Recent content by Kwaminchi

  1. K

    Vyama vya Siasa na Matawi ya Ughaibuni

    Sidhani kama nchi za kigeni zinaruhusu watu wa nchi nyingine (wageni) wafanye shughulu zao za kisiasa nchini mwao. Kwa mfano siamini kuwa Tanzania itaruhusu watu wa Rwanda, Burundi, DR congo, Kenya, Zambia, Uganda na kwingineko, waje wafungue matawi ya vyama vyao mabali mbali vya kisiasa. Huo...
  2. K

    Muungano wa Upinzani Umekwamishwa na Nini?

    Nafikiri sababu kubwa ni hii posho/ruzuku. Chama kinachokuwa na wabunge wengi ndicho kinachopata ruzuku nono. Kwa hivi vyama havina njia nyingine ya mapato ya kukidhi, kila chama kinawania kupata wawakilishi/wabunge wengi iwezekanavyo. Wanachama michango yao ni ya kusuasua. Mara nyingi hawatoi...
  3. K

    Tension between Museveni and The Baganda Heightened

    Kila nchi katika dunia ina matatizo yake. Tusiwasahau wenzetu wa Tarime wanaochinjana kila kukicha ndani ya nchi yetu. Na bado nasi tunazungumzia hiyo hiyo E.A.Federation ambayo Makao Makuu yake tunayo Arusha.
  4. K

    Was Gaddafi right to call for Nigeria to split?

    Nyerere, Mroman Catholic, Rais wa Kwanza wa Tanzania, alipotambua kujitenga kwa wa Ibo, Waroman Catholic wa Biafra ya Nigeria hiyo hiyo, huku akitaka muungano wa Afrika, alikuwa shujaa. Gadhafi, Muislamu, Rais wa kudumu wa Libya, anapotaka kujitenga kwa Waislamu na Wakristo wa Nigeria, huku...
  5. K

    Rangi za Uongozi wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM-CWT?

    Umenoa mkuu wangu, Sophia Simba ni wa rangi ya bluu, katafiti zaidi. Thread inaashiria UDINI MTUPU.
  6. K

    Daudi Mwakawago afariki Dunia

    Kwa masikitiko makuu na hudhuni nyingi naipokea taarifa hii. Nilimfahamu Daudi tangu siku za ujana wake akiwa TANU mpaka katika uzee akiwa UN. Alikuwa mchapa kazi mahiri sana, mcheshi na mkarimu. Mungu ampe makazi mema yanayomstahili na awape nguvu wafiwa ya kustahimili msiba huu mkubwa. Ameen!
  7. K

    Masikini Haji Manara!

    Ule msemo wa kisheria unaodai kuwa "mtuhumiwa hana hatia, mpaka pale mahakama itapomtia hatiani" unahitajika hapa. Tuwaonee huruma waliotapeliwa kwa kiwango kile kile tunachohitajika kumwonea huruma aliyetuhumiwa.
  8. K

    Ali Karume kugombea urais Zanzibar 2010

    Kwa hakika Ali Abeid Amani Karume, bila ya kujali jina lake, anayo haki ya msingi ya kikatiba, kugombea nafasi yoyote katika nchi yake ya Tanzania kama alivyo na haki ya kupiga kura na kumchagua kiongozi yeyote anayemtaka. Ni unyanyashaji na ubaguzi wa hali ya juu sana kumnyima haki yake hiyo...
  9. K

    Kwa nini Ulizaliwa Tanzania?

    Usijute kuzaliwa Tanzania. Jilaumu kwa kukaa pembeni ya ulingo na kulalamika. Mvunja nchi ni mwananchi. Nini mchango wako katika kuirekebisha nchi yako? Viongozi wa nchi wanatokana na wananchi wake. Viongozi wabovu wa wananchi wanapatikana miongoni mwa wananchi wabovu. Ukweli unauma.
  10. K

    CHADEMA imefanya nini kustahili dhamana ya Uongozi wa Taifa?

    Wananchi, Kabla hatujalinganisha ufanisi wa miaka 15 ya Chadema na ile miaka 50 ya TANU/ASP/CCM, inatubidi, ili kupata usahihi wa jawabu, inatupasa kwanza tuviweke vyama hivi vyote viwili katika mizani moja na uwanja tambarare wa ushindani. Tumejiuliza? Kwani TANU au ASP ilifanya kitu...
  11. K

    Kakobe vs Vyama vya Upinzani?

    Unapowalinganisha Waalimu ni lazima pia uwalinganishe na wanafunzi wao. Huwezi kusema Mwalimu fulani hodari kuliko mwenzake, eti kwa kuwa wanafunzi wake wengi wamefaulu. Je, wanafunzi waliofeli kule kwa mwenzake wakoje? Kuna wanafunzi wasioweza kufundishika hata wakipewa mwalimu gani. Pamoja...
  12. K

    Kero za Muungano na utatuzi wake - Sehemu ya Pili

    Tukiirudia historia ya Muungano wa Tanganyika kimakini, tutagundua kuwa huu muungano haufanani na muungano wowote uliowahi kutokea kabla yake. Na hicho ndio kiini cha kero zote za muungano tulizonazo na tunazokabiliana nazo. Kusema kweli hatuna muungano wa nchi wala serkali zetu. Muungano huu...
  13. K

    Kuigawanya Serikali ya CCM katika awamu

    Katika vitu vibovu ambavyo tumerithi kutoka TANU/CCM ni ujinga na uwoga. Ujinga wenyewe si wa kusoma shule ni ule wa kutotambua haki zetu na tunapozitambua hatujui jinsi ya kuzipata na tunapozipata hatujui kuzidumisha wala kuzistawisha. Uwoga ni ule wa kutokuwa na ujasiri wa kuthubutu. Ndani...
  14. K

    Ujumbe Wa Maalim Seif Shariff Hamad Kwa Wazanzibar

    Maalim Seif Shariff Hamad na Ibrahim Lipumba maadamu wanakubaliwa kugombea Urais wa Zanzibar na Tanzania na wanachama wao wa CUF kwa mujibu wa katiba ya chama chao, wana haki ya msingi ya kugombea nafasi hiyo kwa miaka 26 na zaidi. Haki hii hata Julius Nyerere alikuwa nayo katika TANU na CCM pia.
  15. K

    JINA LAKO au MAJINA YAKO?

    Waungwana, Mtu jina lake ndilo linalomtambulisha yeye mmoja pekee katika kundi. Mathalan, mtu akisema jina lake John au Kidawa au Ali anakuwa hajajitambulisha kikakamilifu kwa kuwa ametumia jina la kawaida. Kuna akina John au Kidawa au Ali kibao. Na akitumia jina la ukoo pekee, kwa mfano...
Back
Top Bottom