beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba ameomba Bunge kuidhinishia Wizara hiyo Bajeti ya Trilioni 14.94 kwa Mwaka wa Fedha 2022/23.
Akizungumza Bungeni amesema miongoni mwa changamoto zilizoikumba Wizara hiyo ni mfumuko wa bei katika soko la ndani na kasi ndogo na ukuaji wa Pato la Taifa kutokana na athari za Mlipuko wa COVID-19 na vita kati ya Urusi na Ukraine.
Amesema changamoto nyingine ni kuongezeka gharama za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na ununuzi wa vitendea kazi kutokana na mfumuko wa bei, hivyo kuathiri mwelekeo wa bajeti iliyokuwa imeidhinishwa na Bunge.
Akizungumza Bungeni amesema miongoni mwa changamoto zilizoikumba Wizara hiyo ni mfumuko wa bei katika soko la ndani na kasi ndogo na ukuaji wa Pato la Taifa kutokana na athari za Mlipuko wa COVID-19 na vita kati ya Urusi na Ukraine.
Amesema changamoto nyingine ni kuongezeka gharama za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na ununuzi wa vitendea kazi kutokana na mfumuko wa bei, hivyo kuathiri mwelekeo wa bajeti iliyokuwa imeidhinishwa na Bunge.