Kwanini Watu Hawapendi Kulipa Kodi Ya Mapato!?

Afrolink-Tz Consult Ltd

JF-Expert Member
Feb 25, 2018
420
939
Habari zenu

Makala hii naileta ikiwa katika muundo wa swali ambalo kama jamii na wenye mamlaka pia wanapaswa kujiuliza na hatimaye kutafuta njia sahihi za kuifanya jamii ione na iamini ya kuwa kulipa kodi ya mapato ni wajibu wa kila anaestahili na si kwa watu wachache tu kama wafanyabiashara, wajasiriamali ,wafanyakazi na wadau wengineo.

Itambulike ya kwamba kodi ya Mapato ina umuhimu mkubwa sana kwa nchi yoyote duniani kwani ni chanzo kikuu cha mapato kwa serikali ambapo kupitia kodi hii basi maendeleo katika Nyanja mbali mbali kama vile za kielimu, kiafya, huduma na miundombinu hugharamiwa

Ama baada ya utangulizi huo, tukirejea katika Makala yetu ya leo fikirishi ya kwa nini hasaa jamii (si yote) hususani Tanzania haipendi kuwajibika katika ulipaji wa kodi. Hili husababishwa na mambo ambayo twaweza kugawanya katika maeneo makuu mawili
A. Jamii (wafanyabiashara, wajasiriamali, wafanyakazi, wakulima na wadau wengineo)
B. Mamlaka zinazohusika na ukusanyaji wa kodi

A: Jamii husika
Jamii kuu inayolipa kodi imegawanyika katika makundi ya wafanyabiashara, wajasiriamali, wafanyakazi, wakulima na wadau wengineo ambao uwajibikaji wao wa kulipa kodi ya mapato kwa hiyari ni mgumu japo sio wote. Changamoto hii huweza kutokana na:

1. Ukosefu wa elimu juu ya kodi ya mapato
Jamii yetu asilimia kubwa bado kuna changamoto kubwa sana juu ya elimu ya ulipaji wa kodi, kwa nini alipe kodi, namna gani ya ulipaji kodi, kipi kilipiwe kodi na kipi hakilipiwi kodi n.k. kutokuwa na elimu kunaifanya jamii hii kuona hakuna haja ya kulipa kodi. Jamii nyingi za watu waishio maeneo ya vijijini mathalani japo na mijini kuna changamoto hii hawana elimu ya msingi juu ya kodi hivyo kuleta uzito wa kuwajibika katika kulipa kodi.

2. Tabia za jamii (kasumba)
Jamii kuamini kuwa kama utakuwa muwazi katika mapato yako basi ukienda Mamlaka ya Mapato hutokubaliwa unachotaka kulipa bali utalipishwa kodi kwa matakwa ya mtu atakaekusikiliza. Kutokana na khofu hii hata kama jamii husika ikienda basi itatoa maelezo yasiyo sahihi ili tu kujihami dhidi ya kulazimishwa juu ya kiasi gani cha kulipa

3. Mfumo wa ulipaji kodi kuonekana kama una kificho kwa jamii
Hii pia ni kasumba iliyojengeka kwa jamii kuwa kuna mtego katika namna ya ukokotoaji wa kodi kwa kuwa jamii inaamini haupo wazi kwao. Kwa mfano labda kwa nini alipe kiasi fulani cha kodi ilhali biashara aliyofanya haikuzalisha kiasi hicho. Jamii inakuwa inaamini kuwa ukokotoaji wa kodi huwa ‘based on assumptions rather than the facts’ hivyo kusababisha kulipa kodi kubwa na kandamizi

4. Jamii kuwa na mtazamo hasi juu ya matokeo baada ya malipo ya kodi

Hili linatokana na jamii kuona matokeo baada ya kulipa kodi hayana uwiano na kinacholipwa. Maana yake ni kwamba jamii inaamini kulipa kodi basi ipate huduma bora kama za afya, elimu na maji. Sasa nongwa huja iwapo mwanajamii akienda hospitali akikosa tu dawa basi kuamini kodi inawanufaisha wachache

5. Watu wachache kuwajibika kulipa kodi
Hii inatokana na kuamni kuwa wanajamii wachache sana wanalipakodi hivyo kujikuta wanakuwa na kodi za viwango vikubwa ilhali kundi kubwa la jamii halilipi kodi moja kwa moja kama kundi dogo. Kutokana na hili linasababisha jamii kuchukia kulipa kodi ya mapato

Hizi ni baadhi tu ya sababu za jamii.

B: Mamlaka zinazohusika na ukusanyaji wa kodi
Mamlaka kwa ujumla zina sheria, kanuni na taratibu nzuri sana za ulipaji wa kodi kwa kila mwanajamii alie na sifa. Ila kunaweza kukawa na sababu hizi ndani yake ambazo zikasababisha utekelezaji kuwa na mapungufu

1. Watendaji
Hii inakuja pale mtendaji kufanya maamuzi kwa mujibu wa matakwa yake na si kwa mujibu wa sheria zinavyoelekezwa. Hili hupelekea kutoa upendeleo au kumkandamiza mlipaji kodi. Pia mtendaji kutumia ‘advantage’ ya mwanajamii kutokuwa na elimu ya kodi basi anamkandamiza ikiwa kwa nia ya kunufaika na tatizo la mlengwa au kumkandamiza

SULUHISHO
Kutokana na changamoto na kelele zinazozidi kila leo juu ya masuala ya kodi ya mapato, kuna haja serikali kuchukua hatua stahiki zifuatazo:
  • Somo la kodi (basic) liwekwe kwenye mitaala ya elimu kuanzia ngazi za chini ikibidi shule za msingi ili kila mtoto anakuwa akiamini kulipakodi ni wajibu
  • Mamlaka zinazohusika zijitahidi kuongeza idadi ya walipa kodi wa moja kwa moja (tax base) kwn hii itasaidia hata kupunguza kiwango cha kodi kuwa Rafiki zaidi
  • Uadilifu kwa watendaji wa Mamlaka husika za ukusanyaji mapato. Watendaji kuamini ni wajibu wao kutoa elimu kwa mlipa kodi kwani bila kufanya hivyo kila leo kos litakuwa lenye kujirudia kwa mlipa kodi
Karibuni kwa mjadala zaidi.Tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa Letu
 
Pengine kodi ni nyingi mno na haziendani na uhalisia halisi wa maisha ya watu (wa kawaida).

Je, hizo kodi zinatumiwa vyema? Jamii inafaidika nazo au zinaishia kutajirisha 1% ya watawala na marafiki zao; na hata kufanyia mambo yasiyo na tija kwa walipaji wengi?
Hii pia inaweza ikawa sababu jamii kuona kuna kodi nyingi sana na viwangi vya kodi kuwa vikubwa tofauti na uhalisia wa kipato kitokanacho na biashara. Kodi hizo ni kama vile kodi kuu, paye, sdl, sd, wht, vat et al.

Pia jamii kuamn inachajiwa mara mbili au tatu zaidi ktk kipato hicho hicho kwa sura ya jina la kodi tofauti. Lakini elimu juu ya kodi ingesaidia kujua kasumba hii sio sahihi

Kwa matumizi hili halina shaka kwani kuna miradi mingi ambayo jamii inashuhudia inafanyika ikiwa ni matokeo chanya ya matumizi ya kodi inayolipwa
 
Habari zenu

Makala hii naileta ikiwa katika muundo wa swali ambalo kama jamii na wenye mamlaka pia wanapaswa kujiuliza na hatimaye kutafuta njia sahihi za kuifanya jamii ione na iamini ya kuwa kulipa kodi ya mapato ni wajibu wa kila anaestahili na si kwa watu wachache tu kama wafanyabiashara, wajasiriamali ,wafanyakazi na wadau wengineo.

Itambulike ya kwamba kodi ya Mapato ina umuhimu mkubwa sana kwa nchi yoyote duniani kwani ni chanzo kikuu cha mapato kwa serikali ambapo kupitia kodi hii basi maendeleo katika Nyanja mbali mbali kama vile za kielimu, kiafya, huduma na miundombinu hugharamiwa

Ama baada ya utangulizi huo, tukirejea katika Makala yetu ya leo fikirishi ya kwa nini hasaa jamii (si yote) hususani Tanzania haipendi kuwajibika katika ulipaji wa kodi. Hili husababishwa na mambo ambayo twaweza kugawanya katika maeneo makuu mawili
A. Jamii (wafanyabiashara, wajasiriamali, wafanyakazi, wakulima na wadau wengineo)
B. Mamlaka zinazohusika na ukusanyaji wa kodi

A: Jamii husika
Jamii kuu inayolipa kodi imegawanyika katika makundi ya wafanyabiashara, wajasiriamali, wafanyakazi, wakulima na wadau wengineo ambao uwajibikaji wao wa kulipa kodi ya mapato kwa hiyari ni mgumu japo sio wote. Changamoto hii huweza kutokana na:

1. Ukosefu wa elimu juu ya kodi ya mapato
Jamii yetu asilimia kubwa bado kuna changamoto kubwa sana juu ya elimu ya ulipaji wa kodi, kwa nini alipe kodi, namna gani ya ulipaji kodi, kipi kilipiwe kodi na kipi hakilipiwi kodi n.k. kutokuwa na elimu kunaifanya jamii hii kuona hakuna haja ya kulipa kodi. Jamii nyingi za watu waishio maeneo ya vijijini mathalani japo na mijini kuna changamoto hii hawana elimu ya msingi juu ya kodi hivyo kuleta uzito wa kuwajibika katika kulipa kodi.

2. Tabia za jamii (kasumba)
Jamii kuamini kuwa kama utakuwa muwazi katika mapato yako basi ukienda Mamlaka ya Mapato hutokubaliwa unachotaka kulipa bali utalipishwa kodi kwa matakwa ya mtu atakaekusikiliza. Kutokana na khofu hii hata kama jamii husika ikienda basi itatoa maelezo yasiyo sahihi ili tu kujihami dhidi ya kulazimishwa juu ya kiasi gani cha kulipa

3. Mfumo wa ulipaji kodi kuonekana kama una kificho kwa jamii
Hii pia ni kasumba iliyojengeka kwa jamii kuwa kuna mtego katika namna ya ukokotoaji wa kodi kwa kuwa jamii inaamini haupo wazi kwao. Kwa mfano labda kwa nini alipe kiasi fulani cha kodi ilhali biashara aliyofanya haikuzalisha kiasi hicho. Jamii inakuwa inaamini kuwa ukokotoaji wa kodi huwa ‘based on assumptions rather than the facts’ hivyo kusababisha kulipa kodi kubwa na kandamizi

4. Jamii kuwa na mtazamo hasi juu ya matokeo baada ya malipo ya kodi

Hili linatokana na jamii kuona matokeo baada ya kulipa kodi hayana uwiano na kinacholipwa. Maana yake ni kwamba jamii inaamini kulipa kodi basi ipate huduma bora kama za afya, elimu na maji. Sasa nongwa huja iwapo mwanajamii akienda hospitali akikosa tu dawa basi kuamini kodi inawanufaisha wachache

5. Watu wachache kuwajibika kulipa kodi
Hii inatokana na kuamni kuwa wanajamii wachache sana wanalipakodi hivyo kujikuta wanakuwa na kodi za viwango vikubwa ilhali kundi kubwa la jamii halilipi kodi moja kwa moja kama kundi dogo. Kutokana na hili linasababisha jamii kuchukia kulipa kodi ya mapato

Hizi ni baadhi tu ya sababu za jamii.

B: Mamlaka zinazohusika na ukusanyaji wa kodi
Mamlaka kwa ujumla zina sheria, kanuni na taratibu nzuri sana za ulipaji wa kodi kwa kila mwanajamii alie na sifa. Ila kunaweza kukawa na sababu hizi ndani yake ambazo zikasababisha utekelezaji kuwa na mapungufu

1. Watendaji
Hii inakuja pale mtendaji kufanya maamuzi kwa mujibu wa matakwa yake na si kwa mujibu wa sheria zinavyoelekezwa. Hili hupelekea kutoa upendeleo au kumkandamiza mlipaji kodi. Pia mtendaji kutumia ‘advantage’ ya mwanajamii kutokuwa na elimu ya kodi basi anamkandamiza ikiwa kwa nia ya kunufaika na tatizo la mlengwa au kumkandamiza

SULUHISHO
Kutokana na changamoto na kelele zinazozidi kila leo juu ya masuala ya kodi ya mapato, kuna haja serikali kuchukua hatua stahiki zifuatazo:
  • Somo la kodi (basic) liwekwe kwenye mitaala ya elimu kuanzia ngazi za chini ikibidi shule za msingi ili kila mtoto anakuwa akiamini kulipakodi ni wajibu
  • Mamlaka zinazohusika zijitahidi kuongeza idadi ya walipa kodi wa moja kwa moja (tax base) kwn hii itasaidia hata kupunguza kiwango cha kodi kuwa Rafiki zaidi
  • Uadilifu kwa watendaji wa Mamlaka husika za ukusanyaji mapato. Watendaji kuamini ni wajibu wao kutoa elimu kwa mlipa kodi kwani bila kufanya hivyo kila leo kos litakuwa lenye kujirudia kwa mlipa kodi
Karibuni kwa mjadala zaidi.Tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa Letu
Namba 4 na 5 ndio sababu kuu
 
Kwa hapa kwetu, Mamlaka husika hazitoi elimu ipasavyo, mnasikia tu notice kuanzia sasa mnatakiwa mlipe hiki na hiki, hakuna elimu hakuna muda ni hapo hapo utekelezaji...

Mamlaka zinakuja kwenye kampuni yako, na kuomba taarifa za malipo ya mapato ambayo ndiyo kwanza unaanza kuyasikia kutoka kwao, ukiwahoji unaambiwa hilo limepitishiwa wao ni watekelezaji tu...



Cc: mahondaw
 
Hata Tanzania kulipa kodi ni lazima (wajibu). Tatizo je jamii inakubali kuwajibika? Kama hapana kwa nini? Suluhisho lazima litafutwe. Ukiona jamii inalalamika sana juh ya kulipa kodi ina maana kuna mahala hapako sawa

Watz hawana elimu ya kodi wengi wanachukulia kodi kama mateso. Hatuwez lipa kodi kwa hiari mpaka tutafutane
 
Hapo no nne, matokeo baada ya kulipa kodi huduma zinazotolewa havina uwiano. 2 asilimia kubwa ya kodi kutumika kuhudumia serikali, kulipana mishaara minono na marupurupu, kununua magari ya kifahari,
Mf: yule aliye nunua gari ya mil 400 wakati yawezekana kwenye wilaya hiyo kuna upungufu wa madarasa na madawati.
3. Vipaumbele vya serikari kuwa tofauti na vya wananchi, wakati tunanunua ndege kwa cash bila hata kushirikisha bunge kuna sehemu watu wanakufa kwa kukosa dawa hospital, hapa lazima vipaumbele vya serikali viendeane mahitaji ya wananchi.
4.Serikali kutamba tumefanya hiki tumefanya kile, kama vile hizo pesa wametoa kwenye mifuko yao, lazima muwakumbushe wananchi kila hatua ya maendeleo kwenye hii nchi ni kwa sababu ya kodi yao na nyie ni wasimamizi tu na hii itahamasisha wananchi walipe kodi kwa uaminifu.
 
Watz hawana elimu ya kodi wengi wanachukulia kodi kama mateso. Hatuwez lipa kodi kwa hiari mpaka tutafutane
Kuna sababu inayo chabgia hili hatukufika hapa kwa bahati mbaya

Ukiusoma Uzi vizuri paragraph namba 3 4 na 5 zinajieleza vizuri kabisa sababu zinazo wafanya watanzania wakose muamko was kulipa Kodi

Sasa Kama tunalipa Kodi halafu pesa zetu hizo ndio zinatumika kuwa nunua viongozi wa vyama pinzani kwa muktadha huo unadhani Nani ambaye atakuwa na hamasa ya kulipa Kodi bila shurti
 
Kuna sababu inayo chabgia hili hatukufika hapa kwa bahati mbaya

Ukiusoma Uzi vizuri paragraph namba 3 4 na 5 zinajieleza vizuri kabisa sababu zinazo wafanya watanzania wakose muamko was kulipa Kodi

Sasa Kama tunalipa Kodi halafu pesa zetu hizo ndio zinatumika kuwa nunua viongozi wa vyama pinzani kwa muktadha huo unadhani Nani ambaye atakuwa na hamasa ya kulipa Kodi bila shurti

Zile flyover, sgr, barabara za mwenge, ndegr nk zinanuliwa kwa pesa ipi??
 
Habari zenu

Makala hii naileta ikiwa katika muundo wa swali ambalo kama jamii na wenye mamlaka pia wanapaswa kujiuliza na hatimaye kutafuta njia sahihi za kuifanya jamii ione na iamini ya kuwa kulipa kodi ya mapato ni wajibu wa kila anaestahili na si kwa watu wachache tu kama wafanyabiashara, wajasiriamali ,wafanyakazi na wadau wengineo.

Itambulike ya kwamba kodi ya Mapato ina umuhimu mkubwa sana kwa nchi yoyote duniani kwani ni chanzo kikuu cha mapato kwa serikali ambapo kupitia kodi hii basi maendeleo katika Nyanja mbali mbali kama vile za kielimu, kiafya, huduma na miundombinu hugharamiwa

Ama baada ya utangulizi huo, tukirejea katika Makala yetu ya leo fikirishi ya kwa nini hasaa jamii (si yote) hususani Tanzania haipendi kuwajibika katika ulipaji wa kodi. Hili husababishwa na mambo ambayo twaweza kugawanya katika maeneo makuu mawili
A. Jamii (wafanyabiashara, wajasiriamali, wafanyakazi, wakulima na wadau wengineo)
B. Mamlaka zinazohusika na ukusanyaji wa kodi

A: Jamii husika
Jamii kuu inayolipa kodi imegawanyika katika makundi ya wafanyabiashara, wajasiriamali, wafanyakazi, wakulima na wadau wengineo ambao uwajibikaji wao wa kulipa kodi ya mapato kwa hiyari ni mgumu japo sio wote. Changamoto hii huweza kutokana na:

1. Ukosefu wa elimu juu ya kodi ya mapato
Jamii yetu asilimia kubwa bado kuna changamoto kubwa sana juu ya elimu ya ulipaji wa kodi, kwa nini alipe kodi, namna gani ya ulipaji kodi, kipi kilipiwe kodi na kipi hakilipiwi kodi n.k. kutokuwa na elimu kunaifanya jamii hii kuona hakuna haja ya kulipa kodi. Jamii nyingi za watu waishio maeneo ya vijijini mathalani japo na mijini kuna changamoto hii hawana elimu ya msingi juu ya kodi hivyo kuleta uzito wa kuwajibika katika kulipa kodi.

2. Tabia za jamii (kasumba)
Jamii kuamini kuwa kama utakuwa muwazi katika mapato yako basi ukienda Mamlaka ya Mapato hutokubaliwa unachotaka kulipa bali utalipishwa kodi kwa matakwa ya mtu atakaekusikiliza. Kutokana na khofu hii hata kama jamii husika ikienda basi itatoa maelezo yasiyo sahihi ili tu kujihami dhidi ya kulazimishwa juu ya kiasi gani cha kulipa

3. Mfumo wa ulipaji kodi kuonekana kama una kificho kwa jamii
Hii pia ni kasumba iliyojengeka kwa jamii kuwa kuna mtego katika namna ya ukokotoaji wa kodi kwa kuwa jamii inaamini haupo wazi kwao. Kwa mfano labda kwa nini alipe kiasi fulani cha kodi ilhali biashara aliyofanya haikuzalisha kiasi hicho. Jamii inakuwa inaamini kuwa ukokotoaji wa kodi huwa ‘based on assumptions rather than the facts’ hivyo kusababisha kulipa kodi kubwa na kandamizi

4. Jamii kuwa na mtazamo hasi juu ya matokeo baada ya malipo ya kodi

Hili linatokana na jamii kuona matokeo baada ya kulipa kodi hayana uwiano na kinacholipwa. Maana yake ni kwamba jamii inaamini kulipa kodi basi ipate huduma bora kama za afya, elimu na maji. Sasa nongwa huja iwapo mwanajamii akienda hospitali akikosa tu dawa basi kuamini kodi inawanufaisha wachache

5. Watu wachache kuwajibika kulipa kodi
Hii inatokana na kuamni kuwa wanajamii wachache sana wanalipakodi hivyo kujikuta wanakuwa na kodi za viwango vikubwa ilhali kundi kubwa la jamii halilipi kodi moja kwa moja kama kundi dogo. Kutokana na hili linasababisha jamii kuchukia kulipa kodi ya mapato

Hizi ni baadhi tu ya sababu za jamii.

B: Mamlaka zinazohusika na ukusanyaji wa kodi
Mamlaka kwa ujumla zina sheria, kanuni na taratibu nzuri sana za ulipaji wa kodi kwa kila mwanajamii alie na sifa. Ila kunaweza kukawa na sababu hizi ndani yake ambazo zikasababisha utekelezaji kuwa na mapungufu

1. Watendaji
Hii inakuja pale mtendaji kufanya maamuzi kwa mujibu wa matakwa yake na si kwa mujibu wa sheria zinavyoelekezwa. Hili hupelekea kutoa upendeleo au kumkandamiza mlipaji kodi. Pia mtendaji kutumia ‘advantage’ ya mwanajamii kutokuwa na elimu ya kodi basi anamkandamiza ikiwa kwa nia ya kunufaika na tatizo la mlengwa au kumkandamiza

SULUHISHO
Kutokana na changamoto na kelele zinazozidi kila leo juu ya masuala ya kodi ya mapato, kuna haja serikali kuchukua hatua stahiki zifuatazo:
  • Somo la kodi (basic) liwekwe kwenye mitaala ya elimu kuanzia ngazi za chini ikibidi shule za msingi ili kila mtoto anakuwa akiamini kulipakodi ni wajibu
  • Mamlaka zinazohusika zijitahidi kuongeza idadi ya walipa kodi wa moja kwa moja (tax base) kwn hii itasaidia hata kupunguza kiwango cha kodi kuwa Rafiki zaidi
  • Uadilifu kwa watendaji wa Mamlaka husika za ukusanyaji mapato. Watendaji kuamini ni wajibu wao kutoa elimu kwa mlipa kodi kwani bila kufanya hivyo kila leo kos litakuwa lenye kujirudia kwa mlipa kodi
Karibuni kwa mjadala zaidi.Tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa Letu
Kodi za nchi hii ni kubwa mnoo, hazilipiki.

Kuna 18%, then 25% plus plus = 45+

Then kuna kodi nyingine nyingi tu.

Na kibaya zaidi nchi hii wanaolipa kodi si zaidi ya milioni 3 kati ya watanzania Milioni 60.

Na CCM waluvyo vichwa maji kila mwaka wa fedha badala ya kutafuta namna ya kuwezesha watu wengi zaidi walipe k9di, wao wako busy kuwaongezea watu wake wale wanaolipa siku zote.

Tena wakusanya kodi wenyewe wanakuja kwako as if wewe ni mhalifu tayari, ni mwendo wa kuviziana tu.

Any6 tuchikulie hata kama kodi umelipa, bado nchi hii kuna unexpected expenses ambazo hazikuwa hata kwenye prospects za kampuni: Fires, OSHA, TMDA, TBS, TCRA, TCCIA n.k

Bado misaada ya kulazimishwa kutoa na CCM.

Yaani mazingira hayo ndio yanapelekea watu kukwepa kulipa kodi.
 
