Meneja wa Huduma za Utangazaji kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi Andrew Kisaka amesema Tuzo za Samia Kalamu Awards zimeanzishwa baada ya TCRA kubaini mapungufu katika maudhui ya ndani, hivyo wakaona kuna haja ya kutoa hamasa kwa waandishi wa habari kuandika habari...
Katibu Mkuu Umoja wa wazazi Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Ndg. Ally Hapi amewasisitiza Vijana kutoka TK Movement kuwa imara na kuepukana na wale wote wenye nia mbaya na Nchi ya Tanzania hivyo amewasisitiza vijana kushiriki Uchaguzi Mkuu unaotegemea kufanyika hivi karibuni.
Mwanachama wa Chama Cha ACT Wazalendo, Kiza Hussein Mayeye Mei 03, 2025 amejitokeza kuchukua fomu ya kugombea ubunge katika Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya chama hicho.
Kiza Mayeye ambaye pia ni Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mkoa wa Kigoma, amekabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa ACT...
Kamati ya Siasa ya halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi mkoa wa Njombe imetoa maelekezo kwa kamati za siasa wilaya zote mkoani humo kuwachukulia hatua wanachama na viongozi wote wa chama hicho wanaoandika maneno yenye kukejeli na kutukana viongozi mitandaoni.
Akitoa taarifa ya kikao cha...
Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla amesema kuwa baada ya uchaguzi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kitageuka kuwa kama jukwaa la harakati kwa sababu wamepoteza muelekeo na malengo ya chama cha siasa ambayo lenho kuu...
John Forteo, Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenenzi wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Ruvuma ameitaka Jamii na Vyama vya Siasa nchini kuhakikisha wanafuata sheria za nchi zilizowekwa .
John Forteo ameyasema hayo wakati alipomuwakilisha Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Ruvuma Hemed Chale...
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, ametoa wito kwa Wananchi wa Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi na Watanzania kwa ujumla kuendeleza kauli ya kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa awamu nyingine ya uongozi, akisisitiza kuwa kauli ya "Mitano Tena kwa Dkt. Samia" inapaswa kutoka...
Nimemshangaa sana mzee wetu Warioba Kuishangaa Tume na kuzishangaa Kanuni za uchugazi badala ya kuwashangaa Viongozi wa Chadema (Katibu Mkuu) ambaye kwa Jeuri tu walisusia kusaini kanuni hizo za uchaguzi na huku wakitambua kufanya hivyo kutawazuia wao kushiriki uchaguzi Mkuu.
Jambo hilo sio tu...
Kiongozi Mstaafu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema kesho Mei 04, 2025 atachukua fomu ya kuomba ridhaa ya Chama hicho kumteua kuwa Mgombea wa Jimbo la Kigoma Mjini ambapo akishachukua fomu ataongea pia na Wananchi wa Kata ya Bangwe.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa...
Kuna attitude nime observe kwa MASHEKH na hii haina maana ya UDINI.
Maaskofu wakikemea ukiukwaji wa haki za Msingi automatically Mashekhe wanaona hii ni attack kwa Samia, hivyo mashekh wengi wanajibu as defensive Mechanism ya Samia.
Ukiwasikiliza vema Maaskofu unaona kabisa ni intellectual...
Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Boniphace Mwabukusi amesema anataka Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu ufanyika bila mabomu wala virungu.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote...
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Kata ya Manzese, Boniface Shauritanga, amesema vijana wanahitaji kuungwa mkono ili kuhakikisha kila tukio la chama linafanikiwa. Ameongeza kuwa ni muhimu kwa vijana kuacha kuwa na misimamo binafsi na badala yake wafuate miongozo ya chama, hasa katika...
Mwanazuoni na mchambuzi wa masuala ya siasa, Deus Kibamba amesema kuwa kitendo cha mmoja wa Makamishna wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kuwa na historia ya kuwa kiongozi mwandamizi wa chama cha siasa kunaweza waondolea wananchi imani juu ya usimamiaji haki kwenye uchaguzi.
Kibamba...
Demokrasia hasa hii ya vyama vingi sio utamaduni mkongwe katika uongozi wa nchi nyingi duniani. Kihistoria mfumo mkongwe wa uongozi ni mfumo wa kifalme. Katika mfumo huu wakuu wa nchi hawapati haki ya kutawala kwa kuchaguliwa na wananchi, bali hupata haki ya kutawala kwa kuzaliwa kwenye familia...
Leo May 3, 2025, Tundu Lissu ametuma barua ya wazi kwa watanzania akiwa kolokoloni gereza la ukonga.
Barua hii imechapishwa na Maria Sarungi kupitia mtandao wa X kama ifuatavyo,
Barua rasmi ya Lissu kwetu sote! Alituma kwa Kiingereza neno kwa neno kupitia mtu aliyenifikishia na nimeweka hapa...
Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais Mstaafu, Jaji Joseph Warioba akitoa maoni katika kongamano la kitaifa kuhusu uchaguzi mkuu wa 2025 lililoandaliwa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), amesema kwamba hatua ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani, Innocent...
Habari!
Natoa wito kwa viongozi wa CHADEMA na wanaharakati wa haki za binadamu na wadau wengine kuanzisha michango kusaidia familia ya Mdude katika kipindi hiki ambacho hatima ya Mdude bado ni kitendawili.
Huyu Bwana alitoa maisha yake kupambania Taifa hili na watu wake na pia alikuwa ni...
Katika zama hizi za mabadiliko ya kisiasa na kijamii, ni wazi kuwa taifa letu linaendelea kukumbana na changamoto nyingi kila uchaguzi mkuu unapokaribia. Hofu, migawanyiko ya kijamii, matumizi makubwa ya rasilimali, na vurugu za kisiasa zimekuwa zikijirudia kila mara tunapojitayarisha kumchagua...
Erick Kabendera amefanya mahojiano ambayo yako youtube kuelezea kitabu chake alichokiandika (in the name of president (maagizo kutoka juu - kama walivyotafsiri wenyewe kwenye mazungumzo yao)).
Ukiyasikiliza vizuri hasa hasa visa alivyoelezea kuhusu utekaji watu na kuwapoteza...
Polisi hampaswi kujiulizauliza mtu wa kuanza nae ni Farsi Burhan Mwenyekiti wa Uvccm mkoa wa Kagera ambaye mwaka jana alijitangaza kuanza kuteka watu na kuwaonya kuwa inaootokea mtu akatekwa polisi msimtafute.
Anza na huyu mtekaji akiyejitangaza hadharani jamani huenda ndo yupo nyuma ya...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.