mwigulu nchemba

Mwigulu Nchemba
Mwigulu Lameck Nchemba Madelu ni mwanasiasa na mwanachama wa chama cha kisiasa nchini Tanzania, Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mwigulu alikuwa Waziri wa Fedha na Mipango tangu 31 Machi 2021, mpaka July 2023 ambapo wizara hiyo ilivunjwa na kuwa wizara mbili yaani Wizara ya Fedha inayoongozwa na Mwigulu Nchemba na Wizara ya Mipango na Uwekezaji inayosimamiwa na Waziri Kitila Mkumbo.
  1. R

    JamiiForums Tanzania Luhaga Mpina: Mwigulu Nchemba, Mbarawa, Mkurugezi wa TRC na wote waliohusika wakamatwe na kushtakiwa kwa makosa ya Uhujumu Uchumi

    Mpina akiwa anachangia hoja amesema kamati imekiri suala la kutumia mzabuni mmoja lilikataliwa na PPRA ambaye ndio msimamizi mkuu wa manunuzi nchini, lilikataliwa na bodi ya manunuzi, na walikataa sababu sheria za nchi za manunuzi ilikuwa inatekelezwa wakayti huo haziruhusu mambo hayo, lakini...
  2. J

    JamiiForums Tanzania Dkt. Mwigulu asema Nchi haiwezi kupigwa Tsh. 30 Trilioni wakati Bajeti yetu haivuki Tsh. Trilioni 50, Mpina asema Waziri hajui lolote

    Mbunge Mpina asema hii nchi inapigwa kila kona na zaidi ya Tsh. 30 Trilioni zimepigwa na nyingine zimesafirishwa/ kutoroshwa nje ya nchi. Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba PhD amesema anachosema Mpina hakiwezekani kwa sababu Bajeti ya nchi haizidi tsh 50 trilioni. Mpina ameomba Waziri Dr...
  3. JamiiForums Tanzania Ubadhirifu katika Risiti za EFD za TRA

    Hivi karibuni kumeibuka Hoja nyingi juu ya uhalali wa Risiti za EFD, kwa sasa EFD ndio risiti maalumu ya Bidhaa kuuza na kununua popote pale Nchini. Lakini risiti hizi zina utata kutokana na uhalali wake. TRA wana tovuti ya kuhakiki risiti hizi za EFD ambayo ni TRA RISITI lakini asilimia 80%...
  4. L

    JamiiForums Tanzania Mwigulu Nchemba na Kitila Mkumbo waungana "eti" ili kuondoa ushindani jimbo la Iramba

    Hii ni ajabu sana. Hivi majuzi eti Dkt Mwigulu aliamua kuzindua ujenzi wa barabara kutoka Sepuka hadi Ndago ili kuunganisha na Kizaga - pale junction ya barabara Kuu iendayo Magaharibi - Tabora na Shinyanga. Wakiwa katika uzinduzi huo Dkt Kitila akajinadi kuwa hawana tena siasa za majitaka kati...
  5. S

    JamiiForums Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba yuko wapi anguko la Dola?

    Daktari wa Uchumi, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba alijitapa bungeni kuwa Dola zipo za kutosha na hakuna tatizo la Dola na kwamba yeye ni Mbobevu wa Uchumi watanzania wasiwe na mashaka naye wanaweza kujadili mambo ya uganga wa kienyeji tu. Leo Dola zimepotea Waziri yuko Kimya.
  6. S

    JamiiForums Tanzania Tetesi: Mwigulu Nchemba na Januari Makamba wakutana kikao cha dharura baada ya Bunge kutoa mwongozo wa Luhaga Mpina

    KUNA tetesi kuwa baada ya Spika wa Bunge leo 28/6/2023 kumtangaza bungeni Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina kuwa alikuwa sahihi kuhusu kutotekelezwa kwa maagizo ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. Mawaziri Mwigulu Nchemba na Januari Makamba wamekutana kwa kikao cha dharura kujadili uamuzi huo wa...
  7. R

    JamiiForums Tanzania Mwigulu: Kila Mtanzania anapozaliwa anakuwa mwana CCM

    Mwigulu, akiwa anahitimisha kusoma Bajeti ya mwaka 2023 kasema CCM ndio chama pekee chenye nia ya dhati ya kuleta maendeleo hapa nchini na kwamba kila Mtanzania anapozaliwa nchini anakuwa mwana CCM, na kwamba wataendelea kuwashukuru wote wa vyama vingine kwa kuwa na mioyo ya upendo kwa kuendelea...
  8. JamiiForums Tanzania Dkt. Mwigulu: Tusamehe ushuru wa magari ya umeme na Gesi

    Ili kuiwezesha Nchi kuwa na Sera za Kodi zinazotabirika na kuweka mazingira bora ya uwekezaji, Serikali imependekeza kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Ushuru Kwa kuanzisha utaratibu wa kurekebisha viwango vya Ushuru wa Bidhaa kila baada ya miaka mitatu (3) Kuanzia mwaka wa fedha 2023/24...
  9. JamiiForums Tanzania Waziri wa fedha, Mwigulu Nchemba: Kodi sio jambo la Rais, kodi sio jambo la Waziri wa Fedha, kodi sio jambo la TRA, kodi ni jambo la Nchi

    Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba leo June 15,2023 amewasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 Bungeni Jijini Dodoma ambapo moja ya mambo aliyoyasema kwenye hotuba yake ni kwamba kuna baadhi ya Wanasiasa wanasema kodi zinatozwa nchini ni za Rais wa Tanzania...
  10. JamiiForums Tanzania Mwigulu Nchemba: Serikali kuanzisha akiba ya dhahabu nchini

