1) Kutunga nlivokumisi,
mwishoni nitaugua,
Mtima wangu yabisi,
nawe ndio lake jua,
Ya moyoni warahisi,
walimwengu kuyajua,
Kutunga sitokudisi,
amani waniletea.
2) Wafanya kwa ufanisi,
jukumu walichukua,
Wawapita wahandisi,
mabonde kuyafukia,
Wafundisha kirahisi,
vipofu wawafungua,
Kutunga...