Kwanini CCM mambo rahisi hawayaelewi kirahisi?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,278
33,880
Tume ya Jaji Fransici Nyalali iliposema kwamba asilimia themani (80%) ya watanzania wanapendelea kubakia kwenye mfumo chama kimoja lakini wanapendekeza mabadiliko kadhaa yafanyike kwenye CCM, wana CCM wengi walitafsiri kwamba watanzania wamekataa mfumo wa vyama vingi. Kama si uelewa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, leo hii tusingekuwa na vyama vingi.

Mwalimu alisema kwamba, watanzania wanapendelea kubakia kwenye mfumo wa chama kimoja, lakini "lakini" zao ni nyingi sana kiasi kwamba haiwezekani kufanyike marekebisho kwenye Katiba ya CCM na CCM ikabakia ilivyo kama CCM. Mwalimu alisema mapendekezo mengi yanakwenda kinyume na mtizamo, falsafa na Itikadi ya CCM.

Mwalimu akashauri kwamba hao wenye hizo "lakini" wapewe jukwaa nje ya CCM ambako watapata fursa ya kufuata falsafa, Itikadi na mitazamo yao hiyo isiyofanana na CCM. Jambo rahisi la kutafsiri mapendekezo ya Tume ya Jaji Nyalali ukawa ni mzigo mzito sana kwa wana CCM.

Kwa mujibu wa katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano Tanzania, hakuna mahali popote panapoelezwa majukumu na wajibu wa chama kinachokuwa madarakani, lakini kwa kuwa CCM ni wagumu kuelewa mambo rahisi, kila wakati wanadhani serikali ya Tanzania ni mali yao. Utawasikia wakisema "Sisi CCM ndiyo tumekuajiri" "Hii ni serikali ya CCM" "Mwenyekiti wa chama chetu ni Amiri Jeshi Mkuu usimchezee" Yaani jambo rahisi tu la kujua kwamba serikali ni mali ya watanzania wote limewashinda kuelewa.

Nitaendelea kuweka mambo rahisi ambayo wana CCM inakuwa vigumu kuyaelewa!!
 
Tangu mkoloni aondoke aliyeunda serikali ni Tanu na CCM.

Hii ni serikali ya CCM. Hadi pale itakapokuja katiba mpya " labda " teuzi za Rais zia viongozi wa serikali zitapitia bungeni!
 
Kama kweli vile maana tume ya warioba baada kuzunguuka karibu tz nzima na kuja na mapendekezo ya wananchi walio wengi angalia ccm ilivyovuruga.
 
Tume ya Jaji Fransici Nyalali iliposema kwamba asilimia themani (80%) ya watanzania wanapendelea kubakia kwenye mfumo chama kimoja lakini wanapendekeza mabadiliko kadhaa yafanyike kwenye CCM, wana CCM wengi walitafsiri kwamba watanzania wamekataa mfumo wa vyama vingi. Kama si uelewa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, leo hii tusingekuwa na vyama vingi.

Mwalimu alisema kwamba, watanzania wanapendelea kubakia kwenye mfumo wa chama kimoja, lakini "lakini" zao ni nyingi sana kiasi kwamba haiwezekani kufanyike marekebisho kwenye Katiba ya CCM na CCM ikabakia ilivyo kama CCM. Mwalimu alisema mapendekezo mengi yanakwenda kinyume na mtizamo, falsafa na Itikadi ya CCM.

Mwalimu akashauri kwamba hao wenye hizo "lakini" wapewe jukwaa nje ya CCM ambako watapata fursa ya kufuata falsafa, Itikadi na mitazamo yao hiyo isiyofanana na CCM. Jambo rahisi la kutafsiri mapendekezo ya Tume ya Jaji Nyalali ukawa ni mzigo mzito sana kwa wana CCM.

Kwa mujibu wa katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano Tanzania, hakuna mahali popote panapoelezwa majukumu na wajibu wa chama kinachokuwa madarakani, lakini kwa kuwa CCM ni wagumu kuelewa mambo rahisi, kila wakati wanadhani serikali ya Tanzania ni mali yao. Utawasikia wakisema "Sisi CCM ndiyo tumekuajiri" "Hii ni serikali ya CCM" "Mwenyekiti wa chama chetu ni Amiri Jeshi Mkuu usimchezee" Yaani jambo rahisi tu la kujua kwamba serikali ni mali ya watanzania wote limewashinda kuelewa.

Nitaendelea kuweka mambo rahisi ambayo wana CCM inakuwa vigumu kuyaelewa!!
Elimu za kuunga unga hazijawahi kuwa na manufaa
 
[QUOTE="Allen Kilewella, post: 35592943, member: 55849"
,,........ Kama si uelewa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, leo hii tusingekuwa na vyama vingi.

Siyo kweli kwamba Kama si uelewa wa mwl Nyerere HADI LEO HII TUSINGEKUWA NA VYAMA VINGI.
Tume ya nyalali ilifanya kazi miaka 30 iliyopita, mwl Nyerere kafariki miaka 20 iliyopita. Mimi sioni ukweli eti Hadi leo watanzania tungekuwa tuna chama kimoja sababu vyama vingi vilikataliwa miaka 30 iliyopita na watanzania kupitia tume ya nyalali.
Observation yako ya kitoto kulinganisha na taaluma yako ya uanasheria.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Observation yako ya kitoto kulinganisha na taaluma yako ya uanasheria.
Kwanza kila siku nakukatalia kwamba mimi si mwanasheria bali ni machinga mzalendo lakini hutaki kuelewa.

Kama zaidi ya miaka 28 imepita tangu mfumo wa vyama vingi urudishwe tena Tanzania lakini bado CCM wanafanya ugandamizaji wa aina hii kwa vyama vingine vya siasa, ingekuwaje kama Mwalimu asingepigania kuanzishwa kwake??

Utoto ni utoto hata kama unadhani si utoto!!

Ndiyo maana nasema kwenu mambo rahisi inakuwa si rahisi kuyaelewa.
 
Hivi CCM wanaelewa kwamba COVID 19 ni ugonjwa na hauondoki kwa maomb bali kwa kufuata kanuni za kiafya??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom