ccm

Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho chama tawala nchini Tanzania na chama cha pili kwa muda mrefu zaidi barani Afrika, baada ya Chama cha True Whig cha Liberia. Kilianzishwa mwaka 1977, baada ya kuunganishwa kwa Tanganyika African National Union (TANU) na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar.
  1. T

    JamiiForums Tanzania Wananchi tunaona sana tu, tena sisi wengine ni CCM wenzenu!

    Inasikitisha sana sana. Kuanzia Mkulu wa Nchi, Spika, Jaji Mkuu, Mwanasheria Mkuu wa Sirikali, Mkuchika wa Utumishi, Waziri anayehusika na masuala ya kazi. Hawa wote wamejaa ukomoaji. Wanaendesha uongozi wa ki-imla. Wakati Mkulu akidai ananyoosha nchi wananchi wananyanyasika hasa. Hawa wengine...
  2. Samia atosha tukutane2030

    JamiiForums Tanzania Swali: Hivi nini kitafuata baada ya bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa na wabunge wa CCM tu?

    Habari waungwana, Huhitaji kuwa na Degree ya Political Science kuamini hili. Kwa hakika kabisa majimbo yote Tanzania bara yanakwenda kuchukuliwa na CCM kwa gharama yoyote. Ninaposema kwa gharama yoyote nadhani mmenielewa. Labda tu Rais kwa sababu zake yeye mwenyewe aamue kuchagua baadhi ya...
  3. Mmawia

    JamiiForums Tanzania GE2020 Dkt. Bashiru: Wanaotegemea Tume Huru iwape ushindi wanajidanganya! Tume haipigi kura

    Binafsi nimeshindwa kumuelewa kabisa huyu bwana mkubwa wa CCM. Maneno aliyo yaongea na elimu aliyo nayo sidhani kama vinaendana. HOTUBA YA DR. BASHIRU KWA UFUPI CCM inatoa salamu za mwaka mpya 2020, niwahakikishie watanzania kuwa tutaongoza siasa safi,ni mwaka wa kuheshimu maoni na uamuzi wa...
  4. technically

    JamiiForums Tanzania CCM Imepoteza dira, haina hoja tena

    Eti wangepewa muda wajitetee! Majibu ya kujitetea kwa Membe yako wapi? Lissu alijitetea wapi? Nasari alijitetea? Meya wa Jiji mpaka anafungiwa ofisi!, Meya wa Iringa Je? Meya wa Ubungo je? Ccm mmepoteza dira ni chama ambacho hakina hoja mbele ya umma. Naunga Mkono Mbowe Safisha Chama bado kuna...
  5. J

    JamiiForums Tanzania Wanaoamini NCCR Mageuzi itaachiwa majimbo na CCM wanaota ndoto za mchana

    Nijuavyo mimi ni kuwa wale wabunge waliotangulia kuingia CCM wakitokea Chadema na Cuf akina Waitara na wenzake itabidi wapitie utaratibu wa kawaida wa kura za maoni na hakuna mbeleko safari hii. Sasa kama hawa akina Waitara itawalazimu wapambanie ubunge wao hao akina Selasini ubunge wa bure...
  6. G Sam

    JamiiForums Tanzania Mataifa jirani yanatuthibitishia kuwa sisi tunaopiga kelele kwenye mitandao kuhusu Corona tuna uelewa mpana kuliko CCM na Serikali yake

    Hili suala la COVID 19 kabla halijaanza kusambaa huko kwa majirani sisi huku tulipiga kelele sana. Tulipiga kelele tukabezwa, tukadharauliwa, tukatukanwa. Kumbe waliokuwa wakitutukana walikuwa hawajui chochote kuhusu huu ugonjwa. Aibu! Kikundi cha sisi wa kwenye mtandao tumeonyesha mapenzi mema...
  7. Samia atosha tukutane2030

    JamiiForums Tanzania GE2020 Maajabu hayataisha Tanzania, pamoja na yote haya wananchi wataichagua CCM

