Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 962
- 1,909
Jeshi la Polisi nchini limewakamata watu watatu kwa tuhuma za kutumia vibaya mitandao ya kijamii kwa kusambaza matusi na maudhui ya kudhalilisha, wakiwemo waliolenga wajumbe wa Tume ya Uchunguzi wa matukio ya vurugu za Oktoba 29, 2025 na baada ya uchaguzi.
Watuhumiwa hao wamekamatwa katika mikoa ya Arusha, Iringa na Mbeya, huku msako wa kuwabaini na kuwakamata wengine ukiendelea.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Makao Makuu ya Jeshi la Polisi leo, Jumamosi Mei 2, 2026, uchunguzi unaendelea pia kwa wale waliopokea na kusambaza jumbe zenye matusi, kashfa, uchonganishi, chuki na upotoshaji.
Jeshi la Polisi limewashukuru wananchi wanaoendelea kutoa taarifa zinazosaidia kukamatwa kwa wahusika, na kusisitiza kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wote wanaokiuka sheria za makosa ya mtandaoni na sheria nyingine za nchi.
Watuhumiwa hao wamekamatwa katika mikoa ya Arusha, Iringa na Mbeya, huku msako wa kuwabaini na kuwakamata wengine ukiendelea.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Makao Makuu ya Jeshi la Polisi leo, Jumamosi Mei 2, 2026, uchunguzi unaendelea pia kwa wale waliopokea na kusambaza jumbe zenye matusi, kashfa, uchonganishi, chuki na upotoshaji.
Jeshi la Polisi limewashukuru wananchi wanaoendelea kutoa taarifa zinazosaidia kukamatwa kwa wahusika, na kusisitiza kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wote wanaokiuka sheria za makosa ya mtandaoni na sheria nyingine za nchi.

