Ni kweli. Maana hata hizo plugins na themes wanazotumia ni products za hao Coders. Yaani kwa kifupi bila coding na uwepo wa coders hiyo industry ya wordpress haiwezi kuexist.
Hata pesa zikijenga mikoani still watu hawataona umuhimu wa kulipa kodi.
Nikupe mfano mmoja, wakati inajengwa barabara ile bagamoyo msata watu walikuwa wakilalamika kuwa mkwele anajenga kwao, lakini wanasahau ile njia pia watu wanaoenda tanga, kilimanjaro na arusha wanaitumia na inawasaidia...
Safi sana chief. Unajua hivi vitu watu wengi hawavifahamu, mtu anajua ukishalipia tangazo tu facebook basi ni lazima upate sales. Hii ni knowledge ambayo watu wanatakiwa kuipata ili waweze kufanikiwa kwenye kufanya marketing kupitia hiyo mitandao.
Kuna kitu umekieleza hapo mwanzo kuhusu purpose...
Ni kweli jamaa ameangalia vitu vidogo sana, lakini matusi wanayofanya hawa wenye pesa ni hatari......Larry Ellison amenunua private island ya $300 million huko Lanai, Hawaii.....ni shidaaaa.
Nadhani pia ni hulka tu ya mtu na mtu. Larry Ellison, Co-founder wa Oracle Corporation ni mmoja wa mabilionea wakubwa tu ambao wana spend ile mbaya, jamaa anaishi Lavish lifestyle sana, kwahiyo inategemea tu na hulka ya mtu.
Kwa mtazamo wangu nadhani kwa nchi kama Tanzania na nchi nyingi za Africa mtumiaji wa mitandao ndiye anayelipa kodi. Yaani mtu mmoja mmoja na makampuni ambayo yanatangaza kupitia hiyo mitandao kutokana na vifurushi vya data wanavyonunua pamoja na makato ya card za benki wanazotumia kulipia hayo...
Mkuu hapa ulikosea, we uliacha kazi ya kwenye kampuni na kufanya privately lakini still ulikuwa bado unasubiri clients then uwe hired, so you were working on someone else. Developers wengi wametajirika kwa kuja na product ambayo ina demand kubwa na kuipeleka sokoni. Labda ungesema ulidrop...
Mkuu, coding is about practical. Hizo useless apps wengine wanafanya kutest skills walizonazo, kama ulivyosema kwa vile soko huria hata wanafunzi wa vyuo wanaweza kucode hizo apps, lakini kikubwa siyo lazima watengeneze mamilioni ila wanafanya kutest skills walizonazo, ni kama kujaribisha...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.