Habari zenu

Makala hii naileta ikiwa katika muundo wa swali ambalo kama jamii na wenye mamlaka pia wanapaswa kujiuliza na hatimaye kutafuta njia sahihi za kuifanya jamii ione na iamini ya kuwa kulipa kodi ya mapato ni wajibu wa kila anaestahili na si kwa watu wachache tu kama wafanyabiashara, wajasiriamali ,wafanyakazi na wadau wengineo.

Itambulike ya kwamba kodi ya Mapato ina umuhimu mkubwa sana kwa nchi yoyote duniani kwani ni chanzo kikuu cha mapato kwa serikali ambapo kupitia kodi hii basi maendeleo katika Nyanja mbali mbali kama vile za kielimu, kiafya, huduma na miundombinu hugharamiwa

Ama baada ya utangulizi huo, tukirejea katika Makala yetu ya leo fikirishi ya kwa nini hasaa jamii (si yote) hususani Tanzania haipendi kuwajibika katika ulipaji wa kodi. Hili husababishwa na mambo ambayo twaweza kugawanya katika maeneo makuu mawili
A. Jamii (wafanyabiashara, wajasiriamali, wafanyakazi, wakulima na wadau wengineo)
B. Mamlaka zinazohusika na ukusanyaji wa kodi

A: Jamii husika
Jamii kuu inayolipa kodi imegawanyika katika makundi ya wafanyabiashara, wajasiriamali, wafanyakazi, wakulima na wadau wengineo ambao uwajibikaji wao wa kulipa kodi ya mapato kwa hiyari ni mgumu japo sio wote. Changamoto hii huweza kutokana na:

1. Ukosefu wa elimu juu ya kodi ya mapato
Jamii yetu asilimia kubwa bado kuna changamoto kubwa sana juu ya elimu ya ulipaji wa kodi, kwa nini alipe kodi, namna gani ya ulipaji kodi, kipi kilipiwe kodi na kipi hakilipiwi kodi n.k. kutokuwa na elimu kunaifanya jamii hii kuona hakuna haja ya kulipa kodi. Jamii nyingi za watu waishio maeneo ya vijijini mathalani japo na mijini kuna changamoto hii hawana elimu ya msingi juu ya kodi hivyo kuleta uzito wa kuwajibika katika kulipa kodi.

2. Tabia za jamii (kasumba)
Jamii kuamini kuwa kama utakuwa muwazi katika mapato yako basi ukienda Mamlaka ya Mapato hutokubaliwa unachotaka kulipa bali utalipishwa kodi kwa matakwa ya mtu atakaekusikiliza. Kutokana na khofu hii hata kama jamii husika ikienda basi itatoa maelezo yasiyo sahihi ili tu kujihami dhidi ya kulazimishwa juu ya kiasi gani cha kulipa

3. Mfumo wa ulipaji kodi kuonekana kama una kificho kwa jamii
Hii pia ni kasumba iliyojengeka kwa jamii kuwa kuna mtego katika namna ya ukokotoaji wa kodi kwa kuwa jamii inaamini haupo wazi kwao. Kwa mfano labda kwa nini alipe kiasi fulani cha kodi ilhali biashara aliyofanya haikuzalisha kiasi hicho. Jamii inakuwa inaamini kuwa ukokotoaji wa kodi huwa ‘based on assumptions rather than the facts’ hivyo kusababisha kulipa kodi kubwa na kandamizi

4. Jamii kuwa na mtazamo hasi juu ya matokeo baada ya malipo ya kodi

Hili linatokana na jamii kuona matokeo baada ya kulipa kodi hayana uwiano na kinacholipwa. Maana yake ni kwamba jamii inaamini kulipa kodi basi ipate huduma bora kama za afya, elimu na maji. Sasa nongwa huja iwapo mwanajamii akienda hospitali akikosa tu dawa basi kuamini kodi inawanufaisha wachache

5. Watu wachache kuwajibika kulipa kodi
Hii inatokana na kuamni kuwa wanajamii wachache sana wanalipakodi hivyo kujikuta wanakuwa na kodi za viwango vikubwa ilhali kundi kubwa la jamii halilipi kodi moja kwa moja kama kundi dogo. Kutokana na hili linasababisha jamii kuchukia kulipa kodi ya mapato

Hizi ni baadhi tu ya sababu za jamii.