    Habari wakuu! Kwa umri wangu mdogo wa miaka takribani 30 nimejifunza mengi, sijabahatika kuvuka mipaka ya Tanzania lakini nimefika karibu mikoa 20 ya Tanzania bara. Hulka na silka za Watanzania zinafanana. Kwa uelewa wangu wa mambo ya kisiasa niliojifunza mitaani na mitandaoni nimehitimisha...
  8. J

    JamiiForums Tanzania Ahadi za CCM: Binadamu wote ni sawa, Nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko na Sitatoa wala kupokea rushwa. Je, zinatekelezeka?

    Jumapili ya leo najaribu kuvirejea viapo mbalimbali nilivyowahi kuapa na ahadi mbalimbali nilizoahidi kuzitekeleza. Miongoni mwa hizo ni ahadi nilizoahidi wakati napokea kadi yangu ya uanachama wa CCM kutoka kwa mwalimu JK Nyerere katika Uwanja wa Samora mjini Iringa. Hizi ahadi zimekaa vizuri...
  9. F

    JamiiForums Tanzania GE2020 Kamati Kuu ya CCM itakutana lini kutangaza tarehe za kutolewa fomu za wagombea urais Zanzibar? Muda unaenda ujue!!

    Mada hapo juu yahusika. Nashangaa kuna ukimya sana ilihali uchaguzi upo palepale mwezi October. Dr. Shein anamaliza muda wake, sioni wala sisikii cherekochereko za kumtafuta mrithiwe. Ndiyo maana mie Freed nauliza kamati kuu CCM mbona kimya sana?
  10. G Sam

    JamiiForums Tanzania Tazama foleni hii ya wanunuzi wa sukari Morogoro. Juzi Waziri Bashungwa kapitishiwa bajeti ya hovyo iliyoungwa mkono na wanaccm wote Bungeni

    Hii ni foleni ya wanaonunua sukari Morogoro mjini ndani ya duka la mbunge wao. Kinachonikera zaidi juzi waziri wa viwanda na biashara kapitishiwa bajeti mbovu sana huku wabunge wa CCM pamoja na spika wakijikita kuishambulia Chadema. Aidha hawa ni wanunuzi wa jumla. Unapata Corona na sukari...
  11. Mzukulu

    JamiiForums Tanzania Mwenye ukweli kamili juu ya Mzozo wa Mtangazaji Maulid Kitenge (CCM) na John Mrema (CHADEMA) auweke wazi

    Nimeambiwa kuwa Wasafi FM Leo asubuhi wamenichafua saana na kusema kuwa mke wangu ni Mbunge kwa sababu tu nilimtaka Spika wa Bunge aache Propaganda. Ndugu Maulid Kitenge aniombe radhi Ndani ya 24 hours as Sina mke Mbunge na sijawahi kuwa naye. Asipofanya hivyo nitajiongeza! John Mrema
  12. G Sam

    JamiiForums Tanzania TANZIA Katibu wa Jumuiya ya Wazazi (CCM) Mkoa wa Kilimanjaro, ndugu Lugano Mwafongo afariki dunia

    Katibu wa Jumuiya ya wazazi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro ndugu Lugano Mwafongo amefariki dunia muda mfupi uliopita katika hospitali ya rufaa ya KCMC mkoani Kilimanjaro alipokimbizwa kwa matibabu. Bwana alitoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe!
  13. denooJ

    JamiiForums Tanzania Wabunge wa CHADEMA wakubaliana kutohudhuria tena vikao vya Bunge kutokana na janga la COVID-9, Kujiweka Karantini kwa wiki 2

    Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya amesema "Hali ya Corona ni mbaya sana, wabunge kupitia Chadema, leo tumefikia makubaliano ya kutoingia Bungeni na kila mbunge kubaki nyumbani kwake Dodoma, niwatake wananchi huko mlipo mchukue tahadhari kubwa."
  14. J

    JamiiForums Tanzania Je, bunge linaongozwa na Mwenyekiti wa CCM?

