serikali ya majimbo!
Yaani makusanyo yote yaende kwenye majimbo husika! Serikali kuu mara zote ni wezi!
 
viongozi wa kitaifa hawawezi kuzielewa changamoto za kila eneo kwa ziara za siku moja tu. Waziri ambaye ni mbunge wa jimbo la mkoa wa mbali anafika kwa ndege akiwa na escort kufanya ukaguzi wa barabara, anakaa masaa machache halafu anaondoka kesho yake. Hawezi kujua mateso ya barabara, maji, afya na huduma nyingine kuliko wenyeji wanaoishi hapo kila siku.
Nafikiri wakuu wa mikoa na wilaya, wachaguliwe Kwa kuangalia uwenyeji wa mtu husika
 
Back
Top Bottom