B: Mamlaka zinazohusika na ukusanyaji wa kodi
Mamlaka kwa ujumla zina sheria, kanuni na taratibu nzuri sana za ulipaji wa kodi kwa kila mwanajamii alie na sifa. Ila kunaweza kukawa na sababu hizi ndani yake ambazo zikasababisha utekelezaji kuwa na mapungufu

1. Watendaji
Hii inakuja pale mtendaji kufanya maamuzi kwa mujibu wa matakwa yake na si kwa mujibu wa sheria zinavyoelekezwa. Hili hupelekea kutoa upendeleo au kumkandamiza mlipaji kodi. Pia mtendaji kutumia ‘advantage’ ya mwanajamii kutokuwa na elimu ya kodi basi anamkandamiza ikiwa kwa nia ya kunufaika na tatizo la mlengwa au kumkandamiza

SULUHISHO
Kutokana na changamoto na kelele zinazozidi kila leo juu ya masuala ya kodi ya mapato, kuna haja serikali kuchukua hatua stahiki zifuatazo:
  • Somo la kodi (basic) liwekwe kwenye mitaala ya elimu kuanzia ngazi za chini ikibidi shule za msingi ili kila mtoto anakuwa akiamini kulipakodi ni wajibu
  • Mamlaka zinazohusika zijitahidi kuongeza idadi ya walipa kodi wa moja kwa moja (tax base) kwn hii itasaidia hata kupunguza kiwango cha kodi kuwa Rafiki zaidi
  • Uadilifu kwa watendaji wa Mamlaka husika za ukusanyaji mapato. Watendaji kuamini ni wajibu wao kutoa elimu kwa mlipa kodi kwani bila kufanya hivyo kila leo kos litakuwa lenye kujirudia kwa mlipa kodi
Karibuni kwa mjadala zaidi.Tulipe kodi kwa maendeleo ya Taifa Letu
Kodi ni somo pana sana kiasi ambacho, mwananchi wa kawaida hawezi kuelewa na ndio maana kuna wataalam wa mambo yahusuyo kodi. Bahati mbaya sana kuna baadhi ya watu wanaperceive kuwa ndani ya kodi kuna mirage ya siasa ndani yake hivo wananchi wanatatizwa.
But ni suala la elimu tu na kuportray integrity kwa ajili ya taifa
 
Kodi ni somo pana sana kiasi ambacho, mwananchi wa kawaida hawezi kuelewa na ndio maana kuna wataalam wa mambo yahusuyo kodi. Bahati mbaya sana kuna baadhi ya watu wanaperceive kuwa ndani ya kodi kuna mirage ya siasa ndani yake hivo wananchi wanatatizwa.
But ni suala la elimu tu na kuportray integrity kwa ajili ya taifa
Ni kweli somo pana lkn liwekwe somo kupata zile basics za kodi ili itambulike kuanzia ngazi za chini. Suala si tu kuna Tax clubs bali iwe moja ya masomo.
 
Zile flyover, sgr, barabara za mwenge, ndegr nk zinanuliwa kwa pesa ipi??
Kwahiyo Tanzania nzima ipo daresalam ... !? Utajiri wa rasilimali zilizopo nchini na maendeleo yaliyopo Ni vitu viwili ambavyo havifananani hata kwa bahati mbaya ... Nchi ina hazina ya misitu lakini bado watoto zetu wanakaa chini mashuleni
 
Kwahiyo Tanzania nzima ipo daresalam ... !? Utajiri wa rasilimali zilizopo nchini na maendeleo yaliyopo Ni vitu viwili ambavyo havifananani hata kwa bahati mbaya ... Nchi ina hazina ya misitu lakini bado watoto zetu wanakaa chini mashuleni
na magogo yanaend china
 
Hembu nisikilize sio usome nasema nisikilize.

Eneo la biashara.

Kwa mfano Mimi Nina biashara yangu hapa dodoma mjini,pale sabasaba nalipa Kodi ya halmashauri Kwa sababu ni eneo la halmashauri 100,000/=,Bado nalipa Kodi ya nilipopanga (sehemu niliyo weka biashara yangu(frame) Kwa mwenye frame alinikodishia 350,000/= Kwa mwezi 1 nimelipa 1 yr ili niweze kupat return, Kodi ya TRA nalipa 180,000/= Kila baad y miezi 3 baada ya kuwapa fix nyingi.

Nyumbani nilipo panga.

Kodi ya chumba 60,000 Kwa mwezi 1 ntkiw kulipa 4 months Kwa mwenye nyumba, nauli kwenda na kurudi 2800 per day unaenda 400 unrudi 400 Kwa hice, chumba kipo nje y mji kidogo hvyo napanda boda 1000, Kwa asubuhi muda mwingine natembea Kwa mguu. Lazima ule Chakula asubuhi,mchana na usiku, Sana Sana ni mchana na usiku asubuhi huwa najikuta imepita.

Kuchukua mzigo.

Mzigo nachukua DSM Kuna muda unaagiza kukwepa cost mambo yankua Chenga hlf mzigo unakuja hauwezi kutoka, unaenda mwenyewe muda mwingine nauli 20 kwnda na kurudi, hapo silali nikufika nakuondoka, Nimerudi saa kumi, kumi na moja, saa tisa usiku mara nyingi ,nimelala kwenye Mabus mara kibao Sana,sipo single Ila kama nipo single ili niweke mambo sawa sitaki upuuzi na maisha nimefuta wanawake kibao.


Sasa Kwa nini nisipenda kulipa Kodi wakati nahangaika hivyoo, isitoshe unasikia watu wananunua V8,wanakula pesa hvyo muda wa uchaguzi, inshot lami,hospitali, shule na mishahara yenu tunatoa Sisi, hlf wao wkpata mishahara wanaenda kuchukua kilaini wkt cc hatulali hlf wnkuj n Moto tutoe Kodi. Inaumaa

Wala usishangae mtaji na mikodi yote hiyo nimepataje ! Au pesa ya biashara imepatikana vipi, hizo pesa ni baada ya kuhangaikia pensheni Kwa miaka Mingi za marehemu Baba. Ila mambo yanakwenda vizuri maisha ndio hayahaya biashara inagoma mpk unakta tamaa Ila inasimama Kwa kudra za Mungu Baba ni mwaka wa 2 sasa.
Hapo sijaumwa, sijalipa umeme, sijapatwa na msiba ,sijaombwa michango ya harusi na Bado sijasema kuhusu bando langu nalo taipia hapa.
 
Hembu nisikilize sio usome nasema nisikilize.

Eneo la biashara.

Kwa mfano Mimi Nina biashara yangu hapa dodoma mjini,pale sabasaba nalipa Kodi ya halmashauri Kwa sababu ni eneo la halmashauri 100,000/=,Bado nalipa Kodi ya nilipopanga (sehemu niliyo weka biashara yangu(frame) Kwa mwenye frame alinikodishia 350,000/= Kwa mwezi 1 nimelipa 1 yr ili niweze kupat return, Kodi ya TRA nalipa 180,000/= Kila baad y miezi 3 baada ya kuwapa fix nyingi.

Nyumbani nilipo panga.

Kodi ya chumba 60,000 Kwa mwezi 1 ntkiw kulipa 4 months Kwa mwenye nyumba, nauli kwenda na kurudi 2800 per day unaenda 400 unrudi 400 Kwa hice, chumba kipo nje y mji kidogo hvyo napanda boda 1000, Kwa asubuhi muda mwingine natembea Kwa mguu. Lazima ule Chakula asubuhi,mchana na usiku, Sana Sana ni mchana na usiku asubuhi huwa najikuta imepita.

Kuchukua mzigo.

Mzigo nachukua DSM Kuna muda unaagiza kukwepa cost mambo yankua Chenga hlf mzigo unakuja hauwezi kutoka, unaenda mwenyewe muda mwingine nauli 20 kwnda na kurudi, hapo silali nikufika nakuondoka, Nimerudi saa kumi, kumi na moja, saa tisa usiku mara nyingi ,nimelala kwenye Mabus mara kibao Sana,sipo single Ila kama nipo single ili niweke mambo sawa sitaki upuuzi na maisha nimefuta wanawake kibao.


Sasa Kwa nini nisipenda kulipa Kodi wakati nahangaika hivyoo, isitoshe unasikia watu wananunua V8,wanakula pesa hvyo muda wa uchaguzi, inshot lami,hospitali, shule na mishahara yenu tunatoa Sisi, hlf wao wkpata mishahara wanaenda kuchukua kilaini wkt cc hatulali hlf wnkuj n Moto tutoe Kodi. Inaumaa

Wala usishangae mtaji na mikodi yote hiyo nimepataje ! Au pesa ya biashara imepatikana vipi, hizo pesa ni baada ya kuhangaikia pensheni Kwa miaka Mingi za marehemu Baba. Ila mambo yanakwenda vizuri maisha ndio hayahaya biashara inagoma mpk unakta tamaa Ila inasimama Kwa kudra za Mungu Baba ni mwaka wa 2 sasa.
Hapo sijaumwa, sijalipa umeme, sijapatwa na msiba ,sijaombwa michango ya harusi na Bado sijasema kuhusu bando langu nalo taipia hapa.
Tupambane Mkuu
 
Kwahiyo Tanzania nzima ipo daresalam ... !?
Hata pesa zikijenga mikoani still watu hawataona umuhimu wa kulipa kodi.

Nikupe mfano mmoja, wakati inajengwa barabara ile bagamoyo msata watu walikuwa wakilalamika kuwa mkwele anajenga kwao, lakini wanasahau ile njia pia watu wanaoenda tanga, kilimanjaro na arusha wanaitumia na inawasaidia ila lawama zilikuwepo. Kwahiyo hata kodi ikitumika kujenga mikoani mfano Geita huko, mtasema Meko anajenga kwao.

Nadhani sababu si kwamba pesa inatumikaje tu, nadhani pia elimu inahitajika, raia wanapaswa kupewa elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa kulipa kodi na faida zake, lakini pia viwango vya kodi yenyewe viwe nafuu, isiwe kukomoana.
 
Hakuna jamii inayopenda kulipa kodi Dunia hii, bila ya lazima hakuna atakayelipa kodi, ...
 
Back
Top Bottom