    Kwa mfano Spika wa Bunge kwa mujibu wa katiba ya CCM ni mjumbe wa kamati kuu ya chama na anaripoti kwa mwenyekiti. Katibu wa Bunge ni mteule wa Rais ambaye ndiye mwenyekiti wa CCM. Mnadhimu wa bunge ni waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu anayeteuliwa na Rais ambaye ndiye mwenyekiti wa CCM...
  15. chakii

    JamiiForums Tanzania Spika Ndugai: Wabunge watoro warejeshe fedha zote walizolipwa kuanzia Mei 1-17 jumla ya Tsh. Milioni 110

    Spika Job Ndugai amesema wabunge wa CHADEMA ambao hawashiriki vikao vya bunge kwa madai kuwa wapo karantini wanahesabika kama watoro na wanatakiwa kurejesha fedha zote walizolipwa kwa kipindi ambacho hawatakuwepo bungeni. Pia wamepaswa kufanya kipimo cha Covid19 kabla hawajaingia bungeni ==...
  16. Konzo Ikweta

    JamiiForums Tanzania Michango ya wabunge wetu ipo chini sana, hawana HOW kwenye michango yao

    Na Thadei Ole Mushi. Nimekuwa nikifuatilia michango ya wabunge wetu bungeni naona tuna tatizo kubwa mahali. Mbunge anapewa dakika kumi kuchangia mfano wizara ya viwanda na Biashara. Dakika tano anatumia kuwashambulia Chadema. Dakika tatu anasifia Serikali ya awamu ya tano, dakika Moja anasema...
  17. J

    JamiiForums Tanzania Zamani CCM walisema Zidumu fikra " sahihi" za mwenyekiti Sasa Chadema wanasema ' Zidumu fikra za mwenyekiti'

    Najaribu kukumbuka tu kiapo changu cha uanachama na salamu zetu ndani ya chama wakati ule wa awamu ya kwanza. Kwanza tuliitana " ndugu" pili tuliamini katika uhai wa chama ndio tulisema " kidumu chama cha mapinduzi" na tatu tuliamini katika uwezo wa mwenyekiti wetu na tulifahamu kuwa yeye ni...
  18. Chagu wa Malunde

    JamiiForums Tanzania Matumizi mazuri ya dola, uadilifu na Uchapakazi umeijengea imani CCM kwa wananchi

    Hili halina ubishi kabisa kwa sababu kila mtanzania anaona kwa macho yake namna serikali ya awamu ya tano ilivyoweza kufanya mambo makubwa kwa muda mfupi kabisa. Mfano ni utekelezaji wa mradi mkubwa ambao utakuwa mfano mkubwa wa kuigwa mradi wa tril 6+ za kitanzania ambao umepewa jina la JNHPP...
  19. Chagu wa Malunde

    JamiiForums Tanzania Mradi wa REA umeipatia CCM kura 50% kabla hata ya uchaguzi

    Kitendo cha serikali ya rais John Pombe Magufuli kuongeza pesa nyingi na kuwepo na usimamizi mzuri wa mradi wa REA tayari chama cha mapinduzi kimeshajizolea kura kwa 50% za urais hata kabla ya uchaguzi. Hii ni kwa sababu mpaka sasa ni 72% ya vijiji hapa Tanzania vimeshawekewa umeme. Nyumba za...
  20. T

    JamiiForums Tanzania Udhaifu wa Chadema sio Uimara wa CCM!

    Nimeona mjadala mkali na wa kuvutia ukiendelea kuhusu uhai wa vyama vya upinzani hususan Chadema kuelekea 2020. Nikiri mapema kuwa, hatuna vyama vya siasa Bali tuna vikundi vinavyopambana na dola. Hata CCM yenyewe ilikwisha acha siku nyingi kuwa Chama cha siasa badala yake uhai wake unategemea...
Back
Top Bottom