    Waziri Mwigulu Nchemba amesema kuwa Serikali imekamilisha taratibu za kununua dhahabu kupitia Benki Kuu ya Tanzania kwa ajili ya kuanzisha akiba ya dhahabu hapa nchini. Pia soma Tanzania tuhifadhi akiba yetu kwa Dhahabu badala ya Dollar “Kutokana na kukamilika kwa ujenzi wa viwanda vya...
  11. JamiiForums Tanzania Mwigulu Nchemba: Mfumuko wa bei upo chini ya 5%

    Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba leo Bungeni Dodoma amewasilisha Bungeni taarifa ya Hali ya Uchumi wa Kitaifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa Mwaka 2023/2024 ambapo moja ya mambo aliyoyasema ni kwamba mfumuko wa bei nchini umeendelea kuwa ndani ya lengo la wigo...
  12. JamiiForums Tanzania Waziri Mwigulu Nchemba: Tumepokea ushauri wa kuongeza Kodi kwenye Pombe

    Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kuwa wizara imepokea wazo la Mbunge wa Momba, Condester Sichalwe la kuongeza kodi kwenye pombe zinazoingizwa nchini. Akitoa majibu bungeni jijini Dodoma Waziri Mwigulu amesema kuwa wizara imepokea pendekezo hilo, italiafanyia kazi na kutoa...
  13. JamiiForums Tanzania TRA na TANESCO, Kuzifungua mita za umeme kisa kodi ya majengo ni wizi na uonevu

    Jana usiku umeme uliisha kwenye mita yangu. Nikanunua wa shilingi elfu 9 kwa tigopesa, nashangaa muamala unasitishwa kila naponunua. (Ninatumia tarrif ya chini ile) umeme wa elfu 9 unanitosha kwa mwezi mzima. Ikabidi nipige simu tigo, wakaniambia kuwa mita inadaiwa shilingi laki 1 deni ya kodi...
  14. JamiiForums Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba awasilisha Mapendekezo ya Serikali ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Mfumo na Ukomo wa Bajeti ya Serikali 2023/24

    Maelezo ya Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), Waziri wa Fedha na Mipango, akiwasilisha Mapendekezo ya Serikali ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2023/24 na Mfumo na Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2023/24.
  15. JamiiForums Tanzania Clip: Baada ya Kumnanga kwenye Mkutano, Wafanyabiashara Wapiga Selfie na Mwigulu Nchemba

    Jee huu ni UNAFIKI au UPUMBAVU? Seriousness ya Watanzania iko wapi? Ndiyo maana Mwigulu anawadharau anajuwa zile ni mbambamba tu. Angalia wajinga hao kwenye clip wanavyogombea kupata selfie na Mwigulu!! STUPID
  16. JamiiForums Tanzania Mwigulu Nchemba na Ashatu Kijaji ni Mawaziri wenye utendaji unaotia shaka

    Mgomo wa Kariakoo umeibua mengi, lakini pamoja na kuonyesha madudu ya uncontrollable TRA na rushwa za nje nje zilizoishinda serikali kuzikabili, mgomo umeibua jambo serious la utendaji chini ya kiwango wa mawaziri wa Fedha na Mipango, pamoja na yule wa Biashara na Viwanda. Wiazara hizi lazima...
  17. JamiiForums Tanzania Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni: Katika Mgomo wa wafanyabiashara, kosa la Mwigulu Nchemba ni lipi?

    Wakuu Salam, Naomba nitangaze maslahi, mimi ni mfanyabiashara, nipo Kariakoo, nje ya Kariakoo na mkoa wa Pwani. Malalamiko yetu wafanyabiashara mengi ni justifiable, lakini hili la kumlaumu Mwigulu Nchemba bila supporting evidence is ungrounded. Kuna watu wanatumia udhaifu wa migogoro ya...
  18. JamiiForums Tanzania Mwigulu Nchemba, bingwa wa uchumi ever seen here in Tanzania

    Huyu jamaa ni msomi na mahiri mno wa uchumi ndio mana huwezi kukuta anakosolewa na profesa yeyote wa uchumi maana wanamuogopa sana. Maprofesa wengi waliunga unga lakini Mwingulu straight kutoka Mzumbe na alipiga first class UDSM wakati maprofesa wengi hawana hii. Profesa kama Semboja degree yake...
  19. C

    JamiiForums Tanzania Mchumi wetu Mwigulu Nchemba anaupiga Mwingi, hakika Rais Hakukosea

    Kisa cha Wakili Farah Maalim Mohammed na kielelezo cha makuu ya Tanzania. #Zimesambaa video za Naibu Spika wa zamani wa Bunge la Kenya na Mbunge wa sasa wa jimbo la Dabaab Nchini Kenya Mh. wakili msomi na mchumi mwandamizi Faraah Maalim Mohamed akieleza Threat ya kiuchumi Tanzania wanaiweka...
  20. JamiiForums Tanzania Mwigulu Nchemba: Msihofie Mikopo, riba yake ni ndogo

    Waziri wa Fedha na Mipango, Dr. Mwigulu Nchemba akiwa Dar es salaam leo ameishukuru Benki ya Dunia kwa kuwa Mdau Mkuu wa Maendeleo ya Tanzania kwa kutoa mikopo nafuu na misaada mbalimbali inayotumika kutekeleza miradi inayochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya Watu ambapo mpaka sasa, Benki...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…