hapo hata mama yoyo nae ni mzembe, yeye yupo amelala anamuacha housegirl anajiachia na night dress-hajui kulinda mji wake, mi ningemkuta angenieleza anadeki na night dress ya nn wakati usiku ushaisha. ila na wewe mwanaume una macho juu juu usimsingizie shetani.
naona umetumia nguvu kubwa sana kuzima hilo tukio, ila bado unaendelea.
ushauri wangui ubadilike na utulie na mumeo, kutoka nje ya ndoa ni kumdhalilisha mume wako na kumfanya aonekane hawezi kutimiza haja zako. huyo unaechepuka nae kama kweli anakupenda kwann hakukuoa akakuweka ndani.
na alaaniwe yule anaetaka kuona tupu ya shemeji yake, huna adabu, unataka kula anachokula kaka yako ili iweje.
hizi ndo laana za kujitakia.
muheshimu kaka yako
kila mmoja ana nafasi yake na status yake, hawalingani na hawafanani.
mke ni mke atabaki kuwa mke na ndugu ni ndugu atabaki hivyo. usiumize kichwa kuwalinganisha maana HAWALINGANI na hawaingiliani.
hahahaha sidhani kama unamaanisha delila wa Bible maana ukimpata huyo lazma akuuze kwa wafilist, unyolewe nywele na wakung'oe macho shauri zako. otherwise badili hilo jina
hahahaha...huwa sipendi kucheka maneno ya watumishi ila kwa hili pastor nimekushindwa
sidhani kama kuna connection kwenye hilo, shanga zimekuwa zikivaliwa na mabibi zetu tangu enzi na enzi na ndoa zao zimekuwa zikidumu, zingine huvaliwa kama sehemu ya utamaduni wa makabila tofauti.
nadhani...
kwani wewe ni nani hata usipate experience ya kuumizwa na mapenzi kidogo,
kila kitu kinataka experience siku hizi, siku ukija kuingia ndoani unakuwa una uzoefu wa vingi.
ndo maisha hayo, jipange anza upya
poor you...endelea kuwa baba huruma kwa wake za watu, siku waume zao wakiamua kukulipa fadhila kwa kukuinamisha usiache kuja kutuhadithia pia.
mi am bizzzy
kuna vitu viwili naviona kwa your 34 guy...
moja inawezekana labda anataka amalize majukumu yake ya nyumbani like kusomesha wadogo zake ili mkioana asiwe na mzigo mkubwa
ila wasiwasi wangu mahitaji ya nyumbani huwa hayaishi, ni mwendelezo, na wewe una kazi na maisha yako so hutakuwa tegemezi...
pole sana dada yangu, na hongera kwa kujitahidi kulea mwanao,
hayo ni mapito tu ya dunia, una uwezo wa kufanya kazi jitume, kuwa busy na kazi zako lea mtoto wako,
ondoa hicho kisasi ulichikweka moyoni dhidi ya wanaume, si kweli kuwa wanaume wote wana matatizo nakuhakikishia wapo wengi tu...
maamuzi uliyofanya ni ya pupa na umemwaibisha mumeo, kutembea na dereva tax wenu ni aibu kubwa!
huko ulipoenda kwenye suluhisho la pili nako muda si mrefu utakuja tena kuomba msaada wa ushauri...
mumeo nae ana shida kwani kutengeneza fumanizi la kushtukiza ni kukuaibisha na wewe pia...
concern yako unayoombea ushauri ni kigezo cha umri au salary?
mapenzi na ndoa ni maridhiano ya wawili, issue za umri ni nyie wenyewe muangalie je wewe upo comfortable kuwa nae while amekuzidi? je na yeye yupo comfortable pia?
issue ya yeye kukuzidi mshahara jiulize pia maswali hayo hapo...
maisha utakayoenda kuishi ni ya kwako hakuna atakayekusaidia.
usioe kwaajili ya kumuonea mtu huruma, au woga wa shemeji yako, oa mtu unayeona moyo wako una amani nae na utakuwa na furaha.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.