Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Tulisikia "maigizo" ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Humphrey Polepole, akieleza kuwa safari hii kwenye uchaguzi wa mwaka huu wa 2020, hawataruhusu hata kidogo watoa rushwa wenye nia ya kutaka kupendekezwa na chama hicho kwa nia ya kuwa wagombea kwa nafasi yoyote katika uchaguzi ujao mwisho wa mwaka huu, wakitoa rushwa kwa nia ya kuwashawishi wapiga kura ili wampigie kura za kuwa mgombea kwenye chama hicho.
Tulimsikia pia Katibu huyo wa uenezi wa CCM akiwasihi wananchi wote wawarekodi kwa kutumia simu zao na baadaye kuupeleka ushahidi huo kwenye chombo kinachopambana na rushwa nchini cha TAKUKURU ili washughulikiwe
Kuna "principle" moja kubwa katika sheria inayosema sheria haina macho na kumwangalia ni nani amefanya kosa hilo ikiwa na maana kuwa sheria ni msumeno unaokata pande zote, kwa maana nyingine ni kuwa kwenye sheria hakuhitajiki hata kidogo "double standards"
Nimekuwa nikijiuliza hivi ni lini chama hicho kimegeuka kuwa ni chama kinachopambana kwa dhati na watoa rushwa??
Bado tunakumbuka tukio lilitokea miaka michache iliyopita, ambapo aliyekuwa Mbunge wa Chadema, wa jimbo la Aru Meru Mashariki, Joshua Nassari, alimpomrekodi, aliyekuwa Mkuu wa wilaya hiyo wa wakati huo, Alexander Mnyeti akitoa rushwa waziwazi kwa madiwani wa Chadema, ili awashawishi wakiache chama chao cha Chadema na wajiunge na CCM
Mikanda hiyo iliyorekodiwa iliwasilishwa moja kwa moja kwa TAKUKURU ili ifanyiwe uchunguzi
Kilichotokea wananchi wote mnakumbuka kuwa kabla hata uchunguzi wa TAKUKURU haujaanza na kuona kama kweli huyo Mkuu wa wilaya alitoa rushwa hiyo, cha kustaajabisha badala yake, Rais Magufuli alimpandisha cheo "mtoa rushwa" huyo na kuwa mkuu wa mkoa wa Manyara!
Cha kushangaza zaidi ni kwa yule aliyetoa ushahidi huo wa mtoa rushwa huyo, aliyekuwa Mbunge wa Chadema wa jimbo hilo la Aru Meru Mashariki, Joshua Nassari, alivuliwa ubunge wake na Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai, kwa madai kuwa ni mtoro ambaye hajahudhuria vikao vitatu mfululizo vya Bunge!
Ndipo hapo ninaona chama hicho cha CCM hakina nia ya dhati ya kupambana na watoa rushwa hao na badala yake, ni kama kinafanya mchezo wa kuigiza kwa kuwatazama usoni watoa rushwa hao, na kuona kama ni watoa rushwa waliowekwa kwenye "black list" na chama hicho ili washughulikiwe au kama ni wale ambao ni vipenzi vya "Bwana mkubwa" ambao kamwe hawatakiwi kuguswa na mkono wa sheria
Kwa maana hiyo tusitegemee kamwe kama TAKUKURU itakuwa na ubavu wa kuwashughulikia watoa rushwa wa aina hiyo!
Tulimsikia pia Katibu huyo wa uenezi wa CCM akiwasihi wananchi wote wawarekodi kwa kutumia simu zao na baadaye kuupeleka ushahidi huo kwenye chombo kinachopambana na rushwa nchini cha TAKUKURU ili washughulikiwe
Kuna "principle" moja kubwa katika sheria inayosema sheria haina macho na kumwangalia ni nani amefanya kosa hilo ikiwa na maana kuwa sheria ni msumeno unaokata pande zote, kwa maana nyingine ni kuwa kwenye sheria hakuhitajiki hata kidogo "double standards"
Nimekuwa nikijiuliza hivi ni lini chama hicho kimegeuka kuwa ni chama kinachopambana kwa dhati na watoa rushwa??
Bado tunakumbuka tukio lilitokea miaka michache iliyopita, ambapo aliyekuwa Mbunge wa Chadema, wa jimbo la Aru Meru Mashariki, Joshua Nassari, alimpomrekodi, aliyekuwa Mkuu wa wilaya hiyo wa wakati huo, Alexander Mnyeti akitoa rushwa waziwazi kwa madiwani wa Chadema, ili awashawishi wakiache chama chao cha Chadema na wajiunge na CCM
Mikanda hiyo iliyorekodiwa iliwasilishwa moja kwa moja kwa TAKUKURU ili ifanyiwe uchunguzi
Kilichotokea wananchi wote mnakumbuka kuwa kabla hata uchunguzi wa TAKUKURU haujaanza na kuona kama kweli huyo Mkuu wa wilaya alitoa rushwa hiyo, cha kustaajabisha badala yake, Rais Magufuli alimpandisha cheo "mtoa rushwa" huyo na kuwa mkuu wa mkoa wa Manyara!
Cha kushangaza zaidi ni kwa yule aliyetoa ushahidi huo wa mtoa rushwa huyo, aliyekuwa Mbunge wa Chadema wa jimbo hilo la Aru Meru Mashariki, Joshua Nassari, alivuliwa ubunge wake na Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai, kwa madai kuwa ni mtoro ambaye hajahudhuria vikao vitatu mfululizo vya Bunge!
Ndipo hapo ninaona chama hicho cha CCM hakina nia ya dhati ya kupambana na watoa rushwa hao na badala yake, ni kama kinafanya mchezo wa kuigiza kwa kuwatazama usoni watoa rushwa hao, na kuona kama ni watoa rushwa waliowekwa kwenye "black list" na chama hicho ili washughulikiwe au kama ni wale ambao ni vipenzi vya "Bwana mkubwa" ambao kamwe hawatakiwi kuguswa na mkono wa sheria
Kwa maana hiyo tusitegemee kamwe kama TAKUKURU itakuwa na ubavu wa kuwashughulikia watoa rushwa wa aina hiyo!