Introduction to Facebook and Instagram Ads (Matangazo ya sponsored) 2020

Introduction to Facebook and Instagram Ads (Matangazo ya sponsored) 2020

Safi sana chief. Unajua hivi vitu watu wengi hawavifahamu, mtu anajua ukishalipia tangazo tu facebook basi ni lazima upate sales. Hii ni knowledge ambayo watu wanatakiwa kuipata ili waweze kufanikiwa kwenye kufanya marketing kupitia hiyo mitandao.

Kuna kitu umekieleza hapo mwanzo kuhusu purpose au intent ya tangazo, Watu wengi huwa wanakimbilia kuwa na Sales intent bila kujua who actually wants to buy their products, yaan unakuta mtu anataka kufanya sales lakini hajui ni nani hasa anahitaji bidhaa anayouza, hii inapelekea lile tangazo kuonekana na watu ambao hawana interest na bidhaa au huduma anayoitoa, kwahiyo watu wanaishia kulike tu bila hata kuclick link ya tangazo. Kwahiyo ni muhimu kwanza kujua interest na demographics za wateja unaowalenga.

Namshauri mtu ambaye ana purpose ya kufanya sales aanze na Engagement Goal ili kupima maji kwanza kabla hajaamua kuja na sales goal.

By the way hongera, unaonekana unafahamu vitu vingi sana, niko tayari kujifunza kutoka kwako, tupe maarifa watanzania wenzako, mungu atakubariki.
 
Thanks kwa shule nzuri, Hii ya kutoa tangazo bila ku specify audience hata mimi imenikuta...unakuta tangazo linakuwa halina return nzuri...

Lakini pia kwenye kuandika tangazo lisiwe boring pia nahitaji shule zaidi... mfano kama mimi nauza bidhaa ya aina moja kinachotofautiana ni Size na rangi tu!! Kunakipindi nakuwa napost...mpaka mimi mwenyewe ninae post naona I'm boring na tangazo langu, sasa najiuliza audience wangu je?

Naamin hapa nitajifunza namna nzuri ya kutengeneza tangazo linalomvutia mteja kusoma.
 
Asante kwa maelezo mazuri. Tatizo langu ni jinsi ya ku manage Business manager.Nina business page ambayo nilianza kutangaza,bahati mbaya business ad account na business Manager yangu vimekuwa disabled. Nilikuwa appeal wakajibu kuwa waliifunga kimakosa ila bado siwezi kutengeneza ads. Nilitengeneza leads generation ad kabla ya kufungiwa na Facebook.
Ninaomba unisaidie na swala zima la Business Manager kama ifuatavyo:
1.Je, ninaweza kuwa na business manager ngapi ktk 1 business account?
2. Je, ninaweza kuwa na ad accounts ngapi ktk 1 business manager account?
3 Je,ninawezaje kuendelea kutangaza Facebook?
4. Nifanye nini in future ili niwe salama kutangaza Facebook?
Nimekwama kutengeneza ads sababu sijui nifanye nini.Nime appeal tena Facebook hawajanijibu.Ninategemea ads kuendesha biashara. Naomba ushauri tafadhali.
 
Back
Top Bottom