Ni usiku wa manane, na ndoto inanijia,
Leo hii jumanne, ndio imenitokea,
Katika kiza kinene, na wewe umenijia,
Baba tunakukumbuka,ulale pema peponi,
Ni mengi tumeongea, nilipokuwa ndotoni,
Pia ukatuusia, ya kufaa maishani,
Nami nikafurahia, pasi jua ni ndotoni,
Baba tunakukumbuka, ulale pema...