ccm

Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho chama tawala nchini Tanzania na chama cha pili kwa muda mrefu zaidi barani Afrika, baada ya Chama cha True Whig cha Liberia. Kilianzishwa mwaka 1977, baada ya kuunganishwa kwa Tanganyika African National Union (TANU) na Afro-Shirazi Party (ASP) cha Zanzibar.
  1. McLaren

    GE2025 Felista Njau apanda mtumbwi ili kumnadi Rais Samia

    Sema CCM wana siasa za kishamba sana. Hivi kwanini Marekani au nchi zilizoendelea hatuoni theatrics kama hizi. Kama ni kweli alikuwa anataka kuwafikia wapiga kura kulikuwa na haja gani ya kujirekodi akiwa amepanda mtumbwi? Hizi ni dalili ya chama ambacho soon kinaenda kuingia kwenye bed rest...
  2. Mashamba Makubwa Nalima

    Poleni na Kifo cha CCM, ila mimi sijalia

    Poleni na kifo ila mimi sijalia. Nalia na ndugu wa Ali kibao, nalia na ndugu wa Mdude, nalia na wamama hospitali wanapambania afya zao na za watoto wao, nalia na watanzania wanapambana usiku na mchana ila wanakutana na kodi za ajabu kwenye kila kitu. Nalia na waTanzania walio na wanaouawa...
  3. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 CCM naipenda mpaka natamani nikijichanja nitoke damu ya kijani!

    Hivi haya ni mapenzi ya kweli kwa chama au ndio uchawa aonekane kwamba yeye naye yupo? Ila Hao wote ata mimi nikiwapa elfu mbili mbili utawasikia Mkalukungone Mwamba hakuna kama wewe Dunia hii😝😝 Wakuu, ukiwa na mtoto hakikisha anasoma na hana njaa ya kuja kukuaibisha kama hivi, ni fezea...
  4. H

    Kosa kubwa la waTanzania ni kuwaamini viongozi mamluki wa CCM

    Mwenye asili haachi asili yaani wapinzani kuwaamini viongozi wastaafu wa CCM au waliokimbia CCM ni kosa ka jina na hawatokaa waiongoze nchi hii kwa hao ni mamluki na wako kazini kuichafua CCM kwa maslahi ya CCM . Ya wapasa wapinzani wasimame wao wenyewe wasitegemee kina Warioba, Butiku...
  5. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Jimbo la Mchinga watu walizuiwa kuchukua fomu za ubunge, ili Salma Kikwete apite bila kupigwa. Ukweli wote huu hapa!

    Nimemsikiliza huyu mzee ameongea kwa uchungu sana na ameonyesha namna nchi inavyoendeshwa hovyo sana. Anaeleza namna ambavyo mipango ilivyopangwa Mke wa Kikwete Salma Kikwete uchaguzi wa mwaka huu 2025 katika jimbo la Mchinga apite bila kupigwa kwenye kura za maoni na ndicho kilichotokea. Soma...
  6. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Wanachama 7 wa CHADEMA wajiunga CCM

    Kwahiyo wameona kampeni ya No reforms no Election kwao ni ngumu? Au ndio wale CCM wanavalishwa nguo za CHADEMA kionesha umma kutulisha tango pori?! Yaani CHADEMA avumilie kote huko aje kuhama leo? Msitufanye watu wajinga bana😂🤣🤣 ========= Katibu Mkuu wa UWT Ndg. Suzan Peter Kunambi (MNEC)...
  7. H

    Watawala wa Tanzania, viongozi wa CCM na WanaCCM, Wanaimba Amani na Umoja, Lakini Mioyo na Matendo Yao Yanadhihirisha Walivyojaa Ushetani na Uharamia

    Kwa hakika, na kwa jina la Mungu wa Ibrahim, aishiye milele, hakuna chama kilichojaa watu wanafiki, watu ambao ni watumishi waaminifu wa shetani, katika Ulimwengu mzima, kuizidi CCM. Ukiwasikia viongozi wa CCM na Serikali yao, kila mahali wanajinadi kuwa wao ni wahubiri wa amani, wao ni walinzi...
  8. BLACK MOVEMENT

    Kuna watu hata humu JF na mtaani wanajifanya wajanja sana na waelewa ila Wazazi wao wanasombwa na Malori waende kwenye mikutano ya CCM

    Wale Wazazi wanao sombwa na malori kule bushi wana watoto wao mijini na wengine hata ni members wa JF. Ila sasa ukiwakuta huko mjini au humu utawaona ni watu waliopiga hatua kubwa ya upeo wa fikra kumbe ni full wajinga tu. Sasa kupiga hatua ya upeo kuna maana gani kama Wazazi wako wanasombwa...
  9. K

    GE2025 29 Oktoba tunashirikije uchaguzi ikiwa haya hayajafanyiwa kazi?

    Watu wa Tanzania! Sasa ni wakati wa kuandamana na kutoa sauti yetu kwa nguvu ili kuzuia uchaguzi wa udanganyifu tarehe 29 Oktoba 2025. Hapa kuna hoja kuu zinazothibitisha kuwa tunahitaji kubadilisha hali hii mbaya kabla ya kura kupigwa bila haki. Jitokeze kwa wingi na tuungane pamoja! 1...
  10. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Ahamasisha Wafanyabiashara Mbeya Kupiga Kura Oktoba 29

    Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kupitia Mkoa wa Mbeya amekutana na makundi mbalimbali ya wafanyabiashara ndogondogo zaidi ya 3000 jijini Mbeya na kuwaomba kujitokeza kupiga kura Oktoba 29, 2025 Rais Samia, Wabunge na Madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
  11. W

    GE2025 Olesendeka: Kosa ambalo CCM haifanyi ni kumleta mgombea Urais ambae rekodi yake haijathibitika kuwa anaweza kuongoza Nchi hii

    Aliyekuwa Mbunge wa Simanjiro na mwanasiasa mkongwe, Christopher Olesendeka, amesema wagombea wa Urais wa Tanzania kutoka vyama vya upinzani hawawezi kulinganishwa na mgombea wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Akizungumza katika kampeni za ubunge jimbo la Mbulu Mjini mkoani Manyara hivi karibuni...
  12. Nipe Maji

    POTOSHI Wasira amesema 'hapa Tanzania kwaka huu CCM inaogopa CHADEMA, inawakamata ili ishinde uchaguzi'

  13. The Father of All

    GE2025 Japo hajapenya kugombea na ni mara yake Luhaga Mpina anaonekana tishio kwa CCM na ACT Wazalendo

    Japo kuna dhana kuwa ACT-Wazakabwe ni CCM B, kuna kitu naona kwa mgombea wake Luhaga Mpina. Inakuwaje CCM wanamuwekea mapingamizi kila kona? Je, ana kitu kinachofanya wamgwaye isijekuwa kama yale ya Tshekedi na Kabila kule DRC ambaye aliwekwa na Kabila akidhani ni boya kumbe naye alikuwa na...
  14. Mkalukungone Mwamba

    GE2025 Wanachama 453 ACT Wazalendo Zanzibar Wahamia CCM, Wavutiwa na Uongozi wa Dkt. Mwinyi

    Wanachama 453 wa Chama cha ACT Wazalendo Zanzibar wamejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo Septemba 15, 2025 wakibainisha kuvutiwa na uongozi wa mgombea Urais wa Zanzibar kupitia chama hicho Dkt. Hussein Ali Mwinyi. Mwakilishi wa wanachama hao Faki Ali Juma amesema wameamua kujiunga na CCM...
  15. DuaZaMama

    GE2025 Mwanachama CUF: Ahadi za CCM ni zile zile wameshindwa kutimiza ndani ya miaka 30

    Akizungumza leo Septemba 15, 2025 Kutoka Kijiwe cha Kivulini, Mikocheni – Hanifa Mgonela, Mwanachama wa chama cha CUF anaweka wazi namna ambavyo suala la ajira Tanzania limekuwa fumbo lililokosa majawabu.
  16. Roving Journalist

    GE2025 Special Thread: Taarifa za Kampeni za Wagombea Urais kupitia CCM, Samia Suluhu na Dkt. Emmanuel Nchimbi

    Mada Maalum itakayozungumzia ziara nzima kwenye mchakato wa kampeni za mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan na Mgombea Mwenza Dkt. Emmanuel Nchimbi. Agosti 27, 2025 Mwenyekiti wa INEC, Jaji Mstaafu Jacobs Mwambegele kwa mamlaka aliyopewa amemteua Samia Suluhu...
  17. Idugunde

    GE2025 Kigoma: Kwa jinsi Zitto anavyojinadi jukwaani ni dhahiri anashinda Ubunge. Comedian wa CCM anapayuka hovyo.

    Naona sasa Zitto taa ya kijani imewaka. Comedian anapayula hovyo. Zitto anamwaga madini.
  18. R

    GE2025 ACT Wazalendo kumwekea Pingamizi Samia ikidai uteuzi wake haukufuata Katiba na Kanuni za chama hicho

    Chama cha ACT Wazalendo kimetangaza kuwa kitaweka pingamizi dhidi ya uteuzi wa mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, kikidai kuwa uteuzi wake haukufuata Katiba na Kanuni za chama hicho Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 14 Septemba 2025 jijini Dar es...
  19. R

    GE2025 Mkazi wa Mchinga: Tieni akili CCM hawana nia njema, Mbunge wenu Mama Salma anadharau ni akili gani kusema watu wa Mchinga wanamkubali

    Mkazi wa jimbo la Mchinga akerwa na ahadi alizotoa Mbunge wao nakudai anawaomba wananchi waamke maana Chama cha Mapinduzi kinawachezea akili
  20. R

    GE2025 Sheria inasemaje juu ya watoto kuhusishwa kwenye kampeni za Uchaguzi? Maana CCM sasa imefika mbali

    Tume huru ya uchaguzi Tanzania inatgkiwa itoe ufafanuzi wa kanuni na sheria juu ya watoto kuhusishwa kwenye kampeni za siasa Sidhani kama hawa watoto wanauelewa wa chochote ========= Mkutano Wa Uzinduzi wa Kampeni Za Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata Ya Vingunguti, na meya wa jiji la dar ameeleza...
Back
Top Bottom