Kero za Muungano na utatuzi wake - Sehemu ya Pili


Unaona hata hawa jamaa wanazungumzia utumwa! Historia ya utumwa haikwepeki. Wanapozungumzia mauaji ya waarabu wakati wa mapinduzi ni lazima muangalie pia kwa nini palikuwa na chuki kiasi hicho. Si kutokana na simulizi tu bali ni kutokana na vitendo walivyokuwa wakifanyiwa watu weusi. Utumwa haukuwa lele mama.Ukumbuke vile vile hata baada ya BIASHARA ya utumwa kupigwa marufuku, utumwa ulikuwa halali Zanzibar! Hao wanaosifia mchanyiko wa damu Zanzibar inabidi wazungumzie ilipatikana vipi. Wazungumzie upendeleo waliopewa wao kuoa lakini kutoolewa. Unadhani kwa nini Karume mara baada ya kupindua alikimbilia kuoa muarabu na kuhalalisha waarabu na wahindi kuolewa na watu weusi! Ingekuwa ni mazoea pasingekuwa na haja ya kufanya hivyo. Utawala wa Sultan haukuwa benign kama mnavyotaka kutuambia. Maovu mengi yalifanyika. Kwa vile umejiita mtu mweusi nenda kwa watu weusi wenzako ukawaulize ilivyokuwa na watakuambia. Ni sehemu ya historia yako na haikwepeki.

Amandla......
 
Unaona hata hawa jamaa wanazungumzia utumwa! Historia ya utumwa haikwepeki. Wanapozungumzia mauaji ya waarabu wakati wa mapinduzi ni lazima muangalie pia kwa nini palikuwa na chuki kiasi hicho. Si kutokana na simulizi tu bali ni kutokana na vitendo walivyokuwa wakifanyiwa watu weusi. Utumwa haukuwa lele mama.Ukumbuke vile vile hata baada ya BIASHARA ya utumwa kupigwa marufuku, utumwa ulikuwa halali Zanzibar! Hao wanaosifia mchanyiko wa damu Zanzibar inabidi wazungumzie ilipatikana vipi. Wazungumzie upendeleo waliopewa wao kuoa lakini kutoolewa. Unadhani kwa nini Karume mara baada ya kupindua alikimbilia kuoa muarabu na kuhalalisha waarabu na wahindi kuolewa na watu weusi! Ingekuwa ni mazoea pasingekuwa na haja ya kufanya hivyo. Utawala wa Sultan haukuwa benign kama mnavyotaka kutuambia. Maovu mengi yalifanyika. Kwa vile umejiita mtu mweusi nenda kwa watu weusi wenzako ukawaulize ilivyokuwa na watakuambia. Ni sehemu ya historia yako na haikwepeki.

Amandla......

Kwa hiyo kila tunapokaa kwenye viriri iwe kazi yetu ni kuhubiri machungu ya Mapinduzi na utumwa tuu...you are one of the great thinker :confused:
 
Kwa hiyo kila tunapokaa kwenye viriri iwe kazi yetu ni kuhubiri machungu ya Mapinduzi na utumwa tuu...you are one of the great thinker :confused:

Sasa wewe great thinker unayejiita mweusi kwa nini unaogopa kujua historia yako? Au ni kilemba cha ukoka unachotaka kutuvisha? Ukiwa humu ni mweusi mwenzetu lakini ukiwa na ndugu zako ni m-omani! Umesema haujui historia ya nchi yako lakini unachelea kuuliziai? Mwafrika gani wewe usiyetaka kujua ulikotoka? Hivi unaamini kweli sisi uelewa wetu unatokana na kuzungumzia asili yetu kila kukicha? Tunazungumzia mengi zaidi lakini hatuogopi kuzungumzia yalio machungu. Nisehemu ya identity yetu.

Wewe ndiye unayedai mimi ni great thinker. Mwenyewe sijawahi kujihesabu kuwa mmoja wa hao ma-great thinker. Ningekuwa hivyo basi kwa nini nisiwe mhandisi badala ya fundi mchundo?

Amandla......
 
Tukiirudia historia ya Muungano wa Tanganyika kimakini, tutagundua kuwa huu muungano haufanani na muungano wowote uliowahi kutokea kabla yake. Na hicho ndio kiini cha kero zote za muungano tulizonazo na tunazokabiliana nazo. Kusema kweli hatuna muungano wa nchi wala serkali zetu. Muungano huu umesimama katika mambo kumi na moja waliyokubaliana Julius Nyerere na Abeid Amani Karume na haya mambo mengine machache ya ziada yaliyokubaliwa na serikali ya Tanzania na ile ya Zanzibar. Na hata hivyo, kuna baadhi kkatika haya ya ziada ambayo seikali ya Zanzibar inayalalamikia kuwa yameongezwa kinyemela. Wakati Karume Snr. akikubali muungano wa ushirikiano katika yale mambo kumi na moja ya awali, alidai kubaki na nchi yake na serikali yake. Nyerere aliridhia Karume abaki na nchi yake na seikali yake, huku yeye akadai kuiingiza nchi yake ya Tanganyika na serikali ya Tanganyika ndani ya United Republic of Tanzania.
Na wakati huo huo, Nyerere kwa kutaka kuifuta Tanganyika, akawa anasisitiza jina la Tanzania Bara hadi akafikia kuwaita Watanganyika kama Wazanzibara. Mpaka hii leo, imefikia Tanganyika kuitwa Tanzania na Zanzibar kubaki kuwa Zanzibar. Ni mara ngapi tumeshasikia na kusoma Tanzania na Zanzibar? Nchi ya Tanganyika na serikali yake ndio zilizomezwa na Tanzania. Naam, huu ni wakati muafaka wa kudai nchi yetu ya Tanganyika na serikali yake viibuke kutoka Tanzania. Kama tunataka muungano wa kweli, zipo hatua mbili tu za kuchukuliwa: Ya kwanza tuwe na nchi na serikali moja ya Tanzania au ya pili tuwe na Shirikisho la Tanzania na serikali ya Zanzibar na ile ya Tanganyika ziwe ni state governments subsidiary to the Federal Government. Na kero zote za muungano zitatokomea huko.
 
Ninavyojua mimi ni Nyerere ndiye aliyesisitiza Zanzibar ibaki kama nchi tofauti. Karume alitaka Muungano wa jumla, rais akiwa Nyerere na yeye makamu wa rais wa Tanzania. Ni huyo mnayemlaani ndiye aliyesisitiza kuwa identity ya Zanzibar isiathirike. Hivi mnaamini kweli kama Nyerere angetaka kuimeza Zanzibar angeshindwa?

Amandla.....
 
ni muhimu kuwa na serikali ya tanganyika kwani kila mwaka zanzibar wao husherekea siku ya mapinduzi na wana rais wao lakini sisi watanganyika tunasheherekea 9 disenba wakati serikali ya tanganyika haipo. huu ndo wakati wa kuunda serikali ya tanganyika na itasaidia kuupunguza kero zinazoitwa za muungano
 
Ninavyojua mimi ni Nyerere ndiye aliyesisitiza Zanzibar ibaki kama nchi tofauti. Karume alitaka Muungano wa jumla, rais akiwa Nyerere na yeye makamu wa rais wa Tanzania. Ni huyo mnayemlaani ndiye aliyesisitiza kuwa identity ya Zanzibar isiathirike. Hivi mnaamini kweli kama Nyerere angetaka kuimeza Zanzibar angeshindwa?

Amandla.....

Na mawazo yako alifanya hivyo kwa maslahi ya Zanzibar :confused:
Karume hakuwa mtu aliyeona mbali kutokana na shule kuwa ndogo na hata uwezo wake wa kisiasa pia ndio akashindwa kupata 100% ya Zanzibar kama nchi.

Sasa suali kama wewe kweli unajua unachokizungumza, ni kwanini Nyerere alikataa wazo la kuimeza Zanzibar moja kwa moja?---mimi najua jawabu na namfahamu Nyerere alikuwa na plan gani na evidence zipo wazi za utekelezaji wa plan hiyo ya Nyerere.

Ukumbi wako...
 
BONIFACE Meena

UTAFITI wa Taasisi ya Utafiti kuhusu Kuondoa Umaskini (Repoa), kuhusu mabadiliko ya katiba, muungano na madaraka umeonyesha kuwa asilimia 40 ya Watanzania wanataka Bunge lisimamie mchakato mzima wa mabadiliko ya kupatikana Katiba Mpya.


Pia, utafiti huo umebainisha kuwa asilimia 88 ya Watanzania hawataki muungano uvunjwe huku asilimia 23 wakitaka muungano huo uvunjwe.


Mtafiti Mshauri wa Repoa, Costantine Manda alibainisha hayo jana wakati wa uzinduzi wa utafiti huo uliofanyika kati ya Mei 27 hadi Juni 30 mwaka jana.


"Utafiti wetu umetokana na maswali waliyoulizwa watu wa kada tofauti wapatao 2,400 ambapo mbali na asilimia 40 kutaka Bunge lisimamie kupatikana Katiba, asilimia 25 wanataka Rais ndiye asimamie huku asilimia 18 ikitaka vyama vya

kiraia, asilimia 9 ikitaka mahakama na asilimia 6 ikitaka vyama vya siasa vifanye hivyo,"alisema Manda.Alisema mbali na kuangalia upande huo pia wananchi asilimia 54 wametaka mawaziri wote wasitokane na wabunge,hivyo uwekwe utaratibu katika Katiba Mpya ya jinsi ya kuwapata mawaziri hao.


Manda alisema pia waliangalia watu kama wana maoni juu ya Rais kuongoza kwa awamu mbili au la na kati ya wananchi hao waliohojiwa asilimia 87 walieleza kuwa aongoze kwa awamu mbili huku asilimia 12 wakitaka asiwe na ukomo wa kuongoza.


"Wengi wanaonyesha kuwa wanataka Rais aongoze kwa awamu mbili ila kuna wengine ambao wanapinga hilo kama mnavyoona kwenye utafiti wetu,"alisema Manda.


Hata hivyo alisema wananchi asilima 85 wanakubali kufanyika kwa mabadiliko ya katiba iliyopo na kati yao asilimia 71 wanasema ni muhimu iwe hivyo kwa kuwa nchi inakoelekea hivi sasa ni kubaya.

"Lakini kuna wengine asilimia 19 wanaridhishwa na jinsi nchi inavyoongozwa hivi sasa na demokrasia iliyopo,"alisema Manda.

SOURCE: mwananchi 15/02/2013

Edited by MZALENDO.NET

**Heading is misleading, modified to Watanganyika.chanzo. Watanganyika wengi hawataki Muungano uvunjwe - Mzalendo.net
 
BONIFACE Meena

UTAFITI wa Taasisi ya Utafiti kuhusu Kuondoa Umaskini (Repoa), kuhusu mabadiliko ya katiba, muungano na madaraka umeonyesha kuwa asilimia 40 ya Watanzania wanataka Bunge lisimamie mchakato mzima wa mabadiliko ya kupatikana Katiba Mpya.


Pia, utafiti huo umebainisha kuwa asilimia 88 ya Watanzania hawataki muungano uvunjwe huku asilimia 23 wakitaka muungano huo uvunjwe.


Mtafiti Mshauri wa Repoa, Costantine Manda alibainisha hayo jana wakati wa uzinduzi wa utafiti huo uliofanyika kati ya Mei 27 hadi Juni 30 mwaka jana.


“Utafiti wetu umetokana na maswali waliyoulizwa watu wa kada tofauti wapatao 2,400 ambapo mbali na asilimia 40 kutaka Bunge lisimamie kupatikana Katiba, asilimia 25 wanataka Rais ndiye asimamie huku asilimia 18 ikitaka vyama vya

kiraia, asilimia 9 ikitaka mahakama na asilimia 6 ikitaka vyama vya siasa vifanye hivyo,”alisema Manda.Alisema mbali na kuangalia upande huo pia wananchi asilimia 54 wametaka mawaziri wote wasitokane na wabunge,hivyo uwekwe utaratibu katika Katiba Mpya ya jinsi ya kuwapata mawaziri hao.


Manda alisema pia waliangalia watu kama wana maoni juu ya Rais kuongoza kwa awamu mbili au la na kati ya wananchi hao waliohojiwa asilimia 87 walieleza kuwa aongoze kwa awamu mbili huku asilimia 12 wakitaka asiwe na ukomo wa kuongoza.


“Wengi wanaonyesha kuwa wanataka Rais aongoze kwa awamu mbili ila kuna wengine ambao wanapinga hilo kama mnavyoona kwenye utafiti wetu,”alisema Manda.


Hata hivyo alisema wananchi asilima 85 wanakubali kufanyika kwa mabadiliko ya katiba iliyopo na kati yao asilimia 71 wanasema ni muhimu iwe hivyo kwa kuwa nchi inakoelekea hivi sasa ni kubaya.

“Lakini kuna wengine asilimia 19 wanaridhishwa na jinsi nchi inavyoongozwa hivi sasa na demokrasia iliyopo,”alisema Manda.

SOURCE: mwananchi 15/02/2013

Edited by MZALENDO.NET

**Heading is misleading, modified to Watanganyika.chanzo. Watanganyika wengi hawataki Muungano uvunjwe - Mzalendo.net

Pia, utafiti huo umebainisha kuwa asilimia 88 ya Watanzania hawataki muungano uvunjwe huku asilimia 23 wakitaka muungano huo uvunjwe.

my take: 88 + 23 = 111%
 
BONIFACE Meena

UTAFITI wa Taasisi ya Utafiti kuhusu Kuondoa Umaskini (Repoa), kuhusu mabadiliko ya katiba, muungano na madaraka umeonyesha kuwa asilimia 40 ya Watanzania wanataka Bunge lisimamie mchakato mzima wa mabadiliko ya kupatikana Katiba Mpya.


Pia, utafiti huo umebainisha kuwa asilimia 88 ya Watanzania hawataki muungano uvunjwe huku asilimia 23 wakitaka muungano huo uvunjwe.


Mtafiti Mshauri wa Repoa, Costantine Manda alibainisha hayo jana wakati wa uzinduzi wa utafiti huo uliofanyika kati ya Mei 27 hadi Juni 30 mwaka jana.


"Utafiti wetu umetokana na maswali waliyoulizwa watu wa kada tofauti wapatao 2,400 ambapo mbali na asilimia 40 kutaka Bunge lisimamie kupatikana Katiba, asilimia 25 wanataka Rais ndiye asimamie huku asilimia 18 ikitaka vyama vya

kiraia, asilimia 9 ikitaka mahakama na asilimia 6 ikitaka vyama vya siasa vifanye hivyo,"alisema Manda.Alisema mbali na kuangalia upande huo pia wananchi asilimia 54 wametaka mawaziri wote wasitokane na wabunge,hivyo uwekwe utaratibu katika Katiba Mpya ya jinsi ya kuwapata mawaziri hao.


Manda alisema pia waliangalia watu kama wana maoni juu ya Rais kuongoza kwa awamu mbili au la na kati ya wananchi hao waliohojiwa asilimia 87 walieleza kuwa aongoze kwa awamu mbili huku asilimia 12 wakitaka asiwe na ukomo wa kuongoza.


"Wengi wanaonyesha kuwa wanataka Rais aongoze kwa awamu mbili ila kuna wengine ambao wanapinga hilo kama mnavyoona kwenye utafiti wetu,"alisema Manda.


Hata hivyo alisema wananchi asilima 85 wanakubali kufanyika kwa mabadiliko ya katiba iliyopo na kati yao asilimia 71 wanasema ni muhimu iwe hivyo kwa kuwa nchi inakoelekea hivi sasa ni kubaya.

"Lakini kuna wengine asilimia 19 wanaridhishwa na jinsi nchi inavyoongozwa hivi sasa na demokrasia iliyopo,"alisema Manda.

SOURCE: mwananchi 15/02/2013

Edited by MZALENDO.NET

**Heading is misleading, modified to Watanganyika.chanzo. Watanganyika wengi hawataki Muungano uvunjwe - Mzalendo.net


Hapana ni kuwa hawajui kuwa UPO; sababu hawaoni faida yoyote wanayoipata toka huko isipokuwa Presidential rotations na ile chachu ya Umeme...
 
2400 kati ya wangapi???!!!
Asilimia 88 ya watu 2400 au 23???? ya 2400 ndio inatosha kusema Watanzania???? Kati ya milion 40???!!!!

Hili suala la serikali mbili au tatu litazua mengi
 
watu 2400 ni sampuli ndogo sana kubeba taswira ya watu mil 45.maoni tunayoyaheshimu ni yale ya TUME YA MABADILIKO YA KATIBA TU,hizi nyingine porojo tu.watanzania wanataka serikali 3 tu na kama inashindikana basi kuwepo na serikali moja tu.huo utafiti umekaa kikanjanja
 
Pia, utafiti huo umebainisha kuwa asilimia 88 ya Watanzania hawataki muungano uvunjwe huku asilimia 23 wakitaka muungano huo uvunjwe.

my take: 88 + 23 = 111%


Hapa tayari mahesabu ni ya asilielfu sio asilimia. Hili suala la muungano uwepo au usiwepo waaitishe kura ya maoni, a credible one, hii ndio itakata mzizi wa fitina.
 
Kwa nini tusiseme kuwa huo utafiti uko biased? Yaani watanzania 45 mil ukaulize 2,400 mbona sample size ni ndogo sana wala msianze kutuuzia mapendekezo yenu kwa kuyaremba kuwa mmefanya utafiti. Sana sana mmepita sehemu mnazojua mtapata majibu mnayoyataka
 
Huo utafiti wa wajinga repoa na wahuni wao 2400 wapeleke kwa wahuni wenzao....tumesema hatutaki muungano labda wa serikali tatu... full stop
 
REPOA nayo imekuwa kama ile ya Dr Bana? Huyu mtafiti hovyo kabisa!

Kwanza samuli yako ni ndogo. sana. Hata kama angesema wana APPT Maendeleo wengi hawataki muungano uvunjwe, bado watu 2400 kati ya wanachama wote wa APPT-Maendeleo itakuwa ndogo.

Repoa inayoaminika kwa kutoa tafiti zinazoeleweka ndo inakuja na Data kama hizi, 'Pia, utafiti huo umebainisha kuwa asilimia 88 ya Watanzania hawataki muungano uvunjwe huku asilimia 23 wakitaka muungano huo uvunjwe."!!!!????? 88+23=111. Nini maana ya asilimia?
 
Tuachiwe tupumueeeeee hawawezi wakakubari mapepari muungano uvunjwe sababu kuna kisiwa fungu mbaraka kinaitwa kina mafuta hicho kinawatoa roho watanganyika
 
Suluhu hapa ni kuleta kura ya maoni tu.........Zanzibar wawe na yao na Tanganyika wawe na yao tuone! Trust me 100% ya Zanzibar itakataa muungano na 98% ya Tanganyika itakataa muungano.........unfortunately kudai kura ya maoni juu ya muungano ni tantamount na treason !
 
Suluhu hapa ni kuleta kura ya maoni tu.........Zanzibar wawe na yao na Tanganyika wawe na yao tuone! Trust me 100% ya Zanzibar itakataa muungano na 98% ya Tanganyika itakataa muungano.........unfortunately kudai kura ya maoni juu ya muungano ni tantamount na treason !
...Mungano wa kweli ni slerikali 1 haya mengine ya serikali 2,3,au zaidi ya hizo ni kuendelea kuonyesana vidole...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom