unajua kuna watu wengine wengi sana hapa kwetu wamefumba macho, hata wakiambiwa fumbua macho kumeshakucha uone ukweli hataki...hivi kuna hasiyeona mambo ya ubadhilifu yanayotendeka wazi wazi humu nchini na kikundi cha watu wachache ambao wengine unakuta kila awamu ya serikali wamo tu ili kulinda...
asilimia kubwa ya amri za polisi uwa ni shinikizo la ccm hasa katika kulinda masilahi yao binafsi, polisi inatakiwa na wao wajiongeze sio kuburuzwa tu kupiga raia hata pale ambapo HAKI inaporwa
acheni kuweweseka wazee wa kijani, kuna kushinda na kushindwa na ukishindwa kubali tu kwani lazima huyo dogo arithi nafasi ya babake..acheni kulazimisha utawala wa koo
Tunataka haki itendeke, lakini sio itendeke tu kwa maneno, bali haki ionekane ikitendeka maana hawa mumiani wametuchosha na unyang'anyi wa wazi wazi kuiba kura za wanyonge
Mungu kaweka rasilimali nchini ili kila mtanzania anufaike kwa usawa, wao wamegeuza mali za familia kwa utawala wa kifamilia kupasiana kijiti, Mungu ataanza kunyoosha mkono wake kwa kutetea wanyonge na nafsi zinazodhulumika!